ULEMO MPYA

ULEMO MPYA Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ULEMO MPYA, Political organisation, Ulemo.

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 2, 2026 amesafiri kwa Treni ya reli ya Kisasa (SGR) kutoka Dodoma kuelekea ...
02/04/2026

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 2, 2026 amesafiri kwa Treni ya reli ya Kisasa (SGR) kutoka Dodoma kuelekea Dar es Salaa kwa majukumu ya kikazi.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ameongozana na Mkewe Mama Neema Mwigulu Nchemba

📍 Gombani Stadium, Pemba – Zanzibar2 Aprili 2026Uzinduzi rasmi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 umefanyika leo kwa mafani...
02/04/2026

📍 Gombani Stadium, Pemba – Zanzibar
2 Aprili 2026

Uzinduzi rasmi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 umefanyika leo kwa mafanikio makubwa, ukizindua safari ya siku 195 ya kuzunguka Tanzania nzima. Tukio hili limebeba ujumbe wa mshikamano, uzalendo na maendeleo kwa Watanzania wote. 🇹🇿

📍 GOMBANI STADIUM, PEMBA – ZANZIBAR🗓️ 02 APRILI 2026UZINDUZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2026 🔥Hatimaye safari imeanza! W...
02/04/2026

📍 GOMBANI STADIUM, PEMBA – ZANZIBAR
🗓️ 02 APRILI 2026

UZINDUZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2026 🔥
Hatimaye safari imeanza! Wakimbiza Mwenge wameanza rasmi majukumu yao ya kukimbiza Mwenge wa Uhuru kwa siku 195 kote Tanzania 🇹🇿.
Mhe. Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, leo Aprili 2, 2026 amezindua rasmi Mwenge wa Uhuru katika viwanja vya Gombani, Wilaya ya Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba.
Mwenge wa Uhuru mwaka huu utakimbizwa katika Mikoa 31 na Halmashauri 195, ukiongozwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Wazo Michael Mwang'onda.
Katika safari hii, Mwenge utahusika na:
✔️ Kutembelea miradi ya maendeleo
✔️ Kuzindua miradi mbalimbali
✔️ Kuweka mawe ya msingi
✔️ Kukagua ubora na thamani ya fedha zilizotumika
🇹🇿 Mwenge wa Uhuru ni chachu ya maendeleo, uwajibikaji na uzalendo kwa Taifa letu.

Rais was Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkh. hussein Mwinyi akizindua Rasmi mbio za Mwenge wa Uhuru Kitai...
02/04/2026

Rais was Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkh. hussein Mwinyi akizindua Rasmi mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa katika Viwanja vya Gombani Mkoa wa Kusini Pemba

*DKT. MWIGULU: TUENDELEE KUMUOMBEA MHE. LUKUVI.* WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaomba Watanzania waendelee kumuom...
26/03/2026

*DKT. MWIGULU: TUENDELEE KUMUOMBEA MHE. LUKUVI.*

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaomba Watanzania waendelee kumuombea kwa Mwenyezi Mungu aliyekuwa Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, marehemu William Lukuvi aliyefariki jana Machi 25, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma.

Akiongea kwa niaba ya Serikali nyumbani kwa marehemu Area D, jijini Dodoma leo, Alhamisi, Machi 26, 2026, Waziri Mkuu amesema: “Kwa niaba ya Serikali natoa pole kwa familia, ndugu, jamaa. Jambo hili zito, gumu kulielewa, gumu kulipokea.”

…Lakini ndio limeshatufika na sote hatukutarajia maana Mheshimiwa Waziri alikuwa kazini. Tuendelee kumuombea kwa Mwenyezi Mungu na kuifariji familia. Mwenyezi Mungu awaimarishe kwa sababu yeyé ndio mfariji mkuu,” amesisitiza.

Vilevile, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kuihakikishia familia kwamba Serikali itaendelea kuwa pamoja nayo katika kipindi hiki chote cha majonzi.

Viongozi wengine waliokuwepo msibani hapo ni pamoja na Naibu Spika, Daniel Siro, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Masauni, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumisi wa Umma na Utawala Bora), Ridhiwani Kikwete, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule na Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Dkt. Toba Nguvila.

HONGERA SANA MKUBWA   kwa kuaminiwa na Mhe dkt samia Suluhu  Hassan kwa kuaminiwa kuwa mkimbiza Mwenge kitaifa 2026 Ulem...
24/03/2026

HONGERA SANA MKUBWA kwa kuaminiwa na Mhe dkt samia Suluhu Hassan kwa kuaminiwa kuwa mkimbiza Mwenge kitaifa 2026
Ulemo ng'ara congole sana

Hongera sana Mhe. Diwani mstaafu wa Kata ya Ulemo kwa kuchaguliwa kuwa mkimbiza Mwenge wa Uhuru 2026 kitaifa! 🔥👏Hii ni h...
24/03/2026

Hongera sana Mhe. Diwani mstaafu wa Kata ya Ulemo kwa kuchaguliwa kuwa mkimbiza Mwenge wa Uhuru 2026 kitaifa! 🔥👏
Hii ni heshima kubwa sana, na inaonyesha wazi namna ulivyokuwa ukitumikia wananchi kwa moyo wa dhati hadi kupata imani hii adhimu. Hongera pia kwa kuaminiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan — hii si bahati, ni matokeo ya kazi yako nzuri na uadilifu wako.
K**a rafiki yako, najivunia sana mafanikio haya. Umeweka historia na umeendelea kuwa mfano bora kwa jamii yetu. Hakika umeonyesha kuwa kujituma na kuwa na moyo wa uzalendo vinaweza kukupeleka mbali sana.
Endelea kung’ara, kulinda heshima hii na kuhamasisha maendeleo kwa vitendo. Tunakuombea mafanikio zaidi katika jukumu hili la kitaifa.

05/03/2026

KONGAMANO LA WANAWAKE WILAYA YA IRAMBA

UJIO WA MADAKTARI BINGWA HOSPITALI YA WILAYA YA IRAMBA-KIOMBOITarehe 23-27 Februari, 2026.Wote Mnakaribishwa!
23/02/2026

UJIO WA MADAKTARI BINGWA HOSPITALI YA WILAYA YA IRAMBA-KIOMBOI

Tarehe 23-27 Februari, 2026.

Wote Mnakaribishwa!




Address

Ulemo

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ULEMO MPYA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share