17/01/2025
Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa imeendesha Mafunzo ya Utumiaji wa Mfumo wa Kielektroniki wa Manunuzi Tanzania (NeST), kwa Wakuu wa Shule, Wahasibu wa Shule, Maafisa Elimu Kata pamoja na Wadhibiti Ubora wa Shule, lengo ikiwa ni kutatua changamoto wanazokutananazo wakati wa kufanya manunuzi kupitia mfumo huo.
Aidha Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wa kufanya Manunuzi kwa wakati kupitia Mfumo wa NeST ili kuondoa changamoto ya ukamilishaji wa Miradi kwa wakati.
Mafunzo hayo yamefanyika kwa Siku mbili kuanzia Januari 16 hadi 17, 2025 katika Ukumbi wa Shule ya kilwa sekondari.