13/05/2026
WAUGUZI WA MZRH WAWAKILISHA VYEMA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI 2026
Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH) imeshiriki kikamilifu katika maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Arusha, katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha AICC.
Wataalamu hawa(Wauguzi) wamewakilisha vyema taasisi pamoja na wenzao kutoka sehem mbalimbali Tanzania katika kilele cha maadhimisho hayo ya tarehe 12 Mei yenye kauli mbiu “Wauguzi Wetu, Mustakabali Wetu: Wauguzi Waliowezeshwa Huokoa Maisha.”