UVCCM Tz

UVCCM Tz "KULINDA NA KUJENGA UJAMAA"

06/08/2026

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Agrey Mwanri, akizungumza wakati wa mapokezi yaliyofanyika katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma, amesema kuwa yuko tayari kutekeleza kwa moyo wote dhamana aliyoaminiwa na Chama.

Amesema viongozi wanapaswa kusimama imara katika kutekeleza majukumu yao kwa kujituma, uaminifu na uwajibikaji.

β€œTunanyanyuka kwenda kuitenda kazi tuliyoaminiwa nayo. K**a kazi zinaweza kuua, basi tutafia kazini,” amesema Ndugu Mwanri, akisisitiza dhamira yake na Viongozi wote kutekeleza majukumu aliyopewa.

______

CCMIpoKazini

06/08/2026

π“π”π“π€π–π€π‹πˆππƒπ€ 𝐖𝐀𝐍𝐀 π‚π‚πŒ πŠπ–π€ πŠπ”π–π€π“π„ππƒπ„π€ π‡π€πŠπˆ: 𝐂𝐇𝐀𝐂𝐇𝐀

Katibu wa NEC-Oganaizesheni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Komredi Paulo Chacha, amewashukuru wanachama wote wa CCM, hususan wale waliojitokeza kwa wingi katika mapokezi yake yaliyofanyika katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma.

Komredi Chacha amesema atahakikisha kila mwana CCM anatendewa haki na kulindwa maslahi yake bila ubaguzi wa aina yoyote ndani ya Chama, huku akisisitiza kuwa wajibu huo unaenda sambamba na kuheshimu na kuwatendea haki Watanzania wote.

________

06/08/2026

Katibu wa NEC-Oganaizesheni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu, Paulo Chacha, amesema kuwa ujasiri haupaswi kuchanganywa na kiburi, akisisitiza umuhimu wa kuheshimu wazee na viongozi waliotangulia.

Akizungumza leo mbele ya maelfu ya wanachama waliojitokeza katika mapokezi yake, Chacha amesema wazee ni hazina na maktaba ya Taifa na Chama ambayo inapaswa kuthaminiwa na kuheshimiwa kwa nguvu zote.

Amesema alimshauri Heche kumuomba msamaha Mzee Wasira, na kwamba anashukuru kwa hatua hiyo ya kuomba msamaha Kwa njia aliyoitumia kutokana na kauli alizozitoa,na kwamba wakurya hawajafundishwa kiburi Bali ni ujasiri.

________

06/08/2026

Katibu wa Idara ya Fedha na Uchumi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Jamal K. Ali, amemuomba Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi wa masuala ya fedha ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo kisheria, na kutoa taarifa kwa Watanzania kuhusu matokeo ya ukaguzi huo Kwani Chadema inakusanya Fedha Kwa Watanzania na Kisha Viongozi kutumia Kwa maslahi Binafsi, "Kwa Sasa wanachadema Pamoja na Viongozi wenzake HECHE Hawana Imani naye tena Kutokana na ubadhulifu Anaendelea kuufanya ndani ya CHADEMA" Amesema Jamal.

Akizungumza wakati wa mapokezi ya Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM Taifa katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma, Ndugu Jamal ametoa madai kuhusu usimamizi wa fedha ndani ya CHADEMA, akieleza kuwa kuna maswali yanayohitaji ufafanuzi kuhusu matumizi ya fedha za chama hicho.

Aidha, amezungumzia umuhimu wa vyama vya siasa kuwa na mikakati ya kuongeza mapato na kusimamia rasilimali zao kwa ufanisi.

________

UTEUZI
06/08/2026

UTEUZI

06/08/2026

π•πˆπƒπ„πŽ: Katibu wa Idara ya Fedha na Uchumi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Jamal K. Ali, amesema kila mtendaji na kiongozi mwenye jukumu la kusimamia miradi ya Chama anapaswa kujipanga kikamilifu kuhakikisha anatekeleza wajibu wake kwa ufanisi, kwa kuzingatia maelekezo ya Mwenyekiti wa CCM, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza wakati wa mapokezi ya Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM Taifa katika Makao Makuu ya CCM Dodoma, Ndugu Jamal amesema Chama kinaendelea kuimarisha usimamizi wa rasilimali zake, kuongeza mapato na kuibua miradi mipya yenye tija kwa maendeleo ya Chama.

Amesisitiza kuwa kila mtendaji na kiongozi mwenye dhamana ya kusimamia miradi ya CCM anawajibika kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa, akibainisha kuwa hakutakuwa na nafasi ya uzembe katika utekelezaji wa majukumu.

_________

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndugu Aggrey Mwanri, akiwa ameambatana na wajumbe wengine wa Halmas...
06/08/2026

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndugu Aggrey Mwanri, akiwa ameambatana na wajumbe wengine wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, amepokelewa Makao Makuu ya CCM, jijini Dodoma, leo tarehe 6 Agosti 2026. Mapokezi hayo yaliyoandaliwa na CCM Mkoa wa Dodoma, yamehudhuriwa na wanachama, makada na viongozi mbalimbali wa CCM, akiwemo Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CCM (Bara), Mzee Philip Japhet Mangula.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mkutano na Waandishi wa Habari...
06/08/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mkutano na Waandishi wa Habari kufuatia Ziara Rasmi ya Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. ...
06/08/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuhitimisha ziara rasmi ambapo walishuhudia utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga k**a Kituo cha Nishati cha Kikanda kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.

Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini Mhe. Dkt. Musenero Masanza wa Uganda akizungumza kwenye mkutano wa Waandishi wa...
06/08/2026

Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini Mhe. Dkt. Musenero Masanza wa Uganda akizungumza kwenye mkutano wa Waandishi wa Habari baada ya hafla ya utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga k**a Kituo cha Nishati cha Kikanda ulioshuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu, jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.

Address

UVCCM
Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UVCCM Tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share