24/12/2025
KHERI YA X-MASS NA MWAKA MPYA β MTOA SEKONDARI
Ndugu Wanajumuiya wote wa Mtoa Sekondari Wazazi, Wanafunzi, Walimu, Wafanyakazi na Wadau wa Elimu,
Tunapoukaribia mwisho wa mwaka 2025, uongozi wa shule unayo furaha kubwa kuwashukuru kwa ushirikiano wenu wa karibu na wa dhati katika safari yetu ya kukuza elimu bora.
Tunawatakia heri ya Krismasi na mwaka mpya 2026, tukiwaombea amani, afya njema, furaha na mafanikio tele katika familia zenu.
Mwaka huu 2025 umekuwa wa mafanikio makubwa kwa Mtoa Sekondari, ikiwemo:
Kuzaliwa kwa shule mpya ya Sekondari Mtoa Darajani, mradi uliofadhiliwa na Serikali kupitia SEQUIP kwa zaidi ya Tsh milioni 544, tunaishukuru sana Serikali kwa upendo na upeo wake katika sekta ya elimu.
Wanafunzi wa kidato cha kwanza na cha tatu tayari wameanza masomo rasmi kuanzia mwezi Julai 2025, na tunatarajia shule hiyo kukamilika kwa kidato cha pili na cha nne mwaka ujao.
Vilevile, tumefanikisha ujenzi wa matundu 10 ya vyoo(wanaume na wanawake) katika shule mama ya Mtoa Sekondari ili kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia mradi uligharimu kiasi Cha Tsh 16,800,000.
Kwa mafanikio haya na mengine, tunawashukuru sana kwa kila namna mlivyoshiriki kutufikisha hapa.
Tukiukaribisha mwaka mpya 2026, tuuchangamkie kwa Ari mpya, Nguvu mpya na Kasi mpya!
Swali kwa wanafunzi wote waliopitia Mtoa Sekondari tangu 2007 hadi sasa:
"Ni mwalimu gani amekuvutia zaidi na kwa nini?"
Karibuni tushirikiane kumbukumbu nzuri na kuuenzi mchango wa walimu wetu.
Heri ya sikukuu ya X-mass na mwaka mpya!!
Imetolewa na;
Kitengo Cha Habari Mtoa ss.