Tume ya Mipango Zanzibar

Tume ya Mipango Zanzibar Karibu katika ukurasa rasmi wa Tume ya Mipango Zanzibar

Mheshimiwa balozi Mhandisi Katibu wa Baraza la Mapinduzi na katibu  Mkuu Kiongozi Zena Ahmed Said ameongoza kikao kazi c...
21/04/2026

Mheshimiwa balozi Mhandisi Katibu wa Baraza la Mapinduzi na katibu Mkuu Kiongozi Zena Ahmed Said ameongoza kikao kazi cha kupitia Rasimu ya awali ya Mpango wa Maendeleo wa Zanzibar (zadep 11-2031).

Kikao hicho kimechofanyika katika Ukumbi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Maisara kilihusisha Makatibu wakuu Manaibu katibu wakuu pamoja na Viongozi wa Tume ya Mipango Zanzibar.

Tarehe 21/04/2026

Kikao cha maandalizi na majadiliano ya bajeti  kati ya Tume ya Mipango Zanzibar na wajumbe wa k**ati ya baraza la wawaki...
09/04/2026

Kikao cha maandalizi na majadiliano ya bajeti kati ya Tume ya Mipango Zanzibar na wajumbe wa k**ati ya baraza la wawakilishi.

Kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Tume ya Mipango Zanzibar .

Vuga mjini Zanzibar
Tarehe 09/04/2026

07/04/2026
Zanzibar April 7, 2026 — Kaimu Katibu Mtendaji Tume ya Mipango Zanzibar, Dkt. Afua Kh .Mohammed, ameongoza kikao cha Tis...
07/04/2026

Zanzibar April 7, 2026 — Kaimu Katibu Mtendaji Tume ya Mipango Zanzibar, Dkt. Afua Kh .Mohammed, ameongoza kikao cha Tisa kwa mwaka 2025/26 cha kujadili mwenendo wa mfumko wa bei wa mwezi wa Machi 2026. Pamoja na kujadili mapitio ya hali ya Uchumi nchini kwa kipindi cha robo mwaka Oktoba-Disemba, 2025, kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Tume ya Mipango, Vuga Mjini Zanzibar.

Aidha, kikao kimewakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali za Serikali zinazohusika moja kwa moja na masuala ya mfumko wa bei. Miongoni mwa taasisi zilizoshiriki ni Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Tume ya Ushindani Halali wa Biashara, Shirika la Bandari , Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, ZSTC, Kamisheni ya Utalii, (ZURA), Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Serikali (ACGEN), Idara ya Sera na Kodi, Idara ya Bajeti na Mishahara (Payroll), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA).

Katibu mkuu kiongozi na Katibu wa baraza la Mapinduzi Muhandisi Zena Ahmed  Said ameongoza kikao cha mafunzo maalumu kwa...
16/03/2026

Katibu mkuu kiongozi na Katibu wa baraza la Mapinduzi Muhandisi Zena Ahmed Said ameongoza kikao cha mafunzo maalumu kwa Makatibu wakuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar juu ya kuelimisha na kuendeleza zao la karafuu.

Kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Zura Mjini Zanzibar kimeandaliwa na Tume ya Mipango Zanzibar Idara ya Utafiti kwa lengo la kuwapa uelewa Zaidi kuhusu zao hilo kutokana na umuhimu wake.

Mkurugenzi Uendeshaji na Utawala  Tume ya Mipango Zanzibar Ndg, Maryam Nassor Ukki  ameongoza mafunzo kwa maafisa kutoka...
16/03/2026

Mkurugenzi Uendeshaji na Utawala Tume ya Mipango Zanzibar Ndg, Maryam Nassor Ukki ameongoza mafunzo kwa maafisa kutoka Idara ya Uendeshaji na Utumishi juu ya Maradhi yasio ambukizwa.

Maradhi yasio ambukizwa kwa sasa imekuwa tishio kubwa kwa jamii kutokana na jamii kuwa na uekewa mdogo kuhusu maradhi hayo. Maradhi yasioambukizika ni k**a vile Maradhi ya sukari , presha , maradhi ya Akili, kansa nk.

Kwa upande wa washiriki wa mafunzo hayo wametoa shukurani kwa uongozi wa Tume ya Mipango kwa kuwapa mafunzo hayo na kuelewa kwa undani juu ya athari zinazopatikanwa juu ya uwepo wa maradhi hayo.

Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar, Dkt. Afua Mohamed, ameongoza kikao kazi cha mafunzo ya Usimamizi wa M...
27/01/2026

Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar, Dkt. Afua Mohamed, ameongoza kikao kazi cha mafunzo ya Usimamizi wa Mikataba inayohusiana na utekelezaji wa programu na miradi ya maendeleo.

Mafunzo hayo ya siku tatu yameandaliwa na Tume ya Mipango, yakiongozwa na Kamishna wa Idara ya Mipango ya Kitaifa na Maendeleo ya Kisekta, kwa kushirikiana na Benki ya Dunia. Mafunzo hayo yanashirikisha wadau kutoka sekta mbalimbali za Serikali pamoja na Taasisi zisizo za Serikali (NGOs).

Mafunzo hayo yanafanyika katika Ukumbi wa Maji House, Bomani, Zanzibar.

Lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwajengea na kuwaimarisha wahusika wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo uelewa na uwezo katika kusimamia mikataba kwa ufanisi, kwa kuzingatia masharti ya mikataba, viwango vya ubora vinavyokubalika, muda wa utekelezaji uliopangwa pamoja na matumizi bora ya rasilimali.

Hatua hiyo inalenga kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa ufanisi na kutoa thamani halisi ya fedha (value for money) kwa manufaa ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi Zanzibar.

KIKAO CHA KUJADILI HALI YA UCHUMI WA ZANZIBAR (GDP) KWA ROBO YA TATU MWAKA 2025, UKUMBI WA MKUTANO TUME YA MIPANGO.Kaimu...
23/01/2026

KIKAO CHA KUJADILI HALI YA UCHUMI WA ZANZIBAR (GDP) KWA ROBO YA TATU MWAKA 2025, UKUMBI WA MKUTANO TUME YA MIPANGO.

Kaimu Mwenyekiti kutoka Idara ya Uchumi, Ndg. Shamsa Abdalla Mbarouk, ameongoza kikao cha kujadili ripoti ya hali ya Uchumi wa Zanzibar (DGP kwa robo tatu ya mwaka 2025 kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar. Kikao hicho kimefanyika tarehe 11 Januari 2026 katika Ukumbi wa Tume ya Mipango.

Aidha, kikao kimewakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali za Serikali zinazohusika moja kwa moja na masuala ya mfumko wa bei. Miongoni mwa taasisi zilizoshiriki ni Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Tume ya Ushindani Halali wa Biashara, Shirika la Bandari , Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, ZSTC, Kamisheni ya Utalii, (ZURA), Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Serikali (ACGEN), Idara ya Sera na Kodi, Idara ya Bajeti na Mishahara (Payroll), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA).

Kikao hicho ni sehemu ya mfululizo wa vikao vya kitaalamu vinavyofanyika mara kwa mara kwa lengo la kutathmini mwenendo wa Uchumi na kutoa mapendekezo ya Sera yatakayosaidia kudumisha uthabiti wa bei na ukuaji endelevu wa uchumi.

Kaimu katibu mtendaji Tume ya Mipango Zanzibar Dkt Afua Khalfan Muhamed ametoa wito kwa wadau na washiriki wa kikao cha ...
15/01/2026

Kaimu katibu mtendaji Tume ya Mipango Zanzibar Dkt Afua Khalfan Muhamed ametoa wito kwa wadau na washiriki wa kikao cha uwasilishaji wa muhtsari wa sera (policy brief) zinazotokana na matokeo ya Tafiti kuzingatia na kufanyia kazi mafunzo watakayoyapata ili kuhakikisha lengo limefikiwa na kutatua shida zote zilizopo awali .

Akifungua kikao cha uwasilishaji wa muhtasari wa sera (policy brief) katika ukumbi wa maji haouse Miembeni mjini Zanzibar, amesema kuna faida kubwa ya Matokeo ya Tafiti kufanyiwa ufupisho kutokana Tafiti nyingi huwa zina kurasa nyingi ambazo zinasababisha watu wengi kukosa muda wa kusoma kutokana na changamoto hio Tume ya Mipango wameamua kufanya ufupisho wa tafiti hizo kupitia wadau wa tafiti.

Dkt Afua amesema mipango ya Nchi inazingatia ushahidi ambao utaleta matokeo mazuri na kuendeleza mipango endelevu kwa muhtasakabali wa Taifa.

Akiwasilisha mada kuhusu Zero Malaria ndugu Mwinyi Mselem kutoka Maabara ya afya ya jamii Amesema tunatakiwa jamii ibadilike na ichukue tahadhari kwa kuzingatia ushauri wa Wataalam wa afya wanavyotushauri k**a vile kutumia chandarua kupiga dawa majumbani kukata miti na majani pembeni ya nyumba zetu n.k.
Wadau wa muhtasari wa Sera zinazotokana na matekeo ya tafiti ni Tume ya Mipango na kushirikiana na wadau husika kutoka taasisi zilizofanya tafiti hizo.

Address

Vuga
Zanzibar

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tume ya Mipango Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share