Regional Commissioner's Office-Mara

Regional Commissioner's Office-Mara Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Regional Commissioner's Office-Mara, Government Organization, Musoma.

Ukurasa huu wa Facebook ya Mkoa wa Mara ni maalumu katika kuweka matukio mbalimbali yanayofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara katika kutekeleza majukumu yake.

MWANG’ONDA AWAPONGEZA WANANCHI WA NTAGACHA, TARIME Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2026 Ndugu Wazo Mic...
04/08/2026

MWANG’ONDA AWAPONGEZA WANANCHI WA NTAGACHA, TARIME
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2026 Ndugu Wazo Michael Mwang’onda leo amewapongeza wananchi wa Kijiji cha Ntagacha kwa kujitolea shilingi 31,863,800.00 kwa ajili ya kujenga nyumba ya walimu katika Shule ya Msingi Ntagacha, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.
Akizungumza wakati wa kuweka jiwe la msingi katika ujenzi huo, Ndugu Mwang’onda amewapongeza wananchi kwa juhudi zao na kuongeza kuwa kwa kutambua juhudi hizo, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime imeahidi kuongeza shilingi milioni 10 ili kukamilisha ujenzi wa nyumba hiyo ambayo kwa sasa ujenzi wake upo katika hatua ya kupiga lipu.
“Ninawapongeza sana wananchi kwa juhudi mlizozifanya katika kuanzisha ujenzi wa nyumba hii hadi hatua ilipofikia, Mwenge wa Uhuru unatambua juhudi zenu za kujiletea maendeleo katika kijiji chenu” amesema Ndugu Mwang’onda.
Ndugu Mwang’onda amewataka wahandisi wa Halmashauri kusimamia vizuri ujenzi unaofanywa kwa nguvu za wananchi katika maeneo yao ili kupata majengo bora yanayoakisi gharama iliyotumika na kwa kuwa majengo hayo baada ya kukamilika ni mali ya Serikali hivyo yanapaswa kuzingatia michoro na viwango vya utekelezaji wa mradi wa Serikali.
Aidha, akizungumza katika maeneo tofauti tofauti, Ndugu Mwang’onda amewahamasisha wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kulinda amani, utulivu na mshik**ano wa kitaifa katika maeneo yao na kuwaeleza kuwa bila ya amani hamna maendeleo ya mtu binafsi, taasisi wala nchi yanayoweza kufanyika.
Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime umetembelea miradi ya maendeleo saba yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 10 ambayo imejengwa kwa fedha za wananchi, Serikali Kuu, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na wahisani wa maendeleo.
Mwenge wa Uhuru umetembelea kikundi cha vijana Nyamongo Construction Group na ukiwa hapo umepokea taarifa, kukagua mradi na umezindua gari la mizigo la kikundi hicho; umezindua Hoteli ya Silver Spring, umezindua madarasa mawili katika shule ya Msingi Matongo, umezindua daraja la Nyangoto-Matongo na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa maji Genkuru na Msege miradi yote ikiwa katika eneo la Nyamongo.
Aidha, Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi katika mradi wa jengo la Mama na Mtoto katika Kituo cha Afya Magoto na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa nyumba ya watumishi wa Shule ya Msingi Ntagacha.
Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Shule ya Sekondari ya Matongo umetembelea na kuzindua Klabu ya Mazingira na kupanda miti ya matunda na kutembelea Klabu ya Rushwa katika Shule ya Sekondari ya Matongo.
Mkesha wa Mwenge wa Uhuru unaendelea katika Uwanja wa Mwenge Sirari, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na kesho Mwenge wa Uhuru utakabidhiwa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime kuendelea na mbio zake.

MWENGE WA UHURU WATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 1.592 SERENGETI Mbio za Mwenge wa Uhuru zimeingia katika Halmashauri ya Wil...
03/08/2026

MWENGE WA UHURU WATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 1.592 SERENGETI
Mbio za Mwenge wa Uhuru zimeingia katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ambapo umekimbizwa umbali wa kilomita 136 na kutembelea miradi ya maendeleo saba yenye thamani ya shilingi 1,591,775,037.13.
Akizungumza wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Anjelina Marco Lubella amesema kati ya fedha hizo shilingi 132,141,260.00 ni mchango wa Halmashauri, shilingi 1,283,750,383.13 ni mchango wa Serikali Kuu, shilingi 37,335,000.00 mchango wa wananchi na shilingi 137,548,394.00 mchango wa wahisani.
Mwenge wa Uhuru umezindua mradi wa maji wa Vijiji vya Nyansurura, Manyata na Kitembere wenye gharama ya shilingi 569,952,383.13; umetembelea mradi wa kikundi cha wachoraji Mugumu wenye thamani ya shilingi milioni 10; umeweka jiwe la msingi mradi wa Barabara ya Uhuru wenye thamani ya shilingi 463,798,000.00.
Mwenge wa Uhuru umezindua mradi wa ofisi ya Kata ya Morotonga wenye thamani ya shilingi 86,760,260.00; umezindua mradi wa Serengeti Waste Recycling Network wenye thamani ya shilingi 137,548,394.00, umetembelea mradi wa Shule ya Sekondari ya SIA na kuweka jiwe la msingi katika Kituo cha Afya Sedeco.
Katika maeneo mbalimbali Mwenge wa uhuru umepokea taarifa za mapambano dhidi ya dawa za kulevya, mapambano dhidi ya malaria, mapambano dhidi ya UKIMWI, taarifa ya lishe na kunzindua klabu ya rushwa katika Shule ya Sekondari ya Serengeti.
Mkesha wa Mwenge wa Uhuru unafanyika katika uwanja wa Right to Play na baada ya hapo kesho tarehe 04 Agosti, 2026 Mwenge wa Uhuru utakabidhiwa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kwa ajili ya kuendelea na mbio zake.
Kauli Mbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka 2026 ni “Tanzania ni Yetu Sote, Tushik**ane kwa Pamoja kuleta Maendeleo”

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA AWATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA Mwenge wa Uhuru leo tarehe 01 Agosti, 2026 umefanya...
03/08/2026

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA AWATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA
Mwenge wa Uhuru leo tarehe 01 Agosti, 2026 umefanya mbio zake katika Halmashauri ya Mji wa Bunda ambapo kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndugu Wazo Michael Mwang’onda amewataka vijana kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi zinazotolewa na Serikali na wadau wengine ili kujiletea maendeleo yao.
Akizungumza wakati Mwenge wa Uhuru ulipotembelea kikundi cha Vijana cha Nyota Bora, Ndugu Mwang’onda amesema kwa sasa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka dhamira ya dhati ya kuwainua wananchi wake kiuchumi.
“Kwa sasa Serikali imeweka fursa ya mikopo ya Halmashauri ambapo vijana wanapata asilimia 4 ya mapato ya ndani ya Halmashauri na vijana pia wamepewa fursa ya kunufaika na zabuni zinazotolewa na makundi maalum katika jamii” amesema Ndugu Mwang’onda.
Ndugu Mwang’onda amewataka vijana kuchangamkia fursa mbalimbali zinazotolewa katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi ili kuweza kuboresha maisha yao na familia yao na kuwasisitiza kuwa wakijipanga vizuri watafanikiwa katika maisha.
Akiwa katika kikundi hicho, Ndugu Mwang’onda amewapongeza vijana ahao kwa kazi kubwa wanayoifanya na uaminifu waliouonyesha na kuweza kuaminiwa na Halmashauri kupata mikopo ya vijana yenye ambao unabadilisha maisha yao.
Ndugu Mwang’onda amewataka vijana hao kurejesha mkopo huo kwa Halmashauri kwa wakati ili waweze kujenga uaminifu wa kukopesheka tena baadae na marejesho hayo yawasaidie vijana wengine waweze kupata mikopo kubadilisha maisha yao.
Hata hivyo amewataka vijana hao kujiunga na mfumo wa manunuzi ya umma (NEST) na kuutumia mfumo huo kunufaika na zabuni zinazotolewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Serikali ili kupanua zaidi shughuli zao za uchomeleaji.
Ndugu Mwang’onda amewataka vijana hao kufikiria pia mradi mwingine ambao wanaweza kuufanya katika eneo lao ili kujiongezea kipato ikiwemo kutumia bajaji ya mizigo kibiashara, kuanzisha duka la vifaa vya bajaji, duka la mahitaji ya kawaida na biashara nyingine watakayoona inafaa.
Katika maeneo tofauti tofauti Ndugu Mwang’onda amewahamasisha wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda kulinda amani na utulivu uliopo ili kuweza kufanya maendeleo binafsi na ya Taifa na kuwaasa kuwa pasipo amani hamna shughuli yoyote itakayoweza kufanyika.
Ukiwa katika Halmashauri ya Mji wa Bunda, Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa ukumbi wa Hango Garden, umezindua mradi wa kisima cha maji safi cha Changuge, umezindua barabara ya Maduka Saba-Ikizu, umezindua madarasa mawili na Klabu ya wapinga rushwa ya Shule ya Sekondari Manyamanyama.
Aidha, Mwenge wa Uhuru umezindua ofisi ya Mtaa wa Bitaraguru, umezindua ujenzi wa nyumba ya watumishi wa Hospitaji ya Halmashauri ya Mji wa Bunda na kutembelea kikundi cha vijana cha Nyota Njema.
Mbio za Mwenge wa Uhuru zimehitimishwa kwa mkesha unaoendelea katika Uwanja wa Shule ya Msingi Bunda Mjini na kesho Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kuendelea na mbio zake katika Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ambapo pamoja na mambo mengine utawasha Mwenge wa Mwitongo nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mwitongo, Butiama.

MWANG’ONDA AWASHA MWENGE WA MWITONGO Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndugu Wazo Michael Mwang’onda leo tareh...
03/08/2026

MWANG’ONDA AWASHA MWENGE WA MWITONGO
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndugu Wazo Michael Mwang’onda leo tarehe 02 Agosti, 2026 ameongoza hafla ya Mwenge wa Uhuru kuwasha Mwenge wa Mwitongo nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Butiama.
Akizungumza katika maeneo tofauti tofauti, Ndugu Mwang’onda ameongelea kufurahishwa kwake na mambo aliyojifunza Butiama na kujionea kuhusu Baba wa Taifa na historia ya Tanzania.
Aidha, ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kufanikiwa kuunga vikundi 161 katika Mfumo wa Manunuzi Serikalini (NEST) na kuwataka viongozi kuhakikisha kuwa vikundi hivyo vinapata kazi mbalimbali za Serikali zinazotangazwa katika maeneo yao.
Mwenge wa Uhuru umeingia Mwitongo na kupokelewa na viongozi, wanafamilia ya Mwalimu Nyerere na wananchi mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi na kiongozi wa familia ya Mwalimu Nyerere Chifu Japhet Wanzagi.
Mwenge wa Uhuru ukiwa katika eneo hilo, viongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa walipata fursa ya kupata taarifa na historia kuhusiana na Mwenge wa Uhuru, Mwalimu Nyerere na historia ya Tanzania; kuzungumza na wanafamilia ya Mwalimu Nyerere na kuzuru kaburi la Baba wa Taifa.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Mtambi kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Mara amewakaribisha viongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa nyumbani kwa Baba wa Taifa.
Mhe. Mtambi amesema kuwa Mwitongo ndio nyumbani halisi kwa Mwenge wa Uhuru kutokana na ukweli kuwa hapo ni nyumbani alipozaliwa na kuzikwa muasisi wa Mwenge huo.
Kwa upande wake, Chifu Japhet Wanzagi amesema kuwa kwa kuwa Mwalimu Nyerere ni Baba wa Taifa, Mwitongo ni nyumbani kwa watanzania wote wanaopenda amani, umoja na maendeleo.
Chifu Wanzagi amewakaribisha Watanzania wote kutembelea sehemu hiyo ili kujifunza historia, mambo aliyoyafanya na kuyaamini na maisha ya Mwalimu Nyerere katika Makumbusho ya Mwalimu Nyerere Butiama na nyumbani kwa Baba wa Taifa.
Mwenge wa Uhuru ukiwa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama pia umetembelea miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya bilioni 2.
Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Butiama umeweka jiwe la msingi Kituo cha Afya cha Kukilango, umezindua kituo cha mafuta cha GBP, umeweka jiwe la Msingi mradi vyumba vitatu vya maabara katika Shule ya Sekondari ya Mmazami.
Aidha, Mwenge wa Uhuru umetembelea kikundi cha Vijana cha Hope Welding, umeweka jiwe la msingi ujenzi wa Shule ya Sekondari Manyawa, umezindua mradi wa mtandao wa maji katika kijiji cha Nyambili na kuzindua daraja la mawe la Mang’atika.
Mkesha wa Mwenge umefanyika katika eneo la Sirorisimba na baada ya hapo Mwenge wa Uhuru utapelekwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kuendelea na mbio zake.

MWENGE WA UHURU WAANZA MBIO ZAKE MKOA WA MARA Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 01 Agosti,...
03/08/2026

MWENGE WA UHURU WAANZA MBIO ZAKE MKOA WA MARA
Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 01 Agosti, 2026 amewaongoza viongozi na wananchi wa Mkoa wa Mara katika mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru yaliyofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Balili, Halmashauri ya Mji wa Bunda.
Akizungumza baada ya kupokea Mbio za Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Annamringi Macha, Mhe. Mtambi amesema ukiwa katika Mkoa wa Mara Mwenge wa Uhuru utakimbizwa kilomita 966 na utatembelea miradi 63 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 174,806,938,614.49.
“Miradi hiyo imetekelezwa kwa nguvu za wananchi shilingi 12,228,422,300.00; mchango wa Mamlaka za Serikali za Mitaa 2,281,204,818.32; mchango wa Serikali kuu 145,478,997,345.17; na mchango wa wahisani 14,817,694,151.00” amesema Mhe. Mtambi na kuongeza kuwa miradi hiyo ipo katika sekta za Elimu, Afya, Maji, Ujenzi, Kilimo, Mifugo, Mazingira, Ustawi wa Jamii, Viwanda na Biashara.
Mhe. Mtambi amewashukuru viongozi, watumishi, wadau na wananchi wote waliohusika kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha maandalizi ya mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 katika Mkoa wa Mara.
Kanali Mtambi amesema, Mbio za Mwenge wa Uhuru leo zitaanza Halmashauri ya Mji wa Bunda (01/8/2026), Halmashauri ya Wilaya ya Butiama (02/8/2026), Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti (03/8/2026), Halmashauri ya Wilaya ya Tarime (04/8/2026), Halmashauri ya Mji wa Tarime (05/8/2026) na Halmashauri ya Wilaya ya Rorya (06/8/2026).
Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa Mwenge wa Uhuru utakimbizwa Halmashauri ya Manispaa ya Musoma (07/8/2026), Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (08/8/2026) na kuhitimishwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda (09/8/2026) na baadae kukabidhiwa katika Mkoa wa Mwanza makabidhiano yatakayofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Muluseni, Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe tarehe 10 Agosti, 2026.
Ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 unaolenga katika ujenzi wa Amani, Umoja na Mshik**ano wa Kitaifa chini ya kauli mbiu isemayo: “Tanzania ni yetu Sote, Tushik**ane pamoja kuleta Maendeleo”.

MWENGE KUTEMBELEA MIRADI YA BILIONI 174 MARA Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongea na Waandi...
31/07/2026

MWENGE KUTEMBELEA MIRADI YA BILIONI 174 MARA
Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongea na Waandishi wa Habari kuhusiana na mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2026 na kueleleza kuwa Mwenge wa Uhuru utatembelea miradi 63 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 174,806,938,614.49.
Akizungumza katika mkutano huo, Mhe. Mtambi amesema ukiwa katika Mkoa wa Mara, Mwenge wa Uhuru utatembelea Wilaya sita na Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara na utakimbizwa umbali wa Kilomita 966 kuanzia tarehe 01 Agosti, 2026 hadi tarehe 09 Agosti, 2026.
“Miradi hiyo imetekelezwa kwa nguvu za wananchi shilingi 12,228,422,300.00; mchango wa Mamlaka za Serikali za Mitaa 2,281,204,818.32; mchango wa Serikali kuu 145,478,997,345.17; na mchango wa wahisani 14,817,694,151.00” amesema Mhe. Mtambi na kuongeza kuwa miradi hiyo ipo katika sekta za Elimu, Afya, Maji, Ujenzi, Kilimo, Mifugo, Mazingira, Ustawi wa Jamii, Viwanda na Biashara.
Mhe. Mtambi amesema Mwenge wa Uhuru utapokelewa tarehe 01 Agosti, 2026 katika uwanja wa Shule ya Msingi Balili, Halmashauri ya Mji wa Bunda na baada ya hapo utakimbizwa katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.
Mhe. Mtambi amesema maandalizi ya kupokea Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Mara yamekamilika kwa asilimia 100 na kwa sasa Mkoa wa mara upo tayari kwa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2026.
Mhe. Mtambi amewashukuru viongozi, watumishi, wadau na wananchi wote waliohusika kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha maandalizi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 katika Mkoa wa Mara.
Kanali Mtambi amesema, Mbio za Mwenge wa Uhuru zinatarajiwa kukimbizwa Halmashauri ya Mji wa Bunda (01/8/2026), Halmashauri ya Wilaya ya Butiama (02/8/2026), Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti (03/8/2026), Halmashauri ya Wilaya ya Tarime (04/8/2026), Halmashauri ya Mji wa Tarime (05/8/2026) na Halmashauri ya Wilaya ya Rorya (06/8/2026).
Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa Mwenge wa Uhuru utakimbizwa Halmashauri ya Manispaa ya Musoma (07/8/2026), Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (08/8/2026) na kuhitimishwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda (09/8/2026) na baadae kukabidhiwa Mkoa wa Mwanza tarehe 10 Agosti, 2026.
Ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 unaolenga katika ujenzi wa Amani, Umoja na Mshik**ano wa Kitaifa chini ya kauli mbiu isemayo: “Tanzania ni yetu Sote, Tushik**ane pamoja kuleta Maendeleo”.

MTAMBI: WANANCHI MARA WAMEACHANA NA KILIMO CHA BANGI  Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amempokea...
23/07/2026

MTAMBI: WANANCHI MARA WAMEACHANA NA KILIMO CHA BANGI
Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amempokea na kuzungumza na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Ndugu Aretas James Lyimo ambapo amesema kuwa kuna mabadiliko makubwa kwa wananchi wa Mkoa wa Mara kuchangamkia fursa za maendeleo zilizopo na kuachana na kilimo na biashara ya dawa za kulevya.
“Kwa sasa wananchi wanajishughulisha zaidi na shughuli za kuwaletea maendeleo endelevu ikiwemo uchimbaji wa madini, uvuvi, ufugaji wa samamki kwenye vizimba, kilimo na shughuli nyingine halali na hawahangaiki tena na kilimo cha bangi k**a ilivyokuwa hapo awali” amesema Mhe. Mtambi.
Mhe. Mtambi amesema wananchi wengi wameendelea kubadilika kwa kiwango kikubwa kutokana na ushirikiano uliopo kati ya Serikali na wananchi katika kupambana na kilimo, biashara na matumizi ya dawa za kulevya hususan bangi.
Kanali Mtambi amesema baada ya kudhibiti kilimo na biashara za dawa za kulevya matukio ya uhalifu katika Mkoa wa Mara kwa sasa yamepungua kwa kiasi kikubwa na kuongeza kuwa mafanikio haya ni matokeo ya ushirikiano mzuri kati ya Serikali na wananchi.
Kwa upande wake, Kwa upande wake, Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Ndugu Aretas James Lyimo amesema mafanikio yaliyopatikana katika Mkoa wa Mara yanadhihirisha ushirikiano mzuri uliopo baina ya Mamlaka hiyo, viongozi na wananchi wa Mkoa wa Mara.
Akizungumza katika tukio hilo, Ndugu Lyimo amesema kwa sasa takribani asilimia 80 ya wananchi wa Mkoa wa Mara wameachana na kilimo na biashara ya bangi kutokana na ushirikiano mkubwa kati ya DCEA, viongozi na wananchi wa Mkoa wa Mara.
“Hapo zamani ilikuwa ni jambo la kawaida kukuta mashamba ya mahindi au mazao mengine yakiwa na bangi katika Mkoa wa Mara lakini kwa sasa kuna mabadiliko makubwa sana” amesema Ndugu Lyimo.
Ndugu Lyimo ameshukuru ushirikiano unaoendelea kutolewa kwa Mamlaka hiyo na viongozi wa Mkoa wa Mara katika operesheni mbalimbali za kudhibiti dawa za kulevya zinazofanyika katika Mkoa huo jambo ambalo amesema limesaidia kupungua athari za madawa hayo kwa maendeleo ya Taifa na hususan kwa nguvukazi ya vijana na usalama wa rasilimali za nchi.
Ndugu Lyimo amesema baadhi ya mataifa au makundi yenye maslahi hasi yanaweza kutumia dawa za kulevya k**a njia ya kudhoofisha nguvu kazi ya taifa na kupunguza uzalishaji na kuongeza kuwa k**a vijana wengi watakuwa wameathirika na dawa za kulevya inaweza kuhatarisha maendeleo na usalama wa Taifa.

AGIZO LA RC LATEKELEZWA: FAMILIA YA RUHUMBIKA KASANJE YALIPWA FIDIA Familia ya Ndugu Ruhumbika Machumu Kasanje, mkazi wa...
22/07/2026

AGIZO LA RC LATEKELEZWA: FAMILIA YA RUHUMBIKA KASANJE YALIPWA FIDIA
Familia ya Ndugu Ruhumbika Machumu Kasanje, mkazi wa Kijiji cha Chirorwe aliyekuwa anaidai fidia Kampuni ya Wakazi Mining Limited imelipwa kufuatia maelekezo ya Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi aliyoyatoa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho jana tarehe 21 Julai, 2026.
Akizungumza leo tarehe 22 Julai, 2025 baada ya familia hiyo kulipwa fidia na kuhama katika eneo hilo, Mhe. Mtambi amepongeza hatua hiyo kwa kuwa inamaliza mgogoro uliodumu kwa muda mrefu na kuyaondoa maisha ya familia hiyo katika hatari za kiusalama baada ya baadhi ya watu waliokuwa wamepata ajira kwenye mgodi huo kuifanyia vurugu za kuharibu mazao ya familia hiyo baada ya mgodi huo kufungwa.
“Kulipwa kwa fidia hiyo kunatuwezesha kuufungua tena mgodi huo uendelee na shughuli zake za kawaida za uchimbaji wa madini ambapo watu zaidi ya 400 wamepata ajira na maisha yao yanategemea mgodi huo” amesema Mhe. Mtambi.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara, Mhe. Mtambi alitoa saa 24 kwa mwananchi huyo kulipwa fidia ya ardhi kupisha shughuli za uchimbaji wa madini katika eneo hilo na kuitaka kampuni hiyo kulipa fedha za usumbufu kwa familia hiyo pamoja na kodi ya miezi sita kwa ajili ya familia hiyo wakati familia hiyo inaendelea kujenga makazi ya kudumu.
Awali, familia ya Sanje ilitoa malalamiko kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba tarehe 04 Julai, 2026 katika mkutano wa hadhara uliofanyika Suguti, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, kuomba kulipwa fidia kutokana na shughuli za uchimbaji kufanyika karibu na makazi yao na kuwasababishia usumbufu unaotokana na kelele na kurushiwa mawe katika makazi yao.
Akizungumza katika mkutano huo, Waziri Mkuu alimwagiza Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara kuisikiliza kero ya familia hiyo na kutoa mrejesho Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na kuutaka Mkoa wa Mara kuhakikisha mgogoro huo unatafutiwa ufumbuzi wa kudumu na kusitisha shughuli zote za uchimbaji wa madini hadi mgogoro huo utakapotatuliwa.
Baada ya kupokea mrejesho kutokana kwa Afisa Madini, Kamati ya Usalama ya Mkoa imesikiliza pande zote mbili katika mgogoro huo na Mkuu wa Mkoa kuagiza familia hiyo ilipwe fidia ndani ya saa 24 ili kulinda usalama wa familia hiyo na kuhakikisha shughuli za uchimbaji madini haziathiri maisha ya wananchi.
Familia hiyo leo imelipwa shilingi milioni 40 k**a fidia na shilingi milioni 3 kwa ajili ya usumbufu na kodi ya miezi sita kwa ajili ya kuihifadhi familia hiyo wakati inaendelea kutafuta makazi ya kudumu na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma imeisaidia familia hiyo kuhama eneo hilo kwenda kwenye makazi ya muda wakati ikijipanga kupata makazi ya kudumu.
Akizungumzia suala hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Ndugu Msongera Parela amesema tayari familia hiyo imeshapokea malipo ya fidia na wameishukuru Serikali kwa kufanikisha kulipwa kwa fidia hiyo ambayo ilisababisha mgogoro uliodumu kwa muda mrefu.
Ndugu Parela amesema baada ya kupokea fidia hiyo, tayari familia hiyo imeshahama katika eneo hilo na kampuni ya Wakazi Mining Limited ipo huru kuendelea na shughuli za uchimbaji wa madini katika eneo hilo bila kuathiri mtu yoyote.

RC AIPONGEZA BENKI YA CRDB KWA KUCHOCHEA MAENDELEO YA WANANCHI  Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo...
22/07/2026

RC AIPONGEZA BENKI YA CRDB KWA KUCHOCHEA MAENDELEO YA WANANCHI
Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 22 Julai, 2026 amewapokea na kuzungumza na viongozi wa Benki ya CRDB wakiongozwa na Meneja Mwandamizi wa Biashara za Serikali za Mitaa Ndugu Faraja Kaziulaya na kuipongeza benki hiyo kwa kutoa huduma za kifedha zinazochochea maendeleo ya wananchi na ushirikiano na Serikali katika ngazi mbalimbali.
Akizungumza na viongozi hao, Mhe. Mtambi ameitaka benki hiyo kuendelea kutoa mikopo kwa wingi kwa wawekezaji wakubwa na wajasiriamali wadogo ili kurahisisha suala la upatikanaji wa mitaji kwa wananchi wenye mawazo mazuri ya biashara wanaotaka kuwekeza katika sekta mbalimbali za kiuchumi.
“Mkoa wa Mara unazo fursa nyingi za uwekezaji ambazo bado hazijapata uwekezaji wa uhakika katika sekta za kilimo, mifugo, uvuvi, na madini na utalii, hivyo mkiweza kutoa mikopo kwa wingi wananchi watawekeza zaidi” amesema Mhe. Mtambi.
Kwa upande wake, Ndugu Kaziulaya amesema benki hiyo inaendelea kutoa mikopo kwa wananchi wanaojihusisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi na imerahisisha upatikanaji wa huduma ya mikopo kwa mwekezaji anayetaka kuwekeza nje ya eneo analohudumiwa.
“Inawezekana mteja akapatikana Mkoa wa Mara lakini yeye anataka mkopo wa kuwekeza Mkoa wa Lindi, kwa utaratibu wa Benki yetu tawi linalomhudumia

MTAMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUTIMIZA WAJIBU WAOMkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 21 J...
22/07/2026

MTAMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUTIMIZA WAJIBU WAO
Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 21 Julai, 2026 amefanyaziara katika Wilaya ya Musoka kukagua shughuli za maendeleo na kuzungumza na wananchi na kuwatahadharisha watumishi kuwa Serikali haitamvumilia mtumishi asiyetekeleza wajibu wake katika kuwahudumia wananchi.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kitongoji cha Rwakikoro, Kijiji cha Chirorwe, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, baada ya kupokea malalamiko ya wananchi kukosa maji kwa muda wa siku tatu kwa sababu ya umeme kuisha, Mhe. Mtambi amesema Serikali itawachukua hatua za kinidhamu kwa watumishi wa umma watakaobainika kutowajibika.
“Haiwezekani wananchi wanakosa maji kwa siku tatu kwa sababu ya kushindwa kulipia gharama za umeme za shilingi 150,000 na baada ya kupata tatizo hilo na mtumishi wa umma mwenye jukumu hilo badala ya kuchukua hatua anakaa kimya” amesema Mhe. Mtambi.
Mhe. Mtambi amesema mtumishi huyo atachukuliwa hatua za kiutumishi na kuwaonya watumishi wengine kuwajibika ipasavyo kutekeleza majukumu yao na Serikali ya Mkoa wa Mara haitavumilia tabia za uzembe na kutowajibika miungoni mwa watumishi wa umma.
Mhe. Mtambi akiwa katika mkutano huo, alisikiliza na kutatua kero na changamoto mbalimbali za wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Katika ziara hiyo, Mhe. Mtambi alitembelea kiwanda cha uchenjuaji wa dhahabu kinachoendelea kujengwa katika Wilaya ya Musoma na kukagua migodi ya dhahabu ikiwa ni sehemu ya juhudi za serikali za kufuatilia maendeleo katika sekta ya madini na kuhakikisha shughuli za uchimbaji zinafanyika kwa kufuata sheria, usalama na manufaa kwa wananchi.
Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa ameambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Musoma na watumishi kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Address

Musoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Regional Commissioner's Office-Mara posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Regional Commissioner's Office-Mara:

Shortcuts

Share