Wizara ya Kilimo Umwagiliaji Maliasili na Mifugo

Wizara ya Kilimo Umwagiliaji Maliasili na Mifugo Agriculture continues to be among the important economic sectors in Zanzibar as it supports the livelihoods of 70% of the population directly and indirectly.

For the year 2021, agriculture sector accounted for 27.1% of the total GDP, whereby the Livestock

03/09/2026
Naibu Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Dkt. Salum Soud Hamed, akisalimiana na Katibu wa CCM ...
03/09/2026

Naibu Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Dkt. Salum Soud Hamed, akisalimiana na Katibu wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ndugu Haji Machano Juma, kabla ya kuanza ziara ya kuwatembelea vijana wa hamasa wanaojishughulisha na shughuli za kilimo katika Wilaya ya Kaskazini A.

Waziri wa kilimo Umwagiliaji,Maliasili na Mifugo Mhe.Suleiman Masoud Makame amesema wafugaji wanahitaji elimu ya uzalish...
03/09/2026

Waziri wa kilimo Umwagiliaji,Maliasili na Mifugo Mhe.Suleiman Masoud Makame amesema wafugaji wanahitaji elimu ya uzalishaji wa kisasa wa Mifugo utakao wapatia faida

Aliyosema hayo huko Tunguu Mkoa wa kusini Unguja wakati wa Majuisho ya ziara ya kuwatembelea wafugaji wa kuku Mbuzi na Kondoo katika maeneo ya Bwejuu Dongwe Unguja Ukuu tindini, Bungi na Tunguu

Amesema ziara hiyo inalengo la kuona shughuli za wafugaji kuwatambua na kuwashauri namna ya taratibu bora za ufugaji pamoja na changamoto zao na kushauriana namna ya kuzitatuwa.

Aidha Katika ziara hiyo Mhe . Waziri aliweza kuona uzalishaji wa kuku wa nyama na mayai na kuwataka wataalamu wa mifugo kuwasaidia elimu ili waweze kufuga kibiashara na uwezeshwaji kupitia Bank za kilimo.

Katika ziara hiyo Mhe waziri aliongozana na Mkurugenzi Wa Mifugo,kilimo na maafisa wa Mifugo

Afisa Mkuu Utumishi Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Masoud Salum Abdi, amewataka  vijana kuwa wabuni...
03/09/2026

Afisa Mkuu Utumishi Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Masoud Salum Abdi, amewataka vijana kuwa wabunifu katika minyororo wa Usarifu wa taka taka na kubuni vitu vipya ambavyo vitaleta tija kwao na taifa kwa ujumla.
Amesema hayo katika Ukumbi wa Ofisi za Uvuvi MARUHUBI Unguja. wakati akifunga rasmi mafunzo ya siku 3 waliyopatiwa wajasiriamali vijana (WABUZA) wanao sarif takaka kua bidhaa na fursa za biashara yakiwa na Lengo la kuwawezesha vijana kujua thamani ya bidhaa na utunzaji mzuri wa kumbukumbu kwani chachu ya Maendeleo kwa Vijana

Afisa Mkuu wa Utumishi katika Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Masoud Salum Abdi, amesema usarifu wa ...
01/09/2026

Afisa Mkuu wa Utumishi katika Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Masoud Salum Abdi, amesema usarifu wa taka kuwa bidhaa na fursa za biashara ni chachu ya maendeleo na ajira kwa vijana.

Masoud amesema hayo kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa Mipango, Rashid Khamis Rashid, katika Ofisi za Mradi wa ASSP, Maruhubi, Zanzibar, wakati akipokea shukrani kutoka kwa vijana wa Waste Based Business in Zanzibar (WABUZA) walioshiriki Maonesho ya Nane Nane yaliyofanyika Dole Kizimbani.

Amesema Wizara iko tayari kushirikiana na vijana hao katika kuendeleza shughuli zao za kibiashara, huku akiwataka kuongeza juhudi katika kukuza masoko na kutumia taka k**a fursa ya kujikwamua kiuchumi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa WABUZA, Mwanaidi Maneno Abrahmani, amesema ushiriki wao katika maonesho hayo umeongeza hamasa kwa vijana kutumia taka na mabaki ya chakula kuzalisha bidhaa na kujipatia ajira na kipato.

Ametaja bidhaa zinazozalishwa kuwa ni pamoja na mbolea, mapambo, mkaa mbadala na funza lishe.

Naye Meneja Mwandamizi wa HELVETAS, Chioma Nangale, amesema jitihada za vijana hao ni fursa ya kuendelea kuwawezesha kupitia elimu, mafunzo na ujuzi wa biashara ili kuongeza ajira na kipato.

Mlezi wa vijana hao na mwakilishi wa HELVETAS, Masha Saidi Sukwa, amewataka kuendeleza usarifu wa taka kwa kuwa ni njia ya kukuza biashara, ajira na maendeleo endelevu.

Wasilisho kuhusu huduma za upandishaji wa ng’ombe kwa sindano (AI) limewasilishwa na Suleiman Ali Hamad kwa niaba ya tim...
01/09/2026

Wasilisho kuhusu huduma za upandishaji wa ng’ombe kwa sindano (AI) limewasilishwa na Suleiman Ali Hamad kwa niaba ya timu ya wataalamu waliopewa jukumu la kufanya utafiti huo.

Ripoti hiyo ya kitaalamu imetolewa katika kikao kilichowakutanisha wataalamu, wastaafu wa mifugo, wakuu wa taasisi na wadau kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.

Kikao hicho kilifanyika katika Ofisi za Kilimo Maruhubi kupitia Mradi wa Mabadiliko ya Sekta ya Maziwa kwa kuzingatia Mabadiliko ya Tabianchi (CSDTP)

Utafiti huo unalengo la kuboresha huduma za AI kwa kuzingatia ubora wa mifugo, kuongeza uzalishaji wa ng’ombe bora pamoja na kuongeza uzalishaji wa maziwa.

Katika kikao hicho, washiriki walitoa maoni na mapendekezo ya kuboresha ripoti hiyo, katika kuimarisha miundombinu, upatikanaji wa vifaa na kuongeza ujuzi wa wataalamu, ili kuboresha utoaji wa huduma za uhimilishaji wa ng’ombe na kuleta mabadiliko katika sekta ya mifugo nchini

Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Mhe. Suleiman Masoud Makame, amewataka wafanyakazi na walin...
01/09/2026

Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Mhe. Suleiman Masoud Makame, amewataka wafanyakazi na walinzi wa Hifadhi ya Taifa Jozani Ghuba ya Chwaka kuendelea kulinda na kutunza rasilimali zilizopo katika hifadhi hiyo kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Waziri Makame ameyasema hayo wakati wa hafla ya kukabidhi sare za kazi (uniform) kwa wafanyakazi 65 wa Hifadhi ya Taifa ya Jozani, iliyopo Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema utoaji wa sare hizo ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuwawezesha wafanyakazi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi, hususan katika ulinzi na uhifadhi wa rasilimali za hifadhi hiyo, pamoja na kuwabaini watu wasiohusika wanaoingia katika maeneo yaliyohifadhiwa.

Amesema Hifadhi ya Msitu wa Jozani ni miongoni mwa maeneo ya hifadhi yanayotambulika kimataifa, hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kuendelea kuilinda, kuihifadhi na kuiendeleza ili iendelee kuwa kivutio bora kwa watalii wanaoingia nchini.

"Nawaomba tuendelee kuulinda rasilimali hii ya msitu, kwani kufanya hivyo kutasaidia kuongeza kipato kwa wananchi na Taifa kwa ujumla,” alisema Makame.

Aidha, Waziri Makame ametoa wito kwa wafanyakazi na walinzi wa hifadhi hiyo kuendelea kupatiwa mafunzo ya ulinzi na uhifadhi ili wawe na uwezo wa kukabiliana na changamoto mbalimbali, ikiwemo vitendo vya uhalifu vinavyoweza kuhatarisha rasilimali za hifadhi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Misitu, Said Juma Ali, amesema sare hizo zimetolewa kwa lengo la kuwatambulisha wafanyakazi wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao ndani ya hifadhi, pamoja na kuongeza ufanisi katika shughuli za ulinzi na uhifadhi.

Amesema utoaji wa sare hizo ni utaratibu unaofanyika kila baada ya miaka mitatu, ambapo fedha za ununuzi wake hutokana na mapato yanayopatikana katika Hifadhi ya Taifa Jozani.

Amewataka wafanyakazi hao kutumia sare hizo ipasavyo na kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa bidii ili kuhakikisha rasilimali za hifadhi hiyo zinaendelea kulindwa na kunufaisha jamii.

Nae mmoja wa wafanyakazi aliyepokea sare hizo, Mauli Makame Haji, amesema sare hizo zitawasaidia kutambulika kwa urahisi wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao katika hifadhi hiyo.

Ameiomba Idara ya Misitu kuendelea kutoa ajira zaidi ili kuongeza idadi ya wafanyakazi na walinzi, hatua ambayo itasaidia kuimarisha ulinzi na uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa Jozani.

Jumla ya Shilingi milioni 18.65 zimetumika kununua sare hizo, ambazo zitanufaisha walinzi, watembezaji watalii, pamoja na watumishi wa Usafi.

Kikao  cha k**ati Tendaji ya  Mradi wa Uendelezaji wa Mfumo wa Chakula  Matumizi Bora ya Ardhi, Maji na Urejeshaji wa Mi...
01/09/2026

Kikao cha k**ati Tendaji ya Mradi wa Uendelezaji wa Mfumo wa Chakula Matumizi Bora ya Ardhi, Maji na Urejeshaji wa Misitu (FOLUR) kwa mwaka 2026/2027 kimefanyika katika Chuo cha Utalii Maruhubi, Zanzibar.

Kikao hicho kimewakutanisha Maafisa Misitu maji ardhi na wadau wa mradi huo kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kujadili mipango ya utekelezaji wa mradi huo.

Washiriki wa kikao hicho wamejadili mafanikio yaliopo changamoto na mikakati ya kuimarisha Matumizi ya fedha katika matumizi bora ya kuendeleza utuzaji wa ardhi, uhifadhi wa vyanzo vya maji na urejeshaji wa misitu ili kutunza mazingira,

Mradi Huo wa FOLUR unatekelezwa kwa Miaka mitano kwa ufadhili wa Mfuko wa Mazingira Duniani (GEF) chini ya usimamizi wa pamoja wa wizara ya Maliasili na Utalii Tanzania Bara na wizara ya kilimo,Umwagiliaji,Maliasili na Mifugo Zanzibar utekelezaji ukiwa katika eneo la Kaskazini kwa upande wa Unguja na kilimbero Tanzania bara.

Address

Maruhibi/Zanzibar
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wizara ya Kilimo Umwagiliaji Maliasili na Mifugo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share