Manispaa ya Lindi

Manispaa ya Lindi This is the official page of Lindi Municipal Council

17/08/2026

🏆 SHIMISEMITA 2026 | KUNDI LA TIMU

Na Dawla Muni- Mbeya

Timu ya Manispaa ya Lindi ipo Kundi moja na timu za Chamwino DC, Kigoma MC, Kinondoni MC, Babati DC, Nachingwea DC na Tunduru DC.

🔥 Tutarajie ushindani mkali, burudani na mechi zenye hamasa katika kundi hili!

Lindi MC — Twende Kazi! 💪⚽


SHIRIKISHO LA MICHEZO LA WATUMISHI WA SERIKALI ZA MITAA
Samia Suluhu Hassan
Paul Makonda
Mkoa Wa Lindi
Victoria Mwanziva
Juma Mnwele

Juma Mnwele
17/08/2026

Juma Mnwele

Victoria Mwanziva
16/08/2026

Victoria Mwanziva

15/08/2026

🏆 SHEHISEMITA 2026 | MBEYA

Na Dawla Muni-Lindi MC

Timu ya Manispaa ya Lindi imeendelea na maandalizi ya mashindano ya SHIMISEMITA 2026 jijini Mbeya, ambapo leo asubuhi imefanya mazoezi katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge. 💪⚽


Samia Suluhu Hassan
Paul Makonda
Juma Mnwele

13/08/2026

Tupo tayari, let’s go 🏉⚽️😁

KAMATI YA SIASA CCM MKOA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA ELIMU NA UWEZESHAJI VIJANA LINDINa Dawla Muni-Lindi MCKamati...
13/08/2026

KAMATI YA SIASA CCM MKOA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA ELIMU NA UWEZESHAJI VIJANA LINDI

Na Dawla Muni-Lindi MC

Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Lindi, ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Alhaj Hassan M. Jarufu, imeridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Manispaa ya Lindi, ikiwemo uwekezaji katika elimu na uwezeshaji wa vijana.

Kamati hiyo imepongeza ujenzi wa Shule ya Msingi Mmongo, Kata ya Rasbura, unaogharimu Shilingi milioni 314 kupitia mpango wa BOOST, ambapo ujenzi wa jengo la utawala na madarasa mawili ya awali umefikia asilimia 97.

Mhe. Jarufu amesema elimu ni msingi wa maendeleo na amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kujenga shule zenye mazingira bora, huku akihimiza mradi huo ukamilike kwa wakati.

Aidha, Katika ziara hiyo Kamati pia imepongeza utekelezaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana baada ya kukagua Kikundi cha Youth Garage chenye wanachama watano, kilichopatiwa Shilingi milioni 34.

Mkopo huo umewezesha ununuzi wa vifaa vya ufundi magari, vipuri na mashine za rangi, na tayari umezalisha ajira na fursa za mafunzo kwa vijana. Kikundi hicho kimerejesha Shilingi laki saba hadi sasa.

📌Habari PichaChama cha kutetea watu wenye ulemavu wa akili Tanzania Association for Mentally Handicapped (TAMH) kutoka T...
12/08/2026

📌Habari Picha

Chama cha kutetea watu wenye ulemavu wa akili Tanzania Association for Mentally Handicapped (TAMH) kutoka Taifa na Mkoa kimetembelea Halmashauri ya Manispaa ya Lindi leo, Agosti 13, 2026, kwa ajili ya kutambulisha chama na kufanya kikao kazi. Mafunzo kwa wananchi kuhusu haki, ustawi na ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu wa akili yatafanyika kesho, Agosti 14, 2026, katika Ofisi ya Watendaji Ndoro DDC.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, Ndugu David Muharagi, amesema Halmashauri itaendelea kushirikiana na TAMH katika kutetea haki na ustawi wa watu wenye ulemavu wa akili pamoja na kupunguza unyanyapaa katika jamii.

Juma Mnwele

Address

Lindi
255

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Telephone

+255232202164

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Manispaa ya Lindi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Manispaa ya Lindi:

Shortcuts

Share