30/05/2026
SERIKALI ya Mapindunzi Zanzibar kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imetiliana saini na kampuni ya Stabit Corporation Limited na kampuni ya Salem Construction Limited ujenzi wa mikataba miwili chini ya Mradi wa BIG-Z, inayolenga kuimarisha miundombinu ya mijini, usimamizi wa mazingira na huduma za kijamii Zanzibar.
Mikataba hiyo inahusisha ujenzi wa Kituo cha kukusanyia Taka cha Fuoni Chunga (Solid Waste Transfer Station) pamoja na utekelezaji wa mradi salama wa watembea kwa miguu katika maeneo ya Mji Mkongwe (Stone Town Safe and Sustainable Mobility Program).
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Aboud Hussein Mwinyi alisema kusainiwa kwa mikataba hiyo ni hatua muhimu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayolenga kuimarisha maisha ya wananchi pamoja na mazingira ya miji.
Alisisitiza umuhimu wa wakandarasi kuzingatia ubora wa kazi, kusimamia muda wa utekelezaji kwa ufanisi na kuhakikisha kunakuwa na uratibu mzuri katika kipindi chote cha ujenzi.
“Tunatarajia kuona kazi zenye viwango bora, utekelezaji unaokwenda sambamba na muda uliopangwa pamoja na ushirikiano mzuri na jamii inayozunguka maeneo ya miradi,” alisema.
Aidha, aliwataka wakandarasi kuwa na mipango kazi madhubuti itakayosaidia utekelezaji wa miradi hiyo kufanyika bila kusababisha usumbufu kwa wananchi, wafanyabiashara na shughuli nyingine za kijamii katika maeneo husika.
" Kukamilika Kwa miradi hii kutaimarisha miundombinu ya mijini, usimamizi wa taka ngumu pamoja na kuweka mazingira salama na rafiki kwa watembea kwa miguu, hususan katika eneo la Mji Mkongwe ambalo ni kitovu cha urithi wa kihistoria na shughuli za kijamii na kiuchumi Zanzibar." Alisema Mwinyi
Kwa upande wao, wakandarasi waliopewa zabuni hizo walieleza utayari wao wa kutekeleza masharti yote yaliyowekwa katika mikataba hiyo, huku wakiahidi kuzingatia viwango vya ubora, usalama wa wafanyakazi, uhifadhi wa mazingira na maslahi ya jamii inayozunguka maeneo ya utekelezaji wa miradi hiyo.
Abuzer Salem kutoka kampuni ya Salem Construction Limited alisisitiza dhamira yao ya kuhakikisha shughuli za