ZBC Zanzibar

ZBC Zanzibar Ukurasa Rasmi Wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiagana na viongozi mbalimbali katika Uwanja wa...
02/06/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiagana na viongozi mbalimbali katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam, kabla ya kuondoka nchini kuelekea Shirikisho la Urusi kwa ziara ya kitaifa itakayofanyika kuanzia tarehe 3 hadi 5 Juni 2026.

Ziara hiyo inafanyika kwa mwaliko wa Rais wa Shirikisho la Urusi, Mheshimiwa Vladimir Putin, na inalenga kuimarisha ushirikiano na mahusiano ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi.

02/06/2026

Mkurugenzi Mwendeshaji wa ZIC Takaful, Said Basleyum amesema huduma za kampuni hiyo zinapatikana kote nchini kupitia ofisi zake zilizopo Zanzibar na Dar es Salaam pamoja na kupitia benki zinazotoa huduma za kifedha za Kiislamu ikiwemo CRDB, NBC, KCB, PBZ na Amana Bank.

Basleyum amesema huduma za bima zinazotolewa na ZIC Takaful zinafanya kazi kwa utaratibu unaofanana na kampuni nyingine za bima, ambapo mteja hupata fidia pindi anapopata hasara au ajali inayostahili kufidiwa kwa mujibu wa masharti ya bima.

Ameeleza kuwa kwa upande wa bima ya magari, fidia inaweza kutolewa kwa uharibifu wa mali za watu wengine, majengo, magari, pamoja na majeraha au vifo vinavyotokana na ajali za barabarani. Aidha, gharama za matibabu na fidia zinazoweza kuamriwa na mahak**a hulipwa kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa.

Amesema licha ya mteja kulipa kiwango kidogo cha ada ya bima kwa mwaka, huduma hiyo humkinga dhidi ya hasara kubwa ambazo zinaweza kufikia mamilioni ya shilingi endapo atahusika katika ajali au tukio linalostahili kufidiwa.

Basleyum amesisitiza kuwa utaratibu wa ulipaji fidia unasimamiwa na mamlaka ya bima nchini, huku kampuni zote za bima zikifuata sheria na miongozo inayofanana katika utoaji wa huduma hizo.

Amesema hayo katika kipindi cha Asubuhi Njema.


Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika UNESCO, Mhe. Saidi ...
02/06/2026

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika UNESCO, Mhe. Saidi Othman Yakubu, amewasilisha rasmi Hati za Utambulisho kwa Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO, Profesa Khaled El-Enany, katika Makao Makuu ya Shirika hilo jijini Paris, Ufaransa.

Uwasilishaji huo wa hati unamwezesha Mhe. Balozi Yakubu kuanza rasmi majukumu yake k**a Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika UNESCO, shirika la Umoja wa Mataifa linalojihusisha na masuala ya elimu, sayansi, utamaduni na mawasiliano.

Baada ya hafla hiyo, viongozi hao walifanya mazungumzo yaliyolenga kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na UNESCO katika sekta za elimu, sayansi, utamaduni, uhifadhi wa urithi wa dunia pamoja na maendeleo ya rasilimali watu.

Katika mazungumzo hayo, Mhe. Balozi Yakubu aliwasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kueleza dhamira ya Tanzania ya kuendelea kushirikiana kwa karibu na UNESCO katika kutekeleza ajenda za maendeleo endelevu na kukuza ustawi wa wananchi kupitia elimu, sayansi na utamaduni.

Kwa upande wake, Profesa El-Enany amepongeza mafanikio na hatua za maendeleo zinazopatikana nchini Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kueleza kufurahishwa kwake na mchango wa Tanzania ndani ya UNESCO. Aidha, ameahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na UNESCO kwa manufaa ya pande zote mbili.

Sikiliza kipindi cha PAMBAZUKO kupitia ZBC Radio, tukikuletea uchambuzi wa Mada,Habari, Mawio, Magazeti na matangazo ya ...
02/06/2026

Sikiliza kipindi cha PAMBAZUKO kupitia ZBC Radio, tukikuletea uchambuzi wa Mada,Habari, Mawio, Magazeti na matangazo ya Vifo

🎙Mwajuma Khamis

Tunapatika kupitia Unguja 90.6 MHz Pemba 94.1 MHz kuanzia saa 12 kamili tukuletee Habari Mawio na Habari za Vifo.

Kipindi cha Asubuhi Njema kipo LIVE muda huu!Cc. Amina Mkombe,  na   na kwenye uchambuzi wa michezo ni 📺 Washa ZBC Chann...
02/06/2026

Kipindi cha Asubuhi Njema kipo LIVE muda huu!

Cc. Amina Mkombe, na na kwenye uchambuzi wa michezo ni

📺 Washa ZBC Channel 01 kupitia king’amuzi cha BAYT.
Usikose mada ya siku, Jicho la tatu, Ukweli si Uvumi na Uchambuzi wa michezo.


Kurasa za juu za Magazeti ya leo Juni 02 2026.
02/06/2026

Kurasa za juu za Magazeti ya leo Juni 02 2026.

01/06/2026

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imekanusha taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikidai kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemgomea Msajili wa Vyama vya Siasa, ikieleza kuwa taarifa hiyo ni ya uongo na inalenga kupotosha umma.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 1, 2026, Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza, amesema Ofisi ya Msajili iliandika barua mbili kwa CCM tarehe 15 na 19 Mei, 2026 kufuatia matukio yaliyojitokeza katika mikutano ya hadhara ya chama hicho.

Amesema barua ya kwanza ilitakiwa kujibiwa kabla ya Mei 21, 2026, huku ya pili ikitakiwa kujibiwa kabla ya Mei 29, 2026. Kwa mujibu wa Nyahoza, CCM tayari imewasilisha majibu ya barua zote mbili na Ofisi ya Msajili imeyapokea na inaendelea kuyafanyia kazi.

“Kinachoelezwa katika mitandao ya kijamii kwamba CCM wamemgomea Msajili siyo kweli. Tunawaomba Watanzania kupuuza taarifa hizo za upotoshaji,” amesema Nyahoza.

01/06/2026

Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama barabarani Mkoani Arusha limefanikiwa kuwak**ata madereva wawili na kuwafungia leseni zao za udereva kufuatia picha mjongeo inayosambaa katika baadhi ya mitandao ya kijamii ikionesha wakiendesha magari kwa njia hatarishi.

Akifafanua tukio hilo leo Juni 01,2026, Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani mkoani humo, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Zauda Mohamed amewataja madereva hao kuwa ni Reginald Nzonda aliyekuwa anaendesha gari namba T. 869 EJP na Hatibu Kapire aliyekuwa anaendesha gari namba T. 136 EFP yote aina ya Scania.

Aidha, ametoa wito kwa madereva kuhakikisha wanazingatia sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani huku akitoa msisitizo kwa madereva vijana wanaokuwa na mihemko ya kutafuta umaarufu katika mitandao ya kijamii kwa lengo la kupata wafuasi wengi.

Sambamba na hilo amesema kuwa Jeshi hilo litaendelea kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria kwa madereva wote wanaokiuka sheria za usalama barabarani.

Wakizungumza mara baada ya kuk**atwa madereva hao, wamesema kuwa walifanya kitendo hicho kwa lengo la kutafuta wafuasi mitandaoni, ambapo wamejutia kosa hilo ambalo ni kinyume cha sheria na kuwataka madereva wengine kuzingatia sheria wakati wote na kuepuka michezo hatarishi wawapo barabarani.

01/06/2026

Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa , ameishauri serikali kufanya marekebisho ya sheria ili kuongeza adhabu dhidi ya wazazi wanaokwepa majukumu ya malezi na kuwaachia mzigo huo wanawake pekee, akisema adhabu zilizopo sasa ni ndogo na haziendani na uhalisia wa kiuchumi.

Mheshimiwa Kisuo ametoa kauli hiyo leo bungeni mjini Dodoma, wakati akichangia mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Akifafanua hoja yake, Mbunge huyo amebainisha kuwa faini ya sasa ya shilingi laki tano (Tsh 500,000) na kifungo cha kuanzia miezi sita kwa wazazi wanaotelekeza watoto ni adhabu ndogo mno ambayo haikidhi mahitaji halisi ya malezi ya mtoto katika mazingira ya sasa.

Mheshimiwa Kisuo ameongeza kuwa, ukiachilia mbali athari za kiuchumi kwa akina mama, kitendo cha kutelekeza watoto kinachangia kwa kiasi kikubwa mmonyoko wa maadili katika jamii, jambo ambalo hatimaye linajenga mzigo mwingine mzito kwa serikali katika kugharamia na kuhudumia maendeleo ya jamii.

Kufuatia hali hiyo, ameitaka Wizara husika kushirikiana na mamlaka za kisheria kuangalia upya sheria hizo ili kutoa adhabu zitakazokuwa fundisho na zitakazowalazimisha wazazi wote wawili kushiriki kikamilifu katika malezi ya watoto wao.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, atafanya Ziara ya Kitaifa katika Shirikish...
01/06/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, atafanya Ziara ya Kitaifa katika Shirikisho la Urusi kuanzia tarehe 3 hadi 5 Juni 2026, kwa mwaliko wa Rais wa Shirikisho la Urusi, Mheshimiwa Vladimir Putin.
Ziara hii ni ya kihistoria kwa kuwa itakuwa ya pili kufanywa na Rais wa Tanzania nchini Urusi, baada ya ile ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, iliyofanyika mwezi Oktoba mwaka 1969.

Ziara hiyo itaimarisha uhusiano wa muda mrefu wa kidiplomasia, kisiasa, kiuchumi na kihistoria kati ya nchi hizi mbili. Wakati wa ziara hiyo, Rais Dkt. Samia atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake, Rais Putin, katika Ikulu ya Kremlin jijini Moscow.

Mazungumzo yao yatajikita katika kuimarisha ushirikiano katika sekta za kimkakati, ikiwemo biashara na
uwekezaji, elimu, sayansi na teknolojia, nishati, madini, kilimo, miundombinu na utalii.
Ziara hiyo inakuja wakati Tanzania ikiendeleza ajenda yake ya diplomasia ya uchumi kupitia ushiriki wake katika majukwaa makubwa ya kimataifa yanayowakutanisha viongozi wa serikali, wawekezaji, taasisi za fedha, sekta binafsi na watunga sera.

Akiwa nchini Urusi, Rais Dkt. Samia atashiriki na kuhutubia katika Jukwaa la 29 la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg (SPIEF 2026), ambalo ni miongoni mwa majukwaa yenye ushawishi mkubwa duniani kwa mijadala kuhusu maendeleo ya uchumi, biashara na uwekezaji. Ushiriki wake katika kikao hicho cha ngazi ya juu unaakisi kuongezeka kwa nafasi na ushawishi wa Tanzania katika mijadala ya kimataifa kuhusu uchumi.

Address

Zanzibar
Zanzibar
70001

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ZBC Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to ZBC Zanzibar:

Share