12/09/2020
MUKINICHAGUA KUWA MBUNGE WA CHAKE CHAKE KWA KIPINDI CHA 2020-2025 NAAHIDI HAYA
1:Nitakua mbunifu na nitakua na mpango kazi binafsi wa miaka mitano k**a mbunge na siku zote nitatumia nguvu yangu ya ushawishi na kujenga hoja kuishawishi Serekali kutekeleza ile miradi ambayo mm itakua nje ya uwezo wangu, yaani miradi mkubwa.
2: Nitasikiliza hoja, ushauri, mapendekezo na mahitaji ya wananchi wa Chake Chake, na siku zote nitaongozwa na kiu ya kuwatumikia wanaChakeChake.
3: Nitakua tayari kutumia mfuko wa Jimbo kutekeleza miradi yenye kuacha Alama ya kudumu jimboni kwangu siyo kutumia mfuko wa jimbo kisanii na kwa maslahi yangu binafsi, kamwe hilo halitatokea.
4: Nitakua tayari kutumia akili kubwa zilizo mtaani kufanya mikakati ya kuleta maendeleo jimboni,siyo mbunge wa kuogopa kila mwenye akili na mawazo chanya na kumuona mpinzani wangu.
5: Nitakua mfuatiliaji ambaye daima nitataka kujua changamoto za wananchi wenzangu wa Chake Chake kwenye shehia zote,sio mbunge wa kusimuliwa changamoto za jimboni kwake.
6: Nitakua tayari kutumia ninachokipata kuwekeza jimboni kutengeneza fursa mbali mbali.
7: Daima nitakuwa mwananchi wa kwaida siyo mbunge ambaye nitautumia ubunge wangu k**a daraja la kuwa mtu special ambaye hapaswi kushilikiana na kuishi k**a wananchi wengine.
8: Naahidi nitakua mbunge ambaye nafikiwa na makundi yote ya wananchi yaani vijana ,wazee kina mama ,wasomi na wasio wasomi yaani mbunge wa watu wote siyo mbunge wa kuogopwa .Mbunge antisocial siyo wakati wake 2020-2025
9: Nitakua mbunge wa wananchi mwenye Maono ya mbali na sio kuleta ubabe na kutumia nguvu mbele ya wanaChakeChake walionichagua kuwatumikia.
10: Nitakua mhamasishaji mzuri wa shughuli za maendeleo na kijamii siyo mbunge boss yaani mbunge wa kukaa tu Dodoma na kurudi likizo kutafuta wanaompinga jimboni.
11: Nitakua na ofisi yangu binafsi ambayo itasimamiwa na vijana wa Chake Chake wenye weledi ambayo itakua ndio kiunganishi mbaina ya mbunge na wananchi kipindi ambacho mbunge atakua na majukumu ya kikazi nje ya Jimbo langu.
12: Muda wote ambao sitakua na majukumu ya kikazi nje ya jimbo langu, nitakua nipo kwenye Jimbo langu kuhakikisha tunakutana na wananchi na kujadiliana namna bora