27/03/2026
Uwekezaji katika sekta ya kilimo.
Tunajitosheleza kwa chakula kwa asimilia 130.
Msikilize Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Prof. Joseph. C. Ndunguru, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu miradi ya maendeleo na fursa kwa vijana, Machi 24, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
//
Dondoo;
ya miaka mitatu, mamlaka imepata mafanikio makubwa kwa kuhakikisha Tanzania inakuwa na usalama na utoshelevu wa chakula kwa asilimia 130.
kipindi cha miaka mitatu iliyopita, TPHPA imefanikiwa kudhibiti uvamizi wa ndege waharibifu wa mazao aina ya kwelea kwelea wapatao milioni 231 katika halmashauri 23 zenye skimu kubwa za kilimo cha mpunga, uwele na mtama, na kuokoa jumla ya tani 1,600,000 za mazao hayo.
imepata mafanikio makubwa katika kudhibiti balaa la panya lililokuwa likiathiri uzalishaji wa mazao kwa wakulima katika mikoa 16, wilaya 68 na vijiji 1,669, na kuokoa tani 400,008 za mazao ya wakulima.
#*TPHPA katika kipindi cha miaka minne kuanzia mwaka 2021 hadi 2024 imewezesha usafirishaji wa jumla ya tani milioni 6.6 za mazao mbalimbali yakiwemo mbogamboga na nafaka, na mauzo yake kuiingizia nchi dola za Marekani bilioni 6.6 sawa na shilingi trilioni 15.6.*
imewezesha kufunguliwa kwa soko la zao la parachichi katika nchi za Afrika Kusini, India, China na Marekani.
Tumewezesha mazao 14 kupata masoko katika nchi 15, yakiwemo pilipili manga, nanasi, vanila, tumbaku, ndizi, makademia na ngano.
Tumeweza kusajili kampuni 16 za parachichi kusafirisha matunda kwenda nchini China, pamoja na kuwezesha kampuni nyingine 408 kufanya biashara katika soko hilo.
Mamlaka imenunua ndege nyuki (drones) za kisasa kwa ajili ya kuchunguza mashamba ya kilimo na kubaini mapema uwepo wa visumbufu vya mazao ili kuvidhibiti kabla havijasababisha madhara makubwa.
Mamlaka imenunua ndege ya kisasa kwa ajili ya kunyunyizia viuatilifu yenye uwezo wa kunyunyizia katika eneo la ekari 2,400 kwa wakati mmoja.