Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais

Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Karibu Kwenye Ukurasa Rasmi wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar

Kwa upande wa Zanzibar kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kitafanyika Jumamosi tarehe 6 Juni, 2026 kati...
04/06/2026

Kwa upande wa Zanzibar kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kitafanyika Jumamosi tarehe 6 Juni, 2026 katika eneo la Kiwani, Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba, ambapo Makamu wa Pili wa Rais, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.

04/06/2026
04/06/2026

TAARIFA YA KAIMU WA WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS MHESHIMIWA HAMZA HASSAN JUMA KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI.

Kwa upande wa Zanzibar kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kitafanyika Jumamosi tarehe 6 Juni, 2026 katika eneo la Kiwani, Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba, ambapo Makamu wa Pili wa Rais, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika juhudi za kukabiliana na athari za maba...
04/06/2026

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika juhudi za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi ili kulinda mazingira na kuhakikisha maendeleo endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Wito huo umetolewa na, KAIMU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais,Mhe. Hamza Hassan Juma, katika taarifa maalumu ya kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026 aliyoitoa Ofisini kwake Migombani _ Zanzibar.

Amesema mabadiliko ya tabianchi yameendelea kuathiri Zanzibar kupitia kuongezeka kwa joto, kupungua kwa mvua za msimu, mafuriko na mmomonyoko wa fukwe kutokana na kuongezeka kwa kina cha bahari.

Mhe. Hamza ameeleza kuwa Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na changamoto hiyo ikiwemo kutekeleza sera, sheria na mikakati ya mazingira, kuimarisha elimu ya mazingira, kujenga uwezo wa jamii na taasisi pamoja na kuendeleza shughuli mbadala za kiuchumi zinazolinda mazingira.

Aidha, amesema Serikali imetenga shilingi bilioni 5 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya shughuli za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, ikilinganishwa na shilingi bilioni 4.5 zilizotengwa mwaka 2025/2026.

Amesema maadhimisho ya mwaka huu yanafanyika chini ya kaulimbiu ya Zanzibar isemayo, “Jamii inaanza na wewe; chukua hatua kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa kulinda Zanzibar yetu,” ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono kaulimbiu ya kimataifa ya “Climate Action.”

Katika wiki ya maadhimisho, Mhe. Hamza amesema shughuli mbalimbali zimefanyika Unguja na Pemba zikiwemo usafi wa mazingira, upandaji wa miti na mikoko, mafunzo kwa viongozi wa ngazi za jamii pamoja na kampeni za uhamasishaji kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Hatahivyo Mhe. Hamza amewataka wananchi kuendelea kuchukua hatua za kuhifadhi mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa maslahi ya taifa na vizazi vijavyo.

Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kwa Zanzibar kinatarajiwa kufanyika Juni 6, 2026 katika eneo la Kiwani, Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba, ambapo Makamu wa Pili wa Rais, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.

26/05/2026

Eid Aidha njema kwa Waislamu wote na jamii kwa ujumla.
Tuitumie sikukuu hii adhimu kueneza upendo, kuimarisha mshik**ano, kusaidiana kwa moyo wa dhati na kudumisha amani katika jamii yetu.

Tuige mafunzo ya uvumilivu, kujitoa na huruma kwa kuwajali wenye uhitaji na kuendeleza umoja wetu k**a taifa.
Mwenyezi Mungu azikubali ibada zenu, azijaalie familia zenu afya njema, furaha tele, mafanikio na maisha yenye baraka daima.

Eid Mubarak!

26/05/2026

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, inaungana na mataifa mengine duniani katika Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika kila ifikapo tarehe 05 Juni ya kila mwaka. Aidha, maadhimisho haya yana lengo la kuhifadhi mazingira pamoja na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Kaulimbiu ya mwaka huu kwa Zanzibar ni: “Jamii inaanza na wewe; chukua hatua katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa kulinda Zanzibar yetu.”

Aidha, kwa mwaka huu 2026 Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kupitia Idara ya Mazingira itafanya shughuli mbalimbali za uhifadhi na utunzaji wa mazingira ikiwemo:

1. Matembezi ya uhamasishaji kutoka Kendwa hadi Uwanja wa Mauwani
2. Upandaji wa miti ya juu pamoja na mikoko
3. Usafi wa mazingira katika maeneo mbalimbali
4. Mikutano ya uelimishaji wa jamii pamoja na Masheha na Waheshimiwa Madiwani
5. Mafunzo ya usarifu wa asali na vifungashio kwa vikundi vya wafugaji wa nyuki

Kilele cha maadhimisho hayo kitafanyika siku ya jumamosi tarehe 06 Juni 2026 Kiwani, Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba, katika Uwanja wa Mpira wa Mauwani.

Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla

Wananchi wote, taasisi mbalimbali, vikundi vya kijamii pamoja na wadau wa mazingira wanakaribishwa kushiriki kwa wingi katika shughuli hizi muhimu kwa maendeleo endelevu na ustawi wa mazingira yetu.
Kwa pamoja tushirikiane kuilinda Zanzibar dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

“UHIFADHI WA MAZINGIRA NI JUKUMU LETU SOTE.”

KATIBU MKUU OMKR AHIMIZA UHIFADHI WA MAZINGIRA NA UFUGAJI WA NYUKI WA KISASA ZANZIBAR.Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwa...
21/05/2026

KATIBU MKUU OMKR AHIMIZA UHIFADHI WA MAZINGIRA NA UFUGAJI WA NYUKI WA KISASA ZANZIBAR.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Bi.Maryam Juma Abdullah amesema jamii inapaswa kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wa mazingira kupitia upandaji miti, uhifadhi wa mikoko pamoja na kuendeleza ufugaji wa nyuki wa kisasa ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani yaliyofanyika Bumbwini Mafufuni, Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja kupitia Zanzibar Joint Program (ZJP),Bi. Maryam alisema juhudi za pamoja zinahitajika katika kulinda mazingira na kuimarisha maisha ya wananchi.

Alisema shughuli za uhifadhi wa mazingira na ufugaji wa nyuki zina mchango mkubwa katika kulinda bioanuai, kuongeza uzalishaji wa mazao pamoja na kukuza uchumi wa wananchi kupitia bidhaa za asali.

Katika maadhimisho hayo, wananchi walishiriki katika zoezi la upandaji wa miti ya mikoko pamoja na ugawaji wa mizinga ya kisasa kwa vikundi vya wafugaji wa nyuki ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha matumizi ya njia bora za ufugaji zinazolinda mazingira.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania, Ms. Susan Ngongi Namondo, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa pamoja katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kupitia miradi ya uhifadhi wa mazingira na maendeleo endelevu.

Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na wananchi wa Shehia za Bumbwini, wadau mbalimbali wa mazingira, wawakilishi wa Umoja wa Mataifa, mabalozi kutoka Kenya, viongozi kutoka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais pamoja na maafisa kutoka Idara ya Misitu Zanzibar.

Show translation

Address

Migombani
Zanzibar City

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais:

Share