04/09/2026
Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kwa kushirikiana na Idara ya Kazi iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano zimepanga kuimarisha ushirikiano katika utoaji wa elimu kwa wadau kuhusiana na masuala ya fidia kwa wafanyakazi.
Maeneo hayo ni pamoja na kujengeana uwezo na uelewa juu ya haki, wajibu na taratibu za madai ya fidia kwa wafanyakazi kwa lengo la kuhakikisha haki stahiki inapatikana kwa wakati kwa wafanyakazi wanaoumia au kupata ugonjwa unaotokana na kazi zao.
Hayo yamejiri jijini Dodoma leo wakati wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa majukumu ya Idara ya Kazi kwa mwaka 2025/26 kilichowakutanisha maafisa kazi wafawidhi kutoka mikoa yote nchini.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi hicho, Kamishna wa Kazi Bi. Susan Mkangwa aliwakumbusha maafisa kazi juu ya wajibu wao katika kuimarisha usimamizi wa sheria ya kazi nchini, kufanya kaguzi zenye tija na kutoa elimu kwa waajiri na wafanyakazi ili kuimarisha ustawi wa nguvu kazi kazi ya Taifa.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma, pamoja na kuwapongeza maafisa kazi kwa namna wanavyoshirikiana na WCF katika kutoa elimu kwa wadau kuhusu masuala ya fidia kwa wafanyakazi, aliwataka pia kuongeza mkazo katika elimu ya haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi katika kuhakikisha sheria ya fidia kwa wafanyakazi inazingatiwa.
Ofisi ya Waziri Mkuu Hon Deus Sangu Dr. Evaline Wilbard Munisi Zuhura Yunus Maelezo News Msemaji Mkuu wa Serikali