Kitengo cha Elimu ya Afya Zanzibar

Kitengo cha Elimu ya Afya Zanzibar Karibu sana katika ukurasa Rasmi wa Kitengo cha Elimu ya Afya Zanzibar (Zanzibar Health Promotion Unit - HPU) kilicho chini ya Wizara ya Afya Zanzibar

🚨 Mikono yako inaweza kuwa hatari kuliko unavyofikiri!Unaweza kupata ugonjwa wa uharo mkali kwa kula au kugusa kitu kili...
27/04/2026

🚨 Mikono yako inaweza kuwa hatari kuliko unavyofikiri!

Unaweza kupata ugonjwa wa uharo mkali kwa kula au kugusa kitu kilichochafuliwa na mikono michafu.

🧼 Nawa mikono kwa maji tiririka na sabuni kabla ya:

▪️Kuandaa chakula

▪️Kula

▪️Kumlisha mtoto

▪️Kunyonyesha

👉 Kinga ni bora kuliko tiba.

Usisubiri uharo mkali kukupata – anza na mikono safi leo.

Zanzibar

Mafunzo ya Ugonjwa wa uharo mkali kwa wandishi wa habari ambayo yameandaliwa na  kupitia Kitengo cha Elimu ya Afya Zanzi...
24/04/2026

Mafunzo ya Ugonjwa wa uharo mkali kwa wandishi wa habari ambayo yameandaliwa na kupitia Kitengo cha Elimu ya Afya Zanzibar

Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa TC Bububu Wilaya ya Magharibi A Unguja

Teknolojia Inapokutana na Utu: Zanzibar Yaendelea Kuwa Kituo cha Kujifunza Afrika 🌍🤱Wajumbe kutoka Benki ya Dunia pamoja...
16/04/2026

Teknolojia Inapokutana na Utu: Zanzibar Yaendelea Kuwa Kituo cha Kujifunza Afrika 🌍🤱

Wajumbe kutoka Benki ya Dunia pamoja na wawakilishi kutoka nchi mbalimbali za Afrika wametembelea Zanzibar kujifunza kuhusu mafanikio ya mfumo wa huduma ya usafiri wa dharura kwa mama na mtoto unaotekelezwa kupitia Kitengo cha Elimu ya Afya chini ya Wizara ya Afya Zanzibar

Wizara ya Afya Zanzibar kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali CIHEB–Tanzania kupitia Mradi wa Usalama wa Afya wam...
29/03/2026

Wizara ya Afya Zanzibar kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali CIHEB–Tanzania kupitia Mradi wa Usalama wa Afya wameendesha Mafunzo ya Infection Prevention and Control (IPC) kwa wafanyakazi wa hospitali Unguja na Pemba.

Lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo watumishi wa afya ili waweze kutoa elimu kwa wenzao ambao bado hawajapata mafunzo, pamoja na kuimarisha juhudi za kutokomeza maambukizi yanayotokana na ukosefu wa utekelezaji sahihi wa kanuni za IPC.

Mafunzo haya ya siku 10 yamejikita katika mbinu za kitaalamu za kuzuia na kudhibiti maambukizi katika vituo vya kutolea huduma, ikiwa ni hatua muhimu katika kuboresha usalama wa wagonjwa, watoa huduma na jamii kwa ujumla.

Wizara ya Afya Zanzibar kwa kushirikiana na JHPIEGO inawatangazia kuwa imeandaa kambi maalum ya uchunguzi na matibabu ya...
24/03/2026

Wizara ya Afya Zanzibar kwa kushirikiana na JHPIEGO inawatangazia kuwa imeandaa kambi maalum ya uchunguzi na matibabu ya saratani ya matiti kwa jinsia zote na saratani ya mlango wa kizazi kwa wanawake Unguja na Pemba.

Huduma zitaanza saa 2 na nusu asubuhi hadi saa 10 kamili jioni. Shime wananchi! Tujitokeze kwa wingi.

Saratani ikigundulika mapema inatibika!

Tunawatakia Waislamu wote duniani
20/03/2026

Tunawatakia Waislamu wote duniani

18/03/2026

Mambo ya Kuzingatia katika kipindi hiki cha Mvua zinazoendelea kunyesha na Sikukuu ya Eid

07/03/2026

Kheri ya Siku ya Wanawake Duniani.
🇹🇿

01/03/2026

Mungozo wa Afya ndani ya Ramadhan

Meneja wa kitengo cha Elimu ya Afya Zanzibar Dkt. Haji Gora akitukumbusha miongozo mbalimbali ya Afya ili kubaki na siha njema wakati na hata baada ya mfungo wa Ramadhan.

Timu ya wataalamu wa Wizara ya Afya Zanzibar, ikiongozwa na Meneja wa Kitengo cha Elimu ya Afya (HPU), Dkt. Gora Faki Ha...
26/02/2026

Timu ya wataalamu wa Wizara ya Afya Zanzibar, ikiongozwa na Meneja wa Kitengo cha Elimu ya Afya (HPU), Dkt. Gora Faki Haji, imefanya ziara ya siku tano katika Wizara ya Afya Tanzania Bara jijini Dodoma na Dar es Salaam kwa ajili ya kubadilishana uzoefu na kuimarisha mawasiliano ya serikali na uhamasishaji wa afya kwa umma.

Dkt. Gora amesema ziara hiyo imewawezesha HPU kujifunza mbinu mpya za kuboresha kampeni za afya, hasa zile zinazolenga kuzuia magonjwa na kuongeza ushiriki wa jamii katika afua za kinga.

Amesema pia pande zote mbili zimekubaliana kuandaa Mpango wa Ushirikiano utakaoainisha maeneo ya kipaumbele, majukumu na ratiba ya utekelezaji wa shughuli za pamoja.

Hii sio ya kukosa.Usikae mbali na ukurasa wetu wa tiktok leo ifikapo saa 2:30 usiku. Tutakua live kuzungumzia Magonywa y...
26/02/2026

Hii sio ya kukosa.

Usikae mbali na ukurasa wetu wa tiktok leo ifikapo saa 2:30 usiku. Tutakua live kuzungumzia Magonywa ya mripuko na jinsi ya kujikinga.

Address

Zanzibar City

Opening Hours

Monday 08:00 - 15:30
Tuesday 08:00 - 15:30
Wednesday 08:00 - 15:30
Thursday 08:00 - 15:30
Friday 08:00 - 15:30

Telephone

+255776848365

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kitengo cha Elimu ya Afya Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share