05/06/2026
Majaji wa Mahkama ya Zanzibar, Mahakimu na wadau wa Mahkama wakiwemo Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Zanzibar (ZAECA), Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar (DPP), Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Zanzibar pamoja na Jeshi la Polisi, wakiendelea kupata Mafunzo ya Mapitio ya Mwongozo wa Urejeshaji Mali zitokanazo na Makosa ya Jinai (Asset Recovery Guidelines Review) leo tarehe 05/06/2026, ikiwa ni siku ya mwisho ya mafunzo hayo ambayo yalianza tarehe 03/06/2026.
Mafunzo hayo kwa siku ya leo yaliendeshwa na Mhe. Jaji Michael Hopmeier kutoka nchini Uingereza na yanalenga kuwajengea uelewa wa kina washiriki kuhusu mwongozo wa urejeshaji mali zitokanazo na makosa ya jinai na namna unavyotumika katika mfumo wa haki jinai. Kuimarisha uwezo wa taasisi zinazohusika katika kufuatilia, kugundua, kufungia, kukamata na kurejesha mali zilizopatikana kwa njia za uhalifu.
sambamba na hilo, mafunzo yanalenga kuimarisha ushirikiano na uratibu kati ya vyombo vya uchunguzi, Mashtaka, Mahkama na Taasisi nyingine zinazoshughulikia masuala ya urejeshaji mali pamoja kubadilishana uzoefu na mbinu bora za kimataifa katika kushughulikia kesi za urejeshaji mali zitokanazo na makosa ya jinai.
Mafunzo hayo yanadhaminiwa na “Basel Institute on Governance” kutoka nchini Switzerland na yanafanyika katika hoteli ya Golden Tulip, iliyopo Uwanja wa Ndege wa AAKIA Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.