27/03/2026
27 march, 2026
Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Mitihani Zanzibar Dkt. Rashid Abdul-azizi Mukki akizungumza na kufanya uhamasishaji kwa walimu na wazazi wa wanafunzi wa kidato cha pili na darasa la nne kuhusu upimaji wa sampuli wa large scale assessement ambao upimaji huo unatarajiwa kufanyika mwezi wa tisa kwa sampuli ya skuli za serikali na Binafsi
Hafla hiyo imefanyika ukumbi wa TC ya kiembe samaki Mkoa wa Mjini Magharib
Mkurugenzi huyo amesema Elimu imekuwa na mabadiliko makubwa hivyo wazazi na walimu washikamane ili kumuongoza mwanafunzi katika kuyakabili mabadiliko hayo
Aidha amesema walimu wafanye kazi ya ziada kwa wanafunzi ili waweze kukabiliana na upimaji huo.
Nao wazee na walimu amesema baadhi ya skuli hakuna walimu wa masomo, ufuatiliaji wa wanafunzi kwa baadhi ya wazee ni mdogo.
Pia walitoa mapendekezo kwa Wizara iyandae adhabu kwa wazazi waliyokuwa hawahudhurii katika vikao vya walimu, huu upimaji wa large scale assessment uwe muendelezo , kuwepo na zawadi maalum kwa skuli ambazo zitafanya vizuri katika upimaji huo.
Imetolewa na:
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Baraza la Mitihani la Zanzibar