12/06/2026
ZANZIBAR YATAJWA KUWA SALAMA KWA WAWEKEZAJI, MABALOZI SITA WASHIRIKI TAMASHA LA UWEKEZAJI
Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Hassan Idd Mwamweta, amesema Zanzibar ipo katika hali salama na hatua mbalimbali zinazochukuliwa na viongozi Wakuu zinaendelea kuonekana kupitia maendeleo yanayofikiwa katika kipindi cha hivi karibuni.
Amesema maendeleo hayo yanaifanya Zanzibar kuonekana katika sura mpya ya ukuaji wa kiuchumi huku akieleza kuwa kasi ya maendeleo inaweza kuifanya Zanzibar kufanana na maeneo yenye mafanikio makubwa kiuchumi k**a Singapore.
Balozi Mwamweta ameyasema hayo wakati wa Tamasha la Uwekezaji Zanzibar, ambapo kwa mara ya kwanza mabalozi sita walishiriki kwa pamoja katika tukio hilo.
Amesema uwepo wa mabalozi hao unaonesha umuhimu unaowekwa katika kukuza fursa za uwekezaji Zanzibar, huku akieleza kuwa usalama wa wageni ni moja ya sababu zinazoongeza imani kwa wawekezaji kuja kuwekeza katika visiwa hivyo.