14/05/2026
KIHONGOSI: โUMUHIMU WA AMANI UWE NI AJENDA NA KIPAUMBELE CHETU.โ
MUSOMA: Katibu wa NEC, Itikadi Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Kenani Kihongosi amesema madhara ya kupoteza amani ni makubwa kuliko kuilinda amani yenyewe, hivyo amewaasa wananchi kuutambua umuhimu wa amani na kwamba iwe ni ajenda na kipaumbele chao.
Kenani ameeleza hayo leo Mei 14,2026 alipotembelea na kushiriki kikao cha Shina namba Tano Tawi la Veta Kata ya Mwisengwe Veta Musoma Mjini mkoani Mara ikiwa ni mwanzo wa ziara yake ya kikazi katika mkoa huo.
Akizungumza baada ya kusikiliza taarifa fupi ya shina hilo, Kihongosi amesema wamekusanyika na kuhudhuria katika kikao hicho kutokana na amani na utulivu uliopo katika Wilaya ya Musoma na mkoa mzima wa Mara kwa ujumla.
โAmani ndiyo msingi wa maendeleo, amani ndiyo inayoleta kila kitu ndani ya Mkoa wenu wa Mara niwaombe mlinde amani, ikitoweka hakuna atakayelima..watoto hawa hawataenda shule, biashara hamtafungua, umuhimu wa amani iwe ni ajenda na kipaumbele chetu watu wa Musoma,โ amesisitiza Kihongosi.
AmeongezaโMadhara ya kupoteza amani ni makubwa kuliko kulinda amani yenyewe na hapa ni waibie siri ndogo Wazee wetu, waasisi wa nchi hii, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Aman Karume wangekuwa wabinafsi, tusingekuta Jamhuri hii ya Muungano wa Tanzania k**a viongozi wetu wasingelinda amani na utulivu wa taifa hili.โ
Kihongosi aliwataka wananchi wawakatae baadhi ya watu ambao kwa makusudi, kwa tabia mbaya, kwa ajenda zao na kujiangalia wao,wapo tayari nchi iharibike ili wao wafanye mambo yasiyofaa ndani ya taifa hili,
Alisisitiza Mungu amewapa ardhi hivyo hawana nchi nyingine hapa Musoma ndiyo kwao pakiharibika hawana pakukimbilia, hata wakienda nchi jirani atakuwa mkimbizi si kwao, hivyo aliwataka wazazi kuwaelimisha watoto wao na kila kijana aipende nchi yake .
Awali, Katibu wa Shina Namba Tano, Emiliana Kuboja alisoma ajenda ya kikao hicho akieleza kuwa lina wanachama 50 wanaume wakiwa 21 na wanawake 29 na waliolipa ada hadi sasa ni wanachama 35 lakini wameendelea kufanya vikao vya chama pamoja kwa lengo la kuimarisha shughuli za CCM eneo hilo.