Idara ya maendeleo ya Vijana Zanzibar

Idara ya maendeleo ya Vijana Zanzibar Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Idara ya maendeleo ya Vijana Zanzibar, Public & Government Service, Migombani, Zanzibar.

Idara ya Maendeleo ya Vijana Zanzibar inafanya kazi ya kuratibu shughuli za Maendeleo ya Vijana kwa kuhakikisha idadi ya Vijana wa K**e na kiume wanatoa mchango katika maendeleo ya taifa kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini ‘B’, Mhe. Juma Sururu Juma, amesema Programu ya U-Report itawasaidia vijana kupata elimu kuh...
28/04/2026

Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini ‘B’, Mhe. Juma Sururu Juma, amesema Programu ya U-Report itawasaidia vijana kupata elimu kuhusu afya ya uzazi pamoja na kinga dhidi ya maambukizi ya VVU, ili waweze kujitambua na kufanya maamuzi sahihi katika maisha yao.
Ameyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya Programu ya U-Report yaliyofanyika katika Skuli ya Sekondari Mahonda, Wilaya ya Kaskazini ‘B’, inayotoa elimu kwa vijana wa makundi mbalimbali yakiwemo Mabaraza ya Vijana WA Kaskazini 'B',Madereva wa Bodaboda ,Vijana wa Skaut pamoja na Red Cross.
Amesema mafunzo hayo yatawasaidia vijana hao kujenga uelewa wa kufanya maamuzi bora na kukabiliana na changamoto zinazowakabili, ikiwemo ubakaji na mimba katika umri mdogo.
Aidha, ameipongeza Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji pamoja na wafadhili kutoka UNICEF kwa juhudi zao za kuwaelimisha vijana ili kuepukana na vishawishi hatarishi.
Pia amewataka vijana hao kutumia vyema mafunzo hayo kwa kuwa mabalozi wazuri kwa wenzao na kuchangia ustawi wa vijana katika jamii ya Zanzibar.
Kwa upande wake, Mratibu Mkuu wa Programu ya U-Report kutoka Idara ya Maendeleo ya Vijana, Sheila Makungu Mwinyi, amesema mafunzo hayo yanasaidia kuongeza uelewa wa afya ya uzazi, maambukizi ya VVU, magonjwa ya kuambukiza Kuzuia mihemko pamoja na namna ya kukabiliana na msongo wa mawazo.
Ameeleza kuwa vijana wana haki ya kushiriki na kushirikisha katika maamuzi na kueleza changamoto zinazowakabili, huku akibainisha kuwa bado kuna upungufu wa uelewa wa masuala ya afya unaochangia kudhoofisha maendeleo ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.
Naye Mkufunzi kutoka Tume ya Ukimwi Zanzibar, Khamis Hassan, amesema elimu ya kujitambua ni muhimu katika kupunguza maambukizi ya magonjwa, ikiwemo VVU, na kuwahimiza vijana kupima afya zao mara kwa mara, hasa kabla ya kuingia kwenye ndoa.
Ameongeza kuwa vijana wanapaswa kuepuka tabia hatarishi na kuwa waaminifu katika mahusiano ili kujikinga na maambukizi.
Aidha, ameeleza kuwa matumizi sahihi ya dawa za kufubaza makali ya VVU (ARV) husaidia kupunguza virusi mwilini na kuimarisha kinga ya mwili.
Kwa upande wake, Afisa kutoka Kitengo cha Afya ya Mama na Mtoto Wizara ya Afya, Fatma Ussi Yahya, amesema uzazi wa mpango husaidia kupanga familia, kulinda afya ya mama na mtoto, pamoja na kuimarisha ustawi wa familia.
Amewataka vijana kujenga utamaduni wa kupima afya mara kwa mara, akisisitiza kuwa afya ya kijana ni msingi wa ustawi wa taifa.
Mafunzo ya Programu ya U-Report yamefanyika katika wilaya tano za Unguja na nne za Pemba, yakifadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF.

Mratibu wa program ya U-report ndugu Sheilla Makungu Mwinyi amewataka Vijana waliopata Mafunzo ya elimu ya Afya ya Uzazi...
25/04/2026

Mratibu wa program ya U-report ndugu Sheilla Makungu Mwinyi amewataka Vijana waliopata Mafunzo ya elimu ya Afya ya Uzazi na HIV kuwa mabalozi wazuri Kwa Vijana wenzao.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo ya kujilinda na maambukizi ya VVU na HIV, afya ya uzazi, kujitambua, kuhimili msongo na kuhimili mihemko pamoja na kujiunga na program ya U-report amesema kuwa elimu iliyotolewa ni muhimu kwa Vijana kulingana na mada rafiki za Stadi za Maisha zinazosaidia mistakbali wa maendeleo ya Vijana hao .

Nae afisa vijana wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Zanzibar Ubwa Haji Tuwani amesema kuwa mafunzo ya afya uzazi, HIV na Program ya U-Report wamepatiwa vijana wa makundi mbalimbali kwa ajili ya kuwapa elimu juu ya kujitambua na kuwataka vijana kwenda kuwafundisha wenzao na jamii kwa ujumla.

Kwa Upande wa wawezeshaji Khairat Suleiman Amen a Asia Rashid Bakar kutoka vituo vya Huduma Rafiki YFS Rahaleo wamewataka Vijana kuvitumia Vituo hivyo ili kupata elimu za Stadi za Maisha jambo ambalo litawasaidia kukabiliana na mihemko ya kihisia kujielewa kujiamini kuzidhamini pamoja na kuwa na maamuzi sahihi ya kutatua changamoto zao.

Mafunzo hayo yamefadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto Duniani
(UNICEF) Kupitia Program ya U-report kwa wilaya 5 za Unguja na wilaya 4 za Pemba yakihusisha vijana kutoka makundi mbalimbali, ikiwemo mabaraza ya vijana, wanafunzi wa vyuo vikuu, Scout, Red Cross, makundi vya kiuchumi na michezo, pamoja na vijana wenye mahitaji maalumu.

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Wilaya ya Kati Daud Suleiman Haji amewataka Vijana waliopata Mafunzo ya elimu ya Afya ya ...
24/04/2026

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Wilaya ya Kati Daud Suleiman Haji amewataka Vijana waliopata Mafunzo ya elimu ya Afya ya Uzazi, kujikinga na maambuziki ya VVU na HIV kuwa mabalozi wazuri Kwa Vijana wenzao .

Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya Programu ya U-report kwa Vijana wa makundi mbalimbali Katika ukumbi wa TC Dunga .

Amesema elimu iliyotolewa ni muhimu Kwa Vijana kulingana na mada rafiki za Stadi za Maisha zinazosaidia mistakbali wa maendeleo ya Vijana hao .

Kwa Upande wa Muezeshaji Asia Rashid kutoka kituo cha Huduma Rafiki (YFS) Rahaleo amewataka Vijana kuvitumia Vituo hivyo ili kupata elimu za Stadi za Maisha jambo ambalo litawasaidia kukabiliana na mihemko ya kihisia kujielewa kujiamini kuzidhamini pamoja na kuwa na maamuzi sahihi ya kutatua changamoto zao.

Mafunzo yaliotelewa kupitia program ya U-report afya ya uzazi, kijilinda na maambukizi ya VVU na HIV, kujitambua, kuhimili msongo na kuhimili mihemko.

Mafunzo hayo yamefadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto Duniani (UNICEF) Kupitia Program ya U-report kwa wilaya 5 za Unguja na wilaya 4 za Pemba yakihusisha vijana kutoka makundi mbalimbali, ikiwemo mabaraza ya vijana, wanafunzi wa vyuo vikuu, Scout, , Red Cross, makundi vya kiuchumi na michezo, pamoja na vijana wenye mahitaji maalumu.

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Wilaya ya Magharibi 'A' Abdulrazak Khamis Sheha amewataka Vijana waliopata Mafunzo  ya el...
23/04/2026

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Wilaya ya Magharibi 'A' Abdulrazak Khamis Sheha amewataka Vijana waliopata Mafunzo ya elimu ya Afya ya Uzazi na HIV kuwa mabalozi wazuri Kwa Vijana wenzao .
Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya Programu ya U-report kwa Vijana wa makundi mbali mbali Katika Skuli ya Mwera Regeza Mwenge .

Amesema elimu iliyotolewa ni muhimu Kwa Vijana kulingana na mada rafiki za Stadi za Maisha zinazosaidia mistakbali wa maendeleo ya Vijana hao .

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Wilaya ya Magharibi ‘A’, Abdulrazak Khamis Sheha, amewataka vijana waliopata mafunzo ya elimu ya afya ya uzazi na VVU/UKIMWI kuwa mabalozi wazuri kwa wenzao ili kusaidia kueneza uelewa sahihi katika jamii.

Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya programu ya U-Report kwa vijana kutoka makundi mbalimbali yaliyofanyika katika Skuli ya Mwera Regeza Mwenge,
alisisitiza kuwa elimu hiyo ni muhimu kwa vijana kwani inahusisha mada rafiki za stadi za maisha zitakazowawezesha kufanya maamuzi sahihi na kujenga mustakabali bora wa maendeleo yao.

Nae Mratibu wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Zanzibar, Maryam Omar Rashid, amesema kuwa mafunzo ya Program ya U-Report yanatarajiwa kutolewa katika wilaya mbalimbali za Unguja na Pemba Kwa lengo la kuwajengea uwezo Vijana wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi katika mwenendo wa maisha yao.

Amesema vijana wengi wanakumbana na changamoto zinazohusiana na afya ya uzazi, hali ambayo huadhiri kufikia ndoto zao. Hivyo, mafunzo hayo yatasaidia kuwajengea uwelewa wa kukabiliana na changamoto zinazowakabili
Aidha, amesisitiza umuhimu wa vijana kujiunga na programu U report kwa lengo ya kupata elimu inayowahusu, Vijana pamoja na kufaidika na huduma mbalimbali zinazotolewa.

Kwa Upande wa Muezeshaji Mwinyi Ameir Mwinyi kutoka kituo cha Huduma Rafiki (Y.F.S) KMKM. amewataka Vijana kuvitumia Vituo hivyo ili kupata elimu za Stadi za Maisha jambo ambalo litawasaidia kukabiliana na mihemko ya kihisia kujielewa kujiamini kuzidhamini pamoja na kuwa na maamuzi sahihi ya kutatua changamoto zao.

Mafunzo hayo yamefadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto Duniani
(UNICEF) Kupitia Program ya U-report kwa wilaya 5 za Unguja na wilaya 4 za Pemba yakihusisha vijana kutoka makundi mbalimbali, ikiwemo mabaraza ya vijana, wanafunzi wa vyuo vikuu, Scout, Red Cross, makundi vya kiuchumi na michezo, pamoja na vijana wenye mahitaji maalumu.

Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Zanzibar, Shaib Mohamed Ibrahim, amezungumza na Baraza la Watendaji kuhusu hi...
22/04/2026

Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Zanzibar, Shaib Mohamed Ibrahim, amezungumza na Baraza la Watendaji kuhusu historia ya kuanzishwa kwa Baraza la Vijana Zanzibar, akieleza kuwa taasisi hiyo ilianzishwa kwa lengo la kuwaunganisha vijana na kuwapa jukwaa la kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Zanzibar.
Akizungumza na Baraza la Watendaji la Baraza la Vijana Zanzibar Ukumbi wa Wizara ya Vijana Ajira na Uwezeshaji huko Mpendae Alisisitiza kuwa baraza hilo ni nyenzo muhimu katika kusimamia na kuendeleza ajenda za vijana nchini
Katika maelezo yake, alifafanua kuwa kuanzishwa kwa Baraza la Vijana Zanzibar kulitokana na hitaji la kuwa na chombo rasmi kitakachowakilisha maslahi ya vijana, kusikiliza changamoto zao na kuwasilisha mapendekezo yao kwa mamlaka husika
Aliongeza kuwa hatua hiyo imechangia kuongeza ushiriki wa vijana katika maamuzi ya kitaifa na mipango ya maendeleo
Aidha, Shaib Mohamed Ibrahim alieleza utendaji kazi wa baraza hilo, akibainisha kuwa linafanya kazi kwa kushirikiana na taasisi za Serikali na binafsi ili kuandaa na kutekeleza miradi mbalimbali inayolenga kuwainua vijana kiuchumi na kijamii
Kwa upande wa Katibu Mtendaji Ali Haji Hassan amesema kuwa baraza hilo limekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu, mafunzo na fursa za ajira kwa vijana
Katika kuelezea majukumu ya Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Zanzibar, alisisitiza kuwa kiongozi huyo ana jukumu la kusimamia utekelezaji wa mipango ya baraza, kuhamasisha ushiriki wa vijana, pamoja na kuhakikisha mawasiliano bora kati ya baraza na wadau mbalimbali
Aliongeza kuwa uongozi thabiti wa mwenyekiti ni nguzo muhimu ya mafanikio ya baraza hilo na alibainisha pia kuwa mwenyekiti anatakiwa kuwa mfano wa kuigwa kwa vijana wengine kwa kuonesha uwajibikaji, ubunifu na uadilifu katika utekelezaji wa majukumu yake hii ni pamoja na kusimamia rasilimali za baraza kwa ufanisi na kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa kwa wakati
Akihitimisha, alitoa wito kwa watendaji kuendelea kushirikiana kwa karibu na Baraza la Vijana Zanzibar ili kuimarisha utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya vijana. Alisisitiza kuwa mafanikio ya baraza hilo yanategemea mshikamano.

Mwenge wa Uhuru Kitaifa umekimbizwa katika Mkoa wa Kaskazini Unguja katika  Wilaya ya Kasakazini A na kutembelea Miradi ...
12/04/2026

Mwenge wa Uhuru Kitaifa umekimbizwa katika Mkoa wa Kaskazini Unguja katika Wilaya ya Kasakazini A na kutembelea Miradi mbalimbali na kuwekewa jiwe la msingi.

Miradi iliotembelewa na kuwekewa jiwe la msingi ni mradi wa kituo cha kufua na kupozea umemeMatemwe Kusini, uwanja wa michezo jumuishi Matemwe Kijini.

Miradi iliotembelewa na kukaguliwa na Mwenge wa Uhuru Kitaifa ni mradi wa Hoteli ya kisasa nyota tano ya Kappa Sense Pwani Mchangani na ujenzi wa barabara Kijini.

Tanzania yetu sote, tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo.

Mwenge wa Uhuru Kitaifa umekimbizwa katika Mkoa wa Kaskazini Unguja katika  Wilaya ya Kasakazini B na kutembelea Miradi ...
11/04/2026

Mwenge wa Uhuru Kitaifa umekimbizwa katika Mkoa wa Kaskazini Unguja katika Wilaya ya Kasakazini B na kutembelea Miradi mbalimbali na kuwekewa jiwe la msingi.

Miradi iliotembelewa na kuwekewa jiwe la msingi ni mradi wa Taifa gasi Kidanzini, uwanja wa mpira Pangatupu,jengo la dahalia skuli ya Ali Juma Shamuhuna Donge, Hoteli ya Palm Beach Resort Kiwengwa na Medexpress Kiwengwa.

Miradi iliotembelewa na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru Kitaifa ni mradi wa barabara ya Kazole, Matetema, Zingwezingwe na Mangapwani.

Tanzania yetu sote, tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo

Mwenge wa Uhuru Kitaifa umekimbizwa katika Mkoa wa Kusini Unguja Wilaya ya Kati na kutembelea Miradi mbalimbali na kuwek...
09/04/2026

Mwenge wa Uhuru Kitaifa umekimbizwa katika Mkoa wa Kusini Unguja Wilaya ya Kati na kutembelea Miradi mbalimbali na kuweka jiwe la msingi.

Miradi iliotembelewa na kuwekewa jiwe la msingi la ufunguzi la mradi wa Swahili Tent village Chwaka,mradi wa viwanja michezo Unguja ukuu Kaebona.
Miradi iliotembelewa na kukagua kwa Mwenge wa Uhuru Kitafa kituo cha afya Tunguu, ujenzi wa daraja la Unguja Ukuu kaepwani na Uzi,ujenzi wa skuli ya Secondary Koani na mradi wa afya jamii Pongwe pwani.

Aidha kiongozi wa Mwenge wa Uhuru Wazo Michael Mwang'onda ameshiriki katika nupandaji miti aina ya mikoko kwa lengo la kuhifadhi mazingira yalioathirika katika ukataji miti ya mikoko Unguja ukuu kaepwani na kufunga kongamano la vijana kuhusu VVU/UKIMWI, dawa za kulevya, Rushwa na kugawa mitungi ya gesi.

Tanzania yetu sote, tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo

Mwenge wa Uhuru Kitaifa umekimbizwa katika  Wilaya ya Magharibi B na kutembelea Miradi mbalimbali na kuweka jiwe la msin...
08/04/2026

Mwenge wa Uhuru Kitaifa umekimbizwa katika Wilaya ya Magharibi B na kutembelea Miradi mbalimbali na kuweka jiwe la msingi.

Miradi iliotembelewa na kuwekewa jiwe la msingi ni nyumba ya daktari Shakani, mradi wa barabara ya ndani kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 1.5 kutoka matogo hadi skuli ya Fuoni.

Pia miradi iliozinduliwa na mwenge wa Uhuru Kitaifa Madarasa manne na ukumbi wa skuli ya maandalizi ya Nyamanzi, Kituo cha Polisi cha Magogoni, Kituo cha vijana chenye programu ya darasa la vijana katika kituo cha tehama kilichofanyiwa ukarabati na kuwekewa vifaa.

Aidha kiongozi wa Mwenge wa Uhuru Wazo Michael Mwang'onda ameshiriki katika ujenzi wa Taifa wa mradi wa nyumba za kisasa (Mwinyi House Scheme) block D Kisakasaka, upandaji miti lengo la kuhifadhi mazingira yalioathirika na uchimbaji wa mchanga skuli ya Magogoni, kufunga mafunzo ya falsafa ya Mwenge wa Uhuru Kitaifana kutembelea mradi wa afya jamii Mwanakwerekwe.

"Tanzania yetu sote, tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo"

Mwenge wa Uhuru Kitaifa umendelea  umekimbizwa katika Mkoa wa Mjini Magharibi Wilaya ya Magharibi A na kutembelea Miradi...
07/04/2026

Mwenge wa Uhuru Kitaifa umendelea umekimbizwa katika Mkoa wa Mjini Magharibi Wilaya ya Magharibi A na kutembelea Miradi mbalimbali na kuweka jiwe la msingi.

Miradi iliotembelewa na Mwenge wa Uhuru Kitaifa ni ujenzi wa Skuli ya msingi Mtopepo na kushiriki katika ujenzi wa taifa, mradi wa maboresho na upatikanaji wa nishati ya umeme.

Aidha kiongozi wa Mwenge wa Uhuru Wazo Michael Mwang'onda amefunga mafunzo kuhusiana na umoja, kupiga vita dawa za kulevya na kupambana dhadi ya rushwa,kutembelea mradi wa afya ya jamii, kupanda miti katika eneo la Jambo spices na Zapline ambapo wanahifadhi mazingira na kugawa mitungi ya gasi kwa wajasiliamali.

"Tanzania yetu sote, tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo"

07/04/2026

Address

Migombani
Zanzibar

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Idara ya maendeleo ya Vijana Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Idara ya maendeleo ya Vijana Zanzibar:

Share