23/09/2025
K**A MKEO ANA MAHUSIANO NA MWANAUME MWINGINE, JUA KWAMBA MKEO NDIO CHANZO CHA HAYO MAHUSIANO NA WALA SIO HUYO MWANAUME.
Mpendwa mwanaume acha tuongeee hili kwa uwazi, kuna vitu ni lazima tuambiane ukweli hata k**a utatatizika kuvichukua.
K**a itatokea siku unagundua mkeo ana uhusiano na mwanaume mwingine, usipoteze muda kugombana na huyo mwanaume, wala usipigane na huyo mwanaume, wala usidhani huyo mwanaume alifanya jitihada nyingi kumpata mkeo, sio kweli. Mwanamke wako alifungua mlango ili jamaa aingie, mwanamke wako alijiweka katika hali ya kupatikana.
Kati ya kitu cha hatari zaidi kwa mwanaume ni kutongoza mke wa mtu, wanaume wanajua hili na huwa wapo makini, hawatongozi mke wa mtu hovyo hovyo, ni hadi pale wanapoona huyo mkeo kaacha nafasi hiyo. Wanaume hawana ujasiri wa kutongoza mke wa mtu, ni hadi pale huyo mkeo akatoa ishara, akaonyesha kuvutiwa na huyo mwanaume, hapo ndipo mwanaume anaangukia kwenye huo mtego.
Elewa kwa uwazi hapa, mara nyingi k**a sio zote mwanamke wako ndio anaanzisha hayo mahusiano bila kusema, kuna vitu anafanya ambavyo yeye anajua anachokifanya, na wanaume huwa wanaelewa vizuri bila kuambiwa neno lolote.
β Zile alama anazo muonyesha mwanaume mwingine.
β Anavyovaa akiwa mbele ya huyo mwanaume.
β Anavyojikesha kwa nguvu hata kwa kitu ambacho hakichekeshi, ikiwa tu aliyeongea ni huyo mwanaume.
β Anavyokaa mbele ya huyo mwanaume, mikao ya kihasara hasara.
β Anamlalamikia kuhusu shida za kwenye mahusiano yake.
β Jinsi anavyomuangalia mwanaume huyo kwa kugonganisha macho kwa muda mrefu.
Hapo ndio humvuta mwanaume huyo, hivyo ndivyo anavyompa ujasiri mwanaume mwingine kuvuka mpaka na kumtaka.
Kwahiyo acha kulaumu mwanaume inapotokea mke wako kasaliti, yeye ndio tatizo.
Mwanamke msaliti wala hajachanganyikiwa, wala hakulazimishwa, alipiga hesabu zake, kakudanganya na akapeleka mwili wake ukatumike na mwanaume mwingine. Na akishakusaliti ataendelea kufanya hivyo tena na tena, weka hilo akilini.
Na wewe k**a mwanaume, acha kukaa na kujadiliana kuhusu usaliti, k**a unasamehe samehe tu ila ukweli ni huo hapo juu. Usitake kujua kilitokea nini hadi ukasalitiwa, usigombane na wanaume wanaolala na mkeo, hawana kosa lolote, kosa ni huyo mwanamke wako.
Ukisalitiwa una machaguo mawili, muache au samehe kwa sababu zako binafsi wala sio kwa sababu alizokupa huyo msaliti.
Lakini kitu muhimu zaidi unachotakiwa kujua ni kwamba, amekusaliti na ataendelea kukusaliti, hiyo wala sio mwisho.
Bye π .