20/08/2019
"Niwaombe tuweke Mazingira safi na kuwa wakarimu kwa wageni, pia wananchi waruhusiwe kuvinjali nakuangalia utalii ndani ya Manispaa ya Iringa"
Kauli hiyo imesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Ally Hapi katika kongamano la utalii karibu kusini lililofanyika ukumbi wa Siasa ni Kilimo ndani ya Manispaa ya Iringa .
Miongoni mwa washiriki katika kongamano hilo ni Pamoja na Wakuu wa Wilaya, Jeshi la polisi, Wamiliki wa mahoteli, Viongozi wa Dini na viongozi mbalimbali wa Serikali nzima kutoka Manispaa ya Iringa. .ryata @