Cgcla.Zanzibar

Cgcla.Zanzibar CGCLA serves as referral laboratory in Zanzibar according to the Laboratory Act No. 10 of 2011

28/04/2026

DNA DAY

28/04/2026
27/01/2026
Maafisa kutoka Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali-Zanzibar wakiendelea kutoa mafunzo ya matumizi na uhifadhi s...
25/11/2025

Maafisa kutoka Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali-Zanzibar wakiendelea kutoa mafunzo ya matumizi na uhifadhi salama wa kemikali kwa _Pool attendant na uwelewa wa vimelea vinavyoweza kuzaliwa nadani ya Bwawa la kuogelea.

Mkemia Mkuu wa serikali Dkt Farid Mzee Mpatani katika kuadhimisha  kilele ya wiki ya huduma kwa wateja Wakala wa Maabara...
11/10/2025

Mkemia Mkuu wa serikali Dkt Farid Mzee Mpatani katika kuadhimisha kilele ya wiki ya huduma kwa wateja Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ilipata fursa ya kujumuika na wateja wetu (wadau wa Kemikali) walipofika katika Ofisi zetu maruhubi.Pia tunajivunia mahusiano mazuri yaliopo baina yetu na wateja.

Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali yaendeleza mafunzo kuhusu usimamizi na usimamizi pamoja na udhibiti salama ...
22/06/2025

Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali yaendeleza mafunzo kuhusu usimamizi na usimamizi pamoja na udhibiti salama wa kemikali kwa Wadau kutoka kampuni mbali mbali.

Muendelezo wa mafunzo hayo umefanyika tarehe 22-06-2025 katika hoteli ya Madinat Al bahar iliyopo Mbeni Mjini Zanzibar.

Ambapo muendelezo wa mafunzo hayo,umefunguliwa na Mkuzugenzi wa Kemikali na Mazingira Ndugu Ussi Makame Kombo kwa kutoa ufupisho wa mafunzo yaliyopita kwa Wadau na kuwataka kuyafanyia kazi na kufuata vyema udhibiti wa kemikali kwa ajili ya usalama wa mtumiaji.

Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Zanzibar yatoa mafunzo kwa Wadau mbali mbali wanaojihusisha na masuala ya k...
21/06/2025

Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Zanzibar yatoa mafunzo kwa Wadau mbali mbali wanaojihusisha na masuala ya kemikali juu ya usimamizi na udhibiti wa matumizi na udhibiti salama wa kemikali.

Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkemia Mkuu wa Serikali Mkurugenzi Utawala,Rasilimali watu, Mipango ,Sera na Utafiti Ndugu.Omary Abadalla Ameir tarehe 21-06-2025 katika eneo la Hotel ya Madinatul bahari liliyopo Mbweni Zanzibar amesema, Taasisi imeamua kufanya mafunzo hayo yenye lengo la kuwajengea uwezo Wadau wanaotumia kemikali katika utoaji wa huduma zao ili kuweza kutumia vyema sheria na kanuni za kemikali pamoja na kulinda usalama wa matumizi.

Sambamba na hayo, Mkurugenzi wa Kemikali na Mazingira Ngugu,Ussi Makame Kombo alifafanua kuwa, udhibiti na usimamizi wa kemikali ni jukumu la pamoja, hivyo aliwataka Wadau kuwa na mashirikiano katika uhifadhi wa kemikali ili kuzuia athari zinazoweza kuathiri afya ya mtumiaji.
Aidha, aliwataka Wadau kusimamia suala zima la kanuni na mfumo wa kemikali unaotarajiwa kuanza kazi hivi karibuni kwa ajili ya utoaji wa vibali alisema,utarahisisha kazi kwa wakati na kushauri Wadau kutumia mfumo huo ili kuweza kuleta mabadiliko.

Akiwasilisha mafunzo juu ya sheria na kanuni juu ya utoaji,uombaji, usambazaji wa bidhaa za kemikali Mwanasheria Kombo Shaame Kombo alieleza kuwa, lengo la mafunzo ni Wadau kujua sheria na kanuni ili kulinda usalama na mazingira ya mtumiaji, hivyo ni lazima Wadau kutambua sheria za Kimataifa pamoja na sheria za ndani ili kuweza kusimamia vizuri kemikali kuwa ni matumizi salama wakati wa utoaji wa huduma.

Mbali na hayo, Mchunguzi Mkemia Ndugu, Ayman Othman Salum akiwasilisha mada ya usalama wa kemikali katika maeneo yanayohifadhiwa kemikali, utambuzi wa kemikali sambamba na njia zinazotakiwa kuchukuliwa na Wadau katika uwekaji na uhifadhi wa kemikali katika usalama.

Kwa upande wake Mkuu wa Divisheni ya Kemikali na Mazingira aliwasisha mada ya dharura za kemikali kwa mazingira na binaaadamu ili Wadau

Address

Maruhubi Zanzibar
Zanzibar City

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Telephone

+255242238123

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Cgcla.Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Cgcla.Zanzibar:

Share