Lake Victoria Basin

Lake Victoria Basin Taasisi iliyo chini ya Wizara ya Maji, inayojishughulisha na Usimamizi wa Rasilimali za Maji

Mwenyekiti, Mkurugenzi na Watumishi wa Bodi ya Maji ya Bonde la Ziwa Victoria wanawatakia Wadau na Watanzania wote HERI ...
25/12/2023

Mwenyekiti, Mkurugenzi na Watumishi wa Bodi ya Maji ya Bonde la Ziwa Victoria wanawatakia Wadau na Watanzania wote HERI YA SIKUKUU YA CHRISMASS 2023

Mwenyekiti, Mkurugenzi na Watumishi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria wanawatakia Wadau na Watanzania kwa ujumla HE...
25/12/2023

Mwenyekiti, Mkurugenzi na Watumishi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria wanawatakia Wadau na Watanzania kwa ujumla HERI YA SIKUKUU YA CHRISMAMASS 2023

UJENZI WA MABWAWA KUSAIDIA KUONDOA CHANGAMOTO YA MAJI WILAYANI MASWA Wajumbe wa Bodi ya saba ya Bonde  la Ziwa Victoria ...
21/12/2023

UJENZI WA MABWAWA KUSAIDIA KUONDOA CHANGAMOTO YA MAJI WILAYANI MASWA

Wajumbe wa Bodi ya saba ya Bonde la Ziwa Victoria wamefanya ziara ya kutembelea miradi ya ujenzi wa bwawa la Igumangobo na bwawa la Ilambambasa yaliyopo wilaya ya Maswa mkoani Simiyu ambayo kwa pamoja yamegharimu shilingi Bilioni 1.4

Mabwawa hayo yamejengwa na Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria na yanatarajia kutumika katika shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo cha umwagiliaji, mifugo na matumizi ya kawaida ya binadamu ambapo bwawa la Igumangobo litahudumia takribani wananchi 6,200 na mifugo 4,000 katika vijiji vitatu na bwawa la Ilambambasa litawanufaisha wananchi zaidi ya 9,000 na mifugo 14,000 katika vijiji 7.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bi. Mwanajumbe Zuberi amesema, mabadiliko ya tabia nchi yameathiri sehemu mbalimbali nchini hivyo uamuzi wa kujenga miundombinu ya kuvuna maji ya mvua itasaidia wananchi kuwa na uhakika wa usalama wa maji. Amewapongeza wataalam wa Bodi hiyo kwa kazi nzuri waliyoifanya ya ujenzi wa mabwawa hayo na kuwataka wahakikishe wanaweka alama za mipaka ili kuzuia shughuli za kibinadamu ambazo zinaweza kuathiri uendelevu wa mabwawa hayo.

Akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa mabwawa hayo, Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria Dkt. Renatus Shinhu amesema, ujenzi wa mabwawa yote mawili umekamilika kwa asilimia 100% na yatakuwa na uwezo wa kutunza maji lita milioni 260, hali itakayopelekea kutatua changamoto ya huduma ya maji kwa wananchi na mifugo inayozunguka maeneo hayo. Amesema ujenzi wake umezingatia mahitaji ya wananchi kwa sasa na baadae katika maeneo yanayozunguka mabwawa hayo.

Amesema ujenzi wa mabwawa hayo unakwenda sambamba na juhudi za serikali za kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo ya vijijini kufikia asilimia 85% ifikapo mwaka 2025 ambapo mradi huu ni moja ya miradi mingi mikubwa hapa nchini ambayo inakuja kuwa na matokeo ya moja kwa moja kwa wananchi wanaozunguka mabwawa hayo.

Poleni sana Hanang, poleni sana Watanzania. 🙏🏾
05/12/2023

Poleni sana Hanang, poleni sana Watanzania. 🙏🏾

WATAALAMU WA SEKTA YA MAJI NA MADINI WAFUNDWA KUHUSU USALAMA WA MABWAWA YA MAJI NA TOPE SUMU.Wizara ya Maji kwa kushirik...
29/11/2023

WATAALAMU WA SEKTA YA MAJI NA MADINI WAFUNDWA KUHUSU USALAMA WA MABWAWA YA MAJI NA TOPE SUMU.

Wizara ya Maji kwa kushirikiana na Chemba ya Migodi Tanzania (TCM) imefanya Warsha ya mafunzo maalum iliyowashirikisha wataalamu kutoka kwa wamiliki wa migodi kwa ajili ya usalama wa mabwawa ya tope sumu (TSF), wamiliki wa mabwawa makubwa ya maji, wataalamu wa mabwawa waliosajiliwa (APPs) na wataalamu kutoka Serikalini ambao wanahusika na shughuli za usimamizi wa mabwawa ya maji na tope sumu na yamelenga kuwaelimisha wadau kuhusu teknolojia za kisasa zilizopo na kuwapa uelewa wa pamoja na fursa ya kuzungumza kuhusu ufuatiliaji wa usalama wa mabwawa hayo ya tope sumu (TSF) na mabwawa ya maji.

Akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika hotel ya Adden Palace Jijini Mwanza, Mkurugenzi wa rasilimali za maji nchini Dkt. George Lugomela amesema “Mabwawa ya maji pamoja na kuwa chanzo muhimu cha maji kwa shughuli za kijamii na kiuchumi, yasipotunzwa vizuri yanaweza kusababisha maafa yatokanayo na mafuriko endapo mabwawa yatabomoka, Vivo hivyo mabwawa ya tope sumu (TSF), mabwawa hayo ni kiungo muhimu katika kuendesha shughuli za uchenjuaji wa madini ambapo shughuli hizo zinahusisha matumizi ya kemikali ambazo sio rafiki wa mazingira” Hivyo isiporatibiwa na kutunzwa vizuri ni hatari kwa uchafuzi wa mazingira na vyanzo vya maji juu na chini ya ardhi, athari kwa mali za jamii na hata vifo”.

Dkt. Lugomela alieleza kuwa Wizara ya Maji kupitia Idara ya Rasilimali za Maji inajukumu la kuhakikisha mabwawa ya maji na tope sumu (TSF) yanakidhi vigezo vya usalama wa mabwawa kwa mujibu wa Sheria.

Mafunzo haya ni ya kwanza kufanyika Tanzania na ni hatua muhimu kuelekea mustakabali endelevu zaidi wa sekta ya madini na usimamizi wa rasilimali za maji nchini, yameandaliwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Maji, Tanzania chember of Mines (TCM), wataalam kutoka OSIMO, SGS Tanzania, Norplan Tanzania, FEMA Mining & Drilling Limited na City Engineering.

Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma
Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria

BODI YA TAIFA YA MAJI YATEMBELEA CHANZO CHA MAJI YA ZIWA VICTORIA- IHELELEWajumbe wa Bodi ya Maji ya Taifa wamefanya zia...
10/11/2023

BODI YA TAIFA YA MAJI YATEMBELEA CHANZO CHA MAJI YA ZIWA VICTORIA- IHELELE

Wajumbe wa Bodi ya Maji ya Taifa wamefanya ziara ya siku moja ya kutembelea chanzo cha Maji ya Ziwa Victoria- Ihelele kilichopo katika kitongoji cha Ihelele, Kijiji cha Nyang’homango, Kata ya Ilujamate, Wilaya ya Misungwi Mkoa wa Mwanza.

Ziara hiyo imeongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Mhandisi Mbogo Futakamba ambae alifuatana na wajumbe wa Bodi hiyo pamoja na wataalam kutoka Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kahama- Shinyanga (KASHWASA).

Lengo kuu la ziara hiyo ni kujionea uhifadhi wa chanzo cha maji cha Ziwa Victoria - Ihelele na shughuli za uzalishaji maji pamoja na uendeshaji wa mradi huo.

Akiwasilisha taarifa ya mradi huo, Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria Dkt. Renatus Shinhu amesema, chanzo hicho ni kati ya miradi mikubwa ya kitaifa ambacho hutoa maji Ziwa Victoria kwa ajili ya kusambaza kwa wananchi ili kuwapatia maji safi na salama.

Chanzo hicho kinatumiwa na kusimamiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Kahama na Shinyanga (KASHWASA) na KASHWASA wanazalisha maji kina uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 63 kwa siku.

Dkt. Shinhu ameongeza kuwa, mradi huo unatoa huduma ya maji kwa watu 1,969,255 katika miji ya Kahama, Shinyanga, Nzega, na Tabora. Idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka zaidi ya watu milioni mbili baada ya kupanuliwa kwenda katika miji ya Urambo, Igunga na Shelui.

Katika jitihada za kutunza na kuhifadhi chanzo hicho, Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria imefanya uhamasishaji na kutoa elimu kwa vijiji 18 vinavyozunguka chanzo, kusimika vigingi 4700 kwa upande wa wilaya ya Misungwi kwa umbali wa Kilomita 197 na upande wa Wilaya ya
Nyang’hwale kwa umbali wa Kilomita 85,` kupanda miche ya miti 25,000 kwenye ekari 120 na kusimika mabango 32 ya katazo pamoja na kuunda jumuiya tatu (3) za watumia maji ambazo ni (i) Jumuia ya Watumia Maji Ihelele (ii) Jumuiya ya Watumia Maji Ligembe juu na (iii) Jumuia ya Watumia Maji Ligembe chini.

ELIMU YA UHIFADHI WA VYANZO  VYA MAJI YATOLEWA WILAYANI KWIMBAEneo la hifadhi ya maji Ardhini Ngudu ni miongoni mwa vyan...
06/11/2023

ELIMU YA UHIFADHI WA VYANZO VYA MAJI YATOLEWA WILAYANI KWIMBA

Eneo la hifadhi ya maji Ardhini Ngudu ni miongoni mwa vyanzo vya maji muhimu vilivyopo katika hifadhi ya Mwamakeremo inayohusisha vitongoji vya Ngumo, Bukagama, Kilyaboya na Kimwaga katikakata ya Ngudu wilaya ya Kwimba mkoa wa Mwanza

Hifadhi hiyo ina ukubwa wa ekari 388 na ndani yake kuna visima 6 vyenye urefu w wastani wa mita 80 hadi mita 100.

Hifadhi hiyo ambayo hutegemewa kwa matumizi mbalimbali ya maji, imeathiriwa kutokana na shughuli za kibinadamu hususani kilimo na kusababisha athari katika wingi na ubora wa maji.

Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria imefanya mkutano wa hadhara na wananchi wanaozunguka hifadhi hiyo na kutoa elimu yenye lengo la kuhakikisha hifadhi hiyo ya maji ardhini inatunzwa, inalindwa na kusimamiwa kwa njia endelevu.

Tayari Bodi imefanya jitihada za kuhifadhi eneo hilo kwa kuchukua hatua kadhaa ikiwemo shughuli za utoaji wa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa kulinda na kutunza eneo la hifadhi hiyo, na kusimika vigingi 110 kwenye eneo la hifadhi, kusimika mabango 10 ya katazo ya shughuli za kibinadamu kufanyika ndani ya eneo la hifadhi pamoja na kupanda miti 2,500 rafiki wa maji ndani ya eneo la hifadhi hiyo.

Imetolewa na;
Kitengo cha mawasiliano na uhusiano kwa umma
Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria.

DC KWIMBA AHIMIZA UHIFADHI WA ENEO LA HIFADHI YA MAJI ARDHINI- NGUDUMkuu wa wilaya ya Kwimba Mhe Ng'wilabuzu Ludigija am...
04/11/2023

DC KWIMBA AHIMIZA UHIFADHI WA ENEO LA HIFADHI YA MAJI ARDHINI- NGUDU

Mkuu wa wilaya ya Kwimba Mhe Ng'wilabuzu Ludigija amefanya kikao kazi chenye lengo la kuhifadhi eneo la hifadhi ya maji ardhini- Ngudu.

Kikao hicho kimehudhuriwa na wataalamu wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria wakiongozwa na Mkurugenzi wa Bodi hiyo Dr. Renatus Shinhu.

Hifadhi ya maji ardhini Ngudu ina ukubwa wa ekari 388 na ndani yake kuna visima 6 vyenye urefu wa wastani wa mita 80 hadi mita 100.

Kwa pamoja visima vina uwezo wa kuzalisha lita 725,000 kwa siku, kwa wastani wa lita 120,000 kwa siku kwa lita kwa kila kisima.

Katika jitihada za kuhifadhi eneo hilo, Serikali kupitia Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria imechukua hatua kadhaa ikiwemo shughuli za utoaji wa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa kulinda na kutunza eneo la hifadhi hiyo, na kusimika vigingi 110 kwenye eneo la hifadhi, kusimika mabango 10 ya katazo ya shughuli za kibinadamu kufanyika ndani ya eneo la hifadhi pamoja na kupanda miti 2,500 rafiki wa maji ndani ya eneo la hifadhi hiyo.

Imetolewa na;
Kitengo cha mawasiliano na uhusiano kwa umma
Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria

Bodi, Menejimenti na Watumishi wa Bodi  ya Maji Bonde la Ziwa Victoria tunaungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanz...
14/10/2023

Bodi, Menejimenti na Watumishi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria tunaungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Watanzania wote katika kuadhimisha kumbukizi ya Miaka 24 ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Mwl. julius K. Nyerere.


UKARABATI WA BWAWA LA ILAMBAMBASA WILAYANI MASWA WAFIKIA ASILIMIA 90%, MAMBO MAZURI YANAKUJA KWA WANANCHI Mradi wa ukara...
06/10/2023

UKARABATI WA BWAWA LA ILAMBAMBASA WILAYANI MASWA WAFIKIA ASILIMIA 90%, MAMBO MAZURI YANAKUJA KWA WANANCHI

Mradi wa ukarabati wa bwawa Ilambambasa wilayani Maswa mkoani Simiyu umefikia asilimia 90% ya utekelezaji na unatarajiwa kuwanufaisha wananchi zaidi ya 9,000 wa vijiji 7 vya Mwabusalu, Igungulyankoma, Mwakabeya, Mwamitumaye, Mbugamita, Senani, Ilambambasa na mifugo ipatayo 14,000.

Bwawa hilo linafanyiwa ukarabati na upanuzi kwa thamani ya shilingi milioni 900 chini ya wizara ya maji kupitia Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria.

Hii inakwenda sambamba na juhudi za serikali za kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo ya vijijini kufikia asilimia 85% ifikapo mwaka 2025 ambapo mradi huu ni moja ya miradi mingi mikubwa hapa nchini ambayo inakuja kuwa na matokeo ya moja kwa moja kwa wananchi wanaolizunguka bwawa hilo.

Bwawa hilo litakuwa na ukubwa wa kubeba maji yenye lita za ujazo milioni 3 na litakapokamilika litanufaisha kuleta maendeleo kwa wananchi kwa kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji kwa wananchi wa vijiji hivyo na kata ya Senani.

Mradi huu ulianza utekelezaji wake Agosti 20, 2023 na utakamilika Oktoba 10, 2023.


Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma
Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria

Bodi ya maji Bonde la Ziwa Victoria imeng'ara kwa kupokea tuzo maalum na cheti cha pongezi  katika maadhimisho  ya 12 ya...
18/09/2023

Bodi ya maji Bonde la Ziwa Victoria imeng'ara kwa kupokea tuzo maalum na cheti cha pongezi katika maadhimisho ya 12 ya siku ya Mto Mara baada ya kuibuka mshindi wa kwanza kwenye uhifadhi wa Bonde la Mto Mara (Mara catchment conservation champion)

Tuzo hiyo imekabidhiwa jana Septemba 15, 2023 Mugumu-Serengeti mkoani Mara na Naibu Waziri wa maji Mhe Mhandisi MaryPrisca Mahundi (Mb) aliyefunga maadhimisho hayo na kupokelewa na Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria Dkt. Renatus Shinhu

Address

P. O. Box 1342
Mwanza
TZ

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Lake Victoria Basin posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Lake Victoria Basin:

Share