Halmashauri ya Mji Njombe

Halmashauri ya Mji Njombe Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Halmashauri ya Mji Njombe, Government Organization, Lunyanywi, Njombe.

Kesho ya mwanao inaanzia kwenye afya bora,ipe kipaumbele afya ya mwanao.Mpeleke akapate matone ya Vitamini A.
04/06/2026

Kesho ya mwanao inaanzia kwenye afya bora,ipe kipaumbele afya ya mwanao.Mpeleke akapate matone ya Vitamini A.

TANGAZO LA USAILI BBT
04/06/2026

TANGAZO LA USAILI BBT

TANGAZO
03/06/2026

TANGAZO

03/06/2026

VIDEO;VITU VYA MSAADA VILIVYO TOLEWA KWA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU KIBENA

NJOMBE TC YATOA MSAADA WA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI MOJA KWA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU KIBENA.Menejimenti ya Halmash...
03/06/2026

NJOMBE TC YATOA MSAADA WA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI MOJA KWA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU KIBENA.

Menejimenti ya Halmashauri ya Mji Njombe imetoa msaada wa maduveti, sabuni, pampas na nyama ya mbuzi wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni moja kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu wa Shule ya Msingi Kibena, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ustawi wao.

Akizungumza Juni 2,2026 kwa niaba ya Mkurugenzi, Afisa Elimu Maalumu Bryson Kingililwe alisema halmashauri itaendelea kuboresha huduma na mazingira ya kujifunzia kwa watoto hao. Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Desperate Mtewele, alishukuru msaada huo akisema umekuja wakati muafaka.

Katika ziara hiyo, menejimenti pia ilitembelea kituo cha mazoezi tiba na kupongeza ubunifu wa Mwalimu wa Elimu Maalumu Bezael Kingilangwa, ambaye amebuni vifaa vya mazoezi vinavyosaidia maendeleo ya watoto wenye mahitaji maalumu. Halmashauri imeahidi kuendelea kutoa ushirikiano ili kuboresha zaidi huduma kwa watoto hao.

Msaada huo uliojumuisha maduveti, sabuni, pampas na nyama ya mbuzi umelenga kuboresha mazingira ya maisha na mahitaji ya kila siku ya watoto hao wanaopata huduma katika shule hiyo.

TAARIFA KWA WAKULIMA, WANUNUZI NA WADAU WOTE WA ZAO LA PARACHICHI
29/05/2026

TAARIFA KWA WAKULIMA, WANUNUZI NA WADAU WOTE WA ZAO LA PARACHICHI

25/05/2026

: AHADI YA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA YATEKELEZWA .

Koingozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026 Ndg.Wazo Michael Mwang'onda Mei 23,2024 wakati wa ukaguzi wa jengo na vifaa vya huduma ya upasuaji katika kituo cha afya mjimwema aliwatembelea akina mama ambao walifanyiwa upasuaji nakutoka salama.Aliwaahidi zawadi na kuchangisha fedha ambazo zilikabidhiwa kwa akina mama hao na Mhe.Juma Sweda Mkuu wa Wilaya ya Njombe akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Mhe.Erasto Mpete ,katibu tawala wa wilaya ya Njombe,Mkurugenzi na mratibu wa shughuli za mbunge Jimbo la Njombe Mjini.

"Tanzania ni yetu sote,tushikamane kwa pamoja na kuleta maendeleo".




 :- Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Mji Njombe, Bi. Kuruthum Sadick, amemkabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkurugenzi ...
24/05/2026

:- Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Mji Njombe, Bi. Kuruthum Sadick, amemkabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Njombe, Christopher Sanga, kwa ajili ya kuendelea na mbio za Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Njombe.

Mwenge wa Uhuru umetembelea, kukagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Mji Njombe yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.9. Miradi hiyo inalenga kuboresha huduma za kijamii na kuchochea maendeleo kwa wananchi wa Njombe.

Makabidhiano hayo yalihudhuriwa na Waheshimiwa Madiwani wakiongozwa na Mhe. Ersto Mpete, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe , wakuu wa idara , watumishi wa halmashauri na wananchi waliojitokeza kushuhudia tukio hilo.

"Tanzania ni yetu sote,tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo"

24/05/2026

Mkesha wa Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Msanii Msaga Sumu

Address

Lunyanywi
Njombe

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halmashauri ya Mji Njombe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Halmashauri ya Mji Njombe:

Share