04/01/2022
Je wajua kilimo cha mwani kinaweza kuwa k**a chanzo bora cha pato mbadala kwa jamii za pwani na kuchangia suala zima la uhifadhi wa mazingira ya pwani yetu?
Moja kati ya kilimo bahari kinachofanyika wilaya ya Pangani mkoani Tanga katika kijiji cha Ushongo mabaoni,Kipumbwi, Sange,Stahabu na Mikocheni ni kilimo cha mwani aina ya Spinosum.
Mwani huu umekuwa ukilimwa kwa miaka mingi sasa,simulizi mbalimbali za wakulima wa vijiji hivi zinasema yakwamba hapo awali walikuwa wakilima aina zote mbili yaani Spinosum na cotonii,kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa kwa sasa imeonekana Spinosum ikifanya vizuri zaidi ya cottonii kwa mazingira haya hivyo ikawalazimu kuhamisha nguvu zao zaidi kwenye aina hii ijapokuwa imekuwa na soko la bei ya chini kwa sasa ukilinganisha na cottonii.
Kilimo hiki kimekuwa msaada kwenye baadhi ya familia ziishizo katika ukanda huo.
Hivi sasa na kipindi cha karibuni soko kuu la mwani huo ni Zanzibar, wakulima wamekuwa wakilima na kuuza Zanzibar.
Kwa makadirio kwa kiwango cha chini kwa mwaka kijiji kimoja chaweza vuna tani 5 mpaka 6 kwa kilimo cha kienyeji na cha hali ya chini,na watu wachache.
Kwa mtazamo huu waweza ona na kutambua fika ya kwamba endapo kilimo hiki kikifanywa kwa utaalamu zaidi na kutafutiwa soko Zuri la uhakika kinaweza kubadili maisha ya jamii ziishizo maeneo hayo hususani kwa wakulima wenyewe.
Kwa mujibu wa maelezo ya baadhi ya wakulima kilio Chao kiko kwenye soko la uhakika na lenye bei nzuri, kwani kwa sasa wamekuwa wakiuza kilo moja chini ya sh 1000/= za kitanzania hali ambayo imekuwa ikimdidimiza mkulima kwaani mwani huu hjpimwa wakati ukiwa umekaushwa hali ambayo huupelekea kuingia kwa wingi kwani unakuwa mwepesi tayari.
Rai,wito na ombi la wakulima hawa:
1.wanaomba watafutiwe masoko mazuri yenye bei nzuri ya ununuzi na ya uhakika.
2.wanahitaji elimu zaidi juu ya kilimo hiki kwa njia za kitaalamu(elimu ya vitendo na nadharia).
3.Wanahitaji kupata safari za kujifunza na kuona toka kwa wengine waliofanikiwa.
na ustawi wa mazingira ya bahari #
and agriculture service for conservation #
coastal community network #
endelevu kwa ustawi wa pwani yetu #
bila mabomu unawezekana #
bila zana haramu unawezekana #
kwa ustawi wa utalii wetu #
πΎπ£π π¦ππ