Singida Manispaa

Singida Manispaa Karibu Katika Ukurasa Rasmi wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida.

Karibu katika Ukurasa wa Halmashauri ya Manispaa Singida
Lengo la Ukurasa huu ni kuwaleta watumishi na wakazi wote wa Singida Manispaa Kwa pamoja na kupeana taarifa mbali mbali za kiutendaji ndani ya Manispaa Singida, Pia kupeana matangazo mbali mbali

03/06/2026

MANISPAA YA SINGIDA YAPOKEA SH MILIONI 544 KUJENGA SHULE MPYA

Serikali imeendelea kuimarisha sekta ya elimu katika Manispaa ya Singida baada ya kutoa Sh milioni 544 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya sekondari katika eneo la Manguanjuki, Kata ya Mandewa.

Fedha hizo zimepokelewa katika kipindi hiki ambacho mwaka wa fedha 2025/26 unakaribia kukamilika, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita za kuboresha mazingira ya kujifunzia na kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu karibu na maeneo wanayoishi bila kulazimika kutembea umbali mrefu.

Akizungumza kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Divisheni ya Elimu Sekondari kwa mwaka wa fedha 2025/26, Afisa Elimu Sekondari wa Manispaa ya Singida, Athumani Mnyusi, alisema serikali ilitoa Sh milioni 185 kwa ajili ya kukamilisha miradi mbalimbali ya miundombinu ya elimu.

Alitaja miradi hiyo kuwa ni ukamilishaji wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Mandewa kwa gharama ya Sh milioni 25, ukamilishaji wa maabara mbili katika Shule ya Sekondari Mughanga kwa Sh milioni 60, maabara mbili katika Shule ya Sekondari Unyianga kwa Sh milioni 60, pamoja na mabweni katika Shule ya Sekondari Mungumaji kwa Sh milioni 40.
Aidha, wadau wa elimu wa CAMFED walitoa Sh milioni 44 zilizotumika kujenga matundu 20 ya vyoo vya wasichana, ambapo matundu 10 yalijengwa katika Shule ya Sekondari Mitunduruni kwa Sh milioni 22 na matundu mengine 10 katika Shule ya Sekondari Senge kwa Sh milioni 22.

Kwa upande mwingine, Serikali Kuu ilitoa Sh milioni 20.4 kwa ajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule za Mtamaa, Mwenge, Uhamaka, Mitunduruni, Maharu na Unyambwa.

Mnyusi aliwataka wazazi na walezi kuendelea kushiriki katika utoaji wa chakula shuleni ili kuwasaidia wanafunzi kusoma katika mazingira bora na kuongeza ufaulu wao wa kitaaluma.

Alisema uwekezaji unaoendelea kufanywa na serikali katika miundombinu ya elimu ni ushahidi wa dhamira yake ya kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora kupitia mazingira rafiki ya kujifunzia na kufundishia.

Watendaji wa kata 18 za Manispaa ya Singida wamepatiwa mafunzo maalum ya mfumo wa Mrejesho yenye lengo la kuwaongezea uw...
01/06/2026

Watendaji wa kata 18 za Manispaa ya Singida wamepatiwa mafunzo maalum ya mfumo wa Mrejesho yenye lengo la kuwaongezea uwezo wa kushughulikia malalamiko na kero za wananchi kuanzia ngazi ya chini.

Mafunzo hayo yametolewa leo Juni 1, 2026 katika ukumbi wa Ofisi za Manispaa ya Singida na Afisa Mwandamizi wa Mrejesho wa manispaa hiyo, Chrispine Nyaulingo, ambapo amesisitiza umuhimu wa watendaji hao kutumia mifumo rasmi ya mrejesho katika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi kwa haraka na kwa ufanisi.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Nyaulingo amesema kuwa mfumo wa E-Mrejesho ni nyenzo muhimu inayowapa wananchi fursa ya kuwasilisha pongezi, maoni, mapendekezo pamoja na malalamiko mbalimbali moja kwa moja kwa idara au taasisi husika ili yafanyiwe kazi kwa uwazi, haraka na kwa tija.

Amesema mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi kupitia ushirikishwaji na mawasiliano ya karibu kati ya serikali na wananchi.

KARIBU MWENGE WA UHURU 2026MANISPAA YA SINGIDA“Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamanekwa Pamoja Kuleta Maendeleo”
01/06/2026

KARIBU MWENGE WA UHURU 2026

MANISPAA YA SINGIDA

“Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane
kwa Pamoja Kuleta Maendeleo”











HABARI PICHA: Picha za matukio mbalimbali wakati wa Kongamano la Vijana Manispaa ya Singida leo Mei 30, 2026 kongamano a...
30/05/2026

HABARI PICHA: Picha za matukio mbalimbali wakati wa Kongamano la Vijana Manispaa ya Singida leo Mei 30, 2026 kongamano ambalo limefanyika katika ukumbi wa Chuo cha Maji.

30/05/2026

“Kwa sisi vijana Halmashauri(Singida MC) yetu imekuwa ikituhamasisha kufanya kazi na kuchukua mikopo sababu vijana wengi wanauwezo wa kufanya kazi shida ni mitaji, mikopo inatolewa lakini changamoto kubwa ni kwa vijana kutojiamini wakati Serikali imetoa nafasi”

30/05/2026

Vijana wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida wamehimizwa kuwa wazalendo na kuendelea kuilinda amani ya nchi, wakielezwa kuwa wao ndiyo nguzo muhimu ya maendeleo ya taifa.

Wito huo umetolewa leo Mei 30, 2026 na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, Christopher Ngonyani, wakati akifungua Kongamano la Vijana la Manispaa ya Singida lenye kauli mbiu isemayo “Uzalendo na Uthubutu Chanzo cha Ustawi wa Vijana.”

Ngonyani alisema vijana wanapaswa kutimiza majukumu yao kwa kuwajibika, kuipenda nchi yao na kuheshimu sheria za nchi, akibainisha kuwa uzalendo huwajengea msingi imara wa maisha na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.

Aidha, aliwataka vijana kuwa mabalozi wa amani katika maeneo yao, akisisitiza kuwa wao ndiyo nguvu kazi ya taifa na wana nafasi kubwa katika kuhakikisha utulivu na mshikamano vinaendelea kudumishwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

30/05/2026
HABARI PICHA:Picha za matukio mbalimbali wakati wa zoezi la usafi leo Jumamosi ya Mei 30, 2026 katika eneo la barabara  ...
30/05/2026

HABARI PICHA:Picha za matukio mbalimbali wakati wa zoezi la usafi leo Jumamosi ya Mei 30, 2026 katika eneo la barabara ya Sabasaba-Gineri zoezi ambalo liliongozwa na Naibu Meya wa Manispaa ya Singida, Abdallah Mkoko akiambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, Christopher Ngonyani pamoja watumishi na wananchi.

29/05/2026

Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, Bi Joanfaith Kataraia, leo Mei 29, 2026 ametembelea na kukagua baadhi ya vituo vya afya na zahanati zilizopo ndani ya manispaa hiyo ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata huduma bora za afya.

Katika ziara hiyo, Bi Kataraia alikagua utoaji wa huduma, hali ya miundombinu pamoja na mazingira ya kazi kwa watumishi wa afya, huku akisisitiza umuhimu wa kuwahudumia wananchi kwa weledi na kwa wakati.

Alieleza kuwa lengo la ukaguzi huo ni kujionea hali halisi ya huduma zinazotolewa na kubaini maeneo yenye changamoto ili yafanyiwe kazi kwa haraka.

Aidha, alisema Manispaa itaendelea kuchukua hatua za kuboresha huduma za afya kwa kutatua changamoto mbalimbali zinazoathiri utoaji wa huduma, ili wananchi wapate matibabu katika mazingira salama, rafiki na yenye viwango vinavyokidhi mahitaji yao.

Address

Ipembe
Singida
236

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:29 - 17:00
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Singida Manispaa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Singida Manispaa:

Share