Wizara ya Kilimo Umwagiliaji Maliasili na Mifugo.

Wizara ya Kilimo Umwagiliaji Maliasili na Mifugo. Wizara ya Kilimo Umwagiliaji Maliasili na Mifugo. Ni Wizara ambayo hushughulika na sekta za kilimo, misitu na mifugo. Makao makuu yapo Maruhubi.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea na juhudi za kuyarejesha mashamba yote ya Misitu ya Unguja na Pemba kwa kup...
30/04/2024

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea na juhudi za kuyarejesha mashamba yote ya Misitu ya Unguja na Pemba kwa kupanda miti ili kukidhi mahitaji ya wananchi KWA Kuni na miti ya Ujenzi

Akizungumza katika Siku ya Upandaji Miti kitaifa katika Shamba la Misitu Chaani-Masingini kwa niaba ya Waziri wa kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Mkuu wa Wilaya ya kaskazini "A" Othman Ali Maulid amesema hatua hiyo itaondoa tatizo la upatikanaji wa nishati ya kupikia na Miti ya Ujenzi na kupunguza Utegemezi wa Misitu ya asili.

Alisema ni vyema kuongeza juhudi za kupanda miti badala ya kuikata pekee ili lengo linalohitajika liweze kufikiwa.

Aidha amefahamisha kuwa Shamba la Misitu la Chaani-Masigini pamoja na Mashamba mengine ya Misitu ya Dunga-Jendele, Kibele na Unguja Ukuu kwa Upande wa Unguja na Maziwa ng'ombe kwa Pemba yalitangazwa kuwa maeneo ya hifadhi katika gazeti rasmi la Serikali la mwaka 1987 ambapo mashamba hayo yalianzishwa kupitia mradi wa kuendeleza Misitu Zanzibar uliofadhiliwa na Shirika la Maendeleo Finland lengo lake kuu ni uanzishaji wa Mashamba hayo ili kuongeza Uzalishaji wa mazao ya Misitu na kupunguza utegemezi wa Misitu ya Asili

" Shughuli yetu hii ya Upandaji miti hapa leo katika mashamba yaliyotajwa hapo juu na maeneo mengine inaendana na Program ya nchi ya kurejesha urithi wa Kijani Zanzibar kwani Urudishaji wa Mashamba haya Utasaidia kupunguza Utegemezi na Ukataji wa Mikoko na Msitu wa Hifadhi ya Akiba wa Kiwengwa-pongwe kwa ajili ya kuni hususani kwa waanika Madagaa wa Fungu refu na Maeneo mengine na Matumizi ya Bekari" alisema Othman.

Othman Aliongeza kwa kutoa Wito kwa Wakulima endapo mkulima anataka kulima katika maeneo hayo basi alime kwa kufuata maelekezo kwa Wataalamu ili kuendelea kulima huku wakitunza Miti iliyopandwa kwani Atakaebainika ameing'oa miti hiyo Wizara haitowacha kuchukua hatua za kisheria Pamoja na kumuondoa katika eneo hilo.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Ali khamis Juma amesema Pamoja na Kuhamasika juu ya Matumizi ya Nishati mbadala ikiwemo gesi na Umeme bado kuna umuhimu wa kuendelezwa Mashamba hayo kwa lengo la awali kutokana na jamii kutumia Nishati za kuni na makaa na Uwepo wa Mashamba ambao utaweza kusaidia kupata huduma hizo.

Hata hivyo alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya kilimo itaendelea kutoa elimu juu ya Upandaji wa miti na Uhifadhi wa Misitu ili itowe tija kwa Serikali na Jamii kwa Ujumla.

Nae Mkurugenzi idara ya Misitu Said Juma Ali na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi mazingira ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais Sheha mjaja juma wamesema shuhuli hiyo ya Upandaji
Miti inakwenda Sambamba na program ya kuiirejesha Zanzibar kuwa ya kijani na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi lengo lake ni kuihamasisha jamii kupenda, kutunza na kupanda miti.

Vile vile Walisema harakati hizo za kurejesha Zanzibar ya kijani wameamua kila mwaka kupanda miti milioni Tatu mjini na Vijijini na kuanzisha Misitu ya Hifadhi ili kurirhiwa na Vizazi Vijavyo.

Wakizungumza kwa niaba ya Wananchi wenzao walioshiriki katika kazi ya upandaji miti mohamed Ali Sheha na Arafa Hamad Bakari wamesema wamewaomba wananchi wenzao kuendelea kuitunza Misitu kwa kupanda Miti na kuepuka kuharibu mazingira ili malengo yalikusudiwa na Serikali yaweze kufikiwa.

Jumla ya Miti yote iliyopandwa katika Shamba hilo ni elf kumi ambapo miti hiyo ni Mivinje, Mikeshia na MISenna ambayo imepandwa katika eneo lenye Ukubwa wa hekta 4.

Mkurugenzi wa Idara ya Umwangiliaji Maji  Haji Hamid Saleh  amezitaka jumuiya za wakulima wa bonde la chaani kuituza na ...
30/04/2024

Mkurugenzi wa Idara ya Umwangiliaji Maji Haji Hamid Saleh amezitaka jumuiya za wakulima wa bonde la chaani kuituza na kuisimamia Miundombinu ya Umwangiliaji iliyojengwa kwa ajili ya kuendeleza kilimo cha mpunga.

Aliyasema hayo huko chaani
Wilaya ya kaskazini A Unguja wakati akifunguwa Mafunzo ya kilimo cha Mpunga kwa wenyeviti wa Jumuiya za wakulima wa bonde la Chaani.

Amesema Lengo la Mafunzo hayo ni kuwawezesha wakulima kujua mbinu bora za kutuza na kuendeleza Miundombinu ya Umwagiliaji na kuitumia kwa kufanikisha kilimo cha umwangiliaji kitakacho ongeza uzalishaji wenye tija kwa wakulima.

Amesema Sirekali imekamilisha mradi wa miundombinu kwa ajili kukiboresha kilimo cha Mpunga ambacho kwa kufata elimu waliyopewa kulima kwa wakati kutasaidia kuongeza uzalisha utakao wanufaisha wakulima.

Nae Mshauri elekezi wa Mradi wa Miundombinu ya Umwangiliaji Jang Jeongryeol Amesema Amesema bonde la chaani linaukubwa wa hekari 71 na Mitaro mikubwa 3 iliyojengo kwa Saruji ambayo yamepunguza upoteaji wa maji na kusaidia kufika katika mashamba ya wakulima kwa urahisi.

Amesema Serekali ya korea itasaidia kuendeleza Mradi huo kwa kusaidi Matrekta na zana za kilimo ili kuweza kuzalisha zaidi na kuwapatia tija wakulima.

Wakitoa maoni yao wakulima wamesema wanaishukru Serekali kwa kuwapatia Mafunzo hayo na kuzigatia kuepuka uharibifu wa miundombinu ya Umwangiliaji.

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Umwangiliaji, Malisili na Mifugo Ali Khamis Juma amesema Serekali ipo tayari  kusimamia Um...
24/04/2024

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Umwangiliaji, Malisili na Mifugo Ali Khamis Juma amesema Serekali ipo tayari kusimamia Umoja wa Wazalishaji na wasambazaji Mbegu ili kuweza kuwa na mbegu zenye Ubora zitakazo leta manufaa kwa Wakulima.

Akizungumza katika hotel ya Maru Maru Forodhani Unguja wakati akifunguwa warsha ya wadau wa Uzalishaji Mbegu iliyowashirikisha wataalamu watafiti, Tasisi binafsi za kilimo,wakulima na Makapuni ya usambazaji wa Mbegu kutoka Zanzibar na Tanzania Bara

Amesema mbegu bora kwenye kilimo ndio msingi wa mafanikio ya uzalishaji wa Mazao hivyo kuwepo kwa mashirikiano na Wazalishaji na wasambazaji wa biashara ya mbegu, kutaisaidia Serekali kujua matatizo na mafanikio katika uzalishaji wa mbegu za Mboga Mboga ,matunda na nafaka.

Aidha alieleza kuwa Zanzibar ina eneo dogo la uzalishaji wa Mazao hivyo uzalishaji wa mbegu na watafiti ni muhimu uzingatiye mbegu zitakazo weza kustahamili ukame,maradhi na miongo tuliyonayo.

Nae Meneja wa Mradi wa usimamizi wa Taasisi ya World Vegetable Center Tanzania Jeremiah Sigallah amesema Lengo la Warsha hiyo ni kupata mawazo kwa wadau na kuweza kutengeneza Umoja utakao weza kutoa tarifa za haraka kwa wazalishaji mbegu na makampuni yanayo sambaza mbegu duniani na kuweza kupata mbegu bora chotara na za asili na kuendeleza biashara ya Mbegu kukuwa zaidi na kuwapatia tija wakulima.

Wakitoa Maoni yao washiriki wa warsha hiyo waishukuru taasisi ya World Vegetable centre kwa kuwapatia mafunzo hayo yatakayo wajengaya uwelewa wa mifumo ya mashirikiano ya biashara ya uzalishaji mbegu duniani.

Warsha hiyo ya siku moja imefadhiliwa na shirika la maendeleo la watu wa Marekani USAID na World Vegetable centre

17/04/2024
17/04/2024

Shamba Darasa la Migomba

Katibu Mkuu kiongozi wa Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar  Muhandisi Zena Ahmed Said amesema  kuwepo kwa Sera ya kilimo ...
24/03/2024

Katibu Mkuu kiongozi wa Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar Muhandisi Zena Ahmed Said amesema kuwepo kwa Sera ya kilimo kutasaidi kusimamia uzalishaji wa mazao na kuleta mabadiliko ya Sekta ya kilimo.

Hayo aliyasema katika ukumbi wa Zura Maisara wakati akifungua kikao cha kupitia Sera ya Kilimo na kupokea maoni kwa Makatibu wakuu na Manaibu katibu wa Mawizara ya Serekali ya Mapinduzi Zanzibar.

Amesema kilimo kina umuhimu Mkubwa katika kuchangia pato la nchi ambapo zanzibar inaonekana kuwa na eneo dogo la uzalishaji wa mazao ya kilimo hivyo Mipango na mikakati ya kusaidia kilimo inahitajika ili kuweza kuwa na mabadiliko ya sekta kilimo nchini.

Aidha amewataka wadau na watunga sera kutoa maoni yao kikamilifu ili kuweza kuwa na sera mpya ya kilimo itakayo kwenda sambamba na mabadiliko na mahitaji ya wananchi,wakulima na wafanyabiasha na kuwa na muelekeo wa kuzalisha mazao kwa malengo na kuachana na ukulima wa kimazowea

Akiwasilisha mada ya mabadiliko ya sera ya kilimo Afisa Mipango Ali Usi Basha amesema kilimo kinamchango mkubwa katika kuhakikisha Usalama na uhakika wa chakula ikiwa bado uzalishaji wetu ni mdogo.hivyo mpango huu wa sera ya kilimo unalenga kuelekea katika uwekezaji ili kupunguza changamato za uhaba wa ardhi,tafiti,wataalamu,maji na pembejeo.

Amesema lengo la kuijadili Sera hiyo ni kutokana na hali mabadiliko katika sekta ya kilimo yaliyo tokana na ongezeko la watu, ukuwaji wa teknologia, uvamizi wa maeneo ya kilimo na mabadiliko ya hali ya hewa

Akitoa maoni yake katika kikao hicho katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Dkt Aboud Suleman Jumbe amesema rasimu ya kilimo ilenge katika mazao ya vipaumbele kwakuwa tunakabiliwa na changamoto za kiuzalishaji hivyo lazima tuoneshe mabadiliko katika sera ili tuweze kuimarisha uzalishaji na kuunganisha mifumo ya katika kuweka mnyororo wa thamani wa mazao na kuweza kuendeleza masoko na utalii kupitia kilimo.

update

Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji Maliasili na Mifugo Shamata Shaame Khamis amesema jukumu kubwa la usimamizi wa Rasilimali ...
22/03/2024

Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji Maliasili na Mifugo Shamata Shaame Khamis amesema jukumu kubwa la usimamizi wa Rasilimali za Misitu linabaki kwa Wanachi kwani wao ndio watumiaji wakubwa wa rasilimali hizo.
Shamata aliyasema hayo huko katika Maadhimisho ya siku ya Misitu duniani yaliyofanyika Jozani Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

Alisema jambo hilo litakuwa la busara ikiwa Wananchi wenyewe wataendelea kuilinda, kuitunza na kuihifadhi Misitu kwa vile kukosekana kwake wao ndio waathirika wa hilo.

"Ningependa kutoa agizo kwamba lazima miti tuliyoipanda leo itunzwe vizuri ili Misitu iweze kuimarika na kutoa huduma zinazostahiki, pia tunatakiwa tuchukuwe juhudi kubwa tena za makusudi kupanda miti kwa wingi," alisema Shamata.

Aidha alifahamisha ikiwa watu wanachukua juhudi za kupanda miti katika maeneo ya wazi ikiwemo mashuleni, hoteli, barabarani na sehemu za vikosi lazima lengo ni kurejesha Zanzibar ya kijani lifikiwe.

Shamata alikemea kuhusu uharibifu unaofanywa na baadhi ya wanajamii wanaokata misitu ovyo kwa kutumia misumeno ya moto na kusafirisha mazao bila kufuata taratibu zilizopo

Akiwa katika sehemu ya upandaji wa miti huko katika kijiji cha charawe Waziri huyo alisema uharibifu wa mazingira umepelekea kuongezeka kwa joto na kupelekea ongezeko kubwa la mabadiliko ya tabianchi.

Alifahamisha kuwa jukumu la utunzaji wa mazingira na upandaji wa miti ni jukumu la kila mmoja sio la watu fulani hivyo wakati umefika kwa vijana na wanafunzi kuwa tayari katika upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira.

Alitoa wito kwa jamii waishio karibu na misitu kwa yeyote atakaye kamatwa ametenda makosa atawajibishwa kisheria bila ya kuonewa huruma.

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ali Khamis Juma alisema jumla ya Sh512,815,155 milioni na Dola za kimarekani 25,598,37 zimetolewa katika kilele hicho kwa wadau wa hifadhi ya taifa ya Jozani, ikiwa ni mapato yanayotokana na utalii katika Msitu wa hifadhi hiyo kwa kipindi cha miezi sita kuanzia July hadi disemba 2023.

Alisema, Wizara yake imekua ikichukua jitihada za dhati ili kuhakikisha mapato hayo yanaongezeka ili mgao huo uwe mkubwa na kuzidi kutoa tija kwa Serikali na wadau husika.

Akisoma risala, Mwenyekiti wa Kamati ya Uhifadhi Shehia ya Pete, Wahida Mohd Ali alisema mikataba inayosimamiwa na wananchi inakabiliwa na changamoto kutokana na kuongezeka na kwa idadi watu na mahitaji yao.

"Sisi wananchi wa Pete tuna ombi kuhusu Mikataba ya CoFMA ambayo imelenga kuwapa fursa wanajamii kusimamia Misitu yao. Mikataba hii inakabiliwa na changamoto kubwa kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu na mahitaji yao,"alisema.

Katibu Mkuu Wizara ya kilimo,Umwangiliaji,Maliasili na Mifugo Ndg: Ali Khamis JumaAmesema ushirikiswaji  wa jamii  katik...
20/03/2024

Katibu Mkuu Wizara ya kilimo,Umwangiliaji,Maliasili na Mifugo Ndg: Ali Khamis Juma
Amesema ushirikiswaji wa jamii katika kutoa maoni yao ndio njia pekee itakayo saidia usimamizi mzuri wa misitu ya hifadhi.

Akizungumza katika kikao cha mpango kazi wa usimamizi wa Msitu wa akiba wa Kidikotundu, Nongwe na Vundwe kilichowashirikisha wa wadau kutoka tasisi za Serekali na binafsi,wasimamizi wa misitu,wanyama pori na wanajamii kutoka Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema lengo la kuwasilisha Mpango wa usimamizi wa msitu wa kidikotundu kwa wadau ni kuwa na Muongozo utakao tumika katika uendeshaji wa shughuli zote za hifadhi Mpya ya misitu huo.

Aidha aliwataka wadau na wanajamii kushiriki kikamilifu katika kutoa maoni juu ya mpango huo kutokana na umuhimu wa uwepo wa misitu na madhara yatakayotokea tukikosa misitu kwa maisha ya wanadamu na wanyama.

Mratibu wa Jumuiya ya uhifadhi wa wanyamapori Tanzania Said Abdallah Faki Amesema adhima ya kuelekeza harakati za uhifadhi misitu imetokana na matokeo ya utafiti kuonesha kwa asilimia 30 ya miti na wanyama adimu hupatikana katika msitu wa Kidikotundu ambayo ndio rasilimali ya nchi na husaidia jamii kupata kipato chao

Akitoa maoni yake kwenye kikao hicho mwanajamii wa Misitu wa hifadhi Muyuni Ismail Suleiman amesema matarajio ni kuwa na mafanikio kwa jamii na kupata maendeleo katika miradi mbali mbali ya uhifadhi

20/03/2024

Waziri wa Kilimo Zanzibar Mhe Shamata Shaame Khamis atembelea viwanja vya maonesho Dole Kizimbani

Waziri wa kilimo,Umwangiliaji,Maliasili na Mifugo Mhe Shamata Shaame khamis amesema mafanikio ya Sekta ya Kilimo inatoka...
20/03/2024

Waziri wa kilimo,Umwangiliaji,Maliasili na Mifugo Mhe Shamata Shaame khamis amesema mafanikio ya Sekta ya Kilimo inatokana na kazi za Utafiti utakao toa Matokeo mazuri yatakayo wezesha kuleta mabadiliko ya uzalishaji wa mazao

Aliyasema hayo katika kikao cha wafanyakazi na watafiti kilichofanyika katika ofisi za utafiti wa kilimo kizimbani.

Amesema ili serekali ifikiye malengo ya kuleta mabadiliko ya kilimo.na kuwa na uhakika wa chakula ni lazima kuwe na uwajibikaji kwa wafanyakazi na watafiti wa mazao ya chakula na biashara na kutoa elimu itakayo wasaidia wakulima kupata mbegu zenye ubora kwa ajili ya kilimo.

Nae katibu Mkuu Wizara ya kilimo,umwangiliaji,maliasili na Mifugo Ali Khamis Juma amewataka wataalamu na wafanyakazi kumpa mashirikiano yatakayo wezesha kufanyakazi kwa ufanisi na mafanikio kwa kutoa huduma za kiutafiti wa mazao yenye ubora zitakazo leta manufaa kwa wakulima

Waziri Shamata alifanya ziara ya kutembelea eneo la maonesho Kizimbani kuona ujezi wa miundombinu ya barabara unavyoende...
20/03/2024

Waziri Shamata alifanya ziara ya kutembelea eneo la maonesho Kizimbani kuona ujezi wa miundombinu ya barabara unavyoendelea katika viwanja vya maonesho dole unavyotekelezwa kufuatia ahadi ya Mhe Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Mhe Hussen Ali Mwinyi.

Address

MARUHUBI
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wizara ya Kilimo Umwagiliaji Maliasili na Mifugo. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share