Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar

Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale imeundwa mnamo tarehe 19/11/2020 mara baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28/11/2020.

Wizara hii imetokana na iliyokuwa Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale

UJIO WA TREY SONGZ ZANZIBAR WAFUNGUA FURSA MPYA ZA UTALII, MUZIKI NA UCHUMIMsanii maarufu wa R&B kutoka Marekani, Trey S...
16/08/2026

UJIO WA TREY SONGZ ZANZIBAR WAFUNGUA FURSA MPYA ZA UTALII, MUZIKI NA UCHUMI

Msanii maarufu wa R&B kutoka Marekani, Trey Songz, Amewasili Zanzibar akitokea Jijini Dar Es Salaam leo katika Kiwanja cha Ndege cha Abeid Aman Karume na Kupokelewa na viongozi wa Serikali, akiwemo Mkurugenzi wa Masoko, Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Rahma Sanya, pamoja na Mkurugenzi wa Utumishi na Uendeshaji, Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale.

Akizungumza mara ya Mapokezi hayo Mkurugenzi Masoko Kamishen ya Utalii Zanzibar amefahamisha kuwa Ujio wa Trey Songz, ambaye ana wafuasi wengi duniani, unaifanya Zanzibar kuendelea kuonekana k**a kituo cha kipekee cha Utalii na burudani kimataifa, huku Uwepo wa mastaa wa kiwango hicho ukitoa fursa ya kuitangaza Zanzibar kupitia Muziki, Mitandao ya kijamii na tasnia ya burudani.

Aidha, Nd. Rahma amesema kua ujio huo unaweza kuchochea fursa za kiuchumi kwa Vijana na Sekta binafsi, kuongeza Mahitaji ya huduma za Utalii, pamoja na kukuza mwingiliano wa Utamaduni na kuimarisha nafasi ya Zanzibar katika ramani ya burudani kimataifa.

Mkurugenzi ameeleza kuwa Zanzibar inaendelea kung'ara si kwa Uzuri wa fukwe na Urithi wake pekee, bali pia k**a sehemu ambayo burudani na Utalii inakutana jambo ambalo limzidi kuongeza Mvuto kimataifa kwa Visiwa hivi .

Rahma Sanya ZanzibarTourism treysongz Ikulu Zanzibar Zanzibar Airports Authority

KAMATI YA UTALII, BIASHARA NA KILIMO KUENDELEA NA ZIARA YA KUTATHMINI FURSA ZA UTALII WA ASILI PEMBA.Katibu Mkuu wa Wiza...
12/08/2026

KAMATI YA UTALII, BIASHARA NA KILIMO KUENDELEA NA ZIARA YA KUTATHMINI FURSA ZA UTALII WA ASILI PEMBA.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Dkt. Aboud Suleiman Jumbe, ameongoza ziara ya kutembelea na kutathmini Maeneo yenye thamani ya Utalii wa Asili katika Kisiwa cha Pemba, ikiwemo Eneo la hifadhi ya Popo wa Kidike na Eneo la hifadhi ya Pango la Samaki lililopo Mwambe - Pemba.

Katika ziara hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Dkt. Aboud aliongozana na Mwenyekiti pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Utalii , Bishara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi na kufanya ziara Eneo la hifadhi ya Popo wa Kidike, ambapo alitoa maelezo ya Mazingira na kuonyesha kwa Michoro Eneo wanayopatikana popo hao.

Dkt. Jumbe alitoa Ufafanuzi kwa Mwenyekiti wa Kamati, Mhe. Tabia Maulid Mwita, pamoja na washiriki wengine wakiwemo Wananchi wa Eneo hilo kuhusu Umuhimu wa Eneo hilo katika Uhifadhi wa Urithi wa Asili na Maendeleo ya Utalii.

Aidha, Kamati ilifika katika Eneo la Pango la Samaki Lililopo Mwambe na Kujionea kwa karibu Muonekano wa pango hilo na mazingira yake, hatua inayolenga kutambua fursa zilizopo na namna Maeneo hayo yanavyoweza kuendelezwa kuwa Vivutio Endelevu vya Utalii.

Ziara hiyo ni Sehemu ya juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar za kuibua, kuhifadhi na kuendeleza Vivutio vya Utalii wa Asili na Urithi wa Zanzibar, hususan Pemba, kwa manufaa ya Wananchi na kuongeza Mvuto wa Zanzibar katika sekta ya Utalii.

Tabia Maulidi Mwita Baraza La Wawakilishi

KAMATI YA UTALII, BIASHARA NA KILIMO YATATHMINI FURSA ZA UTALII PEMBA.Kamati ya Utalii, Biashara na Kilimo ya Baraza la ...
10/08/2026

KAMATI YA UTALII, BIASHARA NA KILIMO YATATHMINI FURSA ZA UTALII PEMBA.

Kamati ya Utalii, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar imefanya ziara katika Eneo la Kihistoria Kichokochwe, Mataka Spice Farm na Kisiwa cha Ndege , kwa lengo la kutathmini hali ya maeneo hayo, fursa zilizopo pamoja na kuongeza mchango katika Sekta ya Utalii na Uchumi wa Zanzibar.

Ziara hiyo imeongozwa na Kaimu Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Mhe. Mudrik Ramadhan Soraga, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Tabia Maulid Mwita, pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, Dkt. Aboud Suleiman Jumbe.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Soraga amesema Pemba ina utajiri mkubwa wa historia, utamaduni, mazingira na vivutio vya asili ambavyo vina nafasi kubwa katika kuimarisha utalii wa Zanzibar.

Amesema Serikali itaendelea kuweka mkazo katika kuhifadhi, kuendeleza na kutangaza vivutio vilivyopo Pemba, ili viweze kuvutia watalii zaidi na kutoa fursa za kiuchumi kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati, Mhe. Tabia Maulid Mwita, amesema ziara hiyo imeiwezesha Kamati kujionea kwa vitendo hali ya maeneo ya Utalii na kutambua fursa pamoja na changamoto zinazohitaji kufanyiwa kazi.
“Tunapotembelea maeneo haya, tunataka kuona kwa vitendo namna utalii unavyoweza kuleta manufaa kwa wananchi, na kuhakikisha historia na vivutio vyetu vinahifadhiwa ”

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, Dkt. Aboud Suleiman Jumbe, amesema Wizara itaendelea kushirikiana na wadau katika kuendeleza maeneo yenye thamani ya kihistoria, kiutamaduni na kimazingira, ili kuongeza wigo wa bidhaa za Utalii Pemba.

Kabla ya ziara hiyo, Kamati ilisomewa Taarifa ya Vivutio vya Utalii katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete, kabla ya kuelekea katika maeneo hayo kwa ajili ya kujionea hali yake na fursa zilizopo.

Ziara hiyo imeonesha kuwa Pemba ina hazina kubwa ya vivutio vinavyoweza kuunganisha historia, utamaduni, kilimo cha viungo na utalii wa mazingira, hivyo kutoa nafasi zaidi ya kukuza ajira, biashara na Uchumi wa Wananchi kupitia Sekta ya Utalii.

09/08/2026

Aboud Jumbe Idara Habari Maelezo Zanzibar

ZIARA YA MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA MAKUMBUSHO YA TAIFA YA OMAN YAANZA ZANZIBARKatibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Mam...
03/08/2026

ZIARA YA MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA MAKUMBUSHO YA TAIFA YA OMAN YAANZA ZANZIBAR

Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Dkt. Aboud Suleiman Jumbe, akiwa ameambatana na Balozi Mdogo wa Oman nchini Tanzania anayewakilisha Zanzibar, Mhe. H.E. Said Salim Al Sinawi, leo wamempokea Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Makumbusho ya Taifa ya Oman, Dkt. Al Mussawi, mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar.

Ziara ya Dkt. Al Mussawi inalenga kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa kihistoria na kitamaduni kati ya Zanzibar na Oman, hususan katika uhifadhi wa urithi wa mambo ya kale, Maendeleo ya makumbusho na kukuza Utalii wa Urithi.

Akiwa Zanzibar, Dkt. Al Mussawi anatarajiwa kutembelea Maeneo mbalimbali ya kihistoria na Urithi wa Kale, ikiwemo Makumbusho ya Amani yaliyopo Mnazi Mmoja, Kasri la Sa'ada, Kibweni Palace na Maeneo Mengine, ambapo atapata fursa ya kujionea juhudi zinazofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa Mashirikiano na Serikali ya Sultan wa Oman katika kuhifadhi na kuendeleza Urithi wa kihistoria kwa Manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Dkt. Aboud Suleiman Jumbe leo tarehe 3 Agosti 2026 ameongoza Kika...
03/08/2026

Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Dkt. Aboud Suleiman Jumbe leo tarehe 3 Agosti 2026 ameongoza Kikao cha Kamati Tendaji ya Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Wizara iliyopo Kikwajuni - Unguja .

Lengo la Kikao hicho ni kupanga mikakati muhimu ya kuimarisha sekta ya utalii ikiwemo Kuwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa robo ya nne ya Wizara. Pia, masuala ya usimamizi bora wa rasilimali na maboresho katika utoaji wa huduma za Utalii kwa wananchi wa Zanzibar, mafanikio na changamoto mbali mbali.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Viongozi na Wakuu wa Idara na Taasisi Mbalimbali za Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale ikiwemo Mamlaka ya Uhifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe, Kamisheni ya Utalii, Idara ya Utalii, Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale, Idara ya Uendeshaji na Utumishi na Chuo cha Maendeleo ya Utalii Marhubi (ZIToD).

ZanzibarTourism Ikulu Zanzibar Officialzitod Zanzibar Mamlaka Ya Mji Mkongwe Makumbusho Zanzibar Aboud Jumbe

Kaimu Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Mheshimiwa Mudrik Ramadhan Soraga, Ijumaa Tarehe 31 Julai 2026, alikuw...
02/08/2026

Kaimu Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Mheshimiwa Mudrik Ramadhan Soraga, Ijumaa Tarehe 31 Julai 2026, alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar (ZITOD), kilichopo Maruhubi.

Mheshimiwa Soraga alisisitiza juu ya umuhimu wa utekelezaji wa haraka wa mageuzi ya mitaala na elimu ya Sekta ya Ukarimu na Huduma za Utalii k**a ilivyoagizwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya Awamu ya Nane, inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, ili kuwapatia vijana ajira zaidi ndani na nje ya nchi kulingana na ushindani wa kimataifa wa Soko la Utalii.

Mheshimiwa Waziri Soraga alisifu mashirikiano ambayo Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar iliyapata katika kufanikisha ugatuzi wa Chuo hicho, Ikiwemo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Wizara ya Maliasili na Utalii Tanzania Bara, Baraza la Usajili na Uthibitishaji wa Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Amali Tanzania (NACTVET), Chuo Kikuu cha Taifa SUZA, na Chuo cha Utalii cha Taifa.

Halikadhalika alisisitiza uwepo wa mashirikiano ya kila siku ya pamoja baina ya Chuo cha Utalii na Sekta Binafsi k**a vila ZATI, ZATO, ZATOGA, HAZ, ZNCC, n.k. hapa Zanzibar ili Chuo kuenda sambamba na mahitaji ya kila siku ya ajira kwa vijana.

Ubunifu katika mageuzi ya mitaala na mashirikiano na vyuo vya kimataifa vya utalii ni nguzo mojawapo ya uhai wa mitaala mipya ya Chuo ambayo inahitajia katika kuwaletea vijana elimu bora na ya ushindani itakayowasaidia kupata ajira na kutoa huduma bora za kisasa ndani ya soko hilo la Utalii. Alisema Mheshimiwa Waziri Soraga.

Aligusia pia suala la Chuo kuibua njia mbali mbali za kutoa huduma na kusimamia rasilmali na hazina ilizo nazo katika kujiendeleza kwa kukusanya mapato yake na wakati huo huo kuendeleza elimu ya utalii nchini.

30/07/2026

Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Dkt. Aboud Suleiman Jumbe ameongoza Kikao Cha kimkakati wa Maendeleo ya Utalii kwa jamii kikiwa na Lengo la kukuza zaidi Ushirikiano wa kuibua fursa kwa Wazanzibar , Kuweka msingi wa ajira na mazingira bora.

Kikao hicho Kimefanyika Leo kati ya Wizara na Ugeni Kutoka EU Blue Economy na GIZ , katika Ukumbi Wa Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar.


GIZ

28/07/2026

KATIBU TAWALA WILAYA YA KUSINI UNGUJA AFUNGUA RASMI MRADI WA BIG Z (SOFT COMPONENT) NGAZI YA WILAYA.

KATIBU TAWALA WILAYA YA KUSINI UNGUJA AFUNGUA RASMI MRADI WA BIG Z (SOFT COMPONENT) NGAZI YA WILAYAKatibu Tawala Wilaya ...
28/07/2026

KATIBU TAWALA WILAYA YA KUSINI UNGUJA AFUNGUA RASMI MRADI WA BIG Z (SOFT COMPONENT) NGAZI YA WILAYA

Katibu Tawala Wilaya ya Kusini Unguja, Ndugu Mbaraka Omar Kasongo, leo amefungua rasmi utekelezaji wa Mradi wa Big Z (Soft Component) katika ngazi ya Wilaya, wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kusini, Kijiji cha Makunduchi, Unguja.

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo, Ndugu Kasongo amesema kuwa mradi huo unaonesha dhamira ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuendelea kuimarisha maendeleo ya sekta ya utalii kwa kuwashirikisha wananchi moja kwa moja katika kuhifadhi na kutumia rasilimali za utalii kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na wananchi ni nguzo muhimu katika kuhakikisha malengo ya Mradi wa Big Z yanafikiwa, hususan katika kuendeleza utalii endelevu, kuongeza fursa za ajira, kukuza uchumi wa maeneo husika na kuimarisha ustawi wa jamii.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na wawakilishi kutoka Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Wizara ya Fedha na Mipango, Masheha, Maafisa wa Wilaya pamoja na baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Kusini Unguja, ambapo washiriki walipata fursa ya kufahamishwa kuhusu malengo na manufaa ya utekelezaji wa Mradi wa Big Z (Soft Component) katika ngazi ya Wilaya.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Nd. Ashura Ali, amesema kuwa utekelezaji wa Mradi wa Big Z (Soft Component) katika ngazi ya Wilaya unalenga kuimarisha ushirikishwaji wa jamii katika maendeleo ya sekta ya utalii na kuhakikisha wananchi wanakuwa sehemu ya kulinda, kuhifadhi na kunufaika na rasilimali za utalii zilizopo katika maeneo yao.

Ameeleza kuwa mafanikio ya mradi huo yanategemea ushirikiano wa karibu kati ya Serikali, viongozi wa maeneo, wadau mbalimbali na wananchi, huku akiwahimiza washiriki kutumia fursa zinazotokana na mradi huo kuchochea maendeleo ya kiuchumi, kuongeza ajira na kuboresha huduma za utalii katika Wilaya ya Kusini Unguja.

Mradi wa Big Z (Soft Component) unalenga kuimarisha ushirikishwaji wa jamii, kuboresha usimamizi wa vivutio vya utalii na urithi wa Zanzibar .

Address

Mnazi Mmoja
Zanzibar
71024

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share