Singida Manispaa

Singida Manispaa Karibu Katika Ukurasa Rasmi wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida.

Karibu katika Ukurasa wa Halmashauri ya Manispaa Singida
Lengo la Ukurasa huu ni kuwaleta watumishi na wakazi wote wa Singida Manispaa Kwa pamoja na kupeana taarifa mbali mbali za kiutendaji ndani ya Manispaa Singida, Pia kupeana matangazo mbali mbali

HABARI PICHA: Bw. Hillary Makundi akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida,  na timu ya...
04/09/2026

HABARI PICHA: Bw. Hillary Makundi akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida, na timu ya mpira wa wavu ufukweni (Beach Volleyball) kutoka Ujerumani, walipotembelea ofisini leo Septemba 4, 2026.

Bw. Makundi amewashukuru kwa ziara hiyo na kusema itakuwa chachu ya kuimarisha mchezo huo na afya ya wananchi.

Mkuu wa Kitengo cha Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Samwel Mwaikenda amesema ujio wa timu hiyo ni fursa kwa vijana wanaopenda mchezo huo. Naye Mwenyekiti wa Mpira wa Kikapu Mkoa wa Singida, Bw. Shabani Dinya, amesema ziara hiyo itasaidia kuibua vipaji kwa vijana wa mkoa huu.

04/09/2026
HABARI PICHA:Picha mbalimbali za matukio ya Juma la Elimu ya Watu Wazima mwaka 2026 lililofanyika katika viwanja vya Shu...
02/09/2026

HABARI PICHA:

Picha mbalimbali za matukio ya Juma la Elimu ya Watu Wazima mwaka 2026 lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Tumaini - Viziwi, Manispaa ya Singida.

Washiriki walijadiliana mafanikio, changamoto na mikakati ya kuhakikisha hakuna mtu anayeachwa nyuma katika mpango wa K.K.K ( Kusoma, Kuandika na Kuhesabu).

Kimkoa maadhimisho yanatarajiwa kufanyika Septemba 16, 2026 katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Kauli mbiu ya mwaka huu ni: *"Kusoma kwa Maarifa ya Watu Duniani na Ustawi wa Jamii"*.

02/09/2026

MFANYABIASHARA, HUDUMA ZA LESENI ZIPO KARIBU NAWE!
Mfanyabiashara wa Manispaa ya Singida, kwa nini uteseke kutafuta huduma za leseni?
Njoo upate elimu kuhusu taratibu za biashara, usajili na leseni, pamoja na huduma muhimu zinazotolewa na Manispaa.
Usifanye biashara bila leseni!
Jifunze, pata huduma sahihi na endesha biashara yako kwa uhalali na kwa kujiamini.
Msikilize Afisa Biashara wa Manispaa ya Singida akieleza zaidi kuhusu huduma hizi.

HABARI PICHA:Picha za matukio mbalimbali katika Kikao cha Lishe cha Robo ya Nne, 2025/26 kilichofanyika leo Septemba 1, ...
02/09/2026

HABARI PICHA:Picha za matukio mbalimbali katika Kikao cha Lishe cha Robo ya Nne, 2025/26 kilichofanyika leo Septemba 1, 2026 katika ukumbi wa Chuo cha Maabara Singida.

DC GONDWE AAGIZA KAMATI YA LISHE KUFUATILIA UTEKELEZAJI WA AFUA YA LISHE MASHULENI.Johnson Soah na  Emmanuel Kimu Mkuu w...
01/09/2026

DC GONDWE AAGIZA KAMATI YA LISHE KUFUATILIA UTEKELEZAJI WA AFUA YA LISHE MASHULENI.
Johnson Soah na Emmanuel Kimu
Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhe. Godwin Gondwe, ameagiza Kamati ya Lishe ngazi ya Wilaya kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa afua ya lishe mashuleni ili kuhakikisha wanafunzi wote wanapata chakula.

Mhe. Gondwe ametoa maagizo hayo leo Septemba 1, 2026 wakati akiongea katika Kikao cha Robo ya Nne ya mwaka 2025/2026 kilichofanyika katika ukumbi Chuo cha Maabara Singida.

Amesema ni muhimu kamati hiyo kushirikiana na Maafisa wa Elimu ngazi zote, Watendaji wa Kata, Vijiji na Mitaa pamoja na Madiwani kuhakikisha wanafika katika shule zote.

"Nawaagiza Watendaji wa Kata kushirikisha viongozi wengine katika kata zenu kuhamasisha lishe mashuleni. Wakaazi, walezi, Madiwani, Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji pamoja na Maafisa Lishe wote mshirikishwe,". Amesisitiza Mhe. Gondwe.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Wilaya ameagiza Idara ya Afya kutoa elimu kwa akina mama wajawazito kuhusu umuhimu wa kuhudhuria kliniki mara kwa mara ili kufuatilia maendeleo yao na kupata ushauri wa wataalamu katika kila hatua ya ukuaji wa mtoto.

Aidha, amewataka wajawazito kuendelea kujifungulia katika vituo vya afya ili kuepuka vifo vinavyoweza kuzuilika, kwani Serikali imewekeza rasilimali za kutosha katika hospitali na vituo vya afya.

Kwa upande wake, Kamati ya Lishe Wilaya ya Singida imesema imepokea maagizo hayo na itaenda kuyatekeleza mara moja.

Address

Ipembe
Singida
236

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:29 - 17:00
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Singida Manispaa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Singida Manispaa:

Shortcuts

Share