Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi

Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ni Taasisi Kuu ya Ukaguzi Tanzania.

Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ni taasisi Kuu ya Ukaguzi nchini Tanzania.Kila mwaka tunatoa ripoti za Ukaguzi ambazo tunaziwasilishwa kwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kabla ya Tarehe 31 Machi.

CAG Akagua Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi MwanzaMdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Char...
06/06/2026

CAG Akagua Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Mwanza

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles E. Kichere, amekagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) Mkoa wa Mwanza katika eneo la Mkolani. Katika ziara hiyo iliyofanyika tarehe 5 Juni 2026, CAG amepokea taarifa ya maendeleo ya mradi huo unaotekelezwa na Kampuni ya "MASASI Construction Company Limited"⁠ chini ya Mshauri Mwelekezi Kampuni ya BICO ya Chuo Kikuu Dar es Salaam⁠.

Akizungumza mara baada ya kukagua, CAG ameeleza kuridhishwa na maendeleo ya mradi huo ambao umefikia asilimia 70 ya utekelezaji na kuwapongeza wasimamizi na wataalam wote kwa usimamizi uliowezesha kazi kuendelea kwa mpango uliopo.

Mradi huo unahusisha ujenzi wa jengo la kisasa la Ofisi lenye ghorofa mbili pamoja na miundombinu muhimu ikiwemo ukumbi wa mikutano, maktaba, kantini, maegesho ya magari na mifumo ya huduma za maji.

Ujenzi wa jengo la NAOT Mwanza unatarajiwa kuboresha mazingira ya kazi, kuongeza ufanisi wa Ukaguzi na kuboresha huduma kwa Wadau wa NAOT Mkoa wa Mwanza.

CAG Afungua Kikao Kazi cha Tathmini ya Ukaguzi wa Mwaka wa Fedha 2024/25 kwa Divisheni ya Ukaguzi wa Serikali KuuMdhibit...
03/06/2026

CAG Afungua Kikao Kazi cha Tathmini ya Ukaguzi wa Mwaka wa Fedha 2024/25 kwa Divisheni ya Ukaguzi wa Serikali Kuu

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles E. Kichere, amefungua kikao kazi cha siku mbili cha Divisheni ya Ukaguzi wa Serikali Kuu, kinacholenga kutathmini kazi ya Ukaguzi wa Mwaka wa Fedha 2024/25 na pamoja na mipango ya maandalizi ya Ukaguzi wa Mwaka wa Fedha 2025/26.

Akizungumza wakati wa ufunguzi, CAG ameipongeza Divisheni ya Ukaguzi wa Serikali Kuu kwa mchango wake katika kuboresha usimamizi wa rasilimali za umma kupitia ukaguzi wa mwaka 2024/25. Pamoja na hilo, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha kazi za Ukaguzi lengo likiwa ni kuweka uwajibikaji katika matumizi sahihi na yenye tija ya rasilimali za umma.

Kwa upande mwingine CAG amewakumbusha Wakaguzi kuzingatia weledi, nidhamu, ushirikiano na maadili ya kazi wakati wote ili kuongeza ufanisi na ubora wa matokeo ya kazi za Ukaguzi.

Kikao hicho kinajumuisha mafunzo na mijadala kuhusu haki na wajibu wa Watumishi, mawasiliano, ushirikiano na usimamizi wa migogoro kazini, kwa lengo la kuimarisha utendaji wa Wakaguzi.

CAG amewahimiza washiriki kushiriki kikamilifu katika kikao hicho ili kuboresha uwezo wao wa Ukaguzi na kuhakikisha Ukaguzi wa Mwaka wa Fedha 2025/26 unafanyika kwa ubora, kwa wakati na kwa kuzingatia viwango vya miongozo ya Ukaguzi ya ndani na ya Kimataifa.

NAOT Yaandaa Kikao Kazi cha Wadau wa MaadiliOfisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) imeandaa Kikao Kazi cha siku mbili kilichoa...
03/06/2026

NAOT Yaandaa Kikao Kazi cha Wadau wa Maadili

Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) imeandaa Kikao Kazi cha siku mbili kilichoanza leo Juni 3–4, 2026 jijini Dodoma kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kubadilishana ujuzi na uzoefu kuhusu usimamizi wa maadili na utawala bora katika Utumishi wa Umma.

Kikao hicho kimefunguliwa na Naibu Mkaguzi Mkuu, Bw. Benja Majura, kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ambae amesema jukwaa hilo muhimu ndani ya Utumishi wa Umma linawakutanisha wawakilishi kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali na Mamlaka za Kitaaluma zinazosimamia maadili, ikiwemo Ofisi ya Rais, TAKUKURU, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, PPRA pamoja na Mabaraza na Bodi za Taaluma za Afya, Uhandisi, Usanifu, Mipango Miji, Ununuzi, Uhasibu na Taaluma nyingine.

Washiriki wanatarajiwa kujadili changamoto za usimamizi wa maadili, kubadilishana uzoefu na kuweka mikakati ya pamoja ya kuimarisha uadilifu, weledi na uwajibikaji kwa manufaa ya Taifa.
tz

27/05/2026
Bonanza la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Kanda ya Kaskazini Laimarisha Afya na Mshik**ano kwa Watumishi.Bonanza la Watumishi...
26/05/2026

Bonanza la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Kanda ya Kaskazini Laimarisha Afya na Mshik**ano kwa Watumishi.

Bonanza la Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Kanda ya Kaskazini lililowakutanisha washiriki kutoka Kilimanjaro, Tanga, Arusha na Manyara limefanyika mwishoni mwa wiki sambamba na mafunzo ya afya yaliyolenga kuimarisha ustawi, afya na mshik**ano wa Watumishi.

Bonanza hilo lilifunguliwa na Mkaguzi Mkuu wa Nje wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Wenzeslaus Nyalusi, huku washiriki wakipata fursa ya kushiriki kwenye michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, kuvuta kamba na mazoezi ya viungo.

Katika michezo mpira wa miguu, timu kombaini ya Arusha na Manyara iliibuka mshindi wa mpira wa miguu baada ya kuifunga timu ya Kilimanjaro na Tanga mabao 3-0. Kwa upande wa kuvuta kamba Wanawake, Kilimanjaro na Tanga waliibuka washindi huku Arusha na Manyara wakishinda upande wa Wanaume.

Mbali na michezo, Watumishi walipata mafunzo kuhusu afya ya akili, Ukimwi na magonjwa yasiyoambukiza k**a kisukari na shinikizo la damu. Wataalamu wa afya waliwahimiza Watumishi kuzingatia lishe bora, kufanya mazoezi mara kwa mara ili kulinda afya zao.

Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Yatajwa Miongoni mwa Washindani Watano wa Tuzo ya AFROSAI-E ya Ripoti Bora ya Ukaguzi wa Ufani...
20/05/2026

Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Yatajwa Miongoni mwa Washindani Watano wa Tuzo ya AFROSAI-E ya Ripoti Bora ya Ukaguzi wa Ufanisi kwa Mwaka 2025!

Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) imetambuliwa kuwa miongoni mwa Taasisi Kuu Tano Bora za Ukaguzi (SAIs) Barani Afrika miongoni mwa Taasisi za Ukanda wa AFROSAI-E ambazo zilipendekezwa kuwania Tuzo ya Heshima ya AFROSAI-E ya Ripoti Bora ya Ukaguzi wa Ufanisi kwa Mwaka 2025.

Hatua hiyo inaakisi jitihada za kuboresha kazi za Ukaguzi na Uongozi mahiri wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (CAG), Charles E. Kichere, unaolenga pamoja na masuala mengine kuimarisha ubora wa kazi za Ukaguzi pamoja na mchango endelevu wa Watumishi NAOT katika utoaji wa huduma za Ukaguzi.

Tuzo hizo zilihusisha Ripoti bora za Ukaguzi wa Ufanisi kutoka Tanzania, Ghana, Kenya, Mauritius na Uganda, zinazolenga kuonesha kuongezeka kwa ubora pamoja na mchango wa Ukaguzi katika maendeleo ya Afrika kwenye ukanda wa AFROSAI-E.

Katika tuzo hizo zilizotolewa wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Bodi ya AFROSAI-E uliofanyika jijini Monrovia, nchini Liberia leo Mei 20, 2026, na kuwasilishwa na Mkaguzi Mkuu wa Sweden, Christina Gellerbrant Hagberg, ambapo Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ya Kenya iliibuka mshindi kupitia ripoti yake ya Ukaguzi kuhusu Mradi wa "Kenya Urban Support Program Phase 1."

Katika mwaka 2025 pekee, Taasisi Kuu za Ukaguzi za Ukanda wa AFROSAI-E ziliandaa jumla ya Ripoti 171 za Ukaguzi wa Ufanisi zilizohusu masuala mbalimbali ikiwemo Miundombinu, Utawala Bora, Utoaji wa Huduma na Matumizi yenye Tija ya Rasilimali za Taifa.

AFROSAI-E ni Taasisi ya Kikanda inayojumuisha nchi 26 za Afrika iliyoanzishwa kwa lengo la kuimarisha uwezo wa Taasisi Kuu za Ukaguzi (SAIs) katika nchi za Afrika zinazotumia lugha ya Kiingereza.

Lengo la kuanzishwa kwa Taasisi hii ni pamoja na kujenga uwezo endelevu wa kukuza viwango vya Ukaguzi Kimataifa kwa Wanachama pamoja na kuimarisha uwajibikaji ili kuboresha Usimamizi wa Rasilimali za Umma Barani Afrika.

CAG AFUNGUA MAFUNZO YA KAMATI ZA BUNGE KUHUSU UFUATILIAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO.Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa He...
18/05/2026

CAG AFUNGUA MAFUNZO YA KAMATI ZA BUNGE KUHUSU UFUATILIAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles E. Kichere, amefungua rasmi mafunzo kwa Wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC), Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) pamoja na Bajeti, yenye lengo la kuongeza uelewa katika usomaji na uchambuzi wa Taarifa za Ukaguzi ili kuimarisha usimamizi wa matumizi ya Fedha za Umma.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika tarehe 16 Mei 2026 Mkoani Morogoro, CAG amesema kuwa Serikali inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo na hivyo ni jukumu la Kamati za Bunge kusimamia na kufuatilia matumizi ya rasilimali za umma ili kuhakikisha Wananchi wanapata thamani halisi ya fedha zinazotengwa kwa ajili ya maendeleo.

Aidha, CAG amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutekeleza wajibu wake wa Kikatiba wa kupokea na kuwasilisha Ripoti za CAG Bungeni kwa wakati.

Pia amempongeza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. M***a Azan Zungu (Mb) kwa Uongozi wake hususani katika kuhakikisha Taarifa za Ukaguzi zinajadiliwa kwa kina na maazimio yake kufanyiwa kazi.

Akihitimisha hotuba yake, CAG amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Bunge, Serikali na Ofisi ya CAG katika kuimarisha uwajibikaji, uwazi na kuhakikisha kila shilingi ya Umma inaleta matokeo yaliyokusudiwa kwa Wananchi.

Katika picha ni matukio mbalimbali ya mafunzo hayo.

Watumishi wa Divisheni ya Mashirika ya Umma NAOT Wakutana Kujadili Maboresho ya UkaguziNaibu Mkaguzi Mkuu, Bw. Salhina M...
13/05/2026

Watumishi wa Divisheni ya Mashirika ya Umma NAOT Wakutana Kujadili Maboresho ya Ukaguzi

Naibu Mkaguzi Mkuu, Bw. Salhina Mkumba, amefungua kwa niaba ya CAG Kikao Kazi cha Divisheni ya Mashirika ya Umma kinachoanza leo Jumatano, Mei 13, 2026 jijini Dodoma.

Kikao kazi hicho kinalenga pamoja na masuala mengine mbalimbali kujadili utekelezaji wa Ukaguzi wa Mashirika ya Umma kwa mwaka wa fedha uliopita sambamba na maboresho ya Ukaguzi ujao lengo kuu likiwa ni kuimarisha uwajibikaji, kuongeza ufanisi na kupanga utekelezaji wa maelekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali katika Ukaguzi wa Mashirika ya Umma ili kuboresha huduma za Ukaguzi kwa maslahi ya Taifa.

Baadhi ya Viongozi wa Taasisi walioshiriki kwenye ufunguzi wa Kikao Kazi hicho ni pamoja na Mkurugenzi wa Utawala na Menenjimenti ya Rasilimaliwatu, Bw. Novati Mfalamagoha, Kaimu Afisa Masuuli, Bw. Aziz Dachi na Mkurugenzi wa Huduma za Sheria, Bi. Elieshi Saidimu.

Katika picha ni matukio mbalimbali ya ufunguzi wa kikao kazi hicho.

CAG Ahimiza Wakaguzi Kuendelea Kujiongezea Ujuzi wa Taaluma ya UkaguziMdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CA...
13/05/2026

CAG Ahimiza Wakaguzi Kuendelea Kujiongezea Ujuzi wa Taaluma ya Ukaguzi

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Charles E. Kichere, amewataka Wakaguzi kuendelea kujijengea uelewa wa kina wa viwango vya taaluma ya ukaguzi, mifumo ya ukaguzi na masuala mbalimbali ya kitaaluma ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya ukaguzi.

CAG amesema uelewa huo utawasaidia Wakaguzi kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika kazi za ukaguzi, pamoja na kuimarisha utoaji wa huduma bora za ukaguzi zinazokidhi viwango vinavyotarajiwa.

Mafunzo ya awamu ya pili Endelevu ya Kitaaluma (CPD) kwa Wakaguzi yamefanyika mapema wiki hii kwa kuandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kupitia Kituo chake cha Mafunzo (NAA) kwa kushirikiana na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania na kuhusisha jumla ya watumishi 376 wa NAOT.

Awamu ya kwanza ya mafunzo hayo ilifanyika kwa njia ya mtandao na kuhudhuriwa na Wakaguzi 610. Mafunzo hayo yamefanyika katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na matumizi ya mifumo ya taarifa katika ukaguzi wa fedha, utawala bora na nafasi ya mkaguzi, ukaguzi wa manunuzi ya umma, maadili na mwenendo wa kitaaluma.

Katika picha ni matukio ya ufunguzi wa mafunzo hayo.

07/05/2026

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Charles E. Kichere, amefungua Mafunzo Elekezi maalumu kwa Wakaguzi Waajiriwa Wapya yanayofanyika katika Ofisi za Taasisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT), Dodoma.

Mafunzo hayo yanalenga pamoja na masuala mengine kuwajengea Wakaguzi hao wenye taaluma mbalimbali, uwezo, maadili ya kazi na weledi katika kutekeleza majukumu ya Ukaguzi ili kuwawezesha kusimamia uwajibikaji na matumizi sahihi ya rasilimali za umma.

UtumishiWaUmma

Address

Dodoma

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 03:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi:

Share