Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi

Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ni Taasisi Kuu ya Ukaguzi Tanzania.

Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ni taasisi Kuu ya Ukaguzi nchini Tanzania.Kila mwaka tunatoa ripoti za Ukaguzi ambazo tunaziwasilishwa kwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kabla ya Tarehe 31 Machi.

WAKAGUZI NAOT WASHIRIKI WARSHA YA KIKANDA YA AFRIKA MASHARIKI KUIMARISHA UBORA NA UKAGUZI Wakaguzi kutoka Ofisi ya Taifa...
01/09/2026

WAKAGUZI NAOT WASHIRIKI WARSHA YA KIKANDA YA AFRIKA MASHARIKI KUIMARISHA UBORA NA UKAGUZI

Wakaguzi kutoka Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) wanashiriki katika Warsha maalumu ya Kikanda ya Afrika Mashariki jijini Arusha, inayolenga kuimarisha Usimamizi wa Ubora na Ukaguzi wa Utendaji katika Taasisi Kuu za Ukaguzi (SAIs).

Akizungumza wakati wa kufungua warsha hiyo kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Mkurugenzi wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu, Bw. Novati Mfalamagoha, amesema kuwa ushirikiano wa Ukaguzi Kikanda ni nguzo muhimu katika kukabiliana na changamoto zinazofanana zinazozikabili Taasisi Kuu za Ukaguzi ndani ya Afrika Mashariki na kwamba fursa hii ni muhimu kwa Wakaguzi kubadilishana ujuzi na uzoefu ili kuzidi kujenga mifumo imara ya usimamizi wa ubora wa Ukaguzi.

Warsha hiyo inawakutanisha Wakaguzi kutoka Mataifa ya Tanzania, Kenya, Rwanda na Uganda, pamoja na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ya Sweden inalenga pamoja na masuala mengine kubadilishana uzoefu ili kuzidi kuzijengea uwezo Taasisi Kuu za Ukaguzi za Afrika Mashariki katika maeneo mbalimbali k**a vile kuimarisha mifumo ya Ukaguzi.

29/08/2026
Heri ya Sikukuu ya Maulid.
25/08/2026

Heri ya Sikukuu ya Maulid.

CAG NA OFISI YA UKAGUZI YA IRAN WAFANYA MAZUNGUMZO YA USHIRIKIANO WA KAZI ZA UKAGUZI WAKATI WA MKUTANO WA 19 WA MWAKA WA...
20/08/2026

CAG NA OFISI YA UKAGUZI YA IRAN WAFANYA MAZUNGUMZO YA USHIRIKIANO WA KAZI ZA UKAGUZI WAKATI WA MKUTANO WA 19 WA MWAKA WA INTOSAI WGFACML, ARUSHA

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Charles E. Kichere na Naibu Rais wa Taasisi Kuu ya Ukaguzi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (Supreme Audit Court of the Islamic Republic of Iran-SAC), Bw. Esmaeil Zarei Koosha, wamefanya mkutano maalumu jijini Arusha, wakati wa Mkutano wa 19 wa Mwaka wa Kikundi Kazi cha INTOSAI cha Kupambana na Rushwa na Utakatishaji Fedha (WGFACML) ambapo kwa pamoja wamejadili na kubadilishana uzoefu wa kazi za Ukaguzi.

Ujumbe wa NAOT uliongozwa na CAG, Bw. Charles E. Kichere, huku ujumbe wa Iran ukiongozwa na Naibu Rais wa SAC, Bw. Esmaeil Zarei Koosha na Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Tanzania, Mhe. Mohammad Javad HemmatPanah, pamoja na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Maafisa waandamizi wa SAC.

Katika mazungumzo hayo, pande zote mbili zilijadili namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya Taasisi hizo Kuu za Ukaguzi katika maeneo yenye maslahi ya pamoja yanayohusu ukaguzi wa sekta ya umma.

Akizungumza katika mkutano huo, CAG amesisitiza dhamira ya NAOT ya kujenga ushirikiano wenye tija na unaolenga matokeo na Taasisi Kuu za Ukaguzi kutoka mataifa mbalimbali. Amebainisha kuwa mkutano huo umeweka msingi wa uhusiano wenye matarajio makubwa ya ushirikiano kati ya NAOT na SAC.

CAG AWAKARIBISHA WASHIRIKI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA 19 WA WGFACML JIJINI, ARUSHAMdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za ...
19/08/2026

CAG AWAKARIBISHA WASHIRIKI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA 19 WA WGFACML JIJINI, ARUSHA

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Charles E. Kichere amewakaribisha washiriki wa mkutano unaofanyika jijini Arusha, Tanzania, kuanzia tarehe 18 hadi 20 Agosti 2026, unaolenga kuimarisha ushirikiano na kubadilishana uzoefu katika mapambano dhidi ya rushwa, utakatishaji fedha (money laundering) na masuala mengine yanayohusiana na uadilifu na uwajibikaji katika usimamizi wa rasilimali za umma.

Mkutano huo wa 19 wa Mwaka wa Kikundi Kazi cha INTOSAI cha Kupambana na Rushwa na Utakatishaji Fedha (WGFACML) unawakutanisha wawakilishi wa Taasisi Kuu za Ukaguzi (Supreme Audit Institutions), Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma Tanzania (PPRA) pamoja na Wadau mbalimbali wa Utawala Bora na mapambano dhidi ya Rushwa.

Miongoni mwa Viongozi na wageni wanaoshiriki ni pamoja na Mkuu wa Sekretarieti ya WGFACML, Bw. Ahmed Almongy ambae anamwakilisha Rais wa Taasisi Kuu ya Ukaguzi ya Misri (ASA) na Mwenyekiti wa WGFACML, Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Tanzania, Mhe. Mohammad Javad HemmatPanah, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bi. Neema Mwakalyelye pamoja na Mkurugenzi Mkuu PPRA, Bw. Dennis Simba.

Mkutano huo ambao unahudhuriwa na wawakilishi wa Taasisi Kuu za Ukaguzi kutoka nchi mbalimbali Duniani unajikita katika kujadili namna ya kutoa mapendekezo ya kiukaguzi yatakayoimarisha mifumo ya kuzuia na kupambana na rushwa na utakatishaji fedha, pamoja na kukuza uwazi, uwajibikaji na matumizi sahihi ya rasilimali za umma. PPRA_Tanzania TAKUKURU.TZ CAG

WAJUMBE WA AFROSAI-E WATEMBELEA UJENZI WA "NATIONAL AUDIT ACADEMY (NAA)"Wajumbe kutoka AFROSAI-E wametembelea mradi wa u...
16/08/2026

WAJUMBE WA AFROSAI-E WATEMBELEA UJENZI WA "NATIONAL AUDIT ACADEMY (NAA)"

Wajumbe kutoka AFROSAI-E wametembelea mradi wa ujenzi wa Kituo cha Mafunzo cha Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (National Audit Academy – NAA), kinachojengwa katika eneo la Msanga, Wilaya ya Chamwino, jijini Dodoma.

Katika ziara hiyo iliyofanyika tarehe 15 Agosti 2026, Wajumbe hao walipata fursa ya kujionea maendeleo na hatua mbalimbali zilizofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo na kupongeza juhudi za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Charles E. Kichere pamoja na Ofisi kwa ujumla za kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kwa kuzingatia viwango na ubora.

Timu hiyo ya Wataalamu kutoka AFROSAI-E pia imepata nafasi ya kutembelea Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) pamoja na Mji wa Serikali, Mtumba, na kujionea maendeleo mbalimbali yanayofanyika Makao Makuu ya nchi.

Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ni Mwanachama wa AFROSAI-E ambayo ni Taasisi ya Kikanda inayoratibu na kuimarisha uwezo wa Taasisi Kuu za Ukaguzi katika nchi za Afrika zinazozungumza Kiingereza.

Katika picha ni matukio mbalimbali ya ziara hiyo. AFROSAI-E

CAG Atembelea Maonesho ya Nanenane 2026 Dodoma.Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Charles E. Kich...
07/08/2026

CAG Atembelea Maonesho ya Nanenane 2026 Dodoma.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Charles E. Kichere, leo Ijumaa, Agosti 7, 2026, ametembelea Maonesho ya Wakulima ya Nanenane yanayoendelea mkoani Dodoma.

Katika ziara yake hiyo, CAG ametembelea mabanda mbalimbali ikiwemo Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Benki ya NMB na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), ambako amepata fursa ya kujionea shughuli za kilimo na ufugaji pamoja na teknolojia na ubunifu unaotumika kuongeza tija katika sekta ya kilimo, uvuvi na ufugaji.

Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nanenane 2026 yanalenga kuhamasisha ubunifu na matumizi ya mbinu endelevu za uzalishaji kwa kuwakutanisha wakulima, wafugaji, wavuvi, wadau wa biashara ya kilimo, watunga sera, washirika wa maendeleo na wadau wengine katika mnyororo mzima wa thamani wa sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.

Katika picha ni matukio mbalimbali kuhusiana na ziara hiyo ya CAG.

07/08/2026

Address

Dodoma

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 03:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi:

Shortcuts

Share