Baraza la Mitihani Zanzibar

Baraza la Mitihani Zanzibar Karibuni katika ukurasa wetu wa facebook ili muweze kupata habari mbali mbali zinazo husiana na Baraza la Mitihani

05/05/2026
27 march, 2026Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Mitihani Zanzibar Dkt. Rashid Abdul-azizi  Mukki akizungumza na kufanya u...
27/03/2026

27 march, 2026
Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Mitihani Zanzibar Dkt. Rashid Abdul-azizi Mukki akizungumza na kufanya uhamasishaji kwa walimu na wazazi wa wanafunzi wa kidato cha pili na darasa la nne kuhusu upimaji wa sampuli wa large scale assessement ambao upimaji huo unatarajiwa kufanyika mwezi wa tisa kwa sampuli ya skuli za serikali na Binafsi
Hafla hiyo imefanyika ukumbi wa TC ya kiembe samaki Mkoa wa Mjini Magharib
Mkurugenzi huyo amesema Elimu imekuwa na mabadiliko makubwa hivyo wazazi na walimu washikamane ili kumuongoza mwanafunzi katika kuyakabili mabadiliko hayo
Aidha amesema walimu wafanye kazi ya ziada kwa wanafunzi ili waweze kukabiliana na upimaji huo.
Nao wazee na walimu amesema baadhi ya skuli hakuna walimu wa masomo, ufuatiliaji wa wanafunzi kwa baadhi ya wazee ni mdogo.
Pia walitoa mapendekezo kwa Wizara iyandae adhabu kwa wazazi waliyokuwa hawahudhurii katika vikao vya walimu, huu upimaji wa large scale assessment uwe muendelezo , kuwepo na zawadi maalum kwa skuli ambazo zitafanya vizuri katika upimaji huo.

Imetolewa na:
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Baraza la Mitihani la Zanzibar

TAARIFA KWA UMMA
27/03/2026

TAARIFA KWA UMMA

Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Mitihani Zanzibar Dkt. Rashid Abdul-azizi  Mukki na Mkurugenzi Idara ya maandalizi na M...
26/03/2026

Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Mitihani Zanzibar Dkt. Rashid Abdul-azizi Mukki na Mkurugenzi Idara ya maandalizi na Msingi Bi Fatma Mode Ramadhani pamoja na watendaji wengine walifanya kikao cha kuwasilisha matokeo ya upimaji wa kitaifa kwa darasa la tatu(3) Kwa mwaka 2026.
Lengo kuu ni kupata Uelewa ili kuchukua hatua za kuimarisha ufundishaji na kukuza stadi za kusoma kuandika na kuhesabu

Hafla hyo imefanyika katika Ofisi za Baraza la Mitihani la Zanzibar tarehe 25/03/2026 huko Vuga– Unguja.

Imetolewa na:
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Baraza la Mitihani la Zanzibar

Asalamu Alykum TAARIFA KWA UMMABaraza la Mitihan la Zanzibar linapenda kuwataarifu kuwa matokeo ya mtihani wa Taifa Kwa ...
26/03/2026

Asalamu Alykum
TAARIFA KWA UMMA
Baraza la Mitihan la Zanzibar linapenda kuwataarifu kuwa matokeo ya mtihani wa Taifa Kwa Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti cha Maandalizi na Msingi Awali (CECE) Kwa mwaka 2025 yametolewa Leo tarehe 26/03/2026
Matokeo hayo yanapatikana kupitia viungo( links) Vifuatavyo:-

https://matokeo.bmz.go.tz/colleges/

https://bmz.go.tz/exam-results/colleges/

BARAZA LA MITIHANI ZANZIBAR YASAIN HATI YA MAKUBALIANO NA IMAGINE WORLDWIDE TANZANIA KATIKA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU YA M...
24/03/2026

BARAZA LA MITIHANI ZANZIBAR YASAIN HATI YA MAKUBALIANO NA IMAGINE WORLDWIDE TANZANIA KATIKA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU YA MSINGI-TEK.

Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Mitihani Zanzibar Dkt. Rashid Abdul-azizi Mukki na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya IMAGINE WORLDWIDE TANZANIA Dr. JACQUELINE H. MGUMIA wamesaini Hati ya Makubaliano yenye lengo la Kuboresha Upimaji na Ujifunzaji wa stadi za Msingi za kusoma, kuandika na kuhesabu kwa kutumia njia ya tablet ( DIGITAL EGRA NA EGMA ) kupitia programu ya MSINGI- TEK .

Hafla ya utiaji saini wa mkataba huo imefanyika katika Ofisi za Baraza la Mitihani la Zanzibar Leo tarehe 24/03/2026 huko Vuga– Unguja.

Imetolewa na:
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Baraza la Mitihani la Zanzibar

Address

Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Baraza la Mitihani Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share