Halmashauri ya Mji Njombe

Halmashauri ya Mji Njombe Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Halmashauri ya Mji Njombe, Government Organization, Lunyanywi, Njombe.

TANGAZO TANGAZO TANGAZO
04/09/2026

TANGAZO TANGAZO TANGAZO

  KWA UMMA
04/09/2026

KWA UMMA

02/09/2026

VIGEZO VYA KUPATA MKOPO WA ASILIMIA 10% NJOMBE

Ni vigezo gani vinapaswa kuzingatiwa na vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ili kupata mkopo wa asilimia 10% wa Halmashauri ya Mji Njombe?

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Enembora Lema, anatoa ufafanuzi kupitia kipindi cha Jicho la Maendeleo kinachorushwa na Uplands FM

02/09/2026

NAMNA YA KUREJESHA MIKOPO YA ASILIMIA 10% HALMASHAURI YA MJI NJOMBE

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Mji Njombe, Enembora Lema, ametoa ufafanuzi kuhusu namna ya kurejesha mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Lema ametoa ufafanuzi huo kupitia kipindi cha Jicho la Maendeleo kinachorushwa na Uplands FM, akieleza utaratibu unaopaswa kufuatwa na wanufaika katika kurejesha mikopo hiyo

02/09/2026

BILIONI 3.9 ZATOLEWA KWA VIKUNDI 233 NJOMBE

Jumla ya shilingi bilioni 3.9 zimetolewa kwa vikundi 233 katika Halmashauri ya Mji Njombe kwa mwaka wa fedha 2025/2026, kupitia mpango wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Mji Njombe, Enembora Lema, amebainisha hayo kupitia kipindi cha Jicho la Maendeleo kinachorushwa na Uplands FM, akieleza kuwa mikopo hiyo imelenga kuwawezesha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kuanzisha na kuendeleza shughuli za kiuchumi.

Lema amesisitiza umuhimu wa wanufaika kutumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa, kuzingatia masharti ya mikopo na kuhakikisha marejesho yanafanyika kwa wakati ili kuwawezesha wananchi wengine kunufaika na fursa hiyo.

WATUMISHI KILIMO, MIFUGO NA UVUVI NJOMBE WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI YA UTUMISHIWatumishi wa Idara ya Kilimo, Mifugo na ...
02/09/2026

WATUMISHI KILIMO, MIFUGO NA UVUVI NJOMBE WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI YA UTUMISHI

Watumishi wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi katika Halmashauri ya Mji Njombe wametakiwa kuzingatia sheria, kanuni, miongozo na maadili ya utumishi wa umma katika kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, weledi na uwajibikaji.

Wito huo umetolewa na Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Mji Njombe, Twilumba Mwalongo, Septemba 1, 2026, wakati akitoa elimu kuhusu haki na wajibu wa mtumishi wa umma katika kikao cha utekelezaji wa shughuli za Idara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Mwalongo amesema uelewa wa haki na wajibu wa mtumishi ni muhimu katika kujenga utumishi wenye tija, huku akiwataka watumishi kutekeleza majukumu yao kwa kufuata taratibu zilizowekwa na Serikali na kuepuka vitendo vinavyoweza kuathiri uadilifu wa utumishi wa umma.

Amesisitiza kuwa mtumishi wa umma anapaswa kutambua haki zake na wakati huo huo kutimiza wajibu wake kwa wananchi na Serikali kwa kuzingatia weledi, nidhamu, uaminifu na matumizi sahihi ya rasilimali za umma.

Sambamba na hilo, watumishi hao wamepatiwa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa katika utoaji wa huduma za kilimo, wakisisitizwa kutoa huduma kwa wananchi kwa usawa na uwazi, bila kudai au kupokea rushwa.

Aidha, wamekumbushwa kuwahudumia wakulima kwa karibu kwa kutoa ushauri sahihi wa kitaalamu na kuwawezesha kutumia mbinu bora za kilimo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji na kipato cha wakulima.

KILUMILE AWATAKA WATUMISHI IDARA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI NJOMBE TC KUWA MFANO WA KUIGWA KATIKA UWAJIBIKAJI. ;- Mkuu w...
01/09/2026

KILUMILE AWATAKA WATUMISHI IDARA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI NJOMBE TC KUWA MFANO WA KUIGWA KATIKA UWAJIBIKAJI.

;- Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Mji Njombe, Nolasco Kilumile, amewataka watumishi wa idara hiyo kuwa mfano wa kuigwa katika uwajibikaji, utendaji kazi na kujenga uchumi kupitia shughuli za uzalishaji.

Kilumile ametoa kauli hiyo Septemba 1, 2026, wakati akizungumza na watumishi wa idara hiyo katika kikao cha kujadili utekelezaji wa shughuli za kazi kwa mwaka wa fedha 2026/2027, ambapo amewahimiza watumishi kutumia fursa zilizopo katika kilimo na shughuli nyingine za kiuchumi ili kujiongezea kipato na kuwa mfano kwa wananchi wanaowahudumia.
“Mjifunze kulima, tufanye shughuli za kiuchumi. Usione shida kwenda kujifunza kwa wengine. Mimi niwaombe tukomae na parachichi, ni zao kubwa sana la kiuchumi,” alisema Kilumile.

Aidha, Kilumile amesisitiza umuhimu wa watumishi kuwa tayari kujifunza kutoka kwa wengine na kutumia maarifa wanayoyapata katika kuboresha utendaji wao wa kila siku, sambamba na kushiriki katika shughuli za kiuchumi zinazoweza kuchangia maendeleo binafsi na ya jamii.

Katika kikao hicho, watumishi hao pia walipatiwa elimu kuhusu njia za kujikinga na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) mahali pa kazi, ikiwa ni sehemu ya kuendelea kujenga uelewa na kuimarisha afya na ustawi wa watumishi.

Kikao hicho kimekuwa sehemu ya utekelezaji wa mipango ya Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2026/2027, huku msisitizo ukiwekwa katika uwajibikaji, kuongeza uzalishaji, shughuli za kiuchumi, afya ya watumishi, haki na wajibu wa utumishi wa Umma na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

MILIONI 32.8 ZACHANGISHWA UKARABATI WA SHULE YA SEKONDARI MBEYELAJumla ya Sh. 32,828,500/= zimepatikana katika harambee ...
30/08/2026

MILIONI 32.8 ZACHANGISHWA UKARABATI WA SHULE YA SEKONDARI MBEYELA

Jumla ya Sh. 32,828,500/= zimepatikana katika harambee ya kuchangia ukarabati wa majengo ya Shule ya Sekondari Mbeyela, Kata ya Njombe Mjini, Halmashauri ya Mji Njombe.

Katika harambee hiyo iliyofanyika tarehe 29 Agosti 2026, wananchi na wadau mbalimbali walijitokeza kuchangia fedha na vifaa kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya shule hiyo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe, Mhe. Erasto Mpete, amesema lengo la harambee hiyo ni kuimarisha miundombinu ya shule ili kuinua kiwango cha taaluma na kuweka mazingira rafiki kwa wanafunzi pamoja na walimu.

“Maendeleo yanaanza na sisi ndugu wananchi. Niombe tushirikiane kwa pamoja kuchangia harambee ya shule yetu,” amesema Mhe. Mpete.

Mhe. Mpete pia amewahimiza wananchi kutumia fursa ya kilimo cha parachichi kwa kupanda angalau miti mitano kwa kila familia, ili kuongeza kipato na uwezo wa kushiriki katika shughuli za maendeleo.

Kwa upande wake, Jimmy Ngumbuke amewashukuru wabunge, madiwani,Viongozi wa serikali, wafanyabiashara, wakulima wa parachichi na wananchi wote waliochangia kufanikisha zoezi hilo.

Kwa mujibu wa matokeo ya harambee hiyo, Shilingi 7,893,500 zilipatikana kwa njia ya fedha taslimu, huku Shilingi 11,400,000 zikiwa ni ahadi za fedha na Shilingi 13,535,000 zikiwa ni ahadi za malighafi, hivyo kufikisha jumla ya Shilingi 32,828,500.

Uongozi wa shule umeeleza kuwa zoezi la uchangiaji bado linaendelea, hivyo wananchi na wadau ambao hawakupata nafasi ya kushiriki katika harambee hiyo wanaendelea kupewa fursa ya kuchangia kupitia akaunti ya NMB 60610003749, yenye jina Joseph Mbeyela Secondary, huku wanaochangia wakitakiwa kuwasilisha slip ya malipo kwa uongozi wa shule kwa ajili ya kumbukumbu.

  ZA PONGEZI
30/08/2026

ZA PONGEZI

29/08/2026

Clemence Manga, Afisa Michezo wa Halmashauri ya Mji Njombe na Mjumbe wa SHIMISEMITA Taifa, akizungumza kuhusu michezo hiyo iliyohitimishwa jijini Mbeya Agosti 29, 2026, pamoja na ushiriki wa timu ya Njombe Mji.

Address

Lunyanywi
Njombe

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halmashauri ya Mji Njombe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Halmashauri ya Mji Njombe:

Shortcuts

Share