Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais

Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Karibu Kwenye Ukurasa Rasmi wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar

29/08/2026

KAMBI NA MATIBABU YA MACHO INAYOENDELEA KUTOA HUDUMA KATIKA MKOA WA KASKAZINI - UNGUJA HADI TAREHE 31 AGOSI, 2026

Awamu ya pili itafanyika Mkoa wa Mjini katika Kituo cha afya -Sebleni kwa Wazee kuanzia tarehe 01 - 04 Septemba, 2026.

29/08/2026

''TUEPUKE KUTUMIA DAWA ZA MACHO BILA YA USHAURI WA WATAALAMU''

KAIMU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Mheshimiwa Hamza Hassan Juma akizungumza na wananchi wakati akifungua Kampeni ya Uchunguzi na Matibabu ya Macho, ilianza katika Mkoa wa Kaskazini,Unguja - leo Agosti 29,2026

29/08/2026

KAIMU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Mheshimiwa Hamza Hassan Juma akizungumza na wananchi wakati akifungua Kampeni ya Uchunguzi na Matibabu ya Macho, ilianza katika Mkoa wa Kaskazini,Unguja - leo Agosti 29,2026.

SERIKALI YAWATAKA WADAU KUSHIRIKIANA KATIKA KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA ZANZIBARKAIMU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa K...
29/08/2026

SERIKALI YAWATAKA WADAU KUSHIRIKIANA KATIKA KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA ZANZIBAR

KAIMU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Mhe. Hamza Hassan Juma, amewataka wadau wa afya kutoka sekta binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuimarisha huduma za afya ya macho nchini.

Wito huo ameutoa katika Kituo cha Afya Kinduni, Wilaya ya Kaskazini A, wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Uchunguzi na Matibabu ya Macho, inayolenga kuwafikishia wananchi huduma za afya ya macho.

Mhe. Hamza amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na wadau mbalimbali katika kusaidia utoaji wa huduma za afya kwa wananchi.

Amesema afya ya macho ni muhimu katika maisha ya kila siku, kwani uwezo wa kuona humwezesha mtu kushiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

Aidha, amesisitiza kuwa watu wenye ulemavu wanapaswa kupata huduma za afya ya macho bila ubaguzi, k**a ilivyo kwa wananchi wengine.

“Ni wajibu wetu sote kuhakikisha kila mtu anapata huduma na hakuna anayeachwa nyuma,” alisisitiza Mhe. Hamza.

Vilevile, amewataka wataalamu wa afya kuendelea kutoa huduma bora na stahiki kwa wananchi, huku akiwahimiza wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja kujitokeza kwa wingi kutumia fursa hiyo ya uchunguzi na matibabu.

Akitoa maelezo kuhusu kambi hiyo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu, Mhandisi Ussy Khamis Debe, amesema tathmini mbalimbali zinaonesha kuwa idadi kubwa ya watu wenye ulemavu wanakabiliwa na changamoto za uoni, hivyo kuwepo kwa kambi hiyo kutasaidia kupunguza tatizo hilo.

Ameeleza kuwa kwa upande wa Kaskazini Unguja, kambi hiyo inalenga kuwafikia wananchi 2,050, ambapo watu 400 wanatarajiwa kupatiwa miwani na wengine 400 kufanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho.

Mhandisi Debe amewashukuru wataalamu kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa kushirikiana na Wizara ya Afya pamoja na wananchi kwa kujitokeza kutumia huduma zinazotolewa katika kambi hiyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Qatar Charity nchini Tanzania, Amjad Altahhan, amesema taasisi hiyo, mbali na kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya macho, inatarajia kushirikiana na Serikali katika kutoa huduma nyingine za afya, ikiwemo kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza, kwa lengo la kusaidia wananchi.

Naye, Mkuu wa Kitengo cha Utafiti na Mafunzo kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Robert Mshiro, amesema kambi hiyo ya siku tatu inatoa huduma za uchunguzi, matibabu pamoja na upasuaji wa mtoto wa jicho.

Amesema upasuaji huo utatumia teknolojia ya kisasa ya matundu, inayolenga kupunguza majeraha na maumivu kwa wagonjwa pamoja na kurahisisha mchakato wa matibabu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Kinga na Elimu ya Afya, Dkt. Faiza Bwanakheri Abbas, ameishukuru Qatar Charity kwa kuleta huduma za matibabu Zanzibar na kuwasogezea wananchi huduma hizo, huku akiwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kutumia fursa hiyo.

Nao wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, akiwemo Thania Rashid Seif, wameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwasogezea huduma za matibabu karibu na maeneo yao, wakisema hatua hiyo itawasaidia kupunguza gharama za kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya.

Kambi hiyo imeandaliwa na Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu kwa kushirikiana na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Wizara ya Afya kwa udhamini waTaasisi ya Qatar Charity.

Katika uzinduzi huo, Mhe. Hamza pia alipata nafasi ya kutembelea gari maalumu la uchunguzi wa macho na kujionea namna huduma za uchunguzi na matibabu zinavyotolewa kwa wananchi.

28/08/2026

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu Zanzibar, Mhandisi Ussy Khamis Debe, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kambi inayolenga kuwafanyia uchunguzi na matibabu ya macho wananchi wa Zanzibar.

Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, leo Agosti 28,2026.

WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KAMBI YA BURE YA UCHUNGUZI NA MATIBABU YA MACHO ZANZIBAR Wananchi wa Zanzibar wametakiwa ku...
28/08/2026

WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KAMBI YA BURE YA UCHUNGUZI NA MATIBABU YA MACHO ZANZIBAR

Wananchi wa Zanzibar wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika Kambi Maalumu ya Uchunguzi na Matibabu ya Macho itakayofanyika kuanzia Agosti 29 hadi Septemba 4, 2026 katika mikoa ya Kaskazini Unguja na Mjini Magharibi, ambapo huduma zote zitatolewa bila malipo.

Wito huo umetolewa leo na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu Zanzibar, Mhandisi Ussy Khamis Debe, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya kambi hiyo, inayolenga kuongeza upatikanaji wa huduma za afya ya macho kwa wananchi.

Alisema kuwa Kambi hiyo inaendeshwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Afya Zanzibar na Hospitali ya Taifa Muhimbili, kwa udhamini wa Qatar Charity, ikiwa na lengo la kuwafanyia uchunguzi wa macho wananchi 2,050.

Kwa mujibu wa Mhandisi Debe, wananchi watakaobainika kuwa na matatizo ya macho watapatiwa huduma stahiki kulingana na mahitaji yao, zikiwemo miwani na upasuaji wa macho.

“Kambi hii ni sehemu ya juhudi za kupunguza changamoto za uoni na kuzuia ulemavu wa macho unaoweza kudhibitiwa au kutibiwa,” alisema Mhandisi Debe.

Alisema awamu ya kwanza ya kambi hiyo itafanyika katika Mkoa wa Kaskazini Unguja kuanzia Agosti 29 hadi 31, 2026 katika Kituo cha Afya Kinduni, huku awamu ya pili ikifanyika Mkoa wa Mjini Magharibi kuanzia Septemba 1 hadi 4, 2026 katika Kituo cha Afya Sebleni.

Alifafanua kuwa katika kambi hiyo, wananchi 400 wanatarajiwa kupatiwa miwani, huku 417 wakitarajiwa kufanyiwa upasuaji wa macho. Wananchi wengine watakaobainika kuwa na matatizo mengine ya macho watapatiwa huduma kulingana na hali zao.

Mhandisi Debe alisema baadhi ya changamoto za macho zinazoweza kusababisha ulemavu hazitokani na hali ya kuzaliwa, bali zinaweza kusababishwa na maradhi au changamoto nyingine za kiafya, hivyo akasisitiza umuhimu wa wananchi kufanya uchunguzi wa macho mapema.

“Uchunguzi wa mapema ni muhimu kwa sababu unasaidia kubaini matatizo ya macho katika hatua za awali na kuwezesha matibabu au udhibiti wa tatizo kabla halijawa kubwa zaidi,” alisema.

Amesema takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya Zanzibar ya mwaka 2022 zinaonesha kuwa asilimia 3.6 ya watu wenye umri wa miaka saba na zaidi Zanzibar waliripoti kuwa na ugumu wa kuona, hali inayofanya tatizo la kuona kuwa miongoni mwa changamoto kubwa za ulemavu zilizoripotiwa.

Mhandisi Debe alisema takwimu hizo zinaonesha umuhimu wa kuongeza upatikanaji wa huduma za uchunguzi na matibabu ya macho, hasa kwa kuzingatia kuwa baadhi ya matatizo ya uoni yanaweza kutibiwa au kudhibitiwa iwapo yatagunduliwa mapema.

Aliwashukuru Qatar Charity kwa udhamini wa programu hiyo na kuitaka jamii kutumia fursa hiyo kwa kufika katika vituo vilivyotengwa ili kupata huduma.

Alisisitiza kuwa, huduma hizo hazitakuwa kwa wananchi wanaoishi katika maeneo ya vituo hivyo pekee, bali wananchi kutoka maeneo mengine wenye changamoto za macho wanaruhusiwa kufika kupata huduma.

Aidha, alisema mipango inaendelea kuhakikisha huduma za aina hiyo zinafika pia kwa wananchi wa Pemba ili kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma za afya ya macho katika Zanzibar.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Qatar Charity nchini Tanzania, Amjad Altahhan, alisema taasisi hiyo imeanzisha na kudhamini kampeni hiyo ikiwa sehemu ya juhudi zake za kijamii za kusaidia wananchi kupata huduma muhimu za afya, hususani huduma za afya ya macho.

Alisema Qatar Charity itashirikiana na Wizara ya Afya Zanzibar pamoja na Hospitali ya Taifa Muhimbili katika kusimamia na kuendesha zoezi hilo ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa.

“Lengo letu ni kuhakikisha wananchi wenye changamoto za macho wanapata huduma wanazohitaji na kupunguza athari zinazoweza kujitokeza kutokana na kutopata matibabu kwa wakati,” alisema.

Naye Mratibu wa Huduma za Afya ya Macho kutoka Wizara ya Afya Zanzibar, Fatma Juma Omar, alisema huduma za uchunguzi na matibabu ya macho zimekuwa zikitolewa mara kwa mara, huku ushirikiano na Qatar Charity ukiwa umeongeza uwezo wa kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Daktari Bingwa wa Maradhi ya Macho kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dk. Johannes Mafwiri, alisema kambi hiyo itatumia mfumo wa huduma ya mkoba, ambapo wataalamu na vifaa vya matibabu husogezwa karibu na wananchi badala ya wananchi kusafiri umbali mrefu kufuata huduma.

“Mfumo huu utasaidia kupunguza gharama na usumbufu kwa wananchi wanaohitaji uchunguzi na matibabu ya macho,” alisema Dk. Mafwiri.

Alisema kambi hiyo itahusisha wataalamu bingwa na bobezi wa maradhi ya macho, ambao watafanya uchunguzi na kutoa matibabu kulingana na aina na ukubwa wa tatizo la kila mgonjwa.

Dk. Mafwiri aliongeza kuwa katika kambi hiyo, kwa mara ya kwanza, wataalamu watafanya baadhi ya upasuaji wa macho kwa kutumia mfumo wa matundu madogo ndani ya gari maalumu la matibabu.

Alisema teknolojia hiyo inatarajiwa kuwasaidia wagonjwa kupata nafuu kwa haraka na kurejea katika shughuli zao za kila siku kwa muda mfupi zaidi.

Kwa kuzingatia umuhimu wa huduma hiyo, Dk. Mafwiri aliwasisitiza wananchi wenye changamoto za kuona kutumia fursa hiyo kwa kufika katika vituo vilivyotengwa ili kupata uchunguzi na matibabu bila malipo.

Kambi hiyo inatarajiwa kuwa sehemu ya juhudi za pamoja za Serikali na wadau wa afya katika kuimarisha huduma za macho Zanzibar, kupunguza changamoto za uoni na kuzuia ulemavu wa macho unaoweza kuzuilika au kutibiwa.

24/08/2026
21/08/2026

Address

Migombani
Zanzibar City

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais:

Shortcuts

Share