Fine Frame Studios

Fine Frame Studios The home of story

PLATFORM OF LOVE.Author: Beatho Benedict .Episode_1. 🎬 SCENE: LOVE AT FIRST SIGHT (Love arrived before the train.) INT. ...
11/07/2026

PLATFORM OF LOVE.

Author: Beatho Benedict .

Episode_1.

🎬 SCENE: LOVE AT FIRST SIGHT (Love arrived before the train.)

INT. KITUO CHA TRENI – MCHANA

Abiria wamesimama wakisubiri treni. Beatho akiwa kimya, macho yake yanatua kwa msichana mrembo aliye mbali kidogo.

Anamkodolea macho bila hata kujitambua.

Msichana anahisi kuna mtu anamtazama. Anainua macho...

MACHO KWA MACHO.

Beatho anashindwa kugeuza macho yake. Msichana anatabasamu kwa upole.

CUT TO:

Treni inaingia kituoni. Kila mmoja anapanda.

Dakika chache baadaye...

Beatho anajikuta amekaa kiti kimoja na yule mrembo.

BEATHO
(akitabasamu kwa aibu)
Oh... kumbe tumekaa siti moja.

Sara anatikisa kichwa kwa tabasamu.

Kimya kifupi...

BEATHO
I'm Beatho... May I know your name, please?

SARA
I have the same feeling.

BEATHO
I'm interested in you.

SARA
You look so stunning boy.

BEATHO
And i like you..

SARA
That's a point, my name is Sara.

BEATHO
Wow... such a lovely name. May I have your number, please?

SARA
Oh, sure.

Wanatabasamiana huku treni ikiendelea na safari yake...
❤️❤️❤️❤️❤️❤️❤️

Usisahau ku-like, ku-comment na kushare. Niambie, ungefanya nini k**a ungekutana na mpenzi wako wa kwanza kwenye treni?

BADO NAKUPENDA. :  Benedict.  ya Pili...JOGOO ANAWIKA?Rebeka aliendelea kumsogelea Beatho taratibu. Beatho, akiwa amecha...
15/06/2026

BADO NAKUPENDA.
: Benedict.
ya Pili...

JOGOO ANAWIKA?
Rebeka aliendelea kumsogelea Beatho taratibu. Beatho, akiwa amechanganyikiwa, alijikuta akijigonga kwenye sofa na kuangukia hapo. Kabla hajajua afanye nini, Rebeka alikuwa tayari amemsogelea zaidi na kuanza kumpapasa na mkono yake laini.
"Rebeka, unataka nini?"
Aliuliza kwa sauti iliyochanganyika na mshangao.
Lakini Rebeka hakujibu. Ukimya uliotanda ulionekana kusema mengi kuliko maneno. Beatho alihisi mapigo ya moyo wake yakiongezeka kasi huku akishindwa kuzuia kilichokuwa kinaendelea mbele yake.
Ghafla, honi ya gari ilisikika nje ya nyumba.
Sauti hiyo ilimrudisha kila mmoja kwenye hali ya kawaida.
Haraka sana Rebeka aliondoka sebuleni na kukimbilia chumbani kwake. Beatho naye akajifanya kutulia kwa kuwasha televisheni, ingawa televisheni yenyewe haikuwa na tatizo lolote. Hapo ndipo alipotambua kuwa shida haikuwa TV, bali kulikuwa na jambo lingine kabisa lililokuwa limepangwa.
Muda mfupi baadaye, wazazi wake waliingia ndani.
"Mzima mwanangu? Naona umetutembelea."
Mama yake alimsalimia kwa upole.
"Nipo salama mama. Habari za majukumu?"
"Nzuri tu. Rebeka yupo?"
"Ndiyo, naamini yupo chumbani kwake."
Mazungumzo yaliendelea k**a kawaida, lakini akili ya Beatho ilikuwa mbali. Alikuwa bado akitafakari tukio la muda mfupi uliopita.
"K**a wazazi wake wasingefika ghafla, ingekuwaje?"
Swali hilo liliendelea kumzunguka kichwani.
Baada ya kukaa kwa muda, Beatho aliaga na kuondoka.
Mara tu alipoondoka, mama yake alimgeukia Rebeka..
"Vipi, umefanikiwa?"
Rebeka alijibu kwa kutikisa kichwa kuashiria ndiyo.
"Ni mzima kweli?"
Safari hii uso wa Rebeka ulijaa aibu.
"Jogoo anawika vizuri kabisa..."
Alijibu kwa sauti ya chini kiasi kwamba iliwalazimu wengine kutazamana kabla ya kucheka.
Hapo ndipo ilipoonekana wazi kuwa kile kilichotokea hakikuwa jambo la bahati mbaya. Kulikuwa na mkono wa wazazi wake Beatho nyuma ya pazia.
Usiku huo, Beatho alipofika nyumbani hakupata amani.
Kila alipojaribu kufikiria jambo lingine, sura ya Rebeka ilijikuta ikirudi tena akilini mwake.
"Huyu msichana ana nini hasa?"
Aliwaza.
Kadiri alivyokumbuka tabasamu lake, sauti yake na namna alivyokuwa akizungumza, ndivyo alivyozidi kupotea kwenye mawazo.
Hatimaye usingizi ulimchukua.
Lakini hata ndotoni, jina lililoendelea kujirudia lilikuwa moja tu.
Rebeka.
Siku iliyofuata, majira ya mchana, Beatho alikuwa akipita mitaani k**a kawaida yake.
Njiani alikatiza karibu na kundi la wasichana waliokuwa wakipiga stori.
Kwa sababu ya mawazo mengi, alipita bila hata kusalimia.
"Wewe Beatho!"
Mmoja wao alimwita.
Akageuka kwa heshima.
"Naam?"
"Mambo?"
"Poa. Habari yako?"
"Sio poa. Mbona unatupita bila salamu?"
Beatho akatabasamu kwa aibu.
"Samahani sana. Mawazo mengi."
"Sawa basi, umesamehewa handsome boy."
"Asante. Ngoja niwahi."
Akaendelea na safari yake.
Baada ya kuondoka, mabinti wale walianza kujadili.
"Wewe bwana! Umeanza tena kumpa sifa?"
Mmoja akamwambia mwenzake.
"Acha bana. Mimi namkubali sana huyo kaka."
"Kweli?"
"Kabisa!"
Wengine wakacheka kwa sauti.
"Mimi nikiona anachelewa kunitongoza, nitamtongoza mwenyewe."
Fatuma alisema huku akiwafanya wenzake wapige kelele za mshangao.
Lakini Sara, aliyekuwa k**a kiongozi wao, alitikisa kichwa.
"Mimi huyo simwelewi kabisa."
"Kwa nini?"
"Ni mpole kupita kiasi. Nimeshawahi kukutana naye club, lakini huwezi kujua anafikiria nini."
Wote wakaanza kujadili tabia ya Beatho.
Kwa wengi, ilikuwa ajabu kuona kijana mwenye sura nzuri, mwenye juhudi na anayeheshimika, lakini bado asiwe na mazoea ya kuwakimbilia wasichana k**a vijana wengi walivyofanya.
Jioni ilipowadia, Beatho na rafiki yake Alto walikuwa kwenye mizunguko yao ya kawaida wakikusanya CD walizokuwa wamekodisha.
Baada ya kupitia sehemu nyingi, Alto alisisitiza waishie kwa Aisha.
Mwisho walifika nyumbani kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ushindi, Mzee Omari Rashimu Abdullah, ambaye alikuwa baba yake Aisha.
Alto alibisha hodi.
Aisha akafungua mlango.
"Samahani, ile CD ya Naina bado sijamaliza. Nitakurudishia kesho."
"Hakuna shida. Tatizo si CD."
"Basi?"
"Kuna mtu anakuhitaji nje."
"Nani?"
"Beatho."
Aisha alishtuka kidogo.
"Aje mwenyewe basi."
Alto alijaribu kumbembeleza, lakini Aisha alibaki msimamo wake.
Baada ya kufikiria kwa haraka, Alto akamshika mkono na kumvuta taratibu.
"Jamani Alto, sitaki..."
Mdomo ulikataa, lakini miguu iliendelea kufuata.
Dakika chache baadaye walifika pale alipokuwa amesimama Beatho.
Beatho mwenyewe hakuwa na habari ya mpango huo.
Alikuwa tayari amewasha pikipiki ili kuondoka.
Lakini Alto alimkaribia, akachomoa funguo na kumnong'oneza:
"Mimi kazi yangu imeisha. Huyu hapa. Ongea naye."
"Lakini..."
"Lakini nini? Uwanja ni wako."
Alto akaondoka na kuwaacha wawili hao wakitazamana.
Sasa, kwa mara ya kwanza, Beatho na Aisha walikuwa uso kwa uso.
Na hakuna aliyekuwa tayari kuvunja ukimya.
⚛️⚛️⚛️ Itaendelea......

next k**a umeipenda,

BADO NAKUPENDAMwandishi: Beatho BenedictSehemu ya KwanzaMZIMA KWELI?Mji mdogo wa Kapunga ulikuwa na vijana wawili waliot...
10/06/2026

BADO NAKUPENDA
Mwandishi: Beatho Benedict
Sehemu ya Kwanza
MZIMA KWELI?
Mji mdogo wa Kapunga ulikuwa na vijana wawili waliotajwa sana kwa ukaribu wao. Beatho na Alto. Urafiki wao ulikuwa wa aina ambayo watu walikuwa wakisema:
"Ukimwona Alto, ujue Beatho hayuko mbali. Ukimkosa Beatho, muulize Alto."
Walishirikiana karibu kila kitu katika maisha yao. Walifanya biashara pamoja, walizunguka pamoja, na hata matatizo yao mengi walikabiliana nayo kwa pamoja.
Lakini kulikuwa na jambo moja lililowatofautisha.
Alto alikuwa tayari ameoa na kubahatika kupata mtoto. Maisha yake ya familia yalikuwa yameshaanza kujengeka.
Beatho alikuwa tofauti kabisa.
Hakuwahi kuonekana akifuatilia wasichana. Hakuwahi kuonekana akimsifia binti yeyote wala kuonyesha dalili za kuwa kwenye mahusiano. Hata marafiki zake walishindwa kuelewa k**a kweli alikuwa na hisia za kimapenzi k**a vijana wengine.
Kila mara walipozungumzia mapenzi, Beatho alikuwa kimya.
Kimya chake kilifanya wengi waamini kwamba mapenzi hayakuwa sehemu ya maisha yake.
Mbali na urafiki wao, wawili hao walikuwa wafanyabiashara wa kazi za sanaa.
Walikuwa wakiuza nyimbo, filamu, memory cards, flash disks na pia kukodisha CD za tamthilia mbalimbali kutoka nchi za nje.
Siku moja walikuwa wakikusanya CD walizokuwa wamekodisha kwa wateja wao.
Walifika nyumbani kwa Aisha.
Aisha alikuwa msichana mrembo aliyependa sana tamthilia za Kihindi. Alikuwa mmoja wa wateja wao wa kudumu.
Baada ya kurudisha CD zake, alitabasamu na kuingia ndani ya nyumba.
Beatho alimfuatilia kwa macho hadi alipopotea mlangoni.
Kisha akavuta pumzi ndefu.
"Aisee..." alisema.
Alto akamgeukia.
"Kuna nini?"
Beatho akatikisa kichwa kidogo.
"Aisha ni mrembo sana. Nimemkubali."
Alto alisimama ghafla kana kwamba amesikia jambo la ajabu.
"Wewe?"
"Ndiyo."
"Wewe ndiye unasema hivyo?"
"Kwani kuna shida gani?"
Alto akaanza kucheka.
"Wewe si ndiye huwa unajifanya padri? Leo umependa?"
Beatho hakujibu.
Aliwasha pikipiki yao na safari ikaendelea.
Lakini kwa mara ya kwanza, Alto aliona upande wa rafiki yake ambao hakuwahi kuuona.
Wakati huo huo, katika nyumba moja ya kifahari, wazazi wa Beatho walikuwa wameketi sebuleni wakikumbushana enzi zao za ujana.
Mzee Benedict na mkewe Antelma walikuwa wakifurahia utulivu wa jioni.
Watoto wao wengi walikuwa tayari wameanza maisha yao.
Isipokuwa mmoja.
Beatho.
Mzee Benedict akacheka.
"Mke wangu..."
"Naam?"
"Unadhani kweli kijana wetu yuko sawa?"
Antelma akakunja uso.
"Sielewi."
"Mbona hakuna hata siku moja mtu amewahi kuja hapa kusema mtoto wako kamtia mimba binti yake?"
Antelma akabaki kimya kwa sekunde chache.
Kisha wote wakacheka.
Lakini ndani ya vicheko hivyo kulikuwa na swali la kweli.
Je, Beatho alikuwa wa kawaida k**a vijana wengine?
Au kulikuwa na jambo ambalo hawakulijua?
Wiki zilipita.
Aisha aliendelea kuonekana kwenye biashara zao.
Lakini Beatho hakuthubutu kumweleza hisia zake.
Kila alipopata nafasi, alikosa ujasiri.
Hatimaye Alto akaamua kuingilia kati.
Siku moja alimtafuta Aisha na kumueleza ukweli wote.
Akamwambia jinsi rafiki yake alivyokuwa akimpenda lakini akashindwa kumweleza.
Aisha alisikiliza kwa makini.
Mwisho akatabasamu.
"K**a ni kweli ananipenda, nataka nisikie kutoka kwake mwenyewe."
Jibu hilo lilimpa matumaini makubwa Alto.
Baada ya kuondoka, Aisha alijifungia chumbani kwake.
Moyo wake ulikuwa ukidunda kwa kasi.
Kwa muda mrefu naye alikuwa akimpenda Beatho.
Swali pekee lililomsumbua lilikuwa moja:
K**a ananipenda kweli, kwa nini ananiogopa?
Jioni moja, Beatho alikuwa ameketi chumbani kwake akichezea laptop yake.
Ghafla simu ikaita.
Alipotazama skrini, aliona jina la Rebeka.
Msichana aliyekuwa akifanya kazi nyumbani kwa wazazi wake.
"Hello," alipokea.
"Kaka, naomba uje uniangalizie TV. Imekataa kuwaka."
"Leo nimechoka sana. Nadhani nitakuja kesho."
"Sasa nitamalizaje tamthilia uliyoniletea juzi?"
Sauti yake ilikuwa ya kubembeleza.
Beatho akashindwa kukataa.
Baada ya dakika chache alikuwa tayari njiani.
Dakika saba baadaye aliwasili nyumbani kwa wazazi wake.
Cha kushangaza, mazingira yalikuwa kimya sana.
Hakukuwa na mwanga wala sauti yoyote.
Aliingia ndani huku akiita:
"Rebeka!"
Hakukuwa na jibu.
Akaendelea mbele.
"Rebeka!"
Bado kimya.
Akawasha tochi ya simu yake na kuanza kutafuta swichi ya taa.
Lakini alipogeuza mwanga upande wa ukuta...
Moyo wake uliruka.
Pale karibu na swichi alisimama Rebeka.
Akiwa amevalia vazi jepesi lililoshindwa kumsitiri vema kwa kiasi maeneo nyeti yenye ushawishi yalikua wazi wazi mbele ya macho ya Beatho .
Tabasamu dogo lilikuwa usoni mwake.
Hakusema neno.
Alianza kumsogelea taratibu.
Hatua moja.
Kisha nyingine.
Beatho akahisi mapigo ya moyo wake yakiongezeka.
Hakuelewa kilichokuwa kinaendelea.
Wakati Rebeka akiendelea kumsogelea, yeye alianza kurudi nyuma.
Hatua kwa hatua.
Bila hata kujua anaelekea wapi.

Itaendelea... 🔥🔥🔥
K**a umependa achia to show unaweza na ukani
za mapenzi na

22/05/2026

FREE TO PLAY sasa inapatikana SportPesa. Cheza GOAL RUSH BURE leo kwa kubofya HAPA!

Address

Mbeya

Opening Hours

Friday 20:00 - 23:00
Sunday 19:30 - 12:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Fine Frame Studios posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category