Tanesco

Tanesco Ukurasa rasmi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)

NAIBU WAZIRI KWAGILWA ATEMBELEA BANDA LA TANESCO KWENYE MAONESHO KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI.📌Aipongeza TANESCO k...
02/06/2026

NAIBU WAZIRI KWAGILWA ATEMBELEA BANDA LA TANESCO KWENYE MAONESHO KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI.

📌Aipongeza TANESCO kuendelea kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kwa umeme.

📌Ahimiza TANESCO kuendelea kupanda miti kwa wingi kwenye vyanzo vya uzalishaji wa umeme

Na. Mariam Juma, Dodoma

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Kwagilwa Reuben leo Juni 01, 2026 ametembelea banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwenye Maonesho kuelekea Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika katika viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Center (JKCC) Jijini Dodoma.

Akizungumza katika banda hilo Mhe. Kagilwa ameipongeza TANESCO kwa jitihada kubwa wanazozifanya katika utunzaji wa Mazingira hasa katika kuendelea kuhamasisha wananchi kupika kwa kutumia Nishati Safi ya umeme hali ambayo inasaidia kupunguza uharibifu wa mazingira.

Aidha ametumia nafasi hiyo kuisisitiza TANESCO kuendelea kupanda miti kwa wingi kwenye vyanzo vya uzalishaji wa umeme ili kuendelea kutunza mazingira.

" Niwapongeze TANESCO kwa kuendelea kuhamasisha utunzaji wa mazingira hususani kupitia Nishati Safi ya kupikia kwa umeme, pia niwasisitize kuongeza juhudi za upandaji miti kwenye vyanzo vya uzalishaji wa umeme".

Awali akielezea ushiriki wa TANESCO katika maonesho hayo Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja Mkoa wa Dodoma James Vesso amesema lengo ni kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kwa umeme hali inayosaidia kuokoa muda na kutunza mazingira.

"Sisi k**a TANESCO tunaendelea kuhamasisha wananchi juu ya umuhimu wa kutumia Nishati Safi ya kupikia kwa umeme ili kutunza mazingira pamoja na kueleza mikakati ya Shirika juu ya utunzaji wa mazingira katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme"

TANESCO YATAMBULIWA K**A SEKTA WEZESHI NA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (UDSM)📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake...
27/05/2026

TANESCO YATAMBULIWA K**A SEKTA WEZESHI NA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi
📍Utambuzi watolewa katika hafla maalum ya kuwapongeza wadau wa maendeleo wa UDSM

Na Mwandishi Wetu

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetambuliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) k**a miongoni mwa sekta wezeshi zinazochangia maendeleo ya elimu jumuishi na ustawi wa wanafunzi chuoni hapo.

Utambuzi huo umetolewa Mei 26, 2026, wakati wa hafla maalum ya kuwatambua na kuwapongeza wadau wa maendeleo wa chuo hicho iliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mhe.Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, amesema mchango wa wadau mbalimbali wakiwemo TANESCO una mchango mkubwa katika kuboresha mazingira ya kujifunzia na maendeleo ya kitaaluma kwa wanafunzi.

“Tunapowasaidia wanafunzi hawa, hatuwafanyii fadhila. Tunathibitisha uwezo wao, utu wao na nafasi yao halali katika elimu ya juu,” amesema Dkt. Kikwete.

Aidha, ameshukuru wadau wote wa maendeleo kwa kuendelea kushirikiana na chuo hicho katika kuhakikisha upatikanaji wa elimu jumuishi kwa wanafunzi wote, wakiwemo wenye mahitaji maalum.

Kwa upande wa TANESCO, cheti hicho cha utambuzi na pongezi kilipokelewa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Irene Gowelle, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Lazaro Twange.

Utambuzi huo umetolewa ikiwa ni ishara ya kuthamini mchango wa TANESCO katika kuboresha mazingira ya kujifunzia na kujisomea kwa wanafunzi pamoja na wakufunzi wenye changamoto mbalimbali za ulemavu na mahitaji maalumu chuoni hapo.

27/05/2026
*TANESCO KINONDONI KUSINI YAKUTANA NA WATEJA WAKUBWA.*📌 Lengo ni kusikiliza maoni na kutatua changamoto zao kwa wakati.
26/05/2026

*TANESCO KINONDONI KUSINI YAKUTANA NA WATEJA WAKUBWA.*

📌 Lengo ni kusikiliza maoni na kutatua changamoto zao kwa wakati.

MKURUGENZI WA RASILIMALI WATU TANESCO AWAHAKIKISHIA USHIRIKIANO MAAFISA HUDUMA KWA WATEJA KUBORESHA UTENDAJI📌 Afunga Mku...
23/05/2026

MKURUGENZI WA RASILIMALI WATU TANESCO AWAHAKIKISHIA USHIRIKIANO MAAFISA HUDUMA KWA WATEJA KUBORESHA UTENDAJI

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao
📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye kujenga taswira chanya ya Serikali na Shirika kwa wananchi

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala TANESCO, Bi. Beatrice Kimoleta, amewahakikishia Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja ushirikiano katika kufanikisha upatikanaji wa nyenzo muhimu zitakazowawezesha kuhudumia wateja kwa ufanisi na ubora wa hali ya juu.

Ametoa kauli hiyo Mei 22, 2026 alipokuwa akifunga mkutano mkuu wa mwaka wa maafisa hao uliofanyika kwa siku tano kuanzia Mei 18, 2026 jijini Dodoma, mkutano ambao hufanyika kila mwaka kwa lengo la kufanya tathmini ya kuboresha utendaji kazi wa kurugenzi ili kufanikisha malengo yaliyowekwa.

“Kwa uongozi wa Shirika, kipaumbele chetu ni kuhakikisha watumishi wanaohudumia wateja moja kwa moja wanakuwa katika mazingira mazuri ya kazi ili waweze kutoa huduma kwa ufanisi. Tunawahakikishia kuwapatia nyenzo muhimu ili muendelee kutoa huduma bora kwa wateja,” ameeleza , Bi. Kimoleta .

Ameeleza kuwa, Uongozi wa Shirika unatambua kazi kubwa inayofanywa na Maafisa hao katika kulipa Shirika sifa njema na utendaji unaojenga imani ya Serikali na Shirika kwa wananchi kupitia utoaji wa huduma bora na yenye ufanisi kwa wateja.

“Nawapongeza kwa kazi kubwa mnayoifanya ya kuwahudumia wateja kwa kujituma. Mchango wenu unajenga taswira chanya ya Serikali na Shirika kwa wananchi. Endeleeni kudumisha uadilifu na weledi katika utendaji kazi wenu.” amebainisha.

MD TWANGE AELEZA KUTORIDHISHWA NA KASI YA MKANDARASI WA MRADI WA HALE📌Ni ule wa kuboresha kituocha kufua umeme📌Amuagiza ...
22/05/2026

MD TWANGE AELEZA KUTORIDHISHWA NA KASI YA MKANDARASI WA MRADI WA HALE

📌Ni ule wa kuboresha kituo
cha kufua umeme
📌Amuagiza kuongeza kasi ya
utekelezaji wa Mradi huo

SALOME: NGUZO ZA ZEGE NA CHUMA KUTUMIKA KUKABILI CHANGAMOTO YA KUANGUKA KWA NGUZO ZA UMEME ZA MITI.Naibu Waziri wa Nisha...
22/05/2026

SALOME: NGUZO ZA ZEGE NA CHUMA KUTUMIKA KUKABILI CHANGAMOTO YA KUANGUKA KWA NGUZO ZA UMEME ZA MITI.

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali kupitia TANESCO inaendelea kubadilisha nguzo chakavu kwa kuweka nguzo imara zaidi, zikiwemo nguzo za zege na chuma, pamoja na kuimarisha misingi ya nguzo katika maeneo yenye udongo laini ili kukabili changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme.

Salome ameeleza hayo leo, Mei 22, 2026, Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Sara Msafiri Ally, Mbunge wa Mvomero, aliyetaka kujua ni lini Serikali itatatua changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme katika Tarafa ya Mgeta.

Akijibu swali hilo, Salome amesema Serikali inatambua uwepo wa changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme katika baadhi ya maeneo ya Tarafa ya Mgeta kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo mvua nyingi, uwepo wa udongo usiohimilivu pamoja na uchakavu wa baadhi ya nguzo.

Amesema Serikali kupitia TANESCO inaendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa miundombinu ya umeme ili kubaini na kushughulikia changamoto hizo mapema pindi zinapojitokeza.

Aidha, Salome amefafanua kuwa Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga bajeti maalum ya kubadilisha nguzo za miti katika maeneo yote yenye unyevunyevu pamoja na maeneo yenye shughuli mbalimbali za kibinadamu.

Kadhalika, ametoa wito kwa wananchi kuacha matumizi mabaya ya ardhi, ikiwemo kuchoma moto ovyo mashambani, jambo ambalo limekuwa likiathiri miundombinu ya umeme kwa kuunguza nguzo za umeme.

MD TWANGE AELEZA KUTORIDHISHWA NA KASI YA MKANDARASI WA MRADI WA HALE📍Ni ule wa kuboresha kituo cha kufua umeme 📍Amuagiz...
22/05/2026

MD TWANGE AELEZA KUTORIDHISHWA NA KASI YA MKANDARASI WA MRADI WA HALE

📍Ni ule wa kuboresha kituo cha kufua umeme

📍Amuagiza kuongeza kasi ya utekelezaji wa Mradi huo

Na Mwandishi Wetu, Korogwe, Tanga

Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Bw. Lazaro Twange ameeleza kutoridhishwa na kasi ya mkandarasi anayetekeleza mradi wa maboresho ya Kituo cha Kufua Umeme cha Hale kutokana na kuchelewa kukamilika kwa Mradi huo ulioanza kutekelezwa tangu mwaka 2022.

Bw. Twange ameyasema hayo leo Aprili 22, 2026 wakati wa ziara yake ya ukaguzi katika mradi wa Hale pamoja na mradi wa usafishaji wa bwawa la Mto Pangani iliyopo katika Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga ambapo amemtaka mkandarasi wa Mradi wa Hale kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo ikiwa ni pamoja na kuongeza wafanyakazi pamoja na muda wa kufanya kazi ili ukamilike kwa wakati.

“Siridhishwi sana na mwenendo wake. Mkandarasi amewahi kuomba nyongeza ya muda mara mbili na nimepata taarifa kuwa yuko kwenye hatua za kuomba nyongeza nyingine ya tatu. Ndio maana nimekuja kuona kuna nini,” amesema Bw. Twange.

Amesema mradi huo una maeneo saba ya utekelezaji ambapo maeneo mawili tayari yamekamilika huku mengine yakiendelea na utekelezaji.

“Nimezungumza na msimamizi wa mradi, mhandisi mshauri pamoja na mkandarasi na nimewaelekeza wakae pamoja kuhakikisha ifikapo mwisho wa mwezi Julai mradi huu uwe umekamilika,” amesema Bw. Twange

Aidha, kuhusu mradi wa usafishaji wa bwawa la Pangani, Bw. Twange amesema matarajio ya TANESCO ni kuhakikisha kazi hiyo inakamilika ndani ya muda uliopangwa ili kuepusha changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa msimu wa mvua.

“Matarajio yetu ni kutoupitiliza mwaka mmoja ili tumalize kabla ya msimu unaokuja wa mvua,” ameongeza.

Katika hatua nyingine, Bw. Twange amesema TANESCO kwa sasa inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ya umeme nchini yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 13.4.

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Mradi wa Hale Mha. Kulwa Byemelo amesema maagizo yaliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji yatatekelezwa ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

TANESCO YAENDELEA KUWAELIMISHA WANAOFANYA SHUGHULI ZA KIUCHUMI KWENYE MIUNDOMBINU YA UMEME📌Ni katika muendelezo wa ukagu...
21/05/2026

TANESCO YAENDELEA KUWAELIMISHA WANAOFANYA SHUGHULI ZA KIUCHUMI KWENYE MIUNDOMBINU YA UMEME

📌Ni katika muendelezo wa ukaguzi wa miundombinu ya umeme Dar es salaam

📌Yatoa rai kwa wananchi kuondoka kwa ajili ya usalama wa maisha na mali zao

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea kuwasisitiza wananchi wanaofanya shughuli zao za kiuchumi katika miundombinu ya umeme kuondoka katika maeneo hayo kwa hiari, kwa kuwa wanahatarisha usalama wa maisha na mali zao.

Akizungumza katika muendelezo wa zoezi la kukagua miundombinu ya umeme Mei 18, katika eneo la Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam, Msimamizi Msaidizi wa Njia Kuu za Kusafirisha Umeme Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Nicholaus Kivelege, amesema TANESCO inafanya jitihada za makusudi kutoa elimu kuhusu athari za kuendelea kufanya shughuli za kiuchumi chini ya njia kubwa za kusafirisha umeme katika maeneo mbalimbali nchini.

Amesema licha ya jitihada hizo, bado baadhi ya wananchi wanaendelea kufanya shughuli hizo, hivyo amewaomba viongozi wa serikali za mitaa katika maeneo husika kuongeza nguvu ya kutoa elimu kuhusu madhara yanayoweza kujitokeza kwa wananchi wanapofanya shughuli zao katika miundombinu ya umeme.

“TANESCO tunaendelea na zoezi la ukaguzi wa miundombinu ya umeme katika maeneo ya Mbagala Zakhem, tunafanya jitihada kubwa kutoa elimu, lakini bado kuna ugumu kwa baadhi ya wananchi. Tunaomba viongozi wa serikali za mitaa watusaidie katika zoezi hili ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza,” alifafanua Bw. Kivelege.

Baadhi ya wananchi, akiwemo Bw. Zahali Maulidi wa maeneo ya Mbagala, licha ya kufahamu kuwa kufanya shughuli chini ya miundombinu ya umeme ni hatari, wameiomba Serikali kuangalia namna ya kuwatafutia maeneo mengine ya kufanyia kazi zao ili waweze kuondoka katika maeneo hatarishi.

MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME CHALINZE–DODOMA KUKAMILIKA AGOSTI 2026 : MD TWANGE📌Utekelezaji wa Mradi wafikia asili...
20/05/2026

MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME CHALINZE–DODOMA KUKAMILIKA AGOSTI 2026 : MD TWANGE

📌Utekelezaji wa Mradi wafikia asilimia 82.5

📌Shilingi bilioni 514 kutumika ajili utekelezaji wa mradi

📌 Amtaka Mkandarasi kuongeza kasi mradi huo wa kimkakati ukamilike kwa wakati

Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Zuzu, Dodoma, unatarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 18, 2026.

Akizungumza Mei 20, 2026 wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo katika mikoa ya Morogoro na Dodoma, Bw. Twange amesema mradi huo ni muhimu kwa kuwa unasafirisha umeme unaozalishwa moja kwa moja kutoka katika Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere ambao unapita Chalinze hadi Dodoma.

Amesema utekelezaji wa mradi huo unaenda sambamba na upanuzi wa vituo vya kupokea na kupoza umeme vya Chalinze na Zuzu, Dodoma, ambapo kukamilika kwake kutaimarisha hali ya upatikanaji wa umeme kwa ajili ya shughuli za uwekezaji pamoja na kuongeza fursa mbalimbali za kiuchumi nchini.

Amesema Serikali Chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetoa kiasi cha Shilingi Bil 514 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi huo ambao utachochea shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii kuendana na kasi ya ongezeko la mahitaji.

“Leo tumefanya ukaguzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Dodoma. Njia hii ni muhimu kwa kuwa inaongeza uwezo wa kusafirisha umeme kutoka Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere kwenda kwa watumiaji mbalimbali. Idadi ya watu imeongezeka na shughuli za kiuchumi zimeongezeka hivyo tumeingia makubaliano sasa mradi huu utakamilika Agosti 18, 2026,” alisisitiza Bw. Twange.

Ameeleza kuridhishwa na hatua iliyofikiwa huku akimtaka mkandarasi kuongeza kasi ya utekelezaji ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

Address

Jamatini Street
Dodoma Outlying
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanesco posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Tanesco:

Share