Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar

Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale imeundwa mnamo tarehe 19/11/2020 mara baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28/11/2020.

Wizara hii imetokana na iliyokuwa Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale

11/06/2026

Aboud Jumbe Ikulu Zanzibar

Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale na Dayosisi ya Kanisa la Anglikan Mkunazini Zanzibar zitaendelea kushirikiana pamoja k...
05/06/2026

Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale na Dayosisi ya Kanisa la Anglikan Mkunazini Zanzibar zitaendelea kushirikiana pamoja katika kutekeleza azma ya Serikali ya kujenga Umoja, Mshik**ano na Amani katika nchi Yetu.

Ameeleza hayo Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Dkt. Aboud Suleiman Jumbe wakati akifungua Kongamano la Kitaifa la Maadhimisho ya Siku ya Upigwaji Marufuku ya Biashara ya Utumwa, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Idris Abdul Wakil, Kikwajuni- Unguja .

Dkt. Aboud ameeleza kuwa busara na hekima za Viongozi Wakuu wa kitaifa, Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Samia Suluhu Hassan, na Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt Hussein Ali Mwinyi katika kuimarisha Sekta ya Utalii na Urithi wa Kihistoria wa Mambo ya Kale, basi ni pamoja na Kuadhimisha Siku hii katika Mantiki ya Mwendelezo wa kuleta Haki, Usawa, Mshik**ano na Maendeleo kwa Taifa.

Aidha Dkt. Jumbe amefahamisha kuwa Siku hii inakwenda sawa na Utekelezaji wa Falsafa ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania za 4R (Reconciliation, Resilience, Reforms & Rebuild) Yaani Maridhiano, Uhimilivu, Mageuzi na Ujenzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nae Kaimu Mkurugenzi Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale Zanzibar Nd. Kei Mohammed amefahamisha kuwa Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku 3 ambapo ni Ijumaa , Jumamosi na Jumapili .

Mkurugenzi amefafanua kua Pamoja na Mada mbali mbali zitakazowasilishwa katika Kongamano hilo , aidha, kutakua na Ziara maalum ya kutembelea Maeneo mbali mbali ya Kihistoria kwa lengo la kupata Uelewa juu ya Masuala mbali mbali yanayohusu Urithi wa Mambo ya Kale na historia ya biashara ya Utumwa pamoja na kupigwa marufuku biashara hiyo.

04/06/2026

Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Dkt. Aboud Suleiman Jumbe amefungua rasmi Semina ya mwanzo na ya ...
03/06/2026

Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Dkt. Aboud Suleiman Jumbe amefungua rasmi Semina ya mwanzo na ya aina yake, inayohusiana na Ukondoishaji wa falsafa ya KAIZEN katika Utoaji huduma, Uimarishaji wa Ufanisi, na Uboreshaji wa Viwango vya Shughuli mbali mbali katika Sekta ya Utalii Endelevu.

Warsha hiyo fupi ameifungua jana tarehe 02,Juni katika Ukumbi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar iliopo Kikwajuni - Unguja.

Akizungumza mara baada ya Ufunguzi huo Dkt. Aboud amewapongeza na kuwashukuru Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Japan (JICA) kwa kushirikiana na Kitengo cha Zanzibar Kaizen Unit (ZKU) kilichopo chini ya Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda, kwa mashirikiano yao ya karibu na Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale pamoja wadau wake k**a ZATO, ZATI, ZATOGA, katika kufanikisha Semina hii.

Dkt. Aboud amefafanua kuwa KAIZEN ni falsafa na Ubunifu ulioanza nchini Japan, unaomaanisha "Uimarishaji wa Uzalishaji bidhaa mbali mbali na Utoaji huduma bora na toshelezi katika Sekta mbali mbali, ikiwemo Utalii, kwa ajili ya Uchumi bora, Maendeleo ya jamii na Uhami wa Mazingira.

Aidha Dkt. Jumbe amefahamisha kwamba Kaizen sio mradi wa muda mfupi unaoishia baada ya Semina bali unatakiwa uwe ni mfumo Enedelevu unaoanzia na ngazi za mdau, Mjasiriamali, Mtaalamu, Mtendaji, Wanajamii, Jumuiya, taasisi ndogo ndogo hadi kufikia ngazi ya kitaifa na hatimae mradi huchangia kuboresha maisha ya kazi, Ufanisi, na Manufaa kwa Wananchi na Taifa.

Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Dkt. Aboud Suleiman Jumbe amefanya Mkutano na Vyombo vya habari k...
02/06/2026

Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Dkt. Aboud Suleiman Jumbe amefanya Mkutano na Vyombo vya habari kueleza kuhusiana na Tamasha la Muziki la Italia na Zanzibar, linalotarajiwa kufanyika chini ya Ufadhili wa Ubalozi wa Italia hapa Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, na Chuo cha Muziki wa Nchi za Majahazi (Dhow Countries Music Academy).

Ameeleza hayo leo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake katika Ukumbi wa Wizara iliyopo Kikwajuni - Unguja.

Dkt. Aboud amesema kwamba Ubalozi wa Italia nchini Tanzania, na Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, kwa pamoja Inawakaribisha Wadau wote katika Tamasha Maalum la Muziki Asilia wa Italia litakalofanyika Zanzibar, na kujumuisha Kikundi cha Muziki Asilia cha Italia kiitwacho Officina Zoe, kikundi cha Dhow Countries Music Academy kutoka Zanzibar .

Dkt. Aboud amefafanua kua Tamasha hili litakuwa ni la siku mbili litaanza tarehe 5 Juni 2026 ambapo Wanasanaa watakuwa katika Eneo la Shambaland Park, Pwani Mchangani na Siku ya Pili, tarehe 6 Juni 2026, Saa Kumi na Moja Jioni, ambapo Wasanii hao watakuwa katika Bustani za Forodhani, Mji Mkongwe.

Aidha Dkt . Aboud amefahamisha kuwa Ziara ya kundi hili nchini Tanzania inafanyika katika maadhimisho ya miaka 80 ya Jamhuri ya Italia, ambayo huadhimishwa kila ifikapo tarehe 2 Juni na Mwaka huu inaadhimishwa Miaka 65 ya Uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Italia.

Sambamba na hayo Dkt. Aboud alipata fursa ya kuwashukuru kwa dhati kabisa Viongozi wa kitaifa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt Hussein Ali Mwinyi, kwa kuendelea kuiongoza vyema nchi ya Tanzania --- na hasa katika kuitangaza Zanzibar na Tanzania katika medani za Utalii.

31/05/2026

KATIBU MKUU WIZARA YA UTALII NA MAMBO YA KALE ZANZIBAR ASHIRIKI MASHINDANO YA NGALAWA CHWAKA, ASISITIZA KUIMARISHWA KWA UTALII WA MICHEZO

Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Dkt. Aboud Suleiman Jumbe, ameshiriki katika sherehe za Mashindano ya Ngalawa yaliyofanyika eneo la Chwaka, Mkoa wa Kusini Unguja, ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za maadhimisho ya Sikukuu ya Eid kwa wananchi wa eneo hilo.

KATIBU MKUU WIZARA YA UTALII NA MAMBO YA KALE ZANZIBAR ASHIRIKI MASHINDANO YA NGALAWA CHWAKA, ASISITIZA KUIMARISHWA KWA ...
31/05/2026

KATIBU MKUU WIZARA YA UTALII NA MAMBO YA KALE ZANZIBAR ASHIRIKI MASHINDANO YA NGALAWA CHWAKA, ASISITIZA KUIMARISHWA KWA UTALII WA MICHEZO.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar,
Dkt. Aboud Suleiman Jumbe, ameshiriki katika sherehe za Mashindano ya Ngalawa yaliyofanyika eneo la Chwaka, Mkoa wa Kusini Unguja, ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za Maadhimisho ya Sikukuu ya Eid kwa Wananchi wa eneo hilo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Aboud S. Jumbe amepongeza juhudi za Wananchi wa Chwaka kwa kuendeleza na kuimarisha Michezo ya baharini, akieleza kuwa hatua hiyo inaendana na Maono ya Serikali ya Zanzibar chini ya uongozi wa Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kuimarisha Uchumi wa Buluu pamoja na kukuza sekta ya Utalii wa Michezo nchini.

Dkt. Jumbe amesema mashindano hayo yana mchango mkubwa katika kutangaza vivutio vya Utalii vya Zanzibar, hususan maeneo ya pwani na Urithi wa Utamaduni wa bahari, huku yakitoa fursa kwa vijana kushiriki katika shughuli za kiuchumi na kijamii zinazochochea Maendeleo ya jamii.

Aidha, ameahidi kuwa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale itaendelea kushirikiana na wananchi wa Chwaka na wadau mbalimbali ili kuyaendeleza mashindano hayo na kuyainua kutoka ngazi ya kijamii hadi kufikia hadhi ya mashindano makubwa ya kitaifa na kimataifa, hatua ambayo itachangia kuongeza idadi ya watalii na kuimarisha mchango wa Sekta ya Utalii katika Uchumi wa Zanzibar.

Katika hatua nyingine, Dkt. Jumbe ametoa wito kwa Wananchi kuendelea kutunza na kuhifadhi mazingira ya pwani na bahari kwa kuhakikisha fukwe zinabaki katika hali ya usafi wakati wote. Amesisitiza kuwa utunzaji wa mazingira ni msingi muhimu wa maendeleo endelevu ya Utalii na Uhifadhi wa rasilimali za bahari kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Mashindano hayo ya Ngalawa yamevutia ushiriki mkubwa wa wananchi na wageni mbalimbali, yakionesha namna michezo ya jadi ya baharini inavyoendelea kuwa sehemu muhimu ya Utamaduni na bidhaa ya Utalii inayoweza kuchangia Maendeleo ya kijamii na kiuchumi Zanzibar.

@zanzibar_tourism
@_pdbzanzibar

Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Dkt Aboud Suleiman Jumbe leo alijumuika na washiriki wa Jukwaa la 29 la Mw...
26/05/2026

Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Dkt Aboud Suleiman Jumbe leo alijumuika na washiriki wa Jukwaa la 29 la Mwaka wa Utafiti la REPOA ambalo
Mada yake Kuu Mwaka huu ilikuwa ni Maendeleo ya Sekta ya Uchumi wa Buluu Nchini Tanzania katika Kufikia Malengo Jumuishi ya Maendeleo Endelevu.

Jukwaa hili la siku mbili lilioandaliwa na Taasisi ya REPOA kwa mashirikiano na Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, lilihitimishwa leo hapo katika Hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar.

Dkt Jumbe alikuwa ni Mwenyekiti wa Kikao cha Nne cha Jukwaa hilo kilichokuwa na Mada iitwayo: Transforming Trade Expansion on Blue Economy - Maritime Transport & Security and Tourism - ambayo iliwajumuisha watoa mada mbali mbali wakiwemo Dr Nomtha Hadi kutoka Afrika ya Kusini, Ndugu Gilbert Boois kutoka Namibia, na Brigadier General Seif Athman Hamisi, Ndugu Salma Omar, Ndugu Salma Omar na Ndugu Latifa Sykes wote wakitokea nchini.

Watoa mada hao waliwakilisha taasisi zao ikiwemo South African International Maritime Institute (SAIMI), Hazaika Energy - Namibia, Mzinga Corporation, Zanzibar Maritime Authority, Zanzibar Association of Tour Operators na Tanzania Aviation Operators Association (TAOA).

Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Dkt Aboud Suleiman Jumbe alikutana na timu ya watafiti wa masuala ya urith...
26/05/2026

Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Dkt Aboud Suleiman Jumbe alikutana na timu ya watafiti wa masuala ya urithi wa mambo ya kale na akiolojia ambao wanashirikiana na Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale katika kufanya na kutangaza tafiti mbalimbali za kiakiolojia zinazoelezea mifumo ya kimaisha ya kijamii Unguja na Pemba katika Karne nyingi zilizopita.

Watafiti hao wakiongozwa na Dr. Akshay Sarathi (Prof. of Archaeology, American University of Sharjah, UAE); pamoja na Kate Rose(Director of Programs, Institute for Field Research, USA); Matylda Brecz (University of Sydney Australia) na Fahad Bagdadi (University of Sydney, Australia) walikutana na uongozi wa Wizara na kuwasilisha kazi zinazoendelea za maeneo mbali mbali ya mashirikiano na Wizara kupitia Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale ikiwemo tafiti mbali mbali ambazo zimechapishwa katika majarida kisayansi ya kimataifa.

Wataalamu kutoka Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Kei Abdallah, wanashirikiana na taasisi mbali mbali za kiakiolojia k**a hizi ambazo zinazotoa fursa za ufanyaji wa tafiti na mafunzo maalum kwa wataalamu wa ndani pamoja na wanajamii kuhusu historia ya visiwa vya Zanzibar na shughuli mbali mbali za karne nyingi zilizopita.

Mojawapo ya mikakati ya Taasisi hizi ni kukuza tafiti shirikishi zinazohusisha wanajamii ili kutoa uelewa zaidi kwao wanajamii kuhusu umuhimu wa tunu za urithi wa mambo ya kale zinazoyazunguka mazingira na maeneo mbali mbali ya kihistoria ya wanajamii hao na kushajiisha ulinzi na uhifadhi wa rasilmali hizi kwa taifa.

Address

Mnazi Mmoja
Zanzibar
71024

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share