01/05/2026
HABARI PICHA: RC MRINDOKO AWAKABIDHI VYETI NA ZAWADI YA Tsh. 500,000/= KILA MFANYAKAZI HODARI
KWA MWAKA 2025/26 KUTOKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA KATAVI
Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko leo Mei 1, 2026 amewakabidhi Vyeti na Fedha Taslimu Laki 5 kwa kila Mfanyakazi Hodari kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi.
Akikabidhi vyeti hivyo kwenye maadhimisho ya Sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani Mei 1, 2026, Mhe. Mrindoko amewapongeza Watumishi hao na Wengine walioshinda kutoka katika Taasisi mbalimbali za Serikali na kuwahimiza kuendelea kufanya kazi kwa bidii.
Waliokabidhiwa vyeti hivyo ni Dr. Omary Yusuph kutoka Idara ya Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, Mr. Othuman Chimwala kutoka Wodi ya ICU, Ms. Grace Nkorabiga kutoka Wodi ya ICU, Ms. Belinda Mollel kutoka Famasi na M. Alphonce Kalobelo kutoka Utawala.
Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi kimkoa yamefanyika katika viwanja vya Kashauriri na Mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni "Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050".