Zanzibar Investment Promotion Authority

Zanzibar Investment Promotion Authority ZIPA is responsible for promotion and facilitation of investment in Zanzibar

Zanzibar Investment Promotion Authority is a semi autonomous government institution operating under the Zanzibar Investment Promotion and Protection Authority Act No. 14 of 2018.

12/06/2026

ZANZIBAR YATAJWA KUWA SALAMA KWA WAWEKEZAJI, MABALOZI SITA WASHIRIKI TAMASHA LA UWEKEZAJI

Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Hassan Idd Mwamweta, amesema Zanzibar ipo katika hali salama na hatua mbalimbali zinazochukuliwa na viongozi Wakuu zinaendelea kuonekana kupitia maendeleo yanayofikiwa katika kipindi cha hivi karibuni.

Amesema maendeleo hayo yanaifanya Zanzibar kuonekana katika sura mpya ya ukuaji wa kiuchumi huku akieleza kuwa kasi ya maendeleo inaweza kuifanya Zanzibar kufanana na maeneo yenye mafanikio makubwa kiuchumi k**a Singapore.

Balozi Mwamweta ameyasema hayo wakati wa Tamasha la Uwekezaji Zanzibar, ambapo kwa mara ya kwanza mabalozi sita walishiriki kwa pamoja katika tukio hilo.

Amesema uwepo wa mabalozi hao unaonesha umuhimu unaowekwa katika kukuza fursa za uwekezaji Zanzibar, huku akieleza kuwa usalama wa wageni ni moja ya sababu zinazoongeza imani kwa wawekezaji kuja kuwekeza katika visiwa hivyo.

11/06/2026

BRAZILI YAONESHA NIA KUWEKEZA ZANZIBAR KATIKA SEKTA YA UCHUMI WA BULUU NA UTENGENEZAJI WA NDEGE

Balozi wa Tanzania nchini Brazil, Dkt. John Stephen Simbachawene, amesema Brazil ni miongoni mwa nchi zinazofanya vizuri katika sekta ya uchumi wa buluu, uvunaji wa samaki pamoja na matengenezo ya magari na ndege.

Dkt. Simbachawene amesema kampuni moja kubwa kutoka Brazil inayojihusisha na utengenezaji wa ndege imeonesha nia ya kuja kuwekeza katika visiwa vya Zanzibar, hatua ambayo inaweza kusaidia kukuza sekta ya usafiri wa anga na kuongeza fursa za kiuchumi nchini.

Amesema Brazil ina uzoefu mkubwa katika matumizi ya rasilimali za bahari, teknolojia ya magari na utengenezaji wa ndege, hivyo kampuni hiyo ipo tayari kuja Tanzania kwa ajili ya kuangalia fursa za uwekezaji.

Kwa mujibu wa Balozi huyo, uwekezaji huo unatarajiwa kuwa sehemu ya jitihada za kuimarisha uhusiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Brazil pamoja na kuchochea maendeleo katika sekta mbalimbali

Ziara ya Rais wa Jamhuri ya Singapore, Mhe. Tharman Shanmugaratnam, nchini Tanzania na Zanzibar imefungua ukurasa mpya w...
11/06/2026

Ziara ya Rais wa Jamhuri ya Singapore, Mhe. Tharman Shanmugaratnam, nchini Tanzania na Zanzibar imefungua ukurasa mpya wa ushirikiano wa kiuchumi, biashara na uwekezaji kati ya Zanzibar na Singapore.

Chini ya uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, viongozi wa pande hizo mbili walifanya mazungumzo yaliyolenga kuimarisha ushirikiano katika sekta mbalimbali za kimkakati, ikiwemo uchumi wa buluu, utalii, nishati, biashara, uwekezaji, teknolojia na maendeleo ya rasilimali watu.

Miongoni mwa matukio muhimu ya ziara hiyo ilikuwa mkutano wa wafanyabiashara na wawekezaji kati ya Singapore na Zanzibar, uliowakutanisha viongozi wa serikali, sekta binafsi na wawekezaji kwa lengo la kujadili fursa za uwekezaji na kuimarisha ushirikiano wa kibiashara kati ya pande hizo mbili.

Akizungumza katika mkutano huo mkurugenzi Mtendaji wa ZIPA Ndg. Saleh Saad Mohamed amesema kuwa ZIPA inaendelea kutekeleza jukumu lake la kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo Zanzibar na kujenga ushirikiano wa kimkakati unaochochea ukuaji wa uchumi, uvumbuzi na maendeleo endelevu ya Zanzibar.

Ameongeza kuwa Zanzibar inaendelea kuimarisha mazingira wezeshi ya uwekezaji kupitia maboresho ya mifumo ya huduma kwa wawekezaji, pamoja na kuendeleza ushirikiano wa kimataifa ili kuvutia mitaji na teknolojia zitakazochochea maendeleo ya sekta za kimkakati.

Aidha, wafanyabiashara na wawekezaji walioshiriki mkutano huo wameeleza kuridhishwa na fursa zilizopo Zanzibar na kuonesha nia ya kuimarisha ushirikiano na kuwekeza katika sekta mbalimbali za kiuchumi.

11/06/2026

Balozi wa Tanzania Nchini Brazili Dkt. John Stephen Simbachawene ameipongeza Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) kwa maandalizi mazuri ya Tamasha la Uwekezaji Zanzibar 2026, huku akisema Tamasha hilo limefana kwa kiwango kikubwa kutoka na muitikio mkubwa wa Wawekezaji kutoka ndani na Nje ya Nchi.

Amesema kwamba, tamasha hilo limekuwa jukwaa muhimu la kuwakutanisha wawekezaji, wadau wa maendeleo na viongozi kwa ajili ya kujadili fursa zilizopo pamoja na namna ya kuendelea kukuza uchumi wa Zanzibar.

Amesema ushiriki wa wawekezaji takribani 700 katika tamasha hilo ni hatua kubwa na mafanikio makubwa kwa Zanzibar, kwani umeonesha ongezeko la imani ya wawekezaji katika mazingira ya uwekezaji yaliyopo.

Aidha, Balozi Chawene amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa jitihada kubwa anazozichukua katika kuboresha uchumi wa Zanzibar na kuimarisha mazingira ya biashara na uwekezaji.

A significant milestone for Zanzibar’s investment landscape as ZIPA and AfriEximbank formalize a strategic partnership t...
04/06/2026

A significant milestone for Zanzibar’s investment landscape as ZIPA and AfriEximbank formalize a strategic partnership through the signing of a Memorandum of Understanding, strengthening collaboration to promote investment, trade and sustainable economic growth.

Fuatilia Tamasha la Uwekezaji Zanzibar 2026 (Zanzibar Investment Summit 2026) mubashara kupitia mitandao ya kijamii ya Z...
03/06/2026

Fuatilia Tamasha la Uwekezaji Zanzibar 2026 (Zanzibar Investment Summit 2026) mubashara kupitia mitandao ya kijamii ya ZIPA, pamoja na Channel Ten, Clouds TV na ZBC.

Usikose kupata taarifa, mijadala na matukio mbalimbali yanayolenga kukuza fursa za uwekezaji Zanzibar.

03/06/2026

Participants at the Zanzibar Investment Summit 2026 are benefiting from a series of expert led training sessions and knowledge sharing discussions designed to enhance understanding of investment opportunities, emerging market trends and sustainable economic development.

The Summit has attracted a strong turnout of investors, business leaders, policymakers and stakeholders from various sectors, providing a valuable platform for networking, collaboration and strategic dialogue on Zanzibar’s investment potential.

Through these engagements, the Summit continues to promote Zanzibar as a competitive investment destination while fostering partnerships that support inclusive and sustainable economic growth.

WASHIRIKI WAPATIWA MAFUNZO KATIKA TAMASHA LA UWEKEZAJI ZANZIBAR 2026Washiriki mbalimbali wameanza kupatiwa mafunzo na ma...
03/06/2026

WASHIRIKI WAPATIWA MAFUNZO KATIKA TAMASHA LA UWEKEZAJI ZANZIBAR 2026

Washiriki mbalimbali wameanza kupatiwa mafunzo na maarifa kupitia Tamasha la Uwekezaji Zanzibar 2026 (Zanzibar Investment Summit 2026) linalofanyika katika Hoteli ya Golden Tulip Airport Zanzibar.

Tamasha limehudhuriwa na washiriki wengi kutoka maeneo mbalimbali, likiwa na mwitikio mzuri na mazingira bora kwa ajili ya kujadili fursa za uwekezaji na maendeleo endelevu Zanzibar.

WAGENI WAANZA KUWASILI SIKU YA KWANZA KATIKA TAMASHA LA UWEKEZAJI ZANZIBAR 2026Wageni mbalimbali wameanza kuwasili katik...
03/06/2026

WAGENI WAANZA KUWASILI SIKU YA KWANZA KATIKA TAMASHA LA UWEKEZAJI ZANZIBAR 2026

Wageni mbalimbali wameanza kuwasili katika Tamasha la Uwekezaji Zanzibar 2026 (Zanzibar Investment Summit 2026) linalofanyika katika Hoteli ya Golden Tulip Airport Zanzibar.

Shughuli za tamasha zimeanza rasmi, huku washiriki wakiendelea kujadili fursa mbalimbali za uwekezaji na maendeleo endelevu Zanzibar.

02/06/2026

MAANDALIZI YA TAMASHA LA UWEKEZAJI ZANZIBAR 2026 YAKAMILIKA

Waziri wa Kazi na Uwekezaji, Mhe. Shariff Ali Shariff, amesema maandalizi ya Tamasha la Uwekezaji Zanzibar 2026 yamekamilika na Zanzibar ipo tayari kuwapokea washiriki kutoka ndani na nje ya nchi katika tamasha hilo litakalofanyika kuanzia Juni 3 hadi 5, 2026 katika Hoteli ya Golden Tulip Airport Zanzibar.

Address

V656+XV Zanzibar
Zanzibar

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zanzibar Investment Promotion Authority posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share