Reality of Christ Church

Reality of Christ Church Reaching out to the nation through biblical teaching, prayer and deliverance, healing, prophecy.

The core mission of Reality of Christ Ministry is to see the life of Christ manifest into the lives of people in the community and nations through the teachings of the word of God, healing, prophecy, deliverance, love and compassion. Mark 16; 15-18
He said to them, "Go into all the world and preach the good news to all creation. Whoever believes and is baptised will be saved, but whoever does not

believe will be condemned. And these signs will accompany those who believe: In my name they will drive out demons; they will speak in new tongues; they will pick up snakes with their hands; and when they drink deadly poison, it will not hurt them at all; they will place their hands on sick people, and they will get well."

Matukio mengi mabaya huwa ni marudio ya kile ambacho kimeshafanyika kwenye ulimwengu wa roho, na tunapoomba rehema tunam...
02/09/2026

Matukio mengi mabaya huwa ni marudio ya kile ambacho kimeshafanyika kwenye ulimwengu wa roho, na tunapoomba rehema tunamuomba Mungu atuepushe na hiyo adhabu.
Ndio maana kwenye;

📖 Kutoka 34:7
mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne. 

Wewe upo kizazi cha ngapi?

📖 Warumi 8:1
Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. 

Ni kwa sababu kuna damu ya Yesu ambayo ilimwagika kwa ajili ya kuturehemu na ndio maana hakuna hukumu ya adhabu juu ya walio katika Kristo Yesu.

Pamoja na hayo yote, ni muhimu pia kujua ni adhabu gani ambayo iliachiliwa kwenye ulimwengu wa roho kutokana na kilichofanyika kutokana na matukio yaliyotokea.

Chochote ambacho kinakutesa au unajitahidi kukiacha na unashindwa ilhali unajua kabisa sio mapenzi ya Mungu, jua lazima kina connection ya damu ya unapotokea, kuna kilichofanyika na kikafanya adhabu ikaachiliwa...hapa hautoki kwa kukemea bali rehema.

📖 Kumbukumbu la Torati 23:2
Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa BWANA; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano wa BWANA. 

Hapa kuna vizazi kumi ambavyo vimekataliwa, k**a mtu amezaliwa vizazi ndani ya hivi kumi anaweza kwenda kanisani, akatamkiwa baraka lakini hatoona matokeo yoyote. Huyu anaweza kuwa na bidii sana lakini akaishia kwenye umasikini, yaani hakuna kinachoenda kwake.

Hawa watu Mungu alikuwa ameachilia adhabu kwao, wewe kwenu kuna adhabu gani iliyoachiliwa? na ni nini kilifanyika kikapelekea adhabu hiyo kuachiwa?

Leo katika siku hii ya tatu ya mfungo tulikuwa na maombi ya rehema tukimuamini Mungu kuturehemu na kuondoa adhabu na madhara ya adhabu yaliyokuwa yameachiliwa kwetu na kwenye koo zetu.

📖 Maombolezo 3:21-23Najikumbusha neno hili, Kwa hiyo nina matumaini. Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, Kwa kuwa reh...
02/09/2026

📖 Maombolezo 3:21-23
Najikumbusha neno hili,
Kwa hiyo nina matumaini.
Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii,
Kwa kuwa rehema zake hazikomi.
Ni mpya kila siku asubuhi;
Uaminifu wako ni mkuu.

Kuokoka ni kutubu, neno rehema ni neno ambalo linahusika na upatanisho.

Anavyosema kuwa rehema zake ni mpya kila asubuhi, maana yake kazi ya rehema ni kutupatanisha kila siku na Mungu. Sasa huwezi kupatanishwa na kitu, mtu au hata siku ambayo haijafarakanishwa na wewe.
Katika ulimwengu wa roho siku imebeba utawala, maamuzi na kuna matukio yamefichwa katika siku.
Katika siku zilizobakia kwenye huu mwezi, ni matukio gani ambayo katika ulimwengu wa roho umeshatengenezewa?

Huwezi kuomba rehema k**a hakuna deni la dhambi.
Kuokoka maana yake ni nafsi yako wewe inakiri juu ya dhambi ambazo umeziishi na kuzitenda.
Dhambi ya asili ni dhambi ambayo umeirithi..na hii dhambi huwa ina makundi mawili; Uasi na Uovu.

Haya ni maneno ambayo yanawiana lakini asili yake ni tofauti.
Dhambi ni kwenda kinyume na maagizo ya Mungu.

📖 1 Yohana 3:4
Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi.

📖 Yakobo 4:17
Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi.

Adamu na Hawa walipotenda dhambi, hili tukio lilihusisha nafsi na kuleta uasi.
Uasi ni kwenda kinyume na mamlaka na sheria iliyowekwa kwa makusudi. Uasi ni hatua ya juu zaidi, na huu hufanyika nje, uovu huanzia katika hali ya ndani ya moyo.
Ili uasi utendeke ni lazima kuwepo na uovu ambao umeanzia ndani kabisa ya moyo.

Uasi ni kitendo cha nje lakini uovu ni kitendo cha ndani.
Pakishakuwepo na uasi na uovu kile kinachotendeka kinampelekea Mungu kuachilia adhabu.
Adamu na Hawa ili wafanye uasi ni lazima kuna uovu ambao ulianzia ndani, na baadae ulipokuja kutoka nje ndio ukawa uasi.

Hukumu za Mungu zinapoachiliwa huachiliwa katika bloodline.

📖Mwanzo 4:7
K**a ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.

Wakati Mungu anamwambia Kaini kuwa dhambi iko mlangoni na inamtamani. Hapa tayari uovu ulikuwa umejaa ndani yake, ikapelekea uasi ambao ukapelekea Mungu kuachilia adhabu.

02/09/2026

DUNAMIS — NGUVU YA KUTENDA NA NGUVU YA KUSIMAMA 🔥

Neno “Power” linamaanisha Dunamis — “Mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu.” (Matendo 1:8)

Dunamis inaelezea mambo mawili:

1️⃣ Uwezo wa Kutenda Miujiza
Ni uwezo wa kufanya kazi za kiroho na kutenda mambo ya kimiujiza ambayo yanazidi uwezo wa kibinadamu.

2️⃣ Uwezo wa Kusimama
Mtu anapobeba Dunamis, hata pale ambapo mazingira na taratibu za kawaida zinakuwa dhidi yake, anapewa uwezo wa kusimama imara.

Huwezi kujengwa na kubaki bila nguvu.
Nguvu ni moja ya ushahidi kwamba umeendelea kujengwa na kukomaa kiroho.

WWW.DUNAMIS.AFRICA

Imani ROC

SIKU 5 ZA KUFUNGA NA KUOMBA (DAY THREE) 🔥Tunamshukuru Mungu kwa kutufikisha siku ya tatu ya mfungo wetu wa siku 5. Tunap...
02/09/2026

SIKU 5 ZA KUFUNGA NA KUOMBA (DAY THREE) 🔥

Tunamshukuru Mungu kwa kutufikisha siku ya tatu ya mfungo wetu wa siku 5. Tunapoendelea kutafuta uso wake katika mwezi huu wa 9, leo tunaelekeza maombi yetu kwenye rehema za Mungu, tukiamini kuwa ni rehema zake zitakazotutangulia na kutufungulia njia katika kila hatua ya maisha yetu.

📖 Maombolezo 3:22-23

Prayer Point:
Rehema za Mungu zikatangulie mbele yetu huu mwezi wa 9.

Tunakukaribisha kuungana nasi kuanzia saa kumi na moja jioni hapa Reality of Christ Church, Sinza Mori kwa ajili ya maombi ya pamoja.
Tutakuwa Live🔴 pia kwenye ukurasa wetu wa YouTube wenye jina REALITY OF CHRIST CHURCH na kupitia ROC TV.

Karibu sana na tunakutakia siku njema ya mfungo.

02/09/2026

DUNAMIS 2026 🔥

Dar es Salaam, Tanzania na dunia kwa ujumla... jiandae kwa kile Mungu anachoenda kufanya!

Kuanzia tarehe 28 Oktoba hadi 1 Novemba, tutakuwa na furaha ya kumpokea tena Apostle Michael Orokpo kutoka Nigeria🇳🇬 
Wengi walishuhudia nguvu na ufunuo wa Mungu kupitia huduma yake alipokuja kwenye DUNAMIS iliyopita, na safari hii tunaamini Mungu atafanya makubwa zaidi kuliko yale aliyofanya mara ya mwisho.

K**a ulikuwepo, unajua kilichotokea. K**a hukuwepo, huu ndio wakati wako!

Panga ratiba yako mapema, waalike wengine na jiandae kwa siku tano za ufunuo, maombi na udhihirisho wa nguvu za Mungu katika DUNAMIS 2026.

Jisajili mapema kupitia website yetu ambayo ni;
www.dunamis.africa 
Na hakikisha unakuwa sehemu ya mkutano huu mkubwa na wa kipekee sana.

Mungu ana jambo kubwa kuliko unavyoweza kufikiria!

Katika ibada ya leo ya mfungo, ikiwa ni siku ya pili, tulianza kwa kumshukuru Mungu kwa kutuingiza salama katika mwezi w...
01/09/2026

Katika ibada ya leo ya mfungo, ikiwa ni siku ya pili, tulianza kwa kumshukuru Mungu kwa kutuingiza salama katika mwezi wa tisa na kwa neema yake inayoendelea kuonekana katika maisha yetu. 

Tuliinua maombi yetu mbele za Mungu tukimwomba atangulie mbele yetu katika mwezi huu mpya, aondoe kila jiwe la kikwazo na kila jambo linaloweza kuzuia safari yetu na ya familia zetu kuelekea katika utimilifu wa ahadi zake.

Pia tuliomba milango ya fursa zilizofichwa ndani ya mwezi huu wa tisa ifunguliwe kwa neema ya Mungu, ili tuweze kuziona, kuzitambua na kuzitumia kwa manufaa ya kusudi lake katika maisha yetu. Pia tulimuomba Bwana atupe uwezo wa kumiliki kila fursa atakayotuwekea mbele yetu.

Kwa kumalizia, tuliomba Mungu atupe alama za ushindi katika mwezi huu wa tisa, pamoja na ushuhuda unaoonekana wa wema Wake, neema Yake na uaminifu Wake. Tunaamini kuwa mwezi huu utakuwa mwezi wa mafanikio, fursa mpya, ushindi na Utukufu wa Mungu kuonekana katika maisha yetu kwa namna ya kipekee.

Kesho tunaendelea na mfungo huu siku ya tatu, andaa moyo wako vema na usisahau kufunga.

01/09/2026

DUNAMIS 2026 🔥

Dar es Salaam, Tanzania na Afrika na dunia kwa ujumla... kuna jambo kubwa linakuja!

Kwa siku tano mfululizo, kuanzia tarehe 28 Oktoba hadi 1 Novemba, Reality Of Christ Church - Tegeta itakuwa kituo cha maelfu ya watu watakaokusanyika kwa ajili ya kukutana na Mungu katika namna ya kipekee.

Mwaka huu tunayo furaha kumpokea Pastor George Mukabwa kutoka Mwanza, pamoja na watumishi wengine wa Mungu kutoka maeneo mbalimbali, kwa ajili ya siku za mafundisho ya kina, maombi yenye matokeo na udhihirisho mkubwa sana wa nguvu za Mungu.

K**a unatafuta muelekeo, ukuaji wa kiroho na hatua mpya katika safari yako ya imani, basi hizi ni tarehe ambazo hutakiwi kukosa. Panga ratiba yako vizuri mapema, waalike marafiki na familia yako, na jiandae kwa DUNAMIS 2026!

Mungu ana jambo kubwa kuliko unavyoweza kufikiria!!!

SIKU 5 ZA KUFUNGA NA KUOMBA (DAY TWO) 🔥Mwezi mpya umeanza, na Mungu ametupa neema ya kuiona siku nyingine tena. Katika s...
01/09/2026

SIKU 5 ZA KUFUNGA NA KUOMBA (DAY TWO) 🔥

Mwezi mpya umeanza, na Mungu ametupa neema ya kuiona siku nyingine tena. Katika siku hii ya pili ya mfungo wetu wa siku 5, tunaungana katika maombi maalum tukiamini kuwa Mungu atatenda makubwa katika mwezi huu wa 9.

Prayer Points:
1. Mshukuru Mungu kwa ajili ya mwezi wa 9.

2. Muombe Bwana Yesu atangulie mbele yako na kwenye kila kitu unachokifanya mwezi wa 9, aondoe kila jiwe (kila kikwazo) kinachozuia safari yako na ya familia yako kuelekea katika ahadi Zake.

3. Omba milango ya fursa iliyoko ndani ya mwezi wa 9 ifunguke, na neema yake ikuwezeshe kumiliki kila fursa atakayoiweka mbele yako.

4. Muombe Mungu akupe alama ya ushindi katika mwezi huu wa 9, ushuhuda unaoonekana wa wema wake, neema yake na uaminifu wake.

Tunakukaribisha kuungana nasi leo saa kumi na moja jioni katika maombi haya ya nguvu. Tunaamini kuwa Mungu atatangulia mbele yako, atafungua njia na kukupa ushindi katika kila eneo la maisha yako.

Tutakuwa Live🔴 pia kwenye ukurasa wetu wa YouTube wenye jina REALITY OF CHRIST CHURCH na kupitia ROC TV.

Karibu sana na tunakutakia siku njema ya mfungo.

Leo tulianza mfungo wetu kwa moyo wa shukrani mbele za Mungu, tukimshukuru kwa wema, ulinzi, neema na mafanikio aliyotup...
31/08/2026

Leo tulianza mfungo wetu kwa moyo wa shukrani mbele za Mungu, tukimshukuru kwa wema, ulinzi, neema na mafanikio aliyotupatia katika mwezi mzima wa August. Tuliendelea kuomba Mungu akamilishe kila kazi njema aliyoianza ndani yetu na kila jambo jema alilotuwezesha kulianza katika mwezi huu unaomalizika.

Pia tuliomba kwa nguvu zote ili kila kinachokwaza baraka, ahadi, mafanikio na upenyo wetu kiondoke kwa Jina la Yesu kabla ya kuingia mwezi mpya wa tisa. Tuliinua sauti zetu tukimwomba Mungu arejeshe kasi katika kila eneo ambalo tumekuwa tukicheleweshwa, ili yale aliyotuahidi yapate kutimia kwa wakati wake.

Kwa kuhitimisha, tuliomba neema ya kuvuka kutoka mwezi wa nane kwenda mwezi wa tisa tukiwa na ushindi wa Kiungu, tukiongozwa na mkono wa Mungu, tukitembea katika favor, ulinzi na mafanikio makubwa zaidi. Tunaamini kwamba Mungu ambaye ametuvusha miezi iliyopita atatuingiza katika mwezi mpya kwa ushindi, ushuhuda na utukufu wake.

Kesho tunaendelea na mfungo huu siku ya pili, andaa moyo wako vema na usisahau kufunga.

31/08/2026

DUNAMIS 2026🔥

Tanzania mpo tayari?
Nchi jirani je, are you reeeeeeady?

Kuanzia tarehe 28 Oktoba hadi 1 Novemba tunakutana sehemu moja tu, Reality Of Christ Church - Tegeta, Dar es Salaam kwa ajili ya siku tano zenye nguvu kubwa na udhihirisho mkubwa sana wa nguvu za Mungu!

Apostle Grace Lubega all the way from Uganda atakuwepo, na sio yeye pekee...kutakuwa na Watumishi wengi wa Mungu kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Panga ratiba yako mapema maana hii sio conference ya kukosa kabisa!

Address

Sinza Mori
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Reality of Christ Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Reality of Christ Church:

Shortcuts

Share