Al -amal charitable foundation

Al -amal charitable foundation PUBLIC GROUP

*AL AMAL CHARITABL FOUNDATION* IS an institution that helps the community in general the elderly, orphans, and vulnerable people as well as solve the challenges of some areas eg college, mosque etc. support our activities
through
Amana:008141901010001
Name : AL AMAL CHARITABLE FOUNDATION
Branch codeSwift code:CORUTZTZ
Branch code:5013
CRDB BANK Acc.no 025731446500
5191576 Voda lipa
5132681 Tigo lipa
AL AMAL CHARITABLE FOUNDATION
mobile 📲: +255716810136
:+255772810136

03/09/2026

_*TAARIFA YA KUKABIDHI BAISKELI YA MATAIRI MATATU - TANGA*_

Ndugu wadau wa _Al Amal Charitable Foundation_,

Siku ya leo _Taasisi ya Al Amal Charitable Foundation_ imefanikiwa kufika katika _Kata ya Tangasisi, Mkoani Tanga_.

_Tumefanikiwa kumkabidhi kijana Abdullah Baiskeli ya Matairi Matatu_ kwa lengo la kumrahisishia shughuli zake za kila siku.

_TUNATOA SHUKRANI ZETU ZA DHATI KWA:_
1. _Ndugu zetu wa Sema - Tanga_ kwa ushirikiano mkubwa katika kutatua changamoto hii
2. _Ndugu yetu Ba Magongo_ kwa kusimamia zoezi zima la upatikanaji wa baiskeli hiyo
3. _Wadau wote_ waliotoa mchango wao

_"Na msaidiane katika wema na taqwa"_ [Al-Maidah: 2]
_Allah awalipe kila kheri na azidishie baraka_
---
_Imeandaliwa na:_
_Katibu_
_Salmin Ganga_
_0674435000_
_Al Amal Charitable Foundation_
_Tarehe: 03/09/2026_

_UCHANGIAJI WA MISAHAFU NA JUZUU - AWAMU YA PILI_  Assalam alaykum ndugu wadau wa Al Amal Charitable Foundation Awamu hi...
03/09/2026

_UCHANGIAJI WA MISAHAFU NA JUZUU - AWAMU YA PILI_

Assalam alaykum ndugu wadau wa Al Amal Charitable Foundation

Awamu hii _tunalenga sana vijiji kwenye madrasa zenye uhitaji_.
Wengi wa watoto wetu hawana Misahafu na Juzuu za kusomea.

_LENGO LETU:_
- _Juzuu: 1000_
- _Misahafu: 500_

_GHARAMA:_
- _Juzuu 1_ = Tsh _800/=_
- _Misahafu 1_ = Tsh _6,000/=_

_"Na msaidiane katika wema na taqwa"_ [Al-Maidah: 2]
Kila Juzuu na Mshafu wako ni sadaka njaria inshaAllah 🙏

_WALIOCHANGIA MPKA SASA:_
_1. Akhy - Misahafu (12)_ ✅

_NAMBA YA KUTUMA MCHANGO:_
_0674435000_
_Jina: Al amal charitable Foundation_

_Allah azidishie kila mchangiaji na awajalie heri duniani na Akhera_
_Jazakumullahu Khairan Kathiran_

_TAARIFA YA UKABIDHISHAJI WA VIFAA VYA SHULE_  _AWAMU YA TATU_ *Alhamdulillah Thumma Alhamdulillah* 🤲Kwa neema za Allah ...
02/09/2026

_TAARIFA YA UKABIDHISHAJI WA VIFAA VYA SHULE_
_AWAMU YA TATU_

*Alhamdulillah Thumma Alhamdulillah* 🤲

Kwa neema za Allah na michango yenu, _AL AMAL CHARITABLE FOUNDATION_ tumefanikiwa kukamilisha _AWAMU YA TATU_ ya kugawa mabegi pamoja na viatu kwa watoto Mayatima.

*Eneo:*
_Pande Mabayani_

*Tarehe ya Ukabidhishaji:*
_Jumamosi, Tarehe 30/08/2026_

*Walionufaika:*
_Watoto Mayatima 3_

*Vifaa Vilivyokabidhiwa:*
1. _Mabegi ya Shule 3_
2. _Viatu__1

*Madhumuni:*
Kuwasaidia watoto Mayatima kupata mahitaji ya shule na kuwapunguzia walezi wao mzigo wa gharama za vifaa vya shule.

Tunamshukuru Allah kwa kutuwezesha na tunawashukuru wote waliotoa michango yao. Allah awalipe kila kheri na awajalie baraka katika mali zenu na familia zenu.

_"Na msaidiane katika wema na taqwa"_
_Jazakallahu Khairan_ 💚
_AL AMAL CHARITABLE FOUNDATION_

31/08/2026

_TAARIFA YA UKABIDHISHAJI WA WALKING FRAME_
_AL AMAL CHARITABLE FOUNDATION_

Kwa baraka za Allah na michango yenu,

tumefanikiwa kukabidhi _WALKING FRAME_ kwa ajili ya kumuwezesha kutembea kwa urahisi.
*Waliyekabidhiwa:*
_Bi. Mwanakombo_
_Waziri Mkazi wa Pande Mabayani_
*Tarehe ya Ukabidhishaji:*
_Jumamosi, Tarehe 30/08/2026_
*Madhumuni:*
Kusaidia Bi. Mwanakombo katika shughuli zake za kila siku na kumpunguza adha ya kutembea.

Tunamshukuru Allah kwa kutuwezesha na tunawashukuru wote waliotoa michango yao. Allah awalipe kila kheri na awajalie afya njema.

_"Na msaidiane katika wema na taqwa"_
_Jazakallahu Khairan_ 💚
_AL AMAL CHARITABLE FOUNDATION_

_*CHANGIA UPATIKANAJI WA JUZUU NA MISAHIFU*__KWA AJILI YA MADRASA ZENYE UHITAJI_  _AL AMAL CHARITABLE FOUNDATION__ALHAMD...
29/08/2026

_*CHANGIA UPATIKANAJI WA JUZUU NA MISAHIFU*_
_KWA AJILI YA MADRASA ZENYE UHITAJI_
_AL AMAL CHARITABLE FOUNDATION_

_ALHAMDULILLAH_
Tusaidie watoto wa madrasa wapate Misahafu na Juzuu ili wasome na waihifadhi Kitabu cha Allah 🤲

*BEI YA VIFAA:*
_1. JUZUU 1_ - Tsh 800/=
_2. MISHAFU_ - Tsh 6,000/=

_"*Khairukum man ta'allamal Qur'an wa 'allamah*"_
_*Bora yenu ni anayejifunza Qur'an na anayemfundisha*_
---
_NAMBA ZA KUCHANGIA:_
_0674435000_
_Jina: AL AMAL CHARITABLE FOUNDATION_

Mchango wowote unakubaliwa 🙏 Hata ukichangia Juzuu 1 au Mshafu 1 umetoa sadaka yako.

Allah awalipe kila kheri watoa sadaka na awajalie wema duniani na Akhera.

_Jazakallahu Khairan_

Tunaendelea kupokea ndugu

_AL AMAL YAKABIDHI PEMPAS KWA BI FATMA - NGAMIAN KUSINI_*TAREHE: 26/08/2026*Ndugu wadau wa _Al Amal Charitable Foundatio...
26/08/2026

_AL AMAL YAKABIDHI PEMPAS KWA BI FATMA - NGAMIAN KUSINI_

*TAREHE: 26/08/2026*

Ndugu wadau wa _Al Amal Charitable Foundation_,

Alhamdullilah siku ya Jana tumefanikiwa kufika katika *Kata ya Ngamian Kusini, Mtaa wa Azimio A*.

Tulifanikiwa kukabidhi *Pempas* kwa mama yetu *Bi. Fatma* kwa lengo la kumuwezesha ndugu yetu.

Aidha, Taasisi imefanikiwa pia *kumuekea miundombinu ya kibaraza nyumbani kwake* kwa lengo la kumrahisishia kupanda na kushuka kwa kutumia kiti.

Taratibu za kumfikishia *matibabu ya hospitali* zinaendelea InshaAllah.

_“Na msaidiane katika wema na taqwa”_ [Al-Maidah: 2]
_Jazakumullahu Khairan_ kwa michango yenu yote.
---
*Imeandaliwa na:*
*Katibu: Salmin Ganga*
*0674435000*
*AL AMAL CHARITABLE FOUNDATION*
*26/08/2026*

*TAARIFA YA UKABIDHISHAJI WA JENEZA - TANGASISI* Ndugu Wadau wa *Al Amal Charitable Foundation*Siku ya jana tarehe *19/0...
20/08/2026

*TAARIFA YA UKABIDHISHAJI WA JENEZA - TANGASISI*

Ndugu Wadau wa *Al Amal Charitable Foundation*

Siku ya jana tarehe *19/08/2026*,
*Taasisi ya Al Amal Charitable Foundation* ikishirikiana na *Taasisi ya Afya Foundation* tulifanikiwa kufika *Kata ya Tangasisi, Masjid Ihsan* kukabidhi *Jeneza*.

Alhamdulillah.
Kwa niaba ya Ustadhi, tunatoa shukran za dhati kwa taasisi zote zilizoshiriki katika ukabidhishaji huu kwani ilikuwa ni changamoto kubwa katika msikiti huo.

_Imeandaliwa na:_
_Salmin Ganga_
_Katibu - Al Amal Charitable Foundation_
_Simu: 0674435000_
_Tarehe: 20/08/2026_

_AL AMAL NA AFYA FOUNDATION YAFIKA AMBONI KUKABIDHI KITI MWENDO_ 🦽*Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakatuh*  Ndugu W...
19/08/2026

_AL AMAL NA AFYA FOUNDATION YAFIKA AMBONI KUKABIDHI KITI MWENDO_ 🦽

*Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakatuh*
Ndugu Wadau wa *Al Amal Charitable Foundation*,

*Alhamdulillah* Siku ya leo *19/08/2026* tumefanikiwa kufika *Kata ya Mzizima, Amboni - Kijiji cha Majimoto, Mtaa wa Mbwa Mkali* katika utekelezaji wa huduma kwa jamii.

Taasisi ya *Al Amal Charitable Foundation* ikishirikiana na *Afya Foundation* imefanikiwa kukabidhi *Kiti Mwendo 1* kwa *Mzee Rashid*.

Mzee Rashid hana miguu, amekatwa miguu kutokana na ugonjwa wa kisukari. Tunamuombea Mwenyezi Mungu ampe afya na subira.

_SHUKRANI_
Taasisi inatoa shukrani za dhati kwa *Ndugu zetu wa Afya Foundation* kwa ushirikiano mkubwa katika kushirikiana kutatua changamoto zinazokabili jamii yetu.
Pia tunawashukuru *wadau wote* wanaendelea kutusaidia kwa fedha, muda na vifa.

Tunaendelea kuwaomba dua ili tuweze kuwafikia wengine zaidi. _Jazakumullahu Khairan_

*Imeandaliwa na:*
*Katibu: Salmin Ganga*
*Al Amal Charitable Foundation*
*Simu: 0674435000*
_19/08/2026_

_AL AMAL NA AFYA FOUNDATION WAKABIDHI KITI MWENDO NGAMIAN KUSINI, TANGA_ 🦽*Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakatuh* ...
18/08/2026

_AL AMAL NA AFYA FOUNDATION WAKABIDHI KITI MWENDO NGAMIAN KUSINI, TANGA_ 🦽

*Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakatuh*
Ndugu Wadau wa *Al Amal Charitable Foundation*,

Napenda kuwataarifu kuwa siku ya leo *18/08/2026* tumefanikiwa kufika *Kata ya Ngamian Kusini, Mtaa wa Azimio A* katika kutekeleza huduma kwa jamii.

*Alhamdulillah* Taasisi ya *Al Amal Charitable Foundation* pamoja na *Afya Foundation* tumeshirikiana katika kukabidhi *Kiti Mwendo 1* kwa *ndugu yetu Bi. Fatuma*.

Bi. Fatuma amepata maradhi ya kupooza baadhi ya sehemu za mwili wake na kwa sasa anaitaji *matibabu ya viungo* ili afya yake iweze kuimarika.

Ziara hii pia ilikuwa na lengo la kusikiliza changamoto za ndugu yetu na kuona namna ya kumsaidia zaidi.

_SHUKRANI_
Taasisi inatoa shukrani za dhati kwa *Ndugu zetu wa Afya Foundation* kwa ushirikiano mkubwa katika kutatua changamoto zinazokabili jamii yetu kwa ujumla.
Pia tunawashukuru *wadau wote* wanaendelea kutusaidia ili tuweze kufikia walengwa zaidi.

Tunaendelea kuwaomba dua na msaada wenu. _Jazakumullahu Khairan_

*Imeandaliwa na:*
*Katibu: Salmin Ganga*
*Al Amal Charitable Foundation*
*Simu: 0674435000*
_18/08/2026_

_RIPOTI YA UJUMLA - KUKABIDHI MSAADA WA VIFAA_*Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakatuh*  Ndugu Wadau wa *Al Amal Cha...
18/08/2026

_RIPOTI YA UJUMLA - KUKABIDHI MSAADA WA VIFAA_

*Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakatuh*
Ndugu Wadau wa *Al Amal Charitable Foundation*,

*RIPOTI YA UJUMLA*
Taasisi ya *Al Amal Charitable Foundation* tunapenda kutoa ripoti ya ujuMLA katika *Kata ya Mabawa, Mtaa wa Mkanjunibi*.

*Alhamdulillah* Taasisi imefanikiwa kukamilisha ziara yake katika Kata ya Mabawa kwa lengo la kutatua changamoto kwa ndugu zetu wenye uhitaji.

_MISAADA ILIYOTOLEWA_
Taasisi imefanikiwa kukabidhi kwa jumla *Ndugu 5 wenye uhitaji*:
1. *Viti Mwendo* kwa *vijana wetu 3*
2. *Vikongo* kwa *Mzee Joni*
3. *Kifaa cha kutembelea* kwa *Bibi yetu 1*

_OMBI LETU_
Hivyo tunawaomba *Wadau* tusiache kushiriki katika kutatua changamoto katika jamii yetu kwa ujumla.
Pia tunawaomba *viongozi wa mashirika mbalimbali* kushiriki nasi katika kutatua changamoto hizi.

_SHUKRANI_
Tunatoa shukrani za dhati kwa *wale wote waliochangia* kupatikana kwa vifaa vyote kwa ujumla.
Pia tunatoa shukrani za dhati kwa *Ndugu zetu Jai* kwa kutusaidia viti hivyo kwaajili ya ndugu zetu wenye uhitaji.

_Jazakumullahu Khairan_ kwa mchango wenu, muda wenu na vifa.

_Jazakumullahu Khairan_

*RIPOTI IMEANDALIWA NA:*
*Katibu: Salmin Abbas Ganga*
*Al Amal Charitable Foundation*
_17/08/2026_

Address

Tanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Al -amal charitable foundation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category