21/10/2019
*No.2* (Namna nyingine ya kutafakari masomi ya leo)
*ASALI MUBASHARA-Jumatatu 21/10/2019*
Karibuni sana wapendwa wa Bwana kwa adhimisho la misa takatifu asubuhi ya leo. Neno la Bwana katika wimbo wetu wa katikati tunakutana na maneno yasemayo katika kiitikio yasemayo: “Atukuzwe Bwana Mungu wa Israeli kwani amewajia watu wake. Hakika amewajia watu wake ili kuwapa wokovu.
Bwana Mungu alikuja kwa watu wake pale Kristo alipokuja ulimwenguni, na kwa kufanya hivi, alitimiza ahadi yake aliyokuwa ameihaidi tangu enzi za Adamu, tangu enzi za Ibrahim. Yesu ndiye atakayekuwa Masiha atakayeukomboa ulimwengu wote. Maneno ya wimbo huu wa katikati yaliimbwa na Zakaria, Baba yake na Yohane Mbatizaji. Alitoa unabii wa furaha kwamba ahadi ya Mungu imetimia kwa ujio wa Kristo, na hivyo sote tunapaswa kumwamini Kristo. Yeye ndiye utimilifu wa Torati yote, na kila kilichoahidiwa tangu Abrahamu.
Maneno haya yanatumika kusisitizia ujumbe wa somo la kwanza wa Paulo kwamba Kristo ndiye utimilifu wa ahadi zote, yeye ndiye kila kilichoahidiwa tangu mababu na hivyo yafaa tumwamini Kristo wetu. Tusitegemee nguvu yetu kila mahali.
Katika somo la injili, Bwana Yesu anatuasa kutokutumia nguvu zetu wenyewe kwa kila kitu bila kumtegemea Mungu. Anatupatia habari za tajiri mmoja aliyejilimbikizia mali na kujisifia kana kwamba amefaulu kwa kila kitu. Mwishowe kumbe amejiwekea hazina ulimwenguni na mali ya ulimwengu ilishindwa kumwokoa. Ni fundisho kwetu kwamba tusiwe k**a huyu tajiri, tuwe watu wa kujiwekea hazina mbinguni, tuwe watu wa sala na wenye kuyabariki maisha yetu.
Katika safari, k**a tumesahau kubeba fedha ya mfukoni, huwa tunashtuka na kupiga simu kila mahali. Tunapaswa mshtuko wa namna hii utupate pale tunaposahau vitu k**a rozari, au tunapokumbuka kwamba hatujasali. Tujitahidi tutambue kwamba unapokuwa na pesa sio kwamba umefaulu kila kitu; na kukosa unyenyekevu. Jua kwamba mengi yanaweza kukunyemelea, yapo magonjwa, majambazi, ajali zaweza kukunyemelea na hizi hasara yake ni mba