02/09/2026
VIJANA NA UHIFADHI WA MALIASILI WAGA YAENDELEA KUJENGA UWEZO KWA JAMII
Tarehe 31 Agosti na 01 Septemba 2026, timu ya watumishi wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Waga, kwa kushirikiana na wataalamu wa wanyamapori kutoka Ofisi za Wakurugenzi wa Mbarali, Iringa na Mufindi, ilifanikiwa kufikisha vifaa vya michezo kwa vijana katika vijiji vya Kisilwa, Mahuninga na Ihanzutwa.
Katika zoezi hilo, jumla ya jezi 48 za mpira wa miguu na mipira 3 zilikabidhiwa kwa vijana, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuwafikia, kuwajengea ushirikiano na kuwashirikisha vijana katika agenda ya uhifadhi wa maliasili na wanyamapori.
Michezo ni nyenzo muhimu ya kuwaunganisha vijana na Uhifadhi. Kupitia shughuli hizi, tunaamini vijana wanaweza kuwa sehemu muhimu ya kulinda na kuhifadhi rasilimali za wanyamapori kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Katika ziara hizo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Waga Bi. FATUMA MBEMBATI alitoa elimu kwa wananchi na vijana kuhusu umuhimu wa uhifadhi, pamoja na faida zinazotokana na uwepo wa Hifadhi ya Wanyamapori Waga.
Uhifadhi si jukumu la mtu mmoja — ni jukumu letu sote,Tukiwafikia vijana leo, tunajenga mabalozi wa uhifadhi wa kesho. Linda maliasili, linda maisha, linda kizazi kijacho
,
NaUhifadhi