Mtwara Mikindani Manispaa

Mtwara Mikindani Manispaa Huu ni Ukurasa rasmi wa Manispaa ya Mtwara_Mikindani Kwa ajili ya kuhabarisha Matukio yote yanayofanyika ndani ya Manispaa.

FANYENI KAZI KWA MALENGO -  BI. JULIANA MANYAMA Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Manispaa ya Mtwara - Mikindani Bi...
26/01/2026

FANYENI KAZI KWA MALENGO - BI. JULIANA MANYAMA

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Manispaa ya Mtwara - Mikindani Bi. Juliana Manyama amewahimiza maafisa usafirishaji wa manispaa hiyo kufanya kazi kwa kujiwekea malengo ili kujikwamua kiuchumi.

Bi. Manyama Ameyasema hayo leo tarehe Januari 26, 2026 katika mafunzo ya Ujasiliamali kwa vikundi vya maafisa Usafirishaji ( Bodaboda) vilivyoomba mkopo katika Manispaa hiyo.

Aidha, amewasihi maafisa hao kuzingatia usalama wa abiria na wao wenyewe pamoja na kuwa na uadilifu na kutumia lugha nzuri kwa wateja wao.

Kwa upande wake, Afisa Biashara wa Manispaa hiyo Bi. Mary Mwakyosi amewataka maafisa hao kuwa waaminifu katika marejesho ya mikopo itakayotolewa na Manispaa hiyo pamoja na Kuwaasa maafisa hao kuwa na ushirikiano mzuri baina ya wao na serikali.

Sambamba na hilo, amewataka maafisa hao kujiwekeza katika kumiliki ardhi kupitia biashara yao na kuhakikisha kipato kinakuwa kikubwa kuliko matumizi.

TIMU YA MKOA YAKAGUA MIRADI YA MWENGE WA UHURU 2026!TIMU YA MKOA YA UFATILIAJI MIRADI YA MWENGE WA UHURU -2026 imefanya ...
23/01/2026

TIMU YA MKOA YAKAGUA MIRADI YA MWENGE WA UHURU 2026!

TIMU YA MKOA YA UFATILIAJI MIRADI YA MWENGE WA UHURU -2026 imefanya ziara ya kutembelea mapendekezo ya miradi mbalimbali itakayopitiwa na Mwenge WA Uhuru Mwezi Mei, ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani na kupendeleza maboresho kadhaa.

Ikiongozwa na Mratibu wa Mwenge Mkoa, Bi. Herinely Chipindula, timu ilitembelea na kutoa mapendekezo katika miradi ifuatayo: -

1) Ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi Sino
2) Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD)
3) Ujenzi wa Ofisi ya Wafanyabiashara za Mkononi (Machinga)
4) Utengenezaji wa Samani Masofa – Masofa Group Rahaleo Chini
5) Ujenzi wa Shade kwa Wafanyabiashara KIYANGU



UMEKTA WAJIPANGA KUBAINI NA KUTATUA MAPUNGUFU YA ELIMU MTWARA-MIKINDANI Umoja wa Maafisa Elimu wa Kata Manispaa ya Mtwar...
22/01/2026

UMEKTA WAJIPANGA KUBAINI NA KUTATUA MAPUNGUFU YA ELIMU MTWARA-MIKINDANI

Umoja wa Maafisa Elimu wa Kata Manispaa ya Mtwara - Mikindani (UMEKTA), wametia nia kutatua na kubaini mapungufu katika sekta ya elimu ili kuboresha ufanisi wa utoaji wa elimu katika ngazi ya kata kwa kufatilia maendeleo ya wanafunzi kwa mwaka 2026.

Maadhimio hayo yamefikiwa leo Januari 22, 2026 wakati wa Kikao cha Kwanza cha Mwaka cha Tathmini ya Taaluma kwa Maafisa Elimu Kata, kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Ufundi VETA-Mtwara.

Akizungumza katika kikao hicho Mwenyekiti wa UMEKTA, Mwl. Banezegwa Rush*ta, amewahimiza maafisa hao kuboresha maeneo mbalimbali ya taaaluma kwa kufanya majaribio ya mara kwa mara kwa wanafunzi ili kuongeza ufaulu katika masomo yao.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Umoja wa walimu wakuu wa shule za Msingi Tanzania Bara, amewataka maafisa hao kuwa na ushirikiano utakaopelekea kufikia malengo ya ufaulu wa wanafunzi kitaaluma katika manispaa hiyo.

Vilevile, kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa umoja wa wakuu wa shule za Sekondari Tanzania Bi. Hadija Mkambala ametoa wito kwa wazazi kwa kuwataka kushiriki katika kufatilia maendeleo ya watoto wao ili waweze kufaulu vizuri.

Aidha, Mwl. Mkambala amemshukuru Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Mwalimu Hassan Nyange kwa jitihada zake kubwa za kuinua elimu katika Manispaa hiyo na kuwawezesha katika miundombinu mbalimbali ikiwemo madarasa na vitabu vya masomo mbalimbali.

Ikumbukwe kuwa kikao cha UMEKTA hufanyika kila mwaka mwezi Januari na hufanya tathmini mwezi Disemba ili kuweza kufanya maboresho na kubaini mapungufu yanayojitokeza katika Sekta ya Elimu.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara, Mwalimu Hassan Nyange, anatoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tan...
22/01/2026

Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara, Mwalimu Hassan Nyange, anatoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwaajiri Watumishi wapya 105, ambao watatumika katika kuimarisha huduma za Manispaa ya Mtwara-Mikindani.

Watumishi walioajiriwa ni kutoka katika Divisheni/Vitengo vifuatavyo:

1️⃣ Elimu Sekondari - 20
2️⃣ Huduma za Afya, Lishe, na Ustawi wa Jamii - 54
3️⃣ Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu - 12
4️⃣ Kilimo, Mifugo, na Uvuvi - 08
5️⃣ Usimamizi wa Fedha - 03
6️⃣ Viwanda, Biashara, na Uwekezaji - 02
7️⃣ TEHAMA - 01
8️⃣ Maendeleo ya Miundombinu ya Vijijini na Mijini - 01
9️⃣ Tathmini na Ufuatiliaji - 01
🔟 Mipango na Uratibu - 01
1️⃣1️⃣ Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu - 02

Asante sana Mama!! 🇹🇿

20/01/2026

🎬 la Mkurugenzi wa Manispaa Mtwara-Mikindani Mwalimu Hassan Nyange, akiwapongeza Wanafunzi wa Kidato Cha pili Shule ya Sekondari Shangani kwa Kuongoza Ufaulu kwa miaka mitatu mfululizo kwa Shule za Sekondari za Kata ndani ya Manispaa.

Katika Matokeo hayo yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) hivi karibuni, Shule hiyo pia imefanikiwa kufuta kabisa Ziro, 'GPA' yake kila mwaka inapanda kwa Shule za Sekondari za Kata, kwa Manispaa na Mkoa kwa jumla

Aidha 'Division 4' zimepungua kulinganisha na shule 22 za Manispaa Mtwara-Mikindani.

"MIRADI MIZURI, ONGEZENI SPIDI' ~ KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI Kamati ya Fedha na Uongozi, Halmashauri ya Manispaa ya Mtwa...
20/01/2026

"MIRADI MIZURI, ONGEZENI SPIDI' ~ KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI 

Kamati ya Fedha na Uongozi, Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara-Mikindani imewaagiza Watendaji na wataalam wanaotekeleza Miradi ya Maendeleo kuongeza kasi katika kukamilisha miradi hiyo kwa muda uliopangwa na iweze kuleta tija kwa Walengwa.

Chini ya Mwenyekiti wake, Mhe. Said Zaid, Kamati imesema inaridhishwa na utekelezaji wa Miradi hiyo ikiksisitiza tu kuongezeke kasi zaidi ili miradi ikamilike na ianze kutumika k**a ilivyokusudiwa.

"Tunawapongezeni kwa kazi nzuri" alisisiza Mhe. Zaid katika moja ya matamko yake Leo.

Kamati hiyo imetembelea, Mradi wa Upanuzi wa Zahanati ya Chuno kuwa Kituo Cha Afya, Ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi Sino, Ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri na Ujenzi wa vyumba 02 vya madarasa Sekondari ya Naliendele.

Pia imetembelea Ujenzi wa vyumba 02 vya madarasa wa na Matundu 6 ya vyoo Shule ya Msingi Mangamba, Ujenzi wa vyumba 04 vya madarasa na Matundu 03 ya vyoo Shule ya Msingi Mlimani pamoja na Ukarabati wa Shule ya Msingi Chikongola.


20/01/2026

🎬Maneno ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara-Mikindani, Mwalimu Hassan Nyange pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Mheshimiwa Abdallah Mwaipaya katika hafla fupi ya kupokea Basi lililonunuliwa kwa Mapato ya ndani!

MD NYANGE AKABIDHI VIFAA SAIDIZI VYA KIDIGITALI KWA WALIMU WENYE ULEMAVUMkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa Mtwara-Mik...
19/01/2026

MD NYANGE AKABIDHI VIFAA SAIDIZI VYA KIDIGITALI KWA WALIMU WENYE ULEMAVU

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa Mtwara-Mikindani, Mwalimu Hassan Nyange amekabidhi vifaa vya kielimu na saidizi kwa walimu wenye ulemavu ili kuwarahisishia Utendaji kazi wao.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mwalimu Nyange aliwahimiza wanufaika kuvitunza vyema, huku akisisitiza kuwa ulemavu haupaswi kuwa kikwazo cha kufikia ndoto na malengo yao. Alieleza kuwa kuna mifano mingi ya watu wenye ulemavu walioweza kufanikiwa na kuacha alama kubwa duniani, hivyo aliwataka walimu hao kuendelea kujituma na kufanya kazi kwa bidii ili kuleta matokeo chanya katika sekta ya elimu.

Vifaa hivyo kutoka Wizara ya Elimu, vimegawiwa Leo katika hafla fupi iliyofanyika katika Shule ya  Mtwara Ufundi ni pamoja na kompyuta mpakato (laptops) mbili (2) kwa walimu wawili viziwi, kofia moja (1), kifaa kimoja cha kurekodi sauti cha kidigitali (Digital Voice Recorder), mafuta maalumu ya kujikinga na jua (sunscreen lotion) kopo 37 kwa mwalimu mmoja mwenye ualbino, na tablet moja (1).

Ikumbukwe kuwa mapema mwezi huu jijini Dodoma, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mheshimiwa Profesa Adolf Mkenda, alizindua zoezi la ugawaji wa vifaa vya kielimu na vya saidizi kwa walimu, wakufunzi na walimu tarajali wenye ulemavu vyenye thamani ya shilingi bilioni 5.3.

Vifaa hivyo vinasambazwa katika shule za msingi 309, shule za sekondari 629 na vyuo vya ualimu 10, kwa ajili ya kuwawezesha walimu, wakufunzi na walimu tarajali wenye mahitaji maalumu katika halmashauri zote 184 nchini.

KAMATI YA MIPANGOMIJI NA MAZINGIRA YATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO MTWARA-MIKINDANI Kamati ya Mipangomiji na Mazingira le...
19/01/2026

KAMATI YA MIPANGOMIJI NA MAZINGIRA YATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO MTWARA-MIKINDANI

Kamati ya Mipangomiji na Mazingira leo 19/01/2026 imefanya Ziara ya kutembelea maeneo mbalimbali inayotekelezwa Miradi ya Maendeleo ndani ya Manispaa ya Mtwara-Mikindani.

Ikiongozwa na Mwenyekiti wake M***a Namtema, Kamati imetembelea Upanuzi wa Kituo Cha Afya Mikindani, Eneo la Litingi Kiwanja Na. 1 -149, Soko la Mitengo, pamoja na Upanuzi wa Zahanati ya Magomeni.

Mingine ni Upanuzi wa Zahanati ya Chuno kuwa Kituo Cha Afya, na Kutembelea eneo la Wazi lililoko Coco Beach!

19/01/2026

🎬Tazama jinsi Basi la Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara–Mikindani, aina ya TATA Marcopolo, lililonunuliwa kupitia mapato ya ndani katika Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026, likiwa safarini kuingia Mtwara likitokea Jijini Dar es Salaam....

MTWARA–MIKINDANI YANUNUA BASI LA WATUMISHI KWA MAPATO YA NDANI SHILINGI MILIONI 178Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara–Mik...
19/01/2026

MTWARA–MIKINDANI YANUNUA BASI LA WATUMISHI KWA MAPATO YA NDANI SHILINGI MILIONI 178

Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara–Mikindani, kupitia mapato yake ya ndani katika bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026, imenunua basi jipya aina ya TATA Marcopolo lenye thamani ya shilingi milioni mia moja sabini na nane (178,000,000).

Basi hilo litatumika kwa usafirishaji wa Waheshimiwa Madiwani pamoja na watumishi wa Manispaa katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kikazi na kiofisi.

Ununuzi wa basi hilo unatarajiwa kupunguza gharama za uendeshaji wa ofisi na usafiri kwa kiasi cha shilingi milioni sitini hadi sabini kwa mwaka.

Uzinduzi wa basi hilo umefanyika leo, Januari 19, 2025, ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Mhe. Abdallah Mwaipaya. Hafla hiyo ilishuhudiwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mtwara–Mikindani, Mhe. Mohamedi Zaid, Waheshimiwa Madiwani pamoja na watumishi wa Manispaa wakiongozwa na Mkurugenzi wa Manispaa, Mwalimu Hassan Nyange.

Taarifa zaidi kuhusu Basi hili zitaendelea kujijia kupitia ukurasa huu...

Timu ya Maafisa Watendaji wa Halmashauri ya Manispaa Mtwara-Mikindani (MTWARA MC) imekataa kabisa urafiki na Kuinyeshea ...
17/01/2026

Timu ya Maafisa Watendaji wa Halmashauri ya Manispaa Mtwara-Mikindani (MTWARA MC) imekataa kabisa urafiki na Kuinyeshea Mvua ya Magoli 4 kwa Sifuri Timu ya Maafisa Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara (MTWARA DC), Katika Mchezo wa Kirafiki uliomalizika jioni hii katika Viwanja vya Chuo Cha Ualimu - Mwasandube.

Mchezo huo ulioshuhudiwa na Wakurugenzi wa Halmashauri zote mbili, ulikua ni wa kuvutia huku MTWARA MC ikitawala asilimia kubwa ya Mchezo huo na kuwafanya wenzao wa MTWARA DC wakitamani Mpira uishe mapema kutokana na kuzidiwa kila Idara.

Akizungumza baada ya Mchezo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa Mtwara-Mikindani, Mwalimu Hassan Nyange aliwataka wachezaji wote kuendelea kujifua zaidi licha ya matokeo hayo, na akaeleza kiu yake ya kutengeneza Timu ya Wilaya ya Mtwara itakayoundwa na wachezaji mahiri kutoka Halmashauri zote 3 za Wilaya ya Mtwara..



ni Umoja, Afya na Mshik**ano

Address

Mikindani
Mtwara

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mtwara Mikindani Manispaa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share