01/06/2026
Maombi huwa tofauti kati ya mtu mmoja na mwingine, na kinachotofautisha ni uzito wa maneno katika maombi, na uzito huu hutegemea mtazamo wako kwa Mungu katika kuwajibika katika hili unaloliona kwako ni tatizo.
Unapoenda mbele za Mungu lazima roho yako iwe sensitive. Uhalisia uliopo ndani ya moyo wako juu ya mtazamo wako kwa Mungu ndio unaokutengenezea uzito wa mtazamo wako kwa Mungu kuhusu kushughulika na case yako.
Mfumo ambao Mungu ameutengeneza kwenye moyo wako ni wewe kuwa na mahusiano mazuri na yeye.
Neno la Mungu linasema kuwa maandalio ya moyo ni ya mwanadamu, sio ya Mungu.
Kukabidhi mwezi maana yake ni kuuk**ata mwezi, unajiandaaje kuupokea na kuenenda kwenye huu mwezi mpya?
Chochote kilichoandikwa nyuma yake kuna roho, k**a kuna kitu kimeandikwa hata ujitahidi vipi, k**a hauna msaada wa Mungu huwezi kuona matokeo.
Ni kitu gani kimeandikwa kinyume na maisha yako kinyume na kufanikiwa? Maana mafanikio yanatakiwa kuonekanika na kushikika.
Ardhi inaweza kuandika habari kinyume na mtu, na popote atakapoenda as long as anakanyaga ardhi, hawezi kufanikiwa.
đź“– Yeremia 22:30
BWANA asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.
Leo haijalishi nini kiliandikwa kinyume na wewe katika ardhi, tumeomba rehema lakini pia kuyafuta hayo matamko kwa Damu ya Yesu!