Ofisi ya Waziri Mkuu

Ofisi ya Waziri Mkuu Huu ni ukurasa rasmi wa Facebook wa Ofisi ya Waziri Mkuu. Tufuatilie ili kupata habari za uhakika, vipaumbele vya Serikali, na maendeleo ya taifa.

Tunatoa taarifa sahihi, matukio, na shughuli za Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na taarifa rasmi za Serikali.

05/09/2026

MKURUGENZI BAHI AMKABIDHI BI. MASEKA MILIONI 2.6 KUFUATIA MAAGIZO YA WAZIRI MKUU

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Bi. Albina William Mtumbuka, leo amemkabidhi Bi. Agnetha Maseka kiasi cha Shilingi milioni 2.6

Fedha hizo ni malipo ya madai ya huduma ya chakula pamoja na usafirishaji wa mizigo. Malipo hayo yanakuja baada ya Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, kutoa agizo la kulipwa papo hapo.

DKT. MWIGULU: KILA KIJIJI KUWA NA SEKONDARIWAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema Serikali imejipanga kufanya mageuz...
05/09/2026

DKT. MWIGULU: KILA KIJIJI KUWA NA SEKONDARI

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema Serikali imejipanga kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya elimu, ikiwemo kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na shule ya sekondari, na zaidi ya vyumba 16,000 vya madarasa vikitarajiwa kujengwa ili kukidhi ongezeko la wanafunzi.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo, Jumamosi, Septemba 05, 2026, wakati akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Bahi, mkoani Dodoma, katika Viwanja vya Halmashauri ya Bahi, alipokuwa katika ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuwasikiliza wananchi na kushughulikia changamoto zinazowakabili.

Amesema uamuzi wa kuongeza muda wa elimu ya lazima hadi kidato cha nne unaleta mahitaji makubwa ya miundombinu ya elimu, yakiwemo madarasa, maabara na maktaba.

“Tunaposema elimu ya lazima itakuwa mpaka kidato cha nne, maana yake tunasema kila kijiji kiwe na sekondari. Tunaongelea mahitaji ya madarasa zaidi ya vyumba 16,000.”

Waziri Mkuu amesema Serikali haitaki kuona watoto wakirejea katika mazingira ya kusoma chini ya miti, kukosa madarasa au kusoma katika mazingira ya msongamano, akisisitiza kuwa maandalizi ya mapema ni muhimu kukabiliana na mahitaji hayo.

Amesema Serikali pia inahitaji kuongeza idadi ya maabara, akieleza kuwa mahitaji yanaweza kufikia takribani maabara 8,000, pamoja na maktaba, ili kuimarisha mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

Aidha, Dkt. Mwigulu amewataka viongozi wa Serikali kubadili baadhi ya taratibu zinazoweza kuokoa fedha na kuelekeza rasilimali hizo kwenye huduma zinazogusa maisha ya wananchi moja kwa moja.

05/09/2026

Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewekeza sana kwenye miundombinu na sisi watendaji wa Serikali tunapaswa kubadili tabia. Kwenye utendaji huku, tuna mambo na sisi lazima tuyafanye na viongozi tuwe wakali wala tusifanye mzaha-Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba.

📍Bahi-Dodoma
🗓️Septemba 5, 2026

————————

Dkt. Mwigulu ametoa agiza hilo wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara Bahi, mkoani Dodoma

05/09/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba aagiza kupandishwa cheo Afisa Elimu Wilaya ya Bahi.

📍Bahi-Dodoma
🗓️Septemba 5, 2026

————————

Dkt. Mwigulu ametoa agiza hilo wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Bahi, mkoani Dodoma

DKT. MWIGULU AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA JENGO LA OFISI ZA HALMASHAURI YA BAHIWaziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo ...
05/09/2026

DKT. MWIGULU AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA JENGO LA OFISI ZA HALMASHAURI YA BAHI

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Jumamosi, Septemba 5, 2026, amekagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Bahi na kuweka jiwe la msingi la mradi huo, unaolenga kuboresha mazingira ya utendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Akiwasilisha taarifa ya mradi huo, Kaimu Mhandisi wa Wilaya ya Bahi, Sassoche Mtenya Maduhu, amesema jengo hilo linatarajiwa kugharimu jumla ya Sh bilioni 4.868 na litajengwa kwa awamu.

Amesema hadi kufikia Agosti 30, 2025, Halmashauri ya Wilaya ya Bahi ilikuwa imepokea jumla ya Sh bilioni 1 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo hilo, ambapo Sh milioni 994.546 zimetumika.

Katika fedha hizo, Sh milioni 980.247 zimetumika kumlipa mkandarasi M/s Hamble Ulpan Engineering Company Limited, huku Sh milioni 14.3 zikitumika kwa ununuzi wa vyuma vilivyoagizwa kutoka Kiwanda cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi umefikia asilimia 100, ukiwa umehusisha maandalizi ya eneo la ujenzi, uchimbaji na ujenzi wa msingi, ujenzi wa nguzo na ring beam, ujenzi wa kuta pamoja na uwekaji wa mifumo ya awali ya maji, umeme na TEHAMA.

Mradi huo pia umechangia ajira 152 kwa wananchi, wakiwemo wanawake 89 na wanaume 63, huku kukamilika kwake kukitarajiwa kuimarisha mazingira ya kazi na kuongeza ufanisi wa watumishi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mbunge wa Bahi, Mhe. Kenneth Nollo, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo, akisema litakapokamilika litakuwa jengo la kisasa litakaloboresha mazingira ya kazi na utoaji wa huduma katika Halmashauri hiyo.

05/09/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba Leo September 05,2026 anaweka jiwe la msingi jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Bahi pamoja na kuzungumza na wananchi

📍Ni Bahi-Dodoma
05/09/2026

📍Ni Bahi-Dodoma

DKT. MWIGULU: IFIKAPO 2030 MWANZA–DODOMA KWA SGR▪︎ Aagiza Wizara ya Fedha na Uchukuzi kuharakisha utekelezaji▪︎ Aelekeza...
04/09/2026

DKT. MWIGULU: IFIKAPO 2030 MWANZA–DODOMA KWA SGR

▪︎ Aagiza Wizara ya Fedha na Uchukuzi kuharakisha utekelezaji
▪︎ Aelekeza leseni za madini zisizoendelezwa kufutwa
▪︎ Asisitiza kupunguzwa kwa matumizi yasiyo ya lazima

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameiagiza Wizara ya Fedha na Wizara ya Uchukuzi, kwa kushirikiana na Shirika la Reli Tanzania (TRC), wakandarasi na taasisi zinazohusika na uhamasishaji wa fedha, kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya Reli ya Kisasa (SGR), akilenga kuona ifikapo mwaka 2030 wajumbe kutoka Mwanza na mikoa ya Kanda ya Ziwa wakisafiri kwa treni kutoka Mwanza hadi Dodoma.

Ametoa agizo hilo leo (Ijumaa, Septemba 04, 2026) wakati akitoa hoja ya kuahirisha Bunge la 13, Mkutano wa Nne, jijini Dodoma.

“Naziagiza Wizara ya Fedha na Wizara ya Uchukuzi, zikishirikiana na Shirika la Reli, wakandarasi waliopewa kazi ya kujenga vipande hivi pamoja na wale waliopewa jukumu la kuhamasisha fedha za miradi hiyo, kupambana usiku na mchana,” amesema.

Amesema Serikali inalenga kuhakikisha vipande vya Mwanza–Isaka, Isaka–Tabora, Tabora–Kigoma na Makutupora–Dodoma vinaendelea kutekelezwa kwa kasi.

“Ikiwezekana, ifikapo mwaka 2030, wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM kutoka Mwanza, Mara, Shinyanga, Geita na Kagera waje Dodoma wakiwa wamepanda SGR kutoka Mwanza hadi Dodoma,” amesema.

Katika hatua nyingine, Dkt. Mwigulu ameiagiza Wizara ya Madini kuchukua hatua za haraka na kali kwa mujibu wa sheria dhidi ya watu wanaoshikilia leseni nyingi za madini bila kuziendeleza, akieleza kuwa hali hiyo inawanyima Watanzania wengine, hususan vijana na wachimbaji wadogo, fursa ya kufanya shughuli za uchimbaji.

“Mheshimiwa Waziri, futeni leseni hizo kwa mujibu wa sheria na gaweni upya maeneo hayo kwa wawekezaji Watanzania, vijana wa Kitanzania na wachimbaji wadogo,” amesema.

Dkt. Mwigulu amewataka Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, watendaji wa Serikali na halmashauri kuhakikisha wanawasikiliza wananchi, wanatatua kero zao kwa wakati na kutoa mrejesho.

Amesema ziara za viongozi wakuu hazipaswi kuwa mbadala wa utatuzi wa kero za wananchi katika ngazi za kawaida za Serikali.

04/09/2026

Waziri wa Fedha alitoa rai kubana
matumizi na kuelekeza fedha kwenye
vipaumbele. Kwa kuzingatia hilo, ninaelekeza hatua zichukuliwe katika maeneo yenye fursa za kupunguza matumizi bila kuathiri ufanisi wa shughuli za Serikali-Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba.

📍Bungeni-Dodoma
🗓️Septemba 04, 2026

————————————

Amesema hayo wakati akitoa hoja ya kuahirisha Bunge la 13, Mkutano wa Nne.

Address

Https://www. Pmo. Go. Tz/
Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ofisi ya Waziri Mkuu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share