Cashewnut Board Of Tanzania

Cashewnut Board Of Tanzania Official page Of Cashewnut Board Of Tanzania

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Francis Alfred, ameeleza kuridhishwa na kazi inayofanywa na timu ya m...
03/09/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Francis Alfred, ameeleza kuridhishwa na kazi inayofanywa na timu ya mpira wa wavu ya Korosho Queens, baada ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa Kombe la Muungano 2026 lililofanyika Zanzibar.

Akizungumza Septemba 3, 2026, Mtwara, wakati timu hiyo ilipomkabidhi kombe hilo, ameitaka Korosho Queens kuendelea kuwa balozi wa tasnia ya korosho kwa kuhamasisha ulaji wa korosho, ubanguaji na matumizi ya bidhaa zitokanazo na zao hilo.

Kwa upande wake, Meneja wa timu, Hussein Kibombwe, amesema kauli mbiu ya “Kula Korosho kwa Afya” imeendelea kuleta matokeo chanya, huku Korosho Queens ikiendelea kutumia michezo na matukio mbalimbali kuitangaza tasnia ya korosho na kuhamasisha jamii kuhusu faida za ulaji wa korosho.

,
.cashew.go.tz

Tangazo la Udhibiti Ubora wa Korosho msimu wa 2026/2027.
01/09/2026

Tangazo la Udhibiti Ubora wa Korosho msimu wa 2026/2027.

Picha na matukio mbalimbali katika Mkutano Mkuu wa Wadau wa Tasnia ya Korosho uliofanyika mkoani Morogoro, Agosti 27, 20...
28/08/2026

Picha na matukio mbalimbali katika Mkutano Mkuu wa Wadau wa Tasnia ya Korosho uliofanyika mkoani Morogoro, Agosti 27, 2026, ambapo wadau walikutana kujadili changamoto, fursa na mikakati ya kuendeleza na kuimarisha tasnia ya korosho nchini.

26/08/2026

Karibu kwenye Mkutano Mkuu wa Wadau wa Tasnia ya Korosho 2026.

Tunawatakia heri ya sikukuu ya Mawlid ya Mtume Muhammad (S.A.W).
25/08/2026

Tunawatakia heri ya sikukuu ya Mawlid ya Mtume Muhammad (S.A.W).

Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) imefanya kikao cha kujadili na kupitia marekebisho ya Sheria ya Tasnia ya Korosho, hatua ...
24/08/2026

Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) imefanya kikao cha kujadili na kupitia marekebisho ya Sheria ya Tasnia ya Korosho, hatua inayolenga kuboresha na kurekebisha sheria ya Tasnia ya Korosho ili kuendana na Uhalisia wa sasa pamoja na kuimarisha mfumo wa kisheria katika usimamizi wa Tasnia ya Korosho nchini.

Kikao hicho kimewakutanisha wajumbe wa Menejimenti ya Bodi ya Korosho Tanzania pamoja na Mawakili wa Serikali kutoka Taasisi na Halmashauri mbalimbali huku majadiliano yakilenga kupitia kwa kina maeneo mbalimbali ya sheria yanayohitaji kufanyiwa marekebisho ili yaendane na mahitaji na mabadiliko ya sasa katika uzalishaji, uongezaji thamani, biashara na maendeleo ya tasnia ya korosho.

Aidha lengo kuu ni kufanya maboresho katika vifungu na masharti ya sheria iliyopo ili kuifanya iendane na mazingira, mahitaji na changamoto za sasa za tasnia, hatua inayotarajiwa kuimarisha usimamizi na uratibu wa shughuli mbalimbali kuanzia Uzalishaji, Ubora, Ubanguaji, Uhifadhi na Masoko.

Kikao hicho kimefanyika agosti 24, 2026 katika ukumbi wa hoteli ya Morena mkoani Morogoro kikiongozwa na Ndg. Gilbert Rweyemam, Afisa Sheria kutoka Bodi ya Korosho Tanzania.

Unaweza pia kutufuatilia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, Instagram na Threads ni , Facebook, LinkedIn na X ni Board of Tanzania, Youtube ni Boardtz, Tovuti ni www.cashew.go.tz, email ni [email protected] na simu ni 0800 112 159 bure.

TANGAZO LA AJIRA YA MUDA
19/08/2026

TANGAZO LA AJIRA YA MUDA

KOROSHO MARATHON 2026 MAMBO NI🔥🔥🔥🔥🔥Ni tarehe 28th November, 2026 katika viwanja vya MILLENIUM BEACH, MTWARA.Jisajili sas...
18/08/2026

KOROSHO MARATHON 2026 MAMBO NI🔥🔥🔥🔥🔥

Ni tarehe 28th November, 2026 katika viwanja vya MILLENIUM BEACH, MTWARA.

Jisajili sasa kwa gharama ya TZS 35,000 kupitia Lipa Namba ya YAS 22633963 na unaweza kushiriki mbio uipendayo!
1. Kids Run 2.5Km
2. ⁠Fun Run 5Km
3. ⁠Corporate Run 10Km
4. ⁠Half Marathon 21.1Km

Washiriki wote (Wakimbiaji na wadhamini) mnakaribishwa kushiriki nasi, wasiliana nasi kwa namba za Simu 0711263429 / 0765410253.

RUN FOR HEALTH
RUN FOR COMMUNITY,
RUN FOR KOROSHO.

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Francis Alfred, Agosti 15, 2026 alitembelea Kijiji cha Njenga, Kata y...
16/08/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Francis Alfred, Agosti 15, 2026 alitembelea Kijiji cha Njenga, Kata ya Ndanda, Wilaya ya Masasi, Mkoani Mtwara, na kutoa pole kwa familia ya marehemu Fatuma Mkopoka, mkulima wa korosho aliyefariki dunia baada ya kupata ajali ya moto wakati akisafisha shamba lake la korosho.

Katika ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu aliambatana na Afisa Kilimo wa CBT kutoka Mtwara, Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Mwenyekiti wa Kijiji cha Njenga, Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Njenga, Afisa Kilimo wa Halmashauri ya Masasi anayehudumia kata ya Ndanda pamoja na Afisa Kilimo wa mpango wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT).

Unaweza pia kutufuatilia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, Instagram na Threads ni , Facebook, LinkedIn na X ni Cashewnut Board of Tanzania, Youtube ni Cashewnut Boardtz na Tovuti ni www.cashew.go.tz au email [email protected] na simu ni 0800 112 159 bure.

16/08/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) Francis Alfred, agosti 15, 2026 ametembelea na kutoa pole kwa familia ya marehemu Fatuma Mkopoka, mkulima wa korosho aliyefariki dunia baada ya kupatwa na ajali ya moto wakati akisafisha shamba lake la korosho katika Kata ya Ndanda, Wilaya ya Masasi, Mkoa wa Mtwara.

Katika ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu alifika katika Kijiji cha Njenga, ambako marehemu alikuwa akiishi, kwa ajili ya kuwafariji ndugu, jamaa na familia ya marehemu kufuatia msiba huo.

Unaweza kushiriki maoni yako kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, Instagram na Threads ni , Facebook, LinkedIn na X ni Cashewnut Board of Tanzania, Youtube ni Cashewnut Boardtz na Tovuti ni www.cashew.go.tz au email [email protected] na simu ni 0800 112 159 bure.

Address

Tanu Road
Mtwara

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00

Telephone

+255232333536

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Cashewnut Board Of Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Cashewnut Board Of Tanzania:

Shortcuts

Share