07/05/2026
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete, akimkabidhi tuzo Mkuu wa Kitengo cha Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Festo Kandonga, kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo kwa kutambua mchango wao katika kufanikisha Mkutano wa Pili wa Mwaka wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma (AAPAM). Tukio hilo limefanyika tarehe 6 Mei jijini Arusha wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo.
.evalinemunisi