Mahkama ya Zanzibar

Mahkama ya Zanzibar Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Mahkama ya Zanzibar, Government Organization, BOX NO 160, ZANZIBAR, Zanzibar.

Majaji wa Mahkama ya Zanzibar, Mahakimu na wadau wa Mahkama wakiwemo Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Zanzibar (...
05/06/2026

Majaji wa Mahkama ya Zanzibar, Mahakimu na wadau wa Mahkama wakiwemo Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Zanzibar (ZAECA), Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar (DPP), Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Zanzibar pamoja na Jeshi la Polisi, wakiendelea kupata Mafunzo ya Mapitio ya Mwongozo wa Urejeshaji Mali zitokanazo na Makosa ya Jinai (Asset Recovery Guidelines Review) leo tarehe 05/06/2026, ikiwa ni siku ya mwisho ya mafunzo hayo ambayo yalianza tarehe 03/06/2026.

Mafunzo hayo kwa siku ya leo yaliendeshwa na Mhe. Jaji Michael Hopmeier kutoka nchini Uingereza na yanalenga kuwajengea uelewa wa kina washiriki kuhusu mwongozo wa urejeshaji mali zitokanazo na makosa ya jinai na namna unavyotumika katika mfumo wa haki jinai. Kuimarisha uwezo wa taasisi zinazohusika katika kufuatilia, kugundua, kufungia, kukamata na kurejesha mali zilizopatikana kwa njia za uhalifu.

sambamba na hilo, mafunzo yanalenga kuimarisha ushirikiano na uratibu kati ya vyombo vya uchunguzi, Mashtaka, Mahkama na Taasisi nyingine zinazoshughulikia masuala ya urejeshaji mali pamoja kubadilishana uzoefu na mbinu bora za kimataifa katika kushughulikia kesi za urejeshaji mali zitokanazo na makosa ya jinai.

Mafunzo hayo yanadhaminiwa na “Basel Institute on Governance” kutoka nchini Switzerland na yanafanyika katika hoteli ya Golden Tulip, iliyopo Uwanja wa Ndege wa AAKIA Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.

04/06/2026
Majaji wa Mahkma Kuu na Mahakimu leo tarehe 3/06/2026 wameshiriki katika Mafunzo ya Mapitio ya Mwongozo wa Urejeshaji Ma...
03/06/2026

Majaji wa Mahkma Kuu na Mahakimu leo tarehe 3/06/2026 wameshiriki katika Mafunzo ya Mapitio ya Mwongozo wa Urejeshaji Mali zitokanazo na Makosa ya Jinai (Asset Recovery Guidelines Review) .

Mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uelewa wa kina washiriki kuhusu mwongozo wa urejeshaji mali zitokanazo na makosa ya jinai na namna unavyotumika katika mfumo wa haki jinai. Kuimarisha uwezo wa taasisi zinazohusika katika kufuatilia, kugundua, kufungia, kukamata na kurejesha mali zilizopatikana kwa njia za uhalifu.

Pia, kuimarisha ushirikiano na uratibu kati ya vyombo vya uchunguzi, Mashtaka, Mahkama na Taasisi nyingine zinazoshughulikia masuala ya urejeshaji mali pamoja kubadilishana uzoefu na mbinu bora za kimataifa katika kushughulikia kesi za urejeshaji mali zitokanazo na makosa ya jinai.

Mafunzo hayo yanadhaminiwa na “Basel Institute on Governance” kutoka nchini Switzerland yanatarajiwa kuwa ya siku tatu kuanzia tarehe 03 hadi 5 Juni, 2026 na yanafanyika katika hoteli ya Golden.

Jaji Mkuu wa  Zanzibar, Mhe. Khamis Ramadhan Abdalla, akimkabidhi zawadi ya Mlango wa Zanzibar (Zanzibar door) Mtaalamu ...
02/06/2026

Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Khamis Ramadhan Abdalla, akimkabidhi zawadi ya Mlango wa Zanzibar (Zanzibar door) Mtaalamu wa Mafunzo ya Mapitio ya Mwongozo wa Urejeshaji Mali zitokanazo na Makosa ya Jinai (Asset Recovery Guidelines Review), Mhe. Jaji Michael Hopmeier kutoka nchini Uingereza. Zawadi hiyo alimkabidhi baada ya kikao cha kubadilishana mawazo juu ya mafunzo hayo kilichofanyika tarehe 02/06/2026 katika ofisi yake iliyopo Mahkama Kuu, Tunguu-Zanzibar.

Mafunzo hayo yanatarajiwa kufanyika tarehe 03-5 Juni, 2026 katika hoteli ya Golden Tulip Zanzibar na yanawalenga waheshimiwa Majaji, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar (DPP), Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Zanzibar (ZAECA), Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Zanzibar pamoja na Jeshi la Polisi, kwa lengo la kuimarisha uelewa na uwezo katika utekelezaji wa taratibu za urejeshaji mali zitokanazo na makosa ya jinai.

Waliokuwa  Majaji wa Mahkama Kuu ya Zanzibar Mhe. Rabia Hussein Mohamed na Mhe. Ibrahim Mzee Ibrahim leo tarehe 26/05/20...
26/05/2026

Waliokuwa Majaji wa Mahkama Kuu ya Zanzibar Mhe. Rabia Hussein Mohamed na Mhe. Ibrahim Mzee Ibrahim leo tarehe 26/05/2026 wamekula kiapo cha kuwa Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania.

Mahkama ya Zanzibar leo tarehe 25 Mei 2026 imetoa elimu kwa wananchi wa  Uroa kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa usikiliza...
25/05/2026

Mahkama ya Zanzibar leo tarehe 25 Mei 2026 imetoa elimu kwa wananchi wa Uroa kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa usikilizaji wa mashauri kwa njia ya kielektroniki, ikiwa ni sehemu ya Maboresho ya huduma za Mahkama na kurahisisha upatikanaji wa haki kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa utoaji wa elimu hiyo, Kadhi wa Wilaya Sheikh Hemed Seleh amesema mfumo huo utasaidia kuongeza uwazi, kuharakisha usikilizaji wa mashauri pamoja na kupunguza usumbufu kwa wadau wa Mahkama.

Wananchi wa Uroa walipata fursa ya kuuliza maswali na kufahamishwa namna mfumo huo fanya Utakanyofanya kazi, huku wakihimizwa kutumia huduma za Mahkama kwa kufuata taratibu na sheria zilizowekwa.

Mahkama ya Zanzibar inaendelea kutoa elimu kwa jamii katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha wananchi wanaelewa maboresho yanayoendelea kufanyika katika sekta ya utoaji haki.

JAJI MKUU WA ZANZIBAR AFUNGUA MAFUNZO YA KUSHUGHULIKIA MIGOGORO YA MIRATHI Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Ramdhan Khamis Ab...
25/05/2026

JAJI MKUU WA ZANZIBAR AFUNGUA MAFUNZO YA KUSHUGHULIKIA MIGOGORO YA MIRATHI

Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Ramdhan Khamis Abdalla, amesema kuwa mafunzo kuhusu namna ya kushughulikia migogoro ya mirathi yatawasaidia kuongeza uwezo na uelewa wa kina katika kutatua changamoto zinazohusiana na masuala ya mirathi, jambo ambalo litachangia kuimarisha utoaji wa haki kwa wananchi na kupunguza migogoro katika jamii.

Mhe. Jaji Mkuu ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kuhusu namna ya kushughulikia migogoro ya mirathi yaliyofanyika katika Hoteli ya Mdinat Al Bahr iliyopo Mbweni, Mkoa wa Mjini Magharibi. Ambapo mafunzo hayo yamejumuisha Majaji wa Mahkama kuu ya Zanzibar pamoja na washiriki mbalimbali katutoka katika taasisi zenye jukumu la kushughulikia masuala ya mirathi ikiwemo Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana Zanzibar.

Amesema kuwa migogoro ya mirathi ni miongoni mwa changamoto zinazojitokeza mara kwa mara katika jamii na wakati mwingine husababisha migawanyiko ndani ya familia pamoja na kuathiri mahusiano ya kijamii. Amesisitiza kuwa kutokuwepo kwa uelewa wa kutosha kuhusu sheria, taratibu na haki za wahusika mara nyingi huwa chanzo cha migogoro hiyo kuendelea kwa muda mrefu.

Aidha, Mhe. Jaji Mkuu amefahamisha kuwa mafunzo hayo yana umuhimu mkubwa kwa washiriki kutokana na mchango wake katika kuongeza maarifa na kuwajengea uwezo wa kushughulikia kesi na migogoro ya mirathi kwa ufanisi zaidi, na ni wajibu wa washiriki kuyapa uzito mafunzo yote yatakayotolewa ili waweze kupata maarifa yatakayowasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Pia amewataka washiriki kutumia nafasi hiyo kujifunza, kuuliza maswali na kubadilishana uzoefu unaoweza kusaidia kuboresha utendaji kazi wao, huku akieleza kuwa elimu inayopatikana kupitia mafunzo hayo itakuwa na manufaa makubwa si kwa washiriki pekee bali pia kwa jamii nzima inayotarajia kupata huduma bora na haki stahiki.

Kwa upande mwingine ameeleza kuwa mafunzo hayo yameandaliwa kwa lengo la kuwajengea uwezo washiriki katika mbinu mbalimbali za kushughulikia migogoro ya mirathi kwa njia ya haki, usawa na kufuata misingi ya sheria, na inatarajiwa kuwa maarifa yatakayopatikana yatachangia kupunguza migogoro ya mirathi katika jamii pamoja na kuimarisha mfumo wa utoaji wa haki Zanzibar.

Mafunzo hayo yanafanyika chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia kupitia mradi wa Maboresho ya Mahkama (Zi-JUMP).

Mahkama ya Zanzibar leo tarehe 22/05/2026 imetoa Elimu ya mfumo mpya wa kusikiliza Mashauri kwa Njia ya Kielentronik kwa...
22/05/2026

Mahkama ya Zanzibar leo tarehe 22/05/2026 imetoa Elimu ya mfumo mpya wa kusikiliza Mashauri kwa Njia ya Kielentronik kwa wananchi wa Shehia ya Gamba, lengo ni kuwapa uweleza wa jinsi ya kufunga mashauri kwa njia ya kielentronik popote ulipo pale mfumo utakapoanza kutumika rasmi

Address

BOX NO 160, ZANZIBAR
Zanzibar
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mahkama ya Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share