03/09/2026
Serikali kwa kushirikiana na wadau wa elimu imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunzia, ikiwemo upatikanaji wa vifaa vinavyowasaidia kukabiliana na changamoto ya uoni na kuimarisha uwezo wao wa kujifunza.
Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Mkurugenzi wa Bodi ya Huduma za Maktaba Zanzibar, Ulfat Abdulaziz Ibrahim, amesema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali kuhakikisha kila mtoto anapata nafasi na haki ya kujifunza katika mazingira yanayomwezesha kufikia malengo yake.