National Health Insurance Fund

National Health Insurance Fund The Management of the Fund is vested in the Board of Directors.

The Official Account of the National Health Insurance Fund (NHIF) of Tanzania I Ukurasa Rasmi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya 🇹🇿

Customer Service Toll Free - 199
Fraud Reporting Toll Free - 0800111163

www.nhif.or.tz The National Health Insurance Fund is a statutory health insurance scheme which was established by Parliamentary Act No.8 of 1999,in order to facilitate access to health services b

y the principal members and their dependants. The main objective for the establishment of the Fund was to administer the scheme and to formulate and promulgate policies for sound administration of the scheme. However, the day to day operations of the Fund are executed by the Director General on behalf of the Board of Directors. Generally, employers and employees in the public sector are obliged by the Law to register themselves and contribute to the Fund a total of six percent of employee’s salary,equally shared between the employer and the employee, except uniformed service men1 whose contribution is 6.25% and where paid by Government.The Fund covers members,their spouses and up to four children and/or dependants. The Membership size of the Fund has increased from 332,650 in June 2009 to 373,326 by June 2010, an increase equivalent to 12.2%.The beneficiaries have been increasing gradually from 1,830,375 in June 2009 to 1,971,251 as of 30th June 2010, equivalent to an increase of 7.7%. Extension of membership coverage has been made possible through the amendments of the NHIF Act,which extended the coverage to include all public servants2 instead of the previous Central Government employees . The following groups were taken on board namely public servants, councilors, and members of the Police force, Prisons, Immigrations, Fire and Rescue as well as other groups of persons. As the scope of membership and beneficiaries increases, the Scheme is expected to ultimately assume its national role as the major universal social health insurance provider. The Fund’s benefits package comprising of Registration and Consultation Fees, Outpatient Services, Medicines, Diagnostic Tests, Inpatient Services, Surgical Services, Physiotherapy and Optical Services. An important inclusion and enhancement in the package was the introduction of the Retirees benefits for the rest of their lives, a great stride in the Scheme’s milestones.The services are provided to beneficiaries through the Fund’s accredited health facilities which include Government, Faith Based and Private facilities that are located throughout the country. During the first two years of operations, the scheme encountered various challenges which hindered its smooth operation.In order to tackle the challenges,the focus was mainly on awareness creation to key stakeholders to ensure that they understand the Scheme and packages offered by NHIF. Now than ever before, stakeholders have started to understand the concept of social health insurance which has lead to increased applications of the excluded groups requesting to join the Fund.This is reflected by the increase of the membership base from 164,708 in 2001/02 to 373,326 observed by June 2010, accounting to an average annual growth rate of 14.1%.

USHIRIKIANO WA KIMKAKATI NHIF/TSN KWENYE UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTEDodoma   06/05/2026Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko...
06/05/2026

USHIRIKIANO WA KIMKAKATI NHIF/TSN KWENYE UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

Dodoma 06/05/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Dkt. Irene Isaka amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Magazeti la Serikali (TSN) Bi. Asha Dachi jijini Dodoma ambapo masuala mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano yalizungumzwa.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa TSN Bi. Dachi, alianza kwa kutoa shukrani kwa Mkurugenzi Mkuu wa NHIF kwa ushirikiano uliopo kati ya taasisi hizi mbili, aliendekea kusema kuwa anatambua kuwa NHIF imebeba agenda kubwa ya kitaifa, agenda ya Bima ya Afya kwa Wote, suala hili ni kubwa hivyo kuhitaji jitihada za pamoja ili kufanikiwa kuwafikia watanzania wote. Aidha Bi. Dachi alimhakikishia Mkurugenzi Mkuu wa NHIF kuwa TSN iko tayari kuibeba agenda hiyo kupitia majukwaa mbalimbali waliyonayo ikiwemo magazeti na mitandao ya kijamii (digital platforms). Kuna maboresho makubwa yamefanyika TSN ambapo kwa sasa magazeti yanasomwa kupitia mtandao (online) sio lazima kusoma nakala ngumu, alisema Bi. Dachi, pia habari zote zinapatikana katika mitandai ya kijamii ya TSN jambo linalofanikisha kufikia watu wengi kwa wakati sahihi.

Bi. Dachi aliendelea kusema kuwa TSN ingetamani kuwepo na mashirikiano ta kimkakati na NHIF katika kujenga uelewa wa Bima ta Afya kwa Wote (UHI) na hatimaye ndoto kubwa ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kutimia.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt. Isaka alikaribisha kwa mikono miwili mawazo yaliyotolewa na Mtendaji Mkuu wa TSN, na kuekezea kuwa mawazo hayo yamekuja wakati sahihi ambapo Mfuko unafanya jitihada khbwa nchi nzima kutoa elimu na kusajili wanachama chini ya Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote. Ujio wenu utasaidia sana kujenga uelewa na hivyo kurahisisha zoezi la usajili wa wanachama, alisema Dkt. Isaka.

Wakihitimisha mazungumzo, watendaji Wakuu wa taasisi hizo, walikubaliana kuingia makubaliano rasmi yenye kuonesha maeneo mbalimbali ya ushirikiano kati ya taasisi hizi kwa lengo la kufikia malengo ya kitaasisi na hatimaye kufanikisha agenda ya kitaifa ya Bima ya Afya kwa Wote.


Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa!
01/05/2026

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa!


WANANCHI WANUFAIKA NA HUDUMA ZA NHIF KATIKA MAONESHO YA OSHA NJOMBEWananchi wameendelea kupata huduma mbalimbali za Mfuk...
30/04/2026

WANANCHI WANUFAIKA NA HUDUMA ZA NHIF KATIKA MAONESHO YA OSHA NJOMBE

Wananchi wameendelea kupata huduma mbalimbali za Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika banda la NHIF lililopo kwenye maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema, mkoani Njombe.

Kupitia banda hilo, wananchi wamepata huduma muhimu za uanachama ikiwemo kujisajili kujiunga na NHIF, kuhuisha taarifa zao, kuongeza wategemezi pamoja na kupatiwa elimu kuhusu vifurushi mbalimbali vya bima ya afya vinavyotolewa na Mfuko. Huduma hizo zimetolewa kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa bima ya afya na kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu umuhimu wa kuwa na kinga ya matibabu.

Maafisa wa NHIF kutoka Ofisi ya Mkoa wa Njombe wamekuwepo kutoa huduma hizo kwa ufanisi, wakisaidiana na wanamichezo wa NHIF walioungana nao katika kuwahudumia wananchi pamoja na kutoa elimu ya afya. Ushirikiano huo umeongeza hamasa na kuvutia wananchi wengi zaidi kufika katika banda hilo.

Wananchi waliotembelea banda hilo wamepongeza juhudi za NHIF kwa kusogeza huduma karibu nao, huku wakieleza kuwa elimu waliyoipata imewasaidia kuelewa zaidi faida za bima ya afya katika kukabiliana na gharama za matibabu.

Ushiriki wa NHIF katika maonesho ya OSHA unaendelea kuwa muhimu kwa lengo la kufikisha huduma na elimu kwa jamii, sambamba na kuhamasisha umuhimu wa afya na usalama katika maisha ya kila siku.

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa!



NHIF YAFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA ROBO YA TATU YA MWAKA WA FEDHA 2025/26Dodoma 29/04/2026Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa ...
29/04/2026

NHIF YAFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA ROBO YA TATU YA MWAKA WA FEDHA 2025/26

Dodoma 29/04/2026

Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), chini ya Mwenyekiti wake Bw. Eliud Sanga, imekutana jijini Dodoma kwa lengo la kupokea taarifa ya maendeleo ya Mfuko kwa kipindi cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2025/26.

Kikao hicho kimefanyika tarehe 29 Aprili, 2026 kikitanguliwa na vikao vya kamati za Bodi vilivyofanyika tarehe 27 - 28 April, 2026. Kamati hizo ni Kamati ya Fedha na Uendeshaji (Finance & Operations Committee) chini ya Mwenyekiti Prof. George Ruhago, Kamati ya Ukaguzi na Hadhari ya Vihatarishi (Audit & Risk Commitee) chini ya Mwenyekiti CPA. Veronica Kishala na Kamati ya Usimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala Bora ( Human Resources and Governance Committee) chini ya Kaimu Mwenyekiti Wakili. Shaaban Kabunga.

Wajumbe wengine wa Bodi waliohudhuria kikao hicho ni Prof. Ramaiya Kaushik na Bi. Zubeda Chande.

Wenyeviti wa Kamati mara baada ya kuwasilisha taarifa zao mbele ya Bodi, Mwenyekiti wa Bodi pamoja na Wajumbe wengine kwa pamoja waliipongeza Menejimenti ya Mfuko kwa mafanikio yaliyopatikana kwa kipindi cha robo ya tatu.

Bodi ilipongeza mafanikio ya usajili wa wanachama yaliyofikia asilimia 58, aidha kuendelea kupungua kwa siku za ulipaji madai kwa watoa huduma (aging), kadhalika Bodi ilipongeza ( investment performance, vilevile Bodi iliendelea kupongeza matokeo mazuri kwenye ukuaji wa rasilimali za Mfuko pamoja na ziada (surplus) inayoendelea kukua zaidi.

Vilevile walipongeza mazoezi kwa watumishi na ushiriki wao kwenye michezo ya Mei Mosi pamoja na marathon ambazo zaidi ya watumishi 168 wamekuwa wakishiriki

Pamoja na pongezi hizo Bodi ilitoa maelekezo kadhaa ili kuboresha za kulinda mafanikio yaliyopatikana;

i. Mfuko uendelee kufanya uwekezaji makini ili kuongeza ukwasi kwa ajili ya kujenga uwezo zaidi wa kifedha na kutengeneza ziada kubwa zaidi;

ii. Kuendelea kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima na kupambana zaidi na vitendo vya udanganyifu,

iii. Bodi ilielekeza kuendelea kutoa elimu kwa watoa huduma kuhusu fursa ya mikopo ya NHIF ili wafunge vifaa vya utambuzi wa wanachama kupitia alama za vidole (biometric verification).

iv. NHIF tuendelee kuwa mfano wa kuigwa katika jitihada za kupambana na magongwa nyemelezi (NCDs) ili jamii na hatimaye kuepukana na gharama kubwa za kutibia magonjwa hayo;

v. Kuendelea kutekeleza ESG kwa kupanda miti na kupunguza matumizi ya karatasi

vi. Mfuko uendelee na hatua mbalimbali za kutatua changamoto za watumishi kupitia njia mbalimbali ikiwemo HR Clinics.

vii. kwa upande mwingine Bodi ilielekeza watumishi nao kutimiza wajibu wao pamoja na kufuata Sheria, miongozo na taratibu katika kutekeleza majukumu yao;

viii. Menejimenti iendelee kufanyia kazi hoja wa wakaguzi wa ndani na ukaguzi wa nje. Vilevile kutekeleza kwa wakati mapendekezo ya Wadhibiti pamoja na Actuarial recommendations.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko Dkt. Irene Isaka aliishukuru Bodi kwa kuendesha kikao vizuri pamoja na miongozo mbalimbali inayotolewa na Bodi, kwani miongozo hiyo imekuwa chachu kubwa ya kuteleleza majukumu ya Mfuko kwa mafanikio. Aidha aliihakikishia Bodi kuwa Menejimenti inafanyia kazi maelekezo yote ya Bodi ili kuboresha zaidi ustawi wa Mfuko.

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa

29/04/2026

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa!




28/04/2026

NHIF NA JIBU LA SWALI LAKO
Swali: Je nawazaje kujisajili na Vifurushi vya NHIF kupitia mfumo wa Self-Service?

Bima ya Afya kwa Wote, jiunge Sasa!



Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa !
28/04/2026

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa !


Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa!
27/04/2026

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa!


NHIF Yatwaa Ubingwa wa Netiboli Mashindano ya OSHA NjombeTimu ya wanawake ya mpira wa pete (netiboli) ya Mfuko wa Taifa ...
27/04/2026

NHIF Yatwaa Ubingwa wa Netiboli Mashindano ya OSHA Njombe

Timu ya wanawake ya mpira wa pete (netiboli) ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) imefanikiwa kutwaa kombe la mshindi wa kwanza katika mashindano ya OSHA yaliyofanyika mkoani Njombe, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya OSHA. Ushindi huo umeonyesha kiwango cha juu cha ushindani dhidi ya timu zilizoshiriki mashindano hayo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi kwa washindi, Kamishna wa Kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Suzan Mkangwa, alisema kuwa bonanza hilo lina faida kubwa kwa watumishi, ikiwemo kuongeza ufanisi kazini, kuleta wafanyakazi pamoja na kuimarisha mshikamano. Alibainisha kuwa michezo huchochea motisha kazini, huboresha mawasiliano, na kuwajengea watumishi uwezo wa kusikilizana pamoja na kushirikiana katika kutatua changamoto mbalimbali kwa ubunifu.

Aidha, aliongeza kuwa taasisi zinazothamini michezo huwa na wafanyakazi wenye ari na morali ya juu ya kazi, hali inayochangia kuongeza tija katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila sikuna pia kuendeleza mapambano dhidi ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza (NCD’s).

Naye kwa upande wake Nahodha wa timu hiyo, Bi. Jacqueline Sikozi akizungumza kwa niaba ya wachezaji wote wa timu ya netiboli alitoa shukurani kwa Mkurugenzi Mkuu wa NHIF Dkt. Irene Isaka kwa kuwezesha ushiriki wa watumishi katika michezo ya Mei Mosi ambayo imekuwa ni sehemu ya kujiimarisha kiafya na kiakili.

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa!

TANZIA.
26/04/2026

TANZIA.

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa !
26/04/2026

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa !


NHIF YAIBOMOA UJENZI 2 KWA 0Timu ya mpira wa miguu ya NHIF imeshinda magoli 2 kwa 0 dhidi ya timu ya Ujenzi katika mechi...
24/04/2026

NHIF YAIBOMOA UJENZI 2 KWA 0

Timu ya mpira wa miguu ya NHIF imeshinda magoli 2 kwa 0 dhidi ya timu ya Ujenzi katika mechi iliyoendelea leo Aprili 24, 2026 huko Mkoani Njombe katika mwendelezo wa kuhamasisha utunzaji wa afya kwa watumishi na wanamichezo kwa ujumla kuelekea sikukuu ya MeiMosi 2026.

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa


Address

NATIONAL HEALTH INSURANCE FUND
Dodoma
P.OBOX1437

Opening Hours

Monday 07:30 - 16:00
Tuesday 07:30 - 16:00
Wednesday 07:30 - 16:00
Thursday 07:30 - 16:00
Friday 07:30 - 16:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when National Health Insurance Fund posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to National Health Insurance Fund:

Share