Geological Survey of Tanzania

Geological Survey of Tanzania The GST is a Government Institution established under the Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act, No. 7 of 2017. It is under the Ministry of Minerals

The government executive agency under the ministry of Energy and Minerals entrusted in collecting, analyzing, archieving and disseminating national geo-scientific data and information

01/05/2026
HOTUBA YA WIZARA YA MADINIViongozi Wakuu wa Wizara ya Madini, watendaji pamoja na wadau wa sekta ya madini wamewasili Bu...
27/04/2026

HOTUBA YA WIZARA YA MADINI

Viongozi Wakuu wa Wizara ya Madini, watendaji pamoja na wadau wa sekta ya madini wamewasili Bungeni kufuatilia uwasilishaji wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.

Hotuba hiyo inawasilishwa na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ikiwa inalenga kueleza vipaumbele, mafanikio na mwelekeo wa maendeleo ya sekta ya madini nchini.

*SAMAMBA ATOA WITO GST KUBORESHA MAZINGIRA YA KAZI, KUIMARISHA USHIRIKIANO**Amesema Mazingira bora ya kazi ni msingi wa ...
09/04/2026

*SAMAMBA ATOA WITO GST KUBORESHA MAZINGIRA YA KAZI, KUIMARISHA USHIRIKIANO*

*Amesema Mazingira bora ya kazi ni msingi wa tija*

*Samaje amesema GST itaendelea kuboresha huduma za maabara na jiosayansi*

Dodoma, Aprili 9, 2026

Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Eng. Yahya Samamba, ameitaka Menejimenti ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kuhakikisha inajenga mazingira rafiki ya kazi yatakayowawezesha watumishi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kujisikia salama kazini.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi la GST uliofanyika katika ukumbi wa Tume ya Madini jijini Dodoma, Eng. Samamba amesema mazingira bora ya kazi ni msingi muhimu wa kuongeza tija, ubunifu na ufanisi katika utumishi wa umma.

Amesisitiza kuwa watumishi wanapaswa kufanya kazi kwa bidii na ubunifu ili kuiwezesha GST kuwa kitovu cha takwimu za jiosayansi zenye ubora na zinazopatikana kwa urahisi kwa wadau mbalimbali.

“Ni wajibu wa kila mtumishi kutekeleza majukumu aliyopewa kwa weledi na kuchangia kikamilifu mafanikio ya taasisi,” amesema Eng. Samamba.

Aidha, amewataka watumishi kuimarisha mshikamano, umoja na ushirikiano kazini, akibainisha kuwa hali hiyo itaongeza ufanisi katika utoaji wa huduma na kuinua hadhi ya utumishi wa umma.

Katika hatua nyingine, Eng. Samamba amewapongeza viongozi wapya wa Baraza la Wafanyakazi la GST, akieleza kuwa baraza hilo lina jukumu muhimu la kushauri uongozi juu ya ufanisi wa kazi, mipango ya maendeleo, pamoja na kuboresha ustawi wa wafanyakazi.

Amebainisha kuwa majukumu ya baraza yanajumuisha pia kujadili mipango ya mapato na matumizi, kupanga mikakati ya maendeleo ya taasisi, na kuimarisha ushirikiano kati ya wafanyakazi na uongozi.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa GST, Eng. Ally Samaje, amesema taasisi hiyo itaendelea kuboresha utendaji wake ili kuchangia kikamilifu maendeleo ya sekta ya madini nchini.

Ameongeza kuwa GST imejipanga kuboresha huduma zake za jiosayansi na maabara, sambamba na kuendana na mabadiliko ya teknolojia, ili kutoa matokeo yenye tija kwa uchumi wa taifa.

Address

903, Kikuyu Avenue
Dodoma
903

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Telephone

+255262323020

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Geological Survey of Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Geological Survey of Tanzania:

Share