Tanzania Wildlife Management Authority - TAWA

Tanzania Wildlife Management Authority - TAWA Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Tanzania Wildlife Management Authority - TAWA, Government Organization, Tafori Building, Morogoro.

Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania(Tanzania Wildlife Management Authority -TAWA) ilianzishwa kwa mujibu wa kifungu cha 8 cha Sheria Ya Wanyamapori Na.5 ya mwaka 2009.

16/08/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Tamasha la Kizimkazi limekuwa sehemu muh...
15/08/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Tamasha la Kizimkazi limekuwa sehemu muhimu ya kuchochea maendeleo ya Kizimkazi na Zanzibar kwa ujumla, kwa kufungua fursa za uwekezaji, biashara na maendeleo ya wananchi.

Rais Samia amesema hayo wakati akifunga Tamasha la 10 la Kizimkazi, akieleza kuwa tamasha hilo limekuwa likiibua miradi ya maendeleo na kuwavutia wawekezaji pamoja na wageni kutoka ndani na nje ya Zanzibar.

Amesema viongozi wanapaswa kuhakikisha fursa zinazopatikana kupitia tamasha hilo zinawafikia wananchi na kuwa na manufaa ya muda mrefu, ikiwemo kuboresha huduma za msingi k**a maji, barabara na miundombinu mingine muhimu.

Aidha, Dkt. Samia amewahimiza wawekezaji kuendelea kutumia fursa zilizopo Kizimkazi na Zanzibar kwa ujumla, huku akiitaka jamii, hususan vijana, kulinda amani na utulivu, akisisitiza kuwa amani ni chachu ya maendeleo na msingi wa kutumia fursa za kiuchumi na kijamii.

Rais Samia pia amewashukuru Kamati ya Maandalizi, wazawa wa Kizimkazi, wadau na wadhamini kwa ushirikiano wao katika kufanikisha tamasha hilo.

Kwa upande wake, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuunga mkono Tamasha la Kizimkazi katika kutangaza na kuenzi mila, silka na utamaduni wa Zanzibar.

Dkt. Mwinyi amesema tamasha hilo ni chachu ya maendeleo kwa Kizimkazi, Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kutokana na uwezo wake wa kuunganisha watu, biashara, utalii na uwekezaji.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Hamida M***a Khamis, amesema tamasha hilo limeibua fursa katika afya, elimu, ajira, biashara na utalii. Wafanyabiashara 129 walisajiliwa kushiriki, huku zaidi ya wafanyabiashara wadogo 200 wakinufaika na shughuli za kibiashara.

Tamasha la Kizimkazi 2026 limeendelea kuwa jukwaa la kuibua fursa za kiuchumi, kutangaza utalii, kuenzi utamaduni na kuchochea uwekezaji kwa maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

TAWA, SOAT WAKUTANA KIJADILI MAENDELEO YA UTELELEZAJI WA SWICA📍 Wawekezaji waalikwa kutumia fursa za AFCON 2027Na Beatus...
12/08/2026

TAWA, SOAT WAKUTANA KIJADILI MAENDELEO YA UTELELEZAJI WA SWICA

📍 Wawekezaji waalikwa kutumia fursa za AFCON 2027

Na Beatus Maganja, Dodoma

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) leo Agosti 12, 2026 imekutana na wadau wa Chama cha Wawekezaji Mahiri (SWICA Operators Association of Tanzania – SOAT) jijini Dodoma kujadili maendeleo ya utekelezaji wa mikataba ya uwekezaji mahiri (SWICA) na kuweka mikakati ya kuongeza tija kwa Serikali, wawekezaji na jamii.

Kikao hicho kilichoongozwa na Kaimu Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA Mlage Yussuf Kabange ni sehemu ya juhudi za Mamlaka za kuimarisha ushirikiano na wawekezaji, kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji pamoja na kujenga mfumo bora wa mawasiliano kati ya TAWA na kampuni zinazotekeleza shughuli za SWICA na wadau wengine.

Akizungumza katika kikao hicho Kabange amewapongeza wawekezaji hao kwa mchango wanaoutoa katika maendeleo ya jamii zinazozunguka maeneo yao ya uwekezaji ikiwemo kusaidia ujenzi wa madarasa na zahanati, kutoa madawati, kusaidia shughuli za michezo kwa vijana pamoja na miradi mingine ya kijamii.

Amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa wawekezaji hao katika kuchochea maendeleo ya jamii sambamba na kusaidia juhudi za uhifadhi wa rasilimali za wanyamapori.

Aidha, Kabange amewahimiza wawekezaji hao kutumia fursa zinazotarajiwa kutokana na mashindano ya AFCON 2027 kwa kuwekeza katika maeneo ya kimkakati yanayosimamiwa na TAWA yakiwemo Makuyuni Wildlife Park mkoani Arusha, Hifadhi ya Pande jijini Dar es Salaam na Hifadhi ya Wami-Mbiki inayopakana na mikoa ya Pwani na Morogoro.

Ameeleza kuwa maeneo hayo yana fursa mbalimbali za uwekezaji katika huduma za utalii, ikiwemo ujenzi wa "tented lodges", kambi za kitalii na miundombinu mingine ya malazi na huduma ambayo inaweza kusaidia kuhudumia wageni watakaotembelea Tanzania wakati wa mashindano hayo.

Katika hatua nyingine, Kabange amewahakikishia wawekezaji hao kuwa TAWA itaendelea kutoa ushirikiano wa kiwango cha juu na kufanya maboresho katika mifumo ya mawasiliano, ikiwemo kuimarisha mawasiliano ya moja kwa moja kati ya Mamlaka na kampuni moja moja ili changamoto zinazojitokeza ziweze kupatiwa ufumbuzi kwa wakati.

Kikao hicho ni cha kwanza kati ya TAWA na SOAT tangu kuanzishwa kwa chama hicho Machi 28, 2026 na kimetoa nafasi kwa pande hizo kujadili masuala mbalimbali ya kimkakati na kufikia maazimio ya pamoja yanayolenga kuimarisha utekelezaji wa SWICA na kukuza uwekezaji endelevu.

Afisa  kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Lucas Goroi, akitoa elimu ya uhifadhi kwa wananchi wal...
08/08/2026

Afisa kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Lucas Goroi, akitoa elimu ya uhifadhi kwa wananchi waliotembelea banda la TAWA katika Maonesho ya 10 ya Kilimo Nane Nane Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Mamlaka za kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa kulinda rasilimali za wanyamapori na mchango wake katika maendeleo ya Taifa.

Katika maonesho hayo, Afisa huyo pia alimkabidhi mmoja wa wageni kalenda yenye ramani ya Tanzania inayoonesha mapori ya akiba yanayosimamiwa na TAWA pamoja na vivutio vinavyopatikana katika maeneo hayo, ikiwa ni njia ya kuendelea kuhamasisha wananchi kuyatambua, kuyathamini na kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wa rasilimali za wanyamapori kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

#2026

08/08/2026

TAWA YAKITA KAMBI NANE NANE ZANZIBAR, YAANIKA FURSA ZA UTALII

MAMIA ya wananchi wanaendelea kumiminika katika viwanja vya Dole, Magharibi A, Zanzibar, kushuhudia Maonesho ya 10 ya Kilimo Nane Nane, huku Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) ikitumia jukwaa hilo kutoa elimu kuhusu uhifadhi, fursa za utalii na umuhimu wa rasilimali za wanyamapori katika kukuza uchumi wa Taifa.

Katika maonesho hayo, TAWA imeweka kambi maalumu inayovuta makundi mbalimbali ya wananchi, wakiwemo wanafunzi kutoka shule za Zanzibar, wanaopata fursa ya kujifunza kwa vitendo kuhusu shughuli zinazotekelezwa na Mamlaka hiyo pamoja na namna rasilimali za wanyamapori zinavyoweza kuwa sehemu ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Akizungumza katika maonesho hayo, Afisa wa Wanyamapori kutoka TAWA, Lucas Goroi, amesema ushiriki wa Mamlaka hiyo Zanzibar una lengo la kuwafikia wananchi na kuwapa uelewa mpana kuhusu umuhimu wa uhifadhi, huku ukitumika pia kutangaza fursa mpya za utalii zinazotarajiwa kuibuliwa kupitia Zanzibar Wildlife Park inayopangwa kuanzishwa eneo la Jambiani Muyuni.

Guroi amesema mradi huo unatarajiwa kuwa miongoni mwa vivutio vitakavyoongeza fursa za utalii Zanzibar, akieleza kuwa wananchi waliofika katika banda la TAWA wameonesha mwamko mkubwa wa kutaka kufahamu zaidi kuhusu wanyamapori, uhifadhi na namna sekta hiyo inavyoweza kunufaisha Taifa.

Ameongeza kuwa hatua hiyo inaendana na juhudi za Serikali hususan juhudi za Mheshimiwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Daktari Samia Suluhu Hassan ambaye alionyesha kwa vitendo namna ya kukuza sekta ya utalii katika andiko la utayarishaji wa filamu ya Royal Tour za kuhamasisha utalii wa ndani na kuongeza idadi ya Watanzania wanaotembelea vivutio vya utalii nchini.

Kwa upande wa elimu, TAWA imeendelea kuwafikia wanafunzi wanaotembelea banda lake, ikiwaelimisha kuhusu umuhimu wa uhifadhi na mchango wa rasilimali za wanyamapori katika uchumi wa Taifa. Ajmal Ali Ramadhan, mwanafunzi kutoka Shule ya Sekondari Mikindani , amesema ziara hiyo imemsaidia kuelewa zaidi tofauti kati ya wanyama wa porini na wanyama wanaofugwa, pamoja na namna rasilimali hizo zinavyoweza kuchangia mapato kupitia utalii.

MNYAMAPORI ANAJUA MPAKA WA HIFADHI?!📍 Nini kifanyike?✍️ Na Beatus Maganja“Njooni muwaondoe tembo wenu, tayari wameshavam...
07/08/2026

MNYAMAPORI ANAJUA MPAKA WA HIFADHI?!

📍 Nini kifanyike?

✍️ Na Beatus Maganja

“Njooni muwaondoe tembo wenu, tayari wameshavamia mashamba yetu” Ni kauli ambayo mhifadhi anaweza kukutana nayo baada ya tembo kutoka katika eneo la hifadhi na kuingia mashambani, wakati mwingine akila au kuharibu mazao.

Kwa mwananchi aliyepoteza mazao aliyoyategemea kwa chakula au kipato, hasira na maumivu yake yanaeleweka na kwakweli inaumiza sana. Lakini katikati ya hali hiyo kuna swali ambalo ni muhimu sana kujiuliza..Je, tembo anajua mpaka wa hifadhi?. Na huu ndio msingi wa makala hii.

Sisi binadamu tuna ramani. Tuna alama za mipaka, vigingi, barabara, vijiji, kata, wilaya, mikoa na hata mipaka ya nchi. Tunaweza kusema, “Kuanzia hapa ni hifadhi, na kuanzia pale ni ardhi ya kijiji.” Lakini kwa tembo au mnyamapori mwingine, dunia yake haisomeki kwa namna hiyo. Mnyama hawezi kusoma bango lililoandikwa “Mwisho wa Hifadhi”, wala hawezi kujua kwamba hatua chache mbele yake amevuka mpaka uliowekwa na binadamu.

Kwa mnyamapori, kinachoongoza mienendo yake zaidi ni mahitaji yake ya msingi katika maisha. Anatafuta maji, chakula, mwenza, eneo salama la kuzaa au njia ya kuelekea kwenye mazingira yanayokidhi mahitaji yake. Baadhi ya wanyamapori hutumia maeneo makubwa na wanaweza kusafiri umbali mrefu kulingana na upatikanaji wa maji, chakula, misimu na hali ya mazingira. Kwao, mfumo ikolojia unaweza kuwa muhimu zaidi kuliko mstari wa mpaka tuliochora kwenye ramani.

Ndiyo maana tunapozungumzia uhifadhi, hatuwezi kuzungumzia hifadhi peke yake. Lazima tuzungumzie pia mapito ya wanyamapori (wildlife corridors), maeneo ya mtawanyiko (dispersal areas) na maeneo yanayounganisha mifumo mbalimbali ya ikolojia. Maeneo haya yanaweza kuwa muhimu kwa wanyama kuhama kutoka sehemu moja kwenda nyingine kutafuta rasilimali muhimu kwa maisha yao. Yakizibwa kabisa na shughuli za kibinadamu, uwezekano wa kukutana kwa binadamu na wanyamapori unaweza kuongezeka.

Kwa upande mwingine. hebu tufikirie jambo hili Kwa pamoja. Njia ambayo leo tunaiita shamba, kijiji au makazi ya watu inaweza kuwa sehemu ya eneo ambalo kwa muda mrefu lilikuwa likitumiwa na wanyamapori kupita. Kadiri idadi ya watu inavyoongezeka na matumizi ya ardhi kubadilika, maeneo ya makazi, kilimo, mifugo na miundombinu yanaweza kusogea karibu zaidi na maeneo wanayotumia wanyamapori. Hapo ndipo wakati mwingine tunapoanza kusema, “Wanyama wamekuja kwetu.” Lakini swali la kutafakari ni hili...Je, katika baadhi ya maeneo, ni wanyamapori waliotufuata, au matumizi yetu ya ardhi ndiyo yaliyokutana na njia zao za muda mrefu?.

Hapa ndipo Mamlaka husika zimekuwa zikifanya kila ziwezavyo kuhakikisha zinatafuta suluhu ya kudumu ya jambo hili, ili kuhakikisha mwananchi anaendelea kuwa salama dhidi ya madhara yanayoweza kusababishwa na wanyamapori hao, na wanyamapori pia k**a rasilimali muhimu ya Taifa kuendelea kuwepo Kwa manufaa ya kizazi chetu na vizazi vijavyo.

Kwahiyo, tunapomuona tembo nje ya hifadhi, ni vyema tusifanye haraka kuhitimisha kwamba “amekosea njia.” Huenda kwa mtazamo wetu yuko nje ya mpaka, lakini kwa mtazamo wa ikolojia anaweza kuwa anafuata maji, chakula au njia ambayo vizazi vya wanyama wa aina yake vimeitumia kwa muda mrefu. Changamoto yetu sisi binadamu ni kutafuta namna ambayo mahitaji ya maendeleo, usalama wa wananchi na mahitaji ya wanyamapori yanaweza kusimamiwa kwa uwiano.

Mwisho wa yote, mnyamapori hajui mpaka wa hifadhi kwa namna tunavyoujua sisi. Hajui kijiji kinaanzia wapi wala hifadhi inaishia wapi. Lakini sisi tunajua. Tuna sayansi, teknolojia, sheria na uwezo wa kupanga matumizi ya ardhi. Hivyo jukumu kubwa zaidi liko kwetu kutumia maarifa hayo kuhakikisha binadamu anaishi kwa usalama huku wanyamapori na makazi yao yakiendelea kuhifadhiwa.

Kwasababu swali kubwa si tu, “Kwa nini mnyama ametoka hifadhini?” bali pia tunapaswa kujiuliza..Je, tumemwachia njia ya kwenda anapohitaji kwenda? Kwa maana uhifadhi ni zaidi ya kulinda mnyama ndani ya mpaka pamoja na kuelewa maisha yake hata pale yanapovuka mpaka.

KWANINI KIPANDE KIDOGO CHA NYAMAPORI KINAWEZA KUSABABISHA ADHABU KUBWA?📍Je, wakati sisi tunakiona kipande, Sheria inaona...
06/08/2026

KWANINI KIPANDE KIDOGO CHA NYAMAPORI KINAWEZA KUSABABISHA ADHABU KUBWA?

📍Je, wakati sisi tunakiona kipande, Sheria inaona nini?!!

✍️ Na Beatus Maganja

Kila mara taarifa zinapotolewa kuhusu mtu aliyek**atwa akiwa na kipande cha nyama ya mnyamapori, ngozi, jino au nyara nyingine, mijadala huibuka mitandaoni. Wapo wanaouliza kwa mshangao, "Inawezekanaje mtu afungwe miaka mingi kwa sababu ya kipande kidogo tu?" Wengine hufikia hatua ya kuiita Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori kuwa kandamizi. Lakini je, tumewahi kusimama na kujiuliza kwa nini sheria imeweka msimamo huo?

Pengine tatizo si ukali wa sheria, bali namna tunavyolitazama kosa lenyewe. Mara nyingi macho yetu huona ukubwa au udogo wa kipande kilichok**atwa, lakini sheria hutazama chanzo cha kipande hicho. *Swali la msingi huwa si, "Ni kikubwa kiasi gani?" bali, "Kimepatikanaje?"*

Hebu fikiria kwa mfano jino la tembo. Halijipeleki lenyewe sokoni, wala halidondoki lenyewe kutoka kwa tembo aliye hai Ili lipatikane, mara nyingi kuna tembo aliyepoteza maisha au nyara iliyochukuliwa kinyume cha sheria. Hivyo, kipande kidogo kinakuwa ushahidi wa mnyororo mpana zaidi wa uhalifu dhidi ya rasilimali za Taifa.

Sheria nyingi duniani zinazohusu ujangili au uhalifu mkubwa hazitazami uzito wa kitu pekee, bali madhara ya kitendo. Ndiyo maana, katika baadhi ya makosa, hata kiasi kidogo cha kitu kinachohusishwa na uhalifu kinaweza kuwa na athari kubwa za kisheria. Mantiki hiyo ndiyo inayotumika pia katika mapambano dhidi ya ujangili au biashara haramu ya nyara za wanyamapori.

Wapo wanaosema, "Lakini huyu alikuwa na kipande kidogo tu." Ni hoja inayostahili kusikilizwa. Hata hivyo, ikiwa sheria ingeruhusu kila mtu kuwa na "kipande kidogo", je, ni vipande vingapi vingekusanywa baada ya mwezi mmoja, mwaka mmoja au miaka mitano? Je, soko la biashara haramu lisingeendelea kukua kwa kujificha nyuma ya hoja ya "kidogo tu"? Wakati mwingine, njia bora ya kuzuia ujangili mkubwa ni kukata mianya yake midogo.

Tusisahau kwamba wanyamapori si mali ya mtu mmoja. Ni urithi wa Watanzania wote na wa vizazi vijavyo. Tembo, faru, simba, chui na wanyamapori wengine wameifanya Tanzania ijulikane duniani, wamechangia ukuaji wa utalii, wamezalisha ajira na mapato ya fedha za kigeni na wameifanya nchi yetu kuwa miongoni mwa mataifa yenye bioanuwai ya kipekee. Kila nyara inayopatikana kinyume cha sheria ni pigo kwa urithi huo.

Hii ndiyo sababu sheria haikulenga tu kumwadhibu anayek**atwa. Lengo lake kubwa ni kutuma ujumbe kwa jamii kwamba biashara haramu ya nyara haikubaliki kwa namna yoyote. Sheria inalinda mnyama ambaye hawezi kujitetea na inalinda maslahi ya Taifa ambayo mara nyingi hayaonekani kwa macho ya haraka.

Ni muhimu pia kutambua kwamba mahak**a hutoa maamuzi kwa kuzingatia sheria, ushahidi uliowasilishwa na mazingira ya kila kesi. Hivyo, si sahihi kudhani kwamba kila mtu anayekutwa na nyara hupata adhabu inayofanana. Kila shauri husikilizwa kwa misingi yake na kwa mujibu wa sheria husika.

Badala ya kuuliza kwa nini adhabu ni kubwa, pengine tuanze kuuliza swali lingine muhimu zaidi..*Kwa nini nyara hizo zilikuwa mikononi mwa mtu bila uhalali?* Tukipata jibu la swali hilo, huenda tukaelewa kwa nini sheria imeamua kulinda rasilimali hizi kwa nguvu kubwa kiasi hicho.

Mwisho wa yote, lengo la Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori si kujaza magereza. Lengo lake ni kulinda rasilimali hizi Kwa ajili ya kikazi chetu na vizazi vijavyo ili viendelee kurithi Tanzania yenye utajiri wa wanyamapori k**a tulivyorithi sisi leo.

Elimu ndiyo silaha bora kuliko adhabu. Kadiri jamii inavyoelewa thamani ya rasilimali za wanyamapori na mantiki ya sheria zinazozilinda, ndivyo tunavyojenga ushirikiano mkubwa zaidi katika uhifadhi. Na pale wananchi wanapokuwa washirika wa uhifadhi ndipo Taifa lote hunufaika.

**a

Kumgonga mnyama pori ni kosa la kisheria. Kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori, Sura ya 283, mkosaji anaweza ...
05/08/2026

Kumgonga mnyama pori ni kosa la kisheria. Kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori, Sura ya 283, mkosaji anaweza kuwajibika kulipa faini kulingana na aina ya mnyama aliyegongwa. Faini zilizoainishwa hapa ni kwa baadhi tu ya wanyamapori.

TAWA inaendelea kuwakumbusha madereva wote kuongeza umakini wanapoendesha katika maeneo yanayopitiwa na wanyamapori, kuzingatia alama za tahadhari na kupunguza mwendo ili kulinda maisha ya wanyamapori na kuepuka hatua za kisheria.

Kumgonga mnyama pori ni kosa la kisheria. Kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori, Sura ya 283, mkosaji anaweza ...
05/08/2026

Kumgonga mnyama pori ni kosa la kisheria. Kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori, Sura ya 283, mkosaji anaweza kuwajibika kulipa faini kulingana na aina ya mnyama aliyegongwa. Faini zilizoainishwa hapa ni kwa baadhi tu ya wanyamapori.

TAWA inaendelea kuwakumbusha madereva wote kuongeza umakini wanapoendesha katika maeneo yanayopitiwa na wanyamapori, kuzingatia alama za tahadhari na kupunguza mwendo ili kulinda maisha ya wanyamapori na kuepuka hatua za kisheria.

Kumgonga mnyama pori ni kosa la kisheria. Kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori, Sura ya 283, mkosaji anaweza ...
05/08/2026

Kumgonga mnyama pori ni kosa la kisheria. Kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori, Sura ya 283, mkosaji anaweza kuwajibika kulipa faini kulingana na aina ya mnyama aliyegongwa. Faini zilizoainishwa hapa ni kwa baadhi tu ya wanyamapori.

TAWA inaendelea kuwakumbusha madereva wote kuongeza umakini wanapoendesha katika maeneo yanayopitiwa na wanyamapori, kuzingatia alama za tahadhari na kupunguza mwendo ili kulinda maisha ya wanyamapori na kuepuka hatua za kisheria.

Ukurasa Rasmi wa Wizara ya Utalii - Tanzania🇹🇿 Hassan Abbas

Address

Tafori Building
Morogoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Wildlife Management Authority - TAWA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share