19/03/2025
Waziri wa Maji, Nishati na Madini Zanzibar Mhe. Shaibu Hassan Kaduara amefungua mradi wa Maji wa Kisima kinachotumia umeme wa jua Weni Wete Pemba.
Mradi huo uliojengwa na kampuni ya Oikos East Africa unazalisha kilowatt 41.4 ambapo umefadhiliwa na Umoja wa Ulaya na kugharimu kiasi cha shilingi za kitanzania milioni 250 kwa Skimu ya Weni na Kizimbani Wete Pemba.
Kitengo cha Uhusiano – ZAWA
19 Machi 2025
Weni Wete Pemba.