Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar

Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Government Official, ZURA BUILDING, MAISARA, Zanzibar City.

Kikao hicho kinalenga kuimarisha  utendaji wa kikosi kazi hicho kwa kuwajengea uwezo wajumbe wa kikosi kazi, pamoja na k...
12/06/2026

Kikao hicho kinalenga kuimarisha utendaji wa kikosi kazi hicho kwa kuwajengea uwezo wajumbe wa kikosi kazi, pamoja na kujadili utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo ya sekta ya ufugaji wa mazao ya baharini nchini.

"Uchumi wa Buluu Kwa Maendeleo Endelevu"
05/06/2026

"Uchumi wa Buluu Kwa Maendeleo Endelevu"

MWANI NI CHAKULA, DAWA NA KIPODOZIZao la mwani ni zao linalolimwa kwa wingi visiwani Zanzibar limeendelea kupata umaaruf...
04/06/2026

MWANI NI CHAKULA, DAWA NA KIPODOZI

Zao la mwani ni zao linalolimwa kwa wingi visiwani Zanzibar limeendelea kupata umaarufu kutokana na matumizi yake mbalimbali katika chakula, dawa na vipodozi.

Akizungumza wakati wa ziara ya Madiwani katika Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Mwenyekiti wa Wakulima wa Mwani katika Kijiji cha Muungoni, Bi Mariam Mohammedi, alisema zao hilo limekuwa na mchango mkubwa katika kuboresha maisha ya wakulima na kukuza uchumi wa jamii .

Ziara hiyo, ambayo leo imeingia siku ya pili, inalenga kuwapa Madiwani fursa ya kujifunza kuhusiana na shughuli mbalimbali zinazochangia maendeleo ya Uchumi wa Buluu nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji na Utumishi Ndugu Issa Suleiman Ali alisema Serikali imefanikiwa kukuza uchumi kupitia kilimo cha mwani na kwamba kuna mipango madhubuti ya kuongeza uwezo wa uzalishaji kwa kuanzisha kiwanda kingine cha kuchakata zao hilo.

Aidha kwa sasa kilo moja ya mwani mkavu unauzwa kwa wastani wa shilingi 12,000 hali inayowapa wakulima Hamasa ya kuendeleza uzalishaji.

Katika mwendelezo wa ziara hiyo, Madiwani walipata fursa ya kutembelea Eneo maalumu la uhifadhi wa viumbe wa Baharini lililopo katika Msitu wa Jozani ambapo walijifunza kuhusu uhifadhi wa mazingira na viumbe mbalimbali wakiwemo kobe wa nchi kavu na Kasa wa Baharini.

Ziara hiyo imeelezwa kuwa ni muhimu katika kuongeza uelewa wa viongozi hao kuhusu fursa za kiuchumi zinazotokana na Rasilimali za Bahari na mazingira ya asili.

"Uchumi wa Buluu Kwa Maendeleo Endelevu"
28/05/2026

"Uchumi wa Buluu Kwa Maendeleo Endelevu"

27/05/2026
Serekali imesema itahakikisha inatunza mazingira ya Bahari ili kulilinda zao la Mwani lisiharibiwe na mabadiliko ya tabi...
26/05/2026

Serekali imesema itahakikisha inatunza mazingira ya Bahari ili kulilinda zao la Mwani lisiharibiwe na mabadiliko ya tabia nchi yanayosababisha uharibifu wa Mazingira na kurejesha nyuma maendeleo ya uzalishaji wa zao hilo.

Akizunguimza katika ufunguzi wa warsha ya 29 ya utafiti kwa mwaka 2026 ya mageuzi ya uchumi wa buluu amesema zao la mwani ni zao lenye tija kwa sasa na ni muhimili wa uchumi wa Zanzibar kupitia rasilimali ya bahari hivyo ni vyema kuhakikisha linapewa kipaumbele kwa kujengewa misingi imara ya usimamizi kwa kupambana na uharibifu wowote unaotakana na mazingira ili wakulima walime kwa bidi.

Aidha amesema warsha hii inalengo la kuonesha jamii namna ya kuzitumia fursa za Uchumi wa Buluu lakini pia kuboresha baadhi ya maeneo ya bahari ambayo ni muhimu kwa uchumi wa Buluu lakini pia na kuyatunza ipaswavyo ili yaweze kutumika kwa matumizi endelevu ya sasa na baadae

Serikali ya Jamhuri ya Muugano kwa kushirikiana pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeandaa Warsha maalum ya ut...
22/05/2026

Serikali ya Jamhuri ya Muugano kwa kushirikiana pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeandaa Warsha maalum ya utekelezaji mpango mpya wa maendeleo yenye lengo la kubadilisha Uchumi ili kufikia malengo yaliyowekwa na Serikali ya Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika kikao cha uzinduzi wa Warsha ya 29 ya utafiti kuhusu mageuzi ya Uchumi wa Buluu , Katibu mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar Kepteni Hamad Bakar Hamad amesema kupitia Warsha hiyo tayari Serekali ya Zanzibar imepanga hatua muhimu za kuanzishwa kwa nyaraka kuu za sera ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar pamoja na mikakati ya utekelezaji huku Serikali ya Muungano ikiendelea kupitia Sera zake kuu ili kuziainisha na mpango wa dira ya maendeleo ya Mwaka 2025 iliyozinduliwa mwaka jana.

Aidha amesema Warsha hiyo itakua na malengo makuu matatu ikiwemo kuibua fursa mahususi zilzomo katika sekta ya Uchumi wa Buluu pamoja na kukabiliana na changamoto zilizomo.

Vilevile kutathimini na kuchambua mikakati ya utekelezaji bora wa Sera na Mipango ya Uchumi wa Buluu ikiwemo kuimarisha uhusiano na sekta nyengine ili kuongeza ushindani wa taifa ikiambatana pamoja na kuimarisha mitazamo ya uchambuzi kuhusu utekelezaji endelevu wa Uchumi wa Buluu kwa kuchunguza uzoefu bora wa Afrika na Duniani.

Kikao cha Maandalizi ya Ushiriki wa Kongamano la 11 la Bahari yetu (Our Ocean Conference OOC 11).Kongamano la 11 la Baha...
22/05/2026

Kikao cha Maandalizi ya Ushiriki wa Kongamano la 11 la Bahari yetu (Our Ocean Conference OOC 11).
Kongamano la 11 la Bahari yetu linatarajiwa kufanyika tarehe 16- 18 Juni, 2026 Mombasa Kenya.

Kongamano hili ni moja ya jitihada za Kimataifa katika kutunza, kuhifadhi na kutumia Bahari kwa Uendelevu.

Aidha Kongamano hili linaendeshwa na Kaulimbiu inayosema "Our Ocean, Our Heritage, Our Future" ikiwa na maana ya Bahari "Yetu, Urithi Wetu, Mustakabali Wetu".

Vile vile Kongamano hili linalenga maeneo makuu ya ustahamilivu wa mabadiliko ya Tabianchi katika Bahari, Uvuvi Uchumi wa Buluu Endelevu,Maeneo yanayolindwa ya Bahari,Usalama wa Bahari na Uchafuzi wa Mazingira.

Kikao cha wadau wa sekta ya mwani Zanzibar  "Zanzibar Seaweed Multi-Stakeholder Action Group (ZSMAG)" Kikao hicho ni mue...
21/05/2026

Kikao cha wadau wa sekta ya mwani Zanzibar "Zanzibar Seaweed Multi-Stakeholder Action Group (ZSMAG)"
Kikao hicho ni muendelezo wa vikao vya kila robo mwaka kinachowakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo taasisi za serikali na binafsi, kujadili maendeleo ya sekta ya mwani, kuimarisha ushirikiano na kutafuta fursa za kukuza uchumi wa buluu Zanzibar.

Address

ZURA BUILDING, MAISARA
Zanzibar City

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share