02/06/2026
PONGEZI KWA UTEUZI WA NDG. UMMY MWALIMU KUWA MSHAURI WA RAIS MASUALA YA AFYA YA UZAZI, MAMA NA MTOTO
Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT) ikiongozwa na Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) unampongeza Ndg. Ummy Mwalimu kufuatia kuaminiwa na kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa Mshauri wa Rais katika masuala ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto.
Uteuzi huu ni uthibitisho wa uzoefu wake mkubwa, weledi, uzalendo na mchango wake uliotukuka katika sekta ya afya nchini. Katika nyadhifa mbalimbali alizowahi kuzitumikia, ameonesha uwezo wa kipekee katika kusimamia na kuimarisha huduma za afya, hususani zinazohusu afya ya uzazi, mama na mtoto.
Tunaamini kuwa kupitia nafasi hii mpya, ataendelea kutoa ushauri wenye tija utakaosaidia kuimarisha sera, mipango na huduma za afya kwa manufaa ya wananchi, hususani wanawake, watoto na familia kwa ujumla.
Hongera sana Ndg. Ummy Mwalimu kwa uteuzi huu muhimu na wa heshima. Mungu akubariki na akuongoze katika utumishi wako.