07/04/2026
Zanzibar April 7, 2026 — Kaimu Katibu Mtendaji Tume ya Mipango Zanzibar, Dkt. Afua Kh .Mohammed, ameongoza kikao cha Tisa kwa mwaka 2025/26 cha kujadili mwenendo wa mfumko wa bei wa mwezi wa Machi 2026. Pamoja na kujadili mapitio ya hali ya Uchumi nchini kwa kipindi cha robo mwaka Oktoba-Disemba, 2025, kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Tume ya Mipango, Vuga Mjini Zanzibar.
Aidha, kikao kimewakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali za Serikali zinazohusika moja kwa moja na masuala ya mfumko wa bei. Miongoni mwa taasisi zilizoshiriki ni Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Tume ya Ushindani Halali wa Biashara, Shirika la Bandari , Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, ZSTC, Kamisheni ya Utalii, (ZURA), Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Serikali (ACGEN), Idara ya Sera na Kodi, Idara ya Bajeti na Mishahara (Payroll), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA).