Idara ya Habari Maelezo Zanzibar

Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Idara ya Habari Maelezo Zanzibar (DIS), Ipo chini ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. Sehemu ya Utumishi na Uendeshaji
2. Sehemu ya Ufundi
5.

Idara ya Habari Zanzibar (ZIS) ni Idara chini ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo . Idara ya Habari MAELEZO Zanzibar inajukumu la kutoa taarifa kuhusu Sera, Mipango na utekelezaji wa miradi ya Maendeleo mbalimbali ya Serikali kwa wananchi. Idara imeanzishwa mwaka 1996 baada ya kutenganishwa kwa Sauti ya Tanzania Zanzibar ambayo sasa ni Shirika la Utangazaji Zanzibar kutoka Idara ya H

abari na Utangazaji iliyoundwa baada ya Mapinduzi ya Januari 12 mwaka 1964. Kwa sasa Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO ni Hassan Vuai na Naibu Mkurugenzi ni Dk Juma Mohammed Salum. Kimuundo wa Utawala, Idara imegawika sehemu tano(5) ambazo ndizo zinazounda Kamati ya Uongozi ya Idara k**a ifuatavyo:-
1. Sehemu ya Habari (Editorial)
3. Usajili wa Magazeti na Majarida
4. Sehemu ya Hesabu


S
MAJUKUMU YA IDARA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
Majukumu ya Idara hii ni pamoja na :-
1. Kuwa msemaji wa mambo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
2. Kuiwekea Serikali kumbukumbu katika kutayarisha na kutoa vielelezo vya sinema, video, majarida, vitabu vya taaluma, tamthilia na burudani.
3. Kusimamia utekelezaji wa Sera ya Habari ya Zanzibar na sheria Na. 5 ya mwaka 1988 inayohusiana na mambo ya vitabu na Magazeti
4. Kutetea msimamo wa Serikali katika kupambana na habari na tuhuma zinazotolewa na vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi dhidi ya Serikali
5. Kuishauri Serikali kuhusu nyendo za vyombo vya habari na kupendekeza hatua muafaka za kuchukuliwa
6. Kusimamia, kutoa au kuzuia vibali vya uanzishwaji wa magazeti na majarida mbalimbali Zanzibar
7. Kusimamia kutoa vitambulisho kwa waandishi wa Habari na wapigapicha wa ndani na nje ya Zanzibar watakaofanya kazi Zanzibar
8. Kuwaelekeza waandishi wa habarui watakaofanyakazi hapa Zanzibar maadili, maeneo na mipaka yao na utendaji

SERIKALI ya Mapindunzi Zanzibar kupitia Wizara ya Fedha na Mipango   imetiliana saini na kampuni ya Stabit Corporation L...
30/05/2026

SERIKALI ya Mapindunzi Zanzibar kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imetiliana saini na kampuni ya Stabit Corporation Limited na kampuni ya Salem Construction Limited ujenzi wa mikataba miwili chini ya Mradi wa BIG-Z, inayolenga kuimarisha miundombinu ya mijini, usimamizi wa mazingira na huduma za kijamii Zanzibar.

Mikataba hiyo inahusisha ujenzi wa Kituo cha kukusanyia Taka cha Fuoni Chunga (Solid Waste Transfer Station) pamoja na utekelezaji wa mradi salama wa watembea kwa miguu katika maeneo ya Mji Mkongwe (Stone Town Safe and Sustainable Mobility Program).

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Aboud Hussein Mwinyi alisema kusainiwa kwa mikataba hiyo ni hatua muhimu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayolenga kuimarisha maisha ya wananchi pamoja na mazingira ya miji.

Alisisitiza umuhimu wa wakandarasi kuzingatia ubora wa kazi, kusimamia muda wa utekelezaji kwa ufanisi na kuhakikisha kunakuwa na uratibu mzuri katika kipindi chote cha ujenzi.

“Tunatarajia kuona kazi zenye viwango bora, utekelezaji unaokwenda sambamba na muda uliopangwa pamoja na ushirikiano mzuri na jamii inayozunguka maeneo ya miradi,” alisema.

Aidha, aliwataka wakandarasi kuwa na mipango kazi madhubuti itakayosaidia utekelezaji wa miradi hiyo kufanyika bila kusababisha usumbufu kwa wananchi, wafanyabiashara na shughuli nyingine za kijamii katika maeneo husika.

" Kukamilika Kwa miradi hii kutaimarisha miundombinu ya mijini, usimamizi wa taka ngumu pamoja na kuweka mazingira salama na rafiki kwa watembea kwa miguu, hususan katika eneo la Mji Mkongwe ambalo ni kitovu cha urithi wa kihistoria na shughuli za kijamii na kiuchumi Zanzibar." Alisema Mwinyi

Kwa upande wao, wakandarasi waliopewa zabuni hizo walieleza utayari wao wa kutekeleza masharti yote yaliyowekwa katika mikataba hiyo, huku wakiahidi kuzingatia viwango vya ubora, usalama wa wafanyakazi, uhifadhi wa mazingira na maslahi ya jamii inayozunguka maeneo ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Abuzer Salem kutoka kampuni ya Salem Construction Limited alisisitiza dhamira yao ya kuhakikisha shughuli za

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuleta mageuzi ya kidijitali katika kujenga uchumi wa kisasa na kuimarisha ...
30/05/2026

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuleta mageuzi ya kidijitali katika kujenga uchumi wa kisasa na kuimarisha misingi ya Utawala Bora pamoja na matumizi ya teknolojia ili kuleta ufanisi nzuri wa kazi.

Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla katika hafla ya Warsha ya Serikali ya Kidigitali iliyofanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Golden Tulip Uwanja wa ndege Zanzibar.

Amesema teknolojia inasaidia katika kuharakisha utoaji wa huduma kwa umma, kuongeza ufanisi wa kiutendaji, kudhibiti mapato, kupunguza gharama za uendeshaji na kuimarisha uwazi katika utendeji wa kazi.

Makamu wa Pili wa Rais amefahamisha kuwa kwa sasa uchumi wa Zanzibar unategemea sana sekta zinazotoa huduma hivyo ni wajibu wa kila mmoja kujifunza kwa kuangalia mbinu mbali mbali zinazotumiwa na nchi ambazo uchumi wake unategemea zaidi huduma kwa kutumia teknolojia.

Mhe. Hemed amesema kuwa safari ya kuwa na Serikali ya kidijitali inajengwa na mifumo hivyo serikali imejipanga katika kuboresha mifumo ili kurahisisha upatikanaji wa huduma mbali mbali katika sekta moja.

Aidha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema muongozo wa matumizi ya Akili Mnemba uliopo utahakikisha matumizi ya Akili Mnemba yanakuwa nyenzo ya kuongeza tija na ubora wa utoaji wa huduma kwa wananchi, kulinda maslahi ya Taifa, kuzingatia usalama wa tarifa, maadili, uwajibikaji na ufanisi wa utoaji wa huduma.

Amesema kuwa Warsha hio itaongeza ujuzi na uelewa kuhusu matumizi sahihi na salama ya mifumo ya TEHAMA, ushirikiano wa wadau na uboreshaji wa Sera ili kuwa na uchumi shindani na wenye kuondoa urasimu katika upatikanaji wa huduma.

Amewaagiza Makatibu wakuu na wakuu wa Taasisi kuhakikisha wanatoa ushirikiano mkubwa katika kufanikisha adhma ya serikali ya kuwa na Serikali ya Kidijitali na matumizi salama ya mifumo inafanikiwa.

Nae Waziri wa Mawasiliano, Teknologia ya Habari na Ubunifu Mhe. MUDRIQ RAMADHAN SURAGA amesema Wizara imejipanga katika kuleta mabadiliko makubwa katika taasisi na wizara zote ili kufikia male

JUMAA MUBARAK
29/05/2026

JUMAA MUBARAK

EID AL ADHA MUBARAK
26/05/2026

EID AL ADHA MUBARAK

SALAMU ZA POLE
26/05/2026

SALAMU ZA POLE

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema hana nia ya kuongeza muda w...
23/05/2026

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema hana nia ya kuongeza muda wa Urais zaidi ya muda uliowekwa kikatiba na kuagiza kusitishwa mara moja kwa mijadala kuhusu suala hilo.

Dkt. Mwinyi amesema kupitia majukwaa mbalimbali, ikiwemo Baraza la Wawakilishi, kumekuwa na mijadala na mapendekezo ya kuongeza muda wa Urais badala ya miaka 10 iliyowekwa na Katiba ya Zanzibar, lakini amesisitiza kuwa hana dhamira hiyo na kwamba mjadala huo hauna tija kwa nchi kwa sasa.

Amesema viongozi wameapa kuilinda Katiba ya Nchi na kuwataka wananchi na viongozi kuelekeza nguvu katika utekelezaji wa maendeleo ya taifa. Ameeleza kuwa kipindi kilichobaki cha uongozi wake kitakuwa cha utekelezaji mkubwa na wa kasi zaidi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na nchi kwa ujumla.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 23 Mei 2026 alipofungua Jukwaa la Wenyeviti na Wakuu wa Taasisi za Umma lililofanyika katika Hoteli ya Golden Tulip Airport, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Wakati huo huo, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali haitakuwa tayari kuendelea kubeba mashirika ya umma yanayoshindwa kujiendesha na kuendelea kutegemea ruzuku kutoka Serikalini.

Amesema bado yapo mashirika ya umma yanayolipwa mishahara na kuendeshwa kwa fedha za Serikali jambo alilosema limepitwa na wakati, huku akiitaka taasisi hizo kujipanga na kujiendesha kwa tija na faida.

Halikadhalika Dkt. Mwinyi amesema Serikali itatoa muda kwa mashirika hayo kufanya mageuzi ya kiutendaji na yale yatakayoshindwa kujiendesha Serikali haitakuwa tayari kuendelea nayo.

Vilevile Dkt. Mwinyi amesisitiza kuendelea kwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050 pamoja na miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo ujenzi na uimarishaji wa bandari, viwanja vya ndege, viwanja vya michezo na miundombinu ya barabara ili kuifanya Zanzibar kuwa kitovu cha uchumi wa kisasa na endelevu.

hmwinyi

UTEUZI
22/05/2026

UTEUZI

JUMAA MUBARAK hmwinyi
22/05/2026

JUMAA MUBARAK

hmwinyi

UTEUZI
21/05/2026

UTEUZI

Address

Rahaleo
Zanzibar

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 13:00

Telephone

+255777416213

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Idara ya Habari Maelezo Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Idara ya Habari Maelezo Zanzibar:

Share